Kashilila hukumtendea haki Lema

Kashilila hukumtendea haki Lema

Zomea zomea inatokana na kupitwa na wakati bunge la Tanzania, wabunge wakongo bado wanaendeza zama zile za kijima za kuogopana na kuoneshana nidhamu ya uoga.
 
Katibu wa Bunge alificha ukweli. Kwani ilimshinda nini spika kukemea au kutoa mwongozo pale alipoona kanuni zinakiukwa? Na pia spika anatumia hisia zaidi kuliko.....
 
kwanza mimi nadhani hyu katibu wa bunge inabidi aombe msaahmaa kwa kuwadharirisha wa tanzania kwa kuwatukana wabunge wtu wapya tuliyo wachagu,,, hawa wapya ambao tuna imainii ndyo watakao tuletea changamoto mpyaaa,yeye alikua anataka tuwachagua wabunge wale wa zamani walio zoea kusinzia sinzia bungenii,,huuu ni udharilishaji mkubwa sanaaa,kwanii yeyey ndyee anayejua kanui zaidi ya wabunge wapya tena wanasheria mashuhurii.....akuana jambo lolote lakuonge ,ukweli ahyo yote ni coz ya incompetence ya spika wabunge?:A S 39:
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Sasa hata kama wewe ukiwa spika au Dr Slaa awe Spika utashikilia midomo ya wabunge wote ili wasilopoke na kusema fungeni milango tupigane! Mimi naona ni tatizo la kupata wabunge wahuni ambao wanashindwa kuelewa hadhi ya bunge na kuona kama wako kijiweni!

Mlengo wa Kati,

Wewe ndiyo mhuni na huyo Kashilila wako!

Kuna mijitu mingine hapa ukumbini ni mavuvuzela wa Chama cha Magamba/Mafisadi-CCM.
Kashilila anaongea upuuzi mtupu hapa. Lakini watu wenye akili timamu they really know who is part of problems or source of problems in our current National Assembly.
Kwanini watu hawataki kukubali UDHAIFU wa spika aliyeko sasa Kibibi ANNE SEMAMBA MAKINDA? Huyu mama ndiyo tatizo kwa sasa kwenye Bunge letu. Mimi naamini kabisa kuwa kama Mhe. Sammy Sitta angelikuwa amekalia kile kiti cha uspika tusingeendelea kushuhudia huu uoza unaoonekana Bungeni kwa sasa!

Madai ya Kashilila kuwa eti Wabunge wengi karibu 70% ni mbumbumbu wa Kanuni za Bunge ni upuuzi!Wabunge wa Upinzani ni aboout 15-20%.The majority ni Wabunge wa Chama cha Magamba!Kwa hiyo Kashilila anataka kutuaminisha kuwa Wabunge wengi wa CCM ndiyo mbumbumbu? Kashilila anajua kabisa michango,umakini na hoja zinazotolewa na Wabunge wa Upinzani hasa CHADEMA zinafuata kanuni za Bunge na ndiyo maana Makinda anapobanwa kuhusu mwongozo wa Spika na waheshimiwa Wabunge(CDM) mara kwa mara anaonekana kuweweseka,kubabaika na mara nyingi kutumia ubabe!

Kashilila lazima akumbuke kuwa hata Wabunge wazoefu wa miaka nenda rudi huwa wanatoa kauli za kuudhi. Mifano iko mingi kama ule wa Malecela enzi za Bunge la chama kimoja miaka ya 70s aliwahi kuwaambia Wadanganyika THEY CAN GO TO HELL kwa kuhoji tu usafiri mbovu wa reli ya Kati wakti yeye akiwa Waziri wa Mawasialiano if I am not mistaken. Tulishasikia FM Mramba enzi zake akiwaambia watu KULA MAJANI ili ndege ya Mhe. Mkapa inunuliwe kwa gharama yoyote. Zote hizi ni kauli za maudhi na zilikuwa zinatolewa na Wabunge wakongwe ndani ya Bunge wenye kuzijua kanuni.

Je,nani sasa ni mbumbumbu wa KANUNI ZA BUNGE kati ya Kashilila,Makinda,Wabunge wa CCM,na Wabunge wa upinzani?


Namaliza kwa kuwasihi Chama cha Magamba-CCM,kwamba kujivua magamba iwe pamoja na kumrudisha Spika Sitta kwenye kiti chake cha Spika maana wote waliofanya MBINU ZA KUMWANGUSHA SITTA NA KUMWEKA MAKINDA kwenye kiti cha uspika wote ni MAFISADI yaani EL,RA na Chenge.
Hapo ndipo mtakapoona Bunge likiendesha kwa STANDARD AND SPEED!!!

Wasaalamu
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Dazu! CCM ni kundi kubwa kuliko tunavyolitazamia. Mbona hajasema kwa nini Spika alitaka kwenda kinyume na taratibu hizo za bunge anazosema wabunge hawana katika mikoba yao? kwani ndo ulikuwa mwanzo wa hayo yaliyotokea na kuyatolea mfano! Waingereza wanasema ''kama watu hawafikiri unavyofikiri wafanye wafanye unachofikiri''. Tutawapeleka kunakotakiwa.
Ahsante
..Swali hili alipaswa kuulizwa na waandishi wa habari waliokuwa wanamsikiliza. Tuna tatizo katika fani ya uanahabari Tanzania... Wengi ni wasikilizaji tu na kureport kama ilivyo....
 
...nawakumbusha-Mbunge kijana wa Mtera (CCM) Job Lusinde a.k.a Bajaj alipata kusikika akisema milango ya bunge ifungwe wapigane.

hii ya Dodoma ni zomeazomea na kauli tu lakini mabunge kama ya Kenya, Israel, India na Uingereza ngumi na zomeazomea ni mambo common, je nako wabunge wengi ni vijana na wageni? Kashilila unajiharibia heshima yako mbele ya jamii.
 
  • Thanks
Reactions: LAT
hahahahaha hajatendewa haki kivipi? nafikiri mtu akiwa mbunge lazima ajijengee ustaarabu fulani: awe na hadhi fulani.
Lema ni Mbunge mzuri lakini bado ana mambo ya kijiweni sana, nimemshuhudia katika maeneo mengi pamoja na kwenye mijadala mbalimbali.

Kama ni uchanga ndo unaowafanya wabunge waropoke (kwangu mimi hiyo ni expression of true feelings) Lema hayoko peke yake, Lusinde wa mtera nafikiri alikuwwa wa kwanza kutangaza ngumi bungeni kama siyo Filikunjombe. Sisi tumewasikia watu wazima wenye uzoefu bungeni wakifanya na kuzungumza mambo yya kitoto bungeni (ndo wazomeaji wakuu). Kama spika angekuwa na uzoefu stahiki angeweza kuli control bunge in such a way kwamba kunakuwa na a modicum of mutual tolerance and respect bungeni. Tuwaache wabunge wafanye kazi zao!
 
Kashililla naye ametumwa.
Bunge letu halina balance kwa maana ya kwamba, sehemu kubwa ni ya wabunge wa ccm A, sehemu ccm B, na tanzu zao. sehemu ndogo iliyobaki ndiyo wabunge wa CDM.
Tangu bunge lilipoanza tuliona shema kubwa ya ushabiki ikitawala kujaribu kuwashusha hadhi wabunge wa upinzani, yaani CDM. Hata wakati wa Kikwete kulihutubia bunge, halafu wabunge wa CDM wakatoka nje tuliona, wote ni mashuhuda wa kile wabunge waliobaki ndani walichofanya; kuzomea, kupiga meza na kutoa maneno mbali mbali yasiyo na heshima mbele ya raisi wao na spika wao, ilionyesha wabunge hao wasivyo na heshima, ukomavu wa mtu mzima hata zaidi kukosa uvumilivu wa kisiasa.
Kwa wengi hata walidhani tendo lile la CDM lilifaa kutolewa adhabu, ilhali wenzao walifanya hivyo baada ya kujua wana haki kisheria kufanya hivyo. Kama wabunge wa ccm A, B na tanzu zao wangelikuwa wanajua kanuni, tungeliona tangu wakati huo, wangelionyesha ukomavu wao kwa kuwa watulivu na kuonyesha staha mbele ya viongozi wao wakuu waliokuwapo mahali pale.
Kinachoharibu bunge ni ile hali ya ushabiki wa kichama hasa unaotokana na chama tawala. Spika anashindwa kusimamia kanuni za bunge kwa kutaka kuwafurahisha waliomtuma, na ili atekeleze malengo ya wale waliomuweka pale, mafisadi.
Huyo daktari asidhani watazamaji ni watu wasio na akili, kila kinachotokea pale bungeni tunakishuhudia. Upitishwaji wa miswada kwa njia ya ushabiki ili kuonyesha upande ulioshinda ni wazi hata bila kujali faida ya muswada ule ni nini kwa walengwa.
Tumeona jinsi ambavyo spika hayuko tayari kukabiliana na changamoto pale wabunge wanapohitaji muongozo wa spika, anahaha na hayuko tayari kutoa nafasi hasa kwa baadhi ya wabunge wa upinzani wanapohitaji kufanya hivyo.
Spika hajui kanuni na ameonyesha udhaifu mkubwa katika kuendesha bunge na bunge ni kichefuchefu
 
Katibu wa bunge bwana Kashillillah aliita waandishi wa habari kuelezea minyukano iliyojitokeza katika mkutano wa 3 wa bunge hili la 10, aliuleza umma kwamba kilichosababisha ni ugeni wa wabunge na sio udhaifu wa Spika. Alienda mbali zaidi kutolea mfano wa mbunge wa Arusha Mh. Godbless Lema kwamba kitendo chake cha kusema 'funga mlango tupigane' kinatokana na uchanga wake bungeni na kwamba hana wala hajasoma kanuni za bunge. Maoni yangu ni kwamba katibu hajamtendea haki Mhe. Lema kwa sababu
1. Ni wabunge wengi ambao walijibizana maneno wakiwemo wakongwe na mawaziri (tulisikia wengine wakisema 'atoke nje');
2. Si kweli kwamba mhe. Lema hana kanuni za bunge;
3. Kila bunge jipya huja na wabunge wapya lakini haya hajajitokeza huko nyuma;
Mtazamo wangu ni kwamba yaliyojitokeza ni mwanzo tu wa kuonesha dhahiri kwamba spika wa sasa hakuwa amewiva vya kutosha kuvaa viatu vya Sitta. Aidha kitendo cha ufafanuzi huu kutolewa na katibu wa bunge ni ushahidi mwingine kwamba Spika kashindwa. Naomba kuwasilisha.

Well done Kashilila, na kweli CHADEMA wanaligeuza bunge kama darasa, wajifunze kanuni na wazielewe ! bunge sio uwanja wa mpira kila mtu anajifanyia kivyake
 
credit to Hon. Lema...... he makes headlines everyday and pose big threat to stalwarts and veteran politicians who proved to be bogus all along their political lifetime

Hon Lema ..... do not hesitate...... neglect suppression and intimidation from sisiem vampires .... go go go.... you have a bright political future ....
 
Huyu bwana asifikiri kuwa watanzania wa sasa niwale wa miaka ya 70. Kama amezoea wabunge wanaolala bungeni bila kutoa michango ya mawazo wanasubiri posho au wakati wa kupitisha hoja/mswada wajibu NDIYOOOOOOOO!!!!!!!!!! AJUE HAO WAMEPITWA NA WAKATI ole wao waliochagua wabunge wa namana hiyo wanarudisha demokrasia nyuma
 
Namaliza kwa kuwasihi Chama cha Magamba-CCM,kwamba kujivua magamba iwe pamoja na kumrudisha Spika Sitta kwenye kiti chake cha Spika maana wote waliofanya MBINU ZA KUMWANGUSHA SITTA NA KUMWEKA MAKINDA kwenye kiti cha uspika wote ni MAFISADI yaani EL,RA na Chenge.
Hapo ndipo mtakapoona Bunge likiendesha kwa STANDARD AND SPEED!!!

Wasaalamu [/QUOTE]

Watu wamekuwa wakiwaongelea mapacha watatu kama Magamba yanayotakiwa kuvuliwa katika CHAMA CHA MAGAMBA lakini magamba ni mengi na kama Makinda aliwekwa na Gamba RA basi naye ni gamba katika chama cha magamba linalotakiwa kunyang'anywa kadi na akisha nyang'anywa kadi automatically anavuliwa ubunge na uspika pia, na hapo wabunge watatafuta Spika Wa Standard and Speed.
 
Henry naona umeanza na moto mkubwa pia nakubaliana na wewe kuwa katibu wa bunge aliongelea kimazoea zaidi,bunge la sasa limebadilika,kama mbunge anaongea pumba kwa nini asizomewe?Hata hivyo karibu sana mkuu japo ulijoin kitambo.
 
wabunge wengi wa ccm ndio wanaotoa kauli za kejeli bungeni, na ndio wanaodai wanazijua kanuni za bunge,katibu wa bunge alizungumza as if hana habari hiyo.
wanashindwa kufanya kazi za bunge,wanafanya kazi za chama wakiwa bungeni.
 
Angemsamehe Lema bure kwani Lema ni form four, aliyepata division four points 29, sasa unategemea nini?

Acha kudanganya watu Lema hajamaliza form four alifukuzwa shule akiwa form two kwa wizi wa godoro form four ya points 29 kaipata wapi.Maneno yake mjengoni ni mwisho wa akili na upeo wake hana anachoweza zaidi ya kubwabwaja na kutoa mitusi hovyo.
 
Livingstone Lusinde wa Mtera alisema wakati anachangia hotuba ya raisi, anaomba siku moja wapigane ngumi ili waonje machungu ya vurugu
Hakuna mwenye uhakika kama ni Lema aliyesema 'funga milango tupigane' but tuna uhakika Lusinde alisema anaomba siku moja wapigane. Hivi kati ya hawa, nani alitakiwa kukemewa kwanza?
 
Acha kudanganya watu Lema hajamaliza form four alifukuzwa shule akiwa form two kwa wizi wa godoro form four ya points 29 kaipata wapi.Maneno yake mjengoni ni mwisho wa akili na upeo wake hana anachoweza zaidi ya kubwabwaja na kutoa mitusi hovyo.

Sioni ajabu kwa Lema kuwa hajamaliza form four, kwani CDM ndio zao hizo kuweka ma bogus kwenye uongozi ili waendelee kuwatawala, si unakumbuka mgombea mwenza wa Slaa alikuwa darasa la 7 mkuu
 
Hivi haya ma-CCM lini yataacha kujidanganya?

Tunafahamu kabisa tatizo la bunge hili ni Spika ambaye hana uelewa wa sheria. Tumeona jinsi alivyochakachua tafasiri ya kambi ya upinzani bungeni.

Tumeona pia jinsi alivyokachuchua hoja ya Mh. Lema kuhusu uongo wa Mizengo Pinda PM. Nitamu quote Mh. Sita aliwahi kusema kwamba Anne Makinda ni Mtu wa kukurupuka hivyo asisimamie hoja ya Richmond.

Tatizo kubwa la Bunge letu ni kwamba Mi-Bunge mingi ya CCM ni mbumbumbu inayopitisha miswaada na hoja kwa wingi wa MIILI yao na sio kwa wingi wa AKILI zao. No wonder ni wabunge wachache sana wa CCM wanaweza wakasimama na Tundu Lissu na kutoa nguvu ya hoja ya kisheria labda Sita au Mwakyembe ndio maana hata Mwanasheria mkuu wa Serikali alitolewa nishai na Tundu Lissu eti hakuna utafiti wowote ambao amewahai kufanyika nchini kuonesha needs za mahakama (sics)

Mi-bunge ya CCM ilizoa kupitisha mambo kama bendera kufuata upepo wamekuja wabunge weledi wa sheria kama Tundu Lissu, Halima Mdee sasa yameanza kuweweseka.

Mbona wakati wa ufunguzi wa bunge wakati wabunge wa CDM walipotoka nje ya ukumbi tulisikia maneno mengi ya kejeli lakini hatukumuona huyui Dk fake akija na statements kama hizi za kipumbavu.

Huyu Kashilila ni sawa tu boss wake Anne Makinda wanaoamini kwamba kama umekaa bungeni mda mrefu basi unakuwa mweledi wa kanuni za bunge. Kwa lugha rahisi ni kwamba kama ukifanya kazi MOI mda mrefu basi siku moja utakuwa neuron surgeon one day bila kwenda shule. Shame on you CCM

Haijalishi gogo limekaa majini muda mrefu kadri gani, haliwezi kugeuka kuwa mamba.

makinda angefuata ushauri wa Msekwa, anahitaji kwenda kusoma sheria ndio aweze kujua vizuri kanuni za bunge.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Acha kudanganya watu Lema hajamaliza form four alifukuzwa shule akiwa form two kwa wizi wa godoro form four ya points 29 kaipata wapi.Maneno yake mjengoni ni mwisho wa akili na upeo wake hana anachoweza zaidi ya kubwabwaja na kutoa mitusi hovyo.

'You are not who you are... you are what you make'.
Whichever way you want to analyse Lema, but lets the truth be told - this young man has exposed Bwana mkubwa's weak side - the PM.
 
Nakumbuka katika kikao cha kwanza Ndugu John Cheyo aliitukana kwa sauti kubwa tu wabunge wenzake wa upinzani kimombo kama hivi 'you fool', 'shut your mouth' akielelekeza haya kwa Tundu Lisu aliposema chama chenye mbunge mmoja kitaongozaje kamati ya bunge kwa mtindo wa kugawana madaraka? Lisu hakutukana lakini aliambulia matusi. swali je, Cheyo naye hafahamu kanuni za bunge? naye ni kijana? hana uzoefu bungeni? This is exasperating!






Ni hivi majuzi tumesoma kwenye baadhi ya magazeti kuwa Mwanasheria mkuu aliitwa kwenye vikao vya CCM kule Dodoma wakati inafanya madaliko katika safu ya uongozi. Na watu walihoji inakuwaje mwanasheria wa Serikali anashiriki kwenye vikao vya chama cha siasa?

Sasa Leo Katibu wa Bunge anaita waandishi wa habari na kuanza kuelezea 'upya' wa wabunge pamoja na madai kwamba baadhi yao hawazijui kanuni! Naomba kama kuna mtu mwenye job description ya katibu wa Bunge atuwekee hapa jamvini ili tujue katibu ana mamlaka gani na anawajibika kwa lipi?

Hizi kanuni za bunge zimekuwa zikiongelewa sana na Mama Makinda na sasa Katibu wa bunge kama some sort of holy gray! Na kuna uwezekano kabisa kuwa walipania kuzipindisha lakini kwa bahati mbaya hawa wabunge 'wapya' ambao wengi wao ni wanasheria wamewazidi 'maarifa' plus wameonesha kuwa kanuni za bunge ni taratibu na lazima zimesomwe pamoja na sheria mama ya nchi yaani katiba.

Mis-calculation ya kuweka Spika, naibu spika na katibu wa bunge ambao wote si wanasheria ndio mwanzo wa sokomoko bungeni. Kashilila aache kuhubiri porojo maana watanzania tumeona zomea zome na mipasho bungeni tofauti kabisa na kipindi kingine chochote hasa kipindi cha Spika Sitta. Kama taifa ni aibu kuona tuliyoona na nadhani ingekuwa busara kwa watu kama wakina Kashilila kuwa na different attitude wanapokaa kwenye viti vya uongozi badala ya kuja na excuses. Mbona kikao alichoongoza Mh. Jenista Mhagama kilikuwa na nidhamu nzuri? Fair play.
 
Back
Top Bottom