Kashilila hukumtendea haki Lema

Kashilila hukumtendea haki Lema

Dhambi ya kumnyima Sitta kuwa mgombea uspika itawatafuna maana katibu alipaswa kutotea ufafanuzi akiwa bungeni iweje afanye kazi za spika.Hakika ccm hawajui kupima mambo mimi naona Anna Abdalla alikuwa bora kuliko huyu anayeishi kwa kanuni na kusahau kutumia uwezo wa akili zake
 
Sasa hata kama wewe ukiwa spika au Dr Slaa awe Spika utashikilia midomo ya wabunge wote ili wasilopoke na kusema fungeni milango tupigane! Mimi naona ni tatizo la kupata wabunge wahuni ambao wanashindwa kuelewa hadhi ya bunge na kuona kama wako kijiweni!

Ndugu yangu mbona hivo? hapo pekundu ninakuunga mkono, ni kweli wabunge wetu wote wana dhamana ya watanzania. Ajira yao ni maalumu siyo kama hizi zingine. Wanatuwakilisha hivyo wana wajibika kwetu, wakikumbuka hili watajirekebisha mara moja. Sikubaliani na wewe kuwaita wahuni. Pressure ya wabunge wa upinzani kuonewa, kuzomewa, kutukanwa, kupigwa vijembe imeundwa mahsusi na wabunge wa chama tawala ili kuwapoteza mwelekeo na ikiwezekana kuwajenga hofu - ni aina fulani ya ugaidi kwa kweli.

Mfano bunge lililopita baadhi ya wabunge wa chama tawala walisikika wakimwambia Mh Tundu Lisu, ''nawe huchoki kusema, kila kitu ni lazima useme?''. Wakati huo huo Mh alikuwa akichangia jambo muhimu sana kwenye muswada wa mahakama ambapo serikali kwenye muswada imeingiza wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa kwenye mabaraza ya maadili ya mahakama. Ni kweli hii inahatarisha uhuru wa mahakama - hili ni jambo la msingi. Hakuna mantiki kulizodoa eti kwa sababu mpinzani kasema. Mwishowe atayeathirika na mfumo wa haki mbovu ni sisi. Mahakama, vituo vya polisi na magereza ni mahali pa kila mtu, hivo ni vyema tukajiridhisha japo kimfumo kwamba haki itatendeka. Hivi karibuni Mh WBM atasimama kizimbani, haijarishi kama mshitakiwa au mtoa ushahidi, atatendewa haki kisheria. Ni vizuri kujenga hoja za msingi.
 
Katibu wa bunge bwana Kashillillah aliita waandishi wa habari kuelezea minyukano iliyojitokeza katika mkutano wa 3 wa bunge hili la 10, aliuleza umma kwamba kilichosababisha ni ugeni wa wabunge na sio udhaifu wa Spika. Alienda mbali zaidi kutolea mfano wa mbunge wa Arusha Mh. Godbless Lema kwamba kitendo chake cha kusema 'funga mlango tupigane' kinatokana na uchanga wake bungeni na kwamba hana wala hajasoma kanuni za bunge. Maoni yangu ni kwamba katibu hajamtendea haki Mhe. Lema kwa sababu
1. Ni wabunge wengi ambao walijibizana maneno wakiwemo wakongwe na mawaziri (tulisikia wengine wakisema 'atoke nje');
2. Si kweli kwamba mhe. Lema hana kanuni za bunge;
3. Kila bunge jipya huja na wabunge wapya lakini haya hajajitokeza huko nyuma;
Mtazamo wangu ni kwamba yaliyojitokeza ni mwanzo tu wa kuonesha dhahiri kwamba spika wa sasa hakuwa amewiva vya kutosha kuvaa viatu vya Sitta. Aidha kitendo cha ufafanuzi huu kutolewa na katibu wa bunge ni ushahidi mwingine kwamba Spika kashindwa. Naomba kuwasilisha.

hongera kwa mawazo mazuri
 
Nakumbuka kwenye mkutano uliopita, yule mbunge wa Mtera (CCM) Livingstone Lusinde alipokuwa akichangia hoja alisema "Milango ifungwe tupigane". Kashilila amelizungumzia hilo?
 
Dr Kashilila kasema kile ambacho tulimtarajia akiseme. Nani kati yenu anaweza kuweka kitumbua chake mchangani ili ashindwe kukitafuna? Tupendekeze tu awepo katibu "kivuli" wa Bunge.
 
Tuende mbele turudi nyuma Bunge letu la sasa limejaa ushabiki wa kiitikadi (KICHAMA) zaidi! Wabunge huwa hawasikilizi hoja vizuri hususani kama imetoka upinzani tena CDM wao watataka kuipotezea bila kuangalia kam hoja iliotolewa inamanufaa kwa nchi au la!

Mfano mzuri ni siku ile PM alipoikubali hoja ya upinzani baada kura ya mmojamoja PM alisema Ndiyo akimaanisha kuikubali, lakini spika akawa anamnganganiza abadili msimamo wake. Hii ni dhamira tosha kuwa Spika wa Bunge letu yuko pale kichama na si kwa maslahi ya nchi.
Haipendezi mtu ukawa shabiki wa chama kupitiliza kisa hoja zinatoka upinzani, kwanza inalishushia hadhi bunge letu linaonekana kuwa ni la vilaza wakati sio kweli wabunge wote ni vilaza ingawa wapo vilaza.

Kwa mukstabali wa nchi hisia zetu za kichama tuziweke kando tujenge nchi bila kujali itikadi zetu za Kichama na Kidini tukifanya hivyo tutaweza kuijenga nchi na ikawa mfano wa kuigwa kwa mataifa mengine
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Ni kweli bunge la sasa lina wabunge wengi wapya wasiojua kanuni na taratibu za bunge.itakuwa ni kosa kubwa sana tukiwahukumu wabunge wapya kwa kosa la kutokujua kanuni za bunge tuwape muda wakujifunza na kuelewa.

Katibu wa bunge Dr Kashalila kasema aliyotakiwa kusema angesema tofauti hata sisi tungemshangaa analinda ugali wake.Yapo madhaifu mengi yaliyofanya na spika wa bunge Mheshimiwa Anna Makinda na waziri mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda nashangaa kwanini hajazungumzia udhaifu wa Pinda au Makinda.

Kauli ya funga mlango tupigane ilitolewa na wabunge wawili mmoja wa upinzani mheshimiwa Lema pia mheshimiwa Lusinde mbunge wa Mtera CCM aliwahi kuitamka chakushangaza Lema anatolewa mfano Lusinde anaachwa !.Katibu wa bunge Dr Kashalila yafaa akae kimya watanzania wa leo si mabwege tunajua anafanyakazi haramu.Wabunge wote waliotumia lugha chafu wasemwe Lusinde,Lema,Cheyo na wengineo wote wasemwe habari za kuchagua/kubagua kwa misingi ya kichama imepitwa na wakati.
 
Sioni ajabu kwa Lema kuwa hajamaliza form four, kwani CDM ndio zao hizo kuweka ma bogus kwenye uongozi ili waendelee kuwatawala, si unakumbuka mgombea mwenza wa Slaa alikuwa darasa la 7 mkuu
[FONT=Book Antiqua said:
Acha kudanganya watu Lema hajamaliza form four alifukuzwa shule akiwa form two kwa wizi wa godoro form four ya points 29 kaipata wapi.Maneno yake mjengoni ni mwisho wa akili na upeo wake hana anachoweza zaidi ya kubwabwaja na kutoa mitusi hovyo.[/FONT][/COLOR][/B]

Tatizo sio Form IV au Phd, tatizo kubwa tulilonalo Watz ni KUTHUBUTU (to Dare)!!! Tunao maprofesa wengi tu lakini ujuzi mwingi unafia vichwani mwao ila Mh. Lema ameonyesha kuwa kama hata angelikuwa STD VII basi anacho deliver kwenye nafasi yake ni zaidi ya wasomi! We endelea kutopenda kufahamu jinsi dunia inavyoenda!!
 
Rafiki yangu Dr kashilila kwa hikli umechemka...hivi ilikuwa lazima kwani kusema chochote??? naomba nikupe ufafanuzi wa kukosa control katika mijadala ya bunge kwa uzito wake nikianzia na zito zaidi

1. Serekali kutaka kuhodhi mamlaka ya bunge kama mhilili

2.serekali kutoelewa kuwa bunge la sasa ni la vyama vingi na sio kimoja

3.uwezo mdogo wa spika makinda ambaye

a. amekubali kuliuza bunge kwa bei rahisi kwa serekali hivyo kulifanya liwe muhuri na si vinginevyo

b. ameshindwa kupambanua na kutenganisha interest za bunge kwa upande mmoja, serekali na chama chake upande mwingine

c. ametawaliwa na jazba (short tempered)

d. uelewa mdogo wa mambo ya sheria

e. kutaka kulazimisha mambo na kutokuwa na busara. mfano ni kura iliyopigwa kuunga mkono au kukataa kifungu kinachowapa wanasiasa na executive mamlaka ya kuangalia mahakama......wabunge wengi hata wa ccm walikataa ule muswada lakini alipotumia njia ya kuita mmoja mmoja waliogopa na kugeuka watendaji wa wizara au kamati ya chama ya bunge....mfano halisi ni pale alipomhoji waziri mkuu mara tatu as if alikuwa anamtaka kubatilisha maoni yake juu ya kuunga mkono maoni ya tundu lissu........kwa namna nyingine pale makinda alikuwa anamchonganisha pinda kwa makusudi na sijui nani alimtuma...KWANI MGETUMIA UTARATIBU WA KUPIGA KURA YA SIRI MNGETOKA DAMU?

e. tabia ya kuwanyamazisha kwa kiburi wabunge wa upinzani ka kukataa hoja zao. spika amekariri kuwa upinzani ni ubomoaji,,

kwa ujumla she is coming from the old school authoritarian class ambalo halina nafasi na haliwezi kuzuia mabadiliko....

4. Uwezo mdogo au makusudi ya viongozi waandamizi wa serekali katika kuandaa miswada ambayo inalea uhuni, ufisadi na uporaji wa mamlaka toka kwa wananchi, na inayokuwa na mrengo wa kupora haki za raia......

5. tabiwa ya watanzania wengi na hasa wanasiasa wetu kuchukulia siasa kama mpira.....kitendo cha waziri kukubali ushauri wa wabunge, tena wale wa upinzani imeonekana kuwa ni defeat na sio maboresho....mawaziri hupigana kufa na kupona kulazimisha miswada ipite hata kama ni ya kipumbafu......


Dr Kashilillah, nadhani sasa ukagombee ubunge uwe mwanasiasa....tena CCM kunakufaa zaidi....
 
Hii nchi ipigwe bei kila mtu apewe chake au? Maana kila anayejisikia anaitisha vyombo vya habari anakoroma tu. Mnatueleza sisi ili iweje? Kama kanuni zikikiukwa si kuna adhabu yake? sasa sie tufanyeje? Waite woote unaoona hawaelewi kanuni uwaelekeze upa au wape adhabu wajifunze kwa vitendo. Iweje mtihani afanye mwanafunzi shuleni masahihisho uyafanye na anayemlipia ada? Waandishi an sisi tulioko huku hatutakaa bungeni utakaaa na haohao vijana. Sasa maelezo uliyoyatoa ni kuwa ulikuwa umetuhumiwa? au wewe ndo Spika? kama Spika kaambiwa ni dhaifu kwa nini asijisemeee, wewe inahuuuuuuuu?????????????!@!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!?

"Kukitumikia chama ambacho hakina muongozo ni sawa na kuwa na mume mleviiiii anyevua nguo hadharani, hata kama anakutia aibu namna gani huwezi kumkana ni mmeo ni mmeo tu" Kashilila na wenzake ni wake wa CCM (mlevi) hawana cha kufanya.
 
naona wengi mnamtolea mfano lema kwan yeye ndo mbunge kijana peke yake? Halaf kwa wanaojua kanuni hebu mtujuze katibu anahaki ya kuzungumzia mazungumzo ya ndani ya bunge? Nawisilisha, kashililah ni kada kama makada wengne ccm.
 
Well done Kashilila, na kweli CHADEMA wanaligeuza bunge kama darasa, wajifunze kanuni na wazielewe ! bunge sio uwanja wa mpira kila mtu anajifanyia kivyake

Badili jina kwenye avatar yako iwe RETARDEDbrain itakufaa kwa upeo wa mawazo unayotoa.
 
Back
Top Bottom