Katibu wa bunge bwana Kashillillah aliita waandishi wa habari kuelezea minyukano iliyojitokeza katika mkutano wa 3 wa bunge hili la 10, aliuleza umma kwamba kilichosababisha ni ugeni wa wabunge na sio udhaifu wa Spika. Alienda mbali zaidi kutolea mfano wa mbunge wa Arusha Mh. Godbless Lema kwamba kitendo chake cha kusema 'funga mlango tupigane' kinatokana na uchanga wake bungeni na kwamba hana wala hajasoma kanuni za bunge. Maoni yangu ni kwamba katibu hajamtendea haki Mhe. Lema kwa sababu
1. Ni wabunge wengi ambao walijibizana maneno wakiwemo wakongwe na mawaziri (tulisikia wengine wakisema 'atoke nje');
2. Si kweli kwamba mhe. Lema hana kanuni za bunge;
3. Kila bunge jipya huja na wabunge wapya lakini haya hajajitokeza huko nyuma;
Mtazamo wangu ni kwamba yaliyojitokeza ni mwanzo tu wa kuonesha dhahiri kwamba spika wa sasa hakuwa amewiva vya kutosha kuvaa viatu vya Sitta. Aidha kitendo cha ufafanuzi huu kutolewa na katibu wa bunge ni ushahidi mwingine kwamba Spika kashindwa. Naomba kuwasilisha.
Maneno hayo ungemwambia aliyesema maneno ha funga mlango tupigane Mbunge wa CCM Deo Filikunjombe munapenda sana kutuhumu na kuchafua jina la LemaSijui lini tutaacha unafiki!lema amekisema kilichokuwa moyoni bila unafiki,matukio kama haya sio mageni duniani,hata bunge la israel panachafuka hadi wabunge hutolewa nje na maafisa usalama.
Lini utaacha hoja za kipumbavu,chambua jambo acha ukuwadi wakati mwingineHahahahahaha! Kweli chadema mnachekesha mnatetea hadi ujinga!
Maneno hayo ungemwambia aliyesema maneno ha funga mlango tupigane Mbunge wa CCM Deo Filikunjombe munapenda sana kutuhumu na kuchafua jina la Lema
Angemsamehe Lema bure kwani Lema ni form four, aliyepata division four points 29, sasa unategemea nini?
simtetei Lema,lakini kuna ubaya kuwa form 4,na kuwa mbunge?kauli kama hii iliwahi kuongelewa na Mh,Job Lucnde,mbona haikuzungumzwa na katibu?kanuni ipi inayosema katibu ndiyo msemaji wa bunge?Acha ushabiki wa kitoto,Angemsamehe Lema bure kwani Lema ni form four, aliyepata division four points 29, sasa unategemea nini?
Angemsamehe Lema bure kwani Lema ni form four, aliyepata division four points 29, sasa unategemea nini?
Sasa hata kama wewe ukiwa spika au Dr Slaa awe Spika utashikilia midomo ya wabunge wote ili wasilopoke na kusema fungeni milango tupigane! Mimi naona ni tatizo la kupata wabunge wahuni ambao wanashindwa kuelewa hadhi ya bunge na kuona kama wako kijiweni!
Kwanza nadhani aliyetamka maneno 'funga milango tupigane' sio Lema, ni mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe Haule. Sielewi kwanini lema anahusishwa na ile kauli
Hahahahahaha! Kweli chadema mnachekesha mnatetea hadi ujinga!
Angemsamehe Lema bure kwani Lema ni form four, aliyepata division four points 29, sasa unategemea nini?