Kashilila hukumtendea haki Lema

Katibu wa bunge bwana Kashillillah aliita waandishi wa habari kuelezea minyukano iliyojitokeza katika mkutano wa 3 wa bunge hili la 10, aliuleza umma kwamba kilichosababisha ni ugeni wa wabunge na sio udhaifu wa Spika. Alienda mbali zaidi kutolea mfano wa mbunge wa Arusha Mh. Godbless Lema kwamba kitendo chake cha kusema 'funga mlango tupigane' kinatokana na uchanga wake bungeni na kwamba hana wala hajasoma kanuni za bunge. Maoni yangu ni kwamba katibu hajamtendea haki Mhe. Lema kwa sababu
1. Ni wabunge wengi ambao walijibizana maneno wakiwemo wakongwe na mawaziri (tulisikia wengine wakisema 'atoke nje');
2. Si kweli kwamba mhe. Lema hana kanuni za bunge;
3. Kila bunge jipya huja na wabunge wapya lakini haya hajajitokeza huko nyuma;
Mtazamo wangu ni kwamba yaliyojitokeza ni mwanzo tu wa kuonesha dhahiri kwamba spika wa sasa hakuwa amewiva vya kutosha kuvaa viatu vya Sitta. Aidha kitendo cha ufafanuzi huu kutolewa na katibu wa bunge ni ushahidi mwingine kwamba Spika kashindwa. Naomba kuwasilisha.


Yeah Kitendo cha Kashilila kujaribu kutetea kwamba spika si dhaifu kimeonyesha udhaifu zaidi badala ya kuweka mambo sawa.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
pole kashilila unacheza ngoma ambayo huiwezi, usidhani watanzania ni wajinga watanzania tunaona jinsi uongozi wa bunge ulivyo pwaya, team ya chadema imetulia tatizo ufisadi umewacost saana mlitoa kifaa mzee wa speeed mkaweka kimeo kwa interest za mafisadi sasa mnahaha kila kukicha kutafuta mchawi, mmechemsha na itaendelea kula kwenu fisadi kashjlila na ccm wenzako, mnakumbuka shuka wakati ni asubui saa tano na joto la chadema mmekwisha, big up chadema team.
 
Sijui lini tutaacha unafiki!lema amekisema kilichokuwa moyoni bila unafiki,matukio kama haya sio mageni duniani,hata bunge la israel panachafuka hadi wabunge hutolewa nje na maafisa usalama.
Maneno hayo ungemwambia aliyesema maneno ha funga mlango tupigane Mbunge wa CCM Deo Filikunjombe munapenda sana kutuhumu na kuchafua jina la Lema
 
Angemsamehe Lema bure kwani Lema ni form four, aliyepata division four points 29, sasa unategemea nini?
simtetei Lema,lakini kuna ubaya kuwa form 4,na kuwa mbunge?kauli kama hii iliwahi kuongelewa na Mh,Job Lucnde,mbona haikuzungumzwa na katibu?kanuni ipi inayosema katibu ndiyo msemaji wa bunge?Acha ushabiki wa kitoto,
 
Angemsamehe Lema bure kwani Lema ni form four, aliyepata division four points 29, sasa unategemea nini?

kapate kikombe kwa babu hali yako mbaya sana,mkeo na baba yako walipata division O na pia usipo wahi kwa babu kwenye kikombe watoto wako wote watapata O mpaka utakapo tubu na kuacha ukada.
 
Hi Spika alivyowaambia wenzake wanafanya mambo ya "KIJINGA" ni neno la busara? Tusipende kuangalia matokeo tu bali tuangalie chanzo pia.
 
Sasa hata kama wewe ukiwa spika au Dr Slaa awe Spika utashikilia midomo ya wabunge wote ili wasilopoke na kusema fungeni milango tupigane! Mimi naona ni tatizo la kupata wabunge wahuni ambao wanashindwa kuelewa hadhi ya bunge na kuona kama wako kijiweni!

Uhuni siku zote hujibiwa Kihuni, uhuni wa kuzomea kama madem! Mwanaume kasema funga milango tuwanyuke!
Uhuni wameanza magamba.
 
Kwanza nadhani aliyetamka maneno 'funga milango tupigane' sio Lema, ni mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe Haule. Sielewi kwanini lema anahusishwa na ile kauli

Kumbe! Ccm hawako makini kabisa, ndiyo maana hata wako na Maji marefu ambaye ujumbe wa mtaa unamzidi uwezo
 
Who cares what Kashilila says?
Na yeye ni mmoja wao, lazima atunze kitumbua chake. Hana ubavu wa kusimamia ukweli..........hana tofauti na Nape Nnauye ambaye anapigia kelele mapacha 3 wajiondoe mapema kwenye chama chake huku pacha wa 4 akitetewa pamoja na familia yake.
 
Hahahahahaha! Kweli chadema mnachekesha mnatetea hadi ujinga!

Ujinga! Kumtia mtu adabu ni ujinga? Ujinga huondolewa na elimu lakini Upumbavu huondolewa kwa fimbo. Hawa wabunge wa ccm wamesoma lakini bado wako vile vile ina maana ni.........
Maana mpumbavu ukimfundsha hadi ukamtwanga kwenye kinu upumbavu haumtoki kamwe hata Biblia imeandika. Dawa Mboko tu.
 
Angemsamehe Lema bure kwani Lema ni form four, aliyepata division four points 29, sasa unategemea nini?

Kuhusu elimu wala usizungumze! Lema is much better by far!! kuna watu hawajafika hata hiyo form four. Kuna madaktari na maprofesa lkn kazi zao bungeni hazionekani na wala hawana mchango wowote kwa taifa hili. Kuna wabunge wamesoma madrasa na wengine si kwa kiwango hicho cha Lema na wapo very productive. Si wote wenye madigrii kuwa ni wazuri na bora. Unaweza kuwa na elimu lkn huna hekima wala busara.
 
Wadau wa jamvi hili, tunapomjadili huyu Katibu wa Bunge Bw. Kashililah inabidi kwanza tumjue yeye ni nani? Kwa utafiti wangu mdogo sana, bwana huyu si lolote si chochote! Kwanza udaktari wake ni wa mashaka achilia mbali uwezo wake wa kazi. Phd yake nasikia ya mtandaoni, wengine wanadai ni ya south Africa lakini bado maswali ni mengi kuliko majibu. Uwezo wake kulisaidia Bunge na kumsaidia Spika wake ni zero. Kwanza atamsaidiaje yule mama wakati yeye mwenyewe alikuwa kibaraka wa mzee Sitta? Ufisadi wao na wizi wa fedha za bunge ndio uliowaunganisha na kuwafanya maswahiba. Sitta alimtaka Kashilila kwa udi na uvumba, alifanya njia zote bwana huyo ateuliwe kuwa Katibu wa Bunge.

Utafiti unaonyesha kuwa Kashilila hakuteuliwa kwa uwezo wake maana waliachwa Wenye uwezo wao na waliokuwa tishio kwa uwezo wa kazi yasemekana walifanyiwa mizengwe na kuhamishwa Bunge. Baada ya Katibu wa Bunge Bw. Foka kustaafu vita ya ukatibu wa Bunge ilianza. Sitta kwa kutafuta mtu atakayelinda maslahi yake alimpigia debe Kashilila aliyekuwa Mkurugenzi ktk mojawapo ya Idara za Bunge kwa muda wa chini ya miaka 2 tu na kuwa Katibu wa Bunge. Ni vema kama angekuwa na uwezo kuliko wengine lakini ni bomu kuliko walioachwa. Natamani ningemuona anatoa lecture siku moja pale UDSM au UDOM na hiyo Phd yake feki kama watu wasingezimia! Nimewahi kumsikia akiongea lugha ya kwa malkia mahali fulani, niliona aibu sana kwa mtu mwenye Phd. Afadhali hata huyo Lema anayedaiwa kuwa ni form four na alipata Div four ya pointi 29, lkn shughuli yake tunaiona!

Kashilila ana ubavu gani wa kuita waandishi wa habari leo na kujifanya kuwakosoa Wabunge? Ni dhihaka kudhani kuwa Wabunge hawazijuwi Kanuni za Bunge, wanazijua vizuri, tena Wabunge wa kambi ya upinzani wanazijua vema kuliko hata hao wa chama tawala! Kwanini Kashilila hasemi kweli nini kilichojiri siku Wabunge walipozozana bungeni? Watanzania ni mashahidi, wana akili, wanaelewa na wanafuatilia mambo. Watendaji wabovu wakiongozwa na Kashilila mwenyewe pengine kwa makusudi na kwa kumhujumu Spika wa sasa aonekane hafai kuvaa viatu vya Sitta hawamshauri vema na pengine hutoa taarifa za kupotosha. Mfano mzuri siku ya tukio, issue ilikuwa ni uchaguzi wa wenyeviti wa Bunge ambapo Kanuni zilipindishwa. Lengo lilikuwa zuri lkn utaratibu ulitaka hilo liweze kufanyika Kanuni ilibidi zitenguliwe. Msaidizi wa Kashilila aliyekuwa Msimamizi wa uchaguzi wakati akitoa maelezo ya taratibu za uchaguzi huo ilibidi atoe maelezo ya ziada kwanini Kanuni zitenguliwe kuruhusu maazimio ya Kamati ya Uongozi kupitisha majina 3 tu na si 6 kama Kanuni zinavyotaka. Hapo ndipo mchezo ulipoanza, mara oh...Kamati ya Uongozi ilitengua Kanuni, mara oh....Wabunge makini wakataka kujua Kanuni zinasemaje? Mie nimebahatika kuzipitia Kanuni kwa sana tu, jamani hakuna mwenye mamlaka ya kutengua Kanuni za Bunge isipokuwa Bunge lenyewe, hata Kamati ya Uongozi wala Tume ya Bunge haina mamlaka hayo. Kuna wakati Msimamizi wa uchaguzi alijaribu kutetea kuwa Kanuni hazijakiukwa na kutaka kuonyesha Wabunge hawazijuwi Kanuni, wote tuiloangalia TV siku ile tuliona Mhe. Halima Mdee akimshushua Katibu huyo wa Bunge kuwa asome Kanuni vizuri na asisome nusunusu, loh ilikuwa aibu! Mhe. Lukuvi kwa haraka alitambua kosa na akaomba sasa Bunge litengue Kanuni ili uchaguzi huo na hayo majina 3 yaliyowasilishwa na Kamati ya uongozi yapigiwe kura.

Bw. Kashilila awe mkweli, amechemka! Kwanza siku ya tukio hakuwa Bungeni wala hakuwa Dodoma, kwa macho yangu nilimuona Dsm akiwa Shopper’s plaza kwenye kliniki ya macho. Kama anabisha akanushe maneno yangu! Kwanza wabunge walioanza kuzomea walikuwa wa CCM tena wengi wao ni mawaziri. Atasemaje aliyesema funga mlango tupigane alikuwa Lema? Kashilila kuita waandishi wa habari anataka kutuambia nini? Ana lipi jipya? Avunje makundi yake Bunge, akae chini afanye kazi na amsaidie Spika! Tangu yule mama kaingia madarakani yasemekana Kashilila hakai ofisini na hampi mama wa watu ushirikiano, kisa swahiba wake Sitta kaikosa nafasi hiyo. Wanachotaka ijengeke picha kuwa Spika kashindwa kazi. Wa-TZ tunazo data za Kashilila asifikiri hatujuwi yanayoendelea huko mjengoni kwao. Asiwe mnafiki wa kujifanya hajuwi kitu. Hivi karibuni alipoulizwa kuhusu ujenzi wa nyumba ya Spika huko Dodoma, eti alijifanya hajuwi kitu, kivipi? Maana yeye ndiye aliyetoa idhini kwa CDA kuendelea na ujenzi wa nyumba hiyo na hata upatikanaji wa mkandarasi etc, inakuwaje anasema hajuwi? Huyu ndiye Kashilila anayetaka kuaminisha watu kuwa yupo makini na kazi yake.

Kashilila kudai kuwa Wabunge wengi ni wapya na ni vijana sio justification ya fujo zinazotokea Bungeni wakati huu. Uzuri ni kwamba pamoja na wengi kuwa wapya na vijana uelewa wao ni mkubwa kuliko wa wakati mwingine wowote. Lazima tukubali kuwa Wabunge wa upinzani pia wameongezeka kulinganisha na bunge lililopita, wasomi ni wengi pia na changamoto zilizopo sasa kama za ufisadi, kupanda kwa gharama za maisha, umasikini wa Wa-TZ unaokua kila uchao ndio sababu za kuongezeka kwa udadisi, ufuatiliaji na uelewa wa wananchi maana hawadanganyiki tena. Watu wanataka kujua A-Z ya hatima ya maisha yao na mustakabali wa nchi hii. Ndio maana wanahoji Bungeni, wanahoji vijiweni, wanahoji magazetini, wanahoji kila mahali....hao ndio Wa-TZ wa leo! Wanataka majibu kwa maswali yao magumu na si blah blah za watu kama akina Kashilila. Kwanza sijuwi kwa nini havuliwi hilo gamba lake hapo Bungeni kama walivyoasisi watu wa chama chake na wateule wake?

Kashilila jivue gamba mwenyewe, maana umeshindwa kuongoza safu ya watendaji wako wa Bunge kumsaidia Spika na kulisaidia Bunge!
 
Back
Top Bottom