Kariakoo kwachafuka, maduka yafungwa...

Kariakoo kwachafuka, maduka yafungwa...

mimi ni muumini mzuri wa dini ya kiislamu lakini uislamu wangu haunifanyi nishindwe kufkikira kwa makini (crtical thinking)nini kinachoendelea hapa dar naomba niweke wazi kwamba sisi waislamu sio watu wa fujo tunapenda amani tofauti na baadhi ya watu ambao sio waislamu wanavyotufikiria juu ya hili na wengine mpk kutukana hali ilipofikia hapa ni sensitive sana na panahitajika maamuzi ya busara sana ili kuweza kusuluhisha hali hii naamini viongozi wa dini ya kiislamu hasa wanaoaminika na kupendwa na waisalamu wakitumiwa vizuri wanaweza kutuliza hali hii,tatizo kubwa linaloawakumba watu ni kushadadia mambo blila ya kujua hasa nini chanzo cha haya yote bila ya kutoa muda katika akili zao kufikiria nini kimetokea,y na nini kinapaswa kifanywe ktk muda husika,najua kwamba kila nchi inasheria zake ambazo inabidi zifuatwe hata kama waislamu wamekosea ktk baadhi ya mambop busara kwanza ingetumika naweza nikakubali kwamba kila nchi inasheria zake na zinabidi zifuatwe lakini kitendo cha kuwapiga watu ni kuongeza chuki kwa watu wengine ambao walikuwa hata hawajui nini kinaendelea busara zitumike ktk kutatua vurugu hizi

waislamu ni watz,wasio waisalamu ni watz,polisi ni watz,nhata wanajeshi pia ni watz wote tunataka amani,tukishadadia kutoka na imani zetu hatutopata suluhu na kuendelea kuwapiga watu ni kupandikiza chuki naa maumivu kwa watu wengiine,

mkuki kwa nguruwe...
 
mimi ni muumini mzuri wa dini ya kiislamu lakini uislamu wangu haunifanyi nishindwe kufkikira kwa makini (crtical thinking)nini kinachoendelea hapa dar naomba niweke wazi kwamba sisi waislamu sio watu wa fujo tunapenda amani tofauti na baadhi ya watu ambao sio waislamu wanavyotufikiria juu ya hili na wengine mpk kutukana hali ilipofikia hapa ni sensitive sana na panahitajika maamuzi ya busara sana ili kuweza kusuluhisha hali hii naamini viongozi wa dini ya kiislamu hasa wanaoaminika na kupendwa na waisalamu wakitumiwa vizuri wanaweza kutuliza hali hii,tatizo kubwa linaloawakumba watu ni kushadadia mambo blila ya kujua hasa nini chanzo cha haya yote bila ya kutoa muda katika akili zao kufikiria nini kimetokea,y na nini kinapaswa kifanywe ktk muda husika,najua kwamba kila nchi inasheria zake ambazo inabidi zifuatwe hata kama waislamu wamekosea ktk baadhi ya mambop busara kwanza ingetumika naweza nikakubali kwamba kila nchi inasheria zake na zinabidi zifuatwe lakini kitendo cha kuwapiga watu ni kuongeza chuki kwa watu wengine ambao walikuwa hata hawajui nini kinaendelea busara zitumike ktk kutatua vurugu hizi

waislamu ni watz,wasio waisalamu ni watz,polisi ni watz,nhata wanajeshi pia ni watz wote tunataka amani,tukishadadia kutoka na imani zetu hatutopata suluhu na kuendelea kuwapiga watu ni kupandikiza chuki naa maumivu kwa watu wengiine,

We mndengereko wakati wa kuandika hii mada cjui ulikuwa unawaza nini.....Huwezi ukaindoa rangi ya mkaa kwa kuupaka chokaa..Hivi ni busara gani ambayo ulikuwa unaitaka wewe katika hilo suala? Je, ni kumchukua m2humiwa kutoka katika mikono ya polisi kwenda kwa Waislamu? Au kuwaacha Waislamu waendelee kuyachoma makanisa?
Katika mambo yanayohitaji kufikiri, jamani tusiwe wavivu kufikiri, najua uliandika huo uzi husika ili ujaribu kulizuia jua kwa ungo lakini hautaweza kamwe.....Ushauri wangu kwako, cku zote unapoyatazama mambo, yatazame kiundani ili kuupata ukweli halisi bila kuangali wewe upo upande gani. Kwani ukiangalia upande uliopo kabla ya kuyachunguza mambo kwa undani ni dhahiri huwezi kuyapata majibu sahihi kwa kupendelea upande uliouegemea.
 
hawa jamaa watata axee, ila nashkuru TZ wame'invest kwenye jeshi kwahiyo hapana shida
 
Nitafurahi kusikia hao wafuasi wameuawa...!

Una roho ngumu sana bosi wangu Remmy. Ungeomba hata wapate wasaa wa kujua mema na mabaya na wajutie dhambi zao. OMG! Tunaenda wapi lakini?
 
Last edited by a moderator:
Mimi binafsi ilani yangu kuwa sishabikii wala sibishanii dini
madhara ya udini ni mkubwa sana
please people acheni huo ubishi kwenye fujo za leo madhara yamewakuta dini zote si waislam pekee na wale wote wanaoshabikia ujue hawakuwa na ndugu,jamaa au marafiki wa karibu kwa hiyo hawajui uchungu
embu fikiria kuwa wewe mkristo una mke/mume kaenda kariakoo kuchukua bidhaa kakumbana na nahayo
je ungekuja humu kupost na kushadadia??
Mi nafikiri hili la waislamu ni zaidi ya udini ni political issue hawa watu hawajielewi wanatumiwa na baadhi ya watu kwa faida zao
ila tunachopanda ndiyo tunachovuna huko tunapoelekea ni kubaya sana
mimi nimeishi nao hawa waisalam hapa huu mwaka wa tatu hapa sijaona fujo zao hapa msikiti wa idrissa ile muamsho wa o alfajiri mie unanisaidia kuamka mapema kuandaa nyumba na kufanya mengine hawatubagui,ujirani mwema ila leo sijaelewa imekuwaje fujo mpaka huku mlangoni??
Leo hii mpaka mda huu watoto wapo shule kwa walimu nimewaambiwa wakae huko mpaka usiku niwafate hali ikitulia
embu fikiria hawa watoto leo wangekuwa nyumbani wanashuhudia hayo na miaka 3 nyuma mtoto mdogo wa chekechea kawekewa bunduki sikioni kama njia ya kumtisha baba yake atoe hela,kashuhudia baba yake akikatwa mapanga,mama yake akishurubiwa na mapanga,umri huo huo kashuhudia watu wanavyorushiana risasi nyumbani kwao,umri huo huo kaona majambazi yalivyouliwa nyumbani kwao,kashuhudia chumba kilivyolowa damu utafikiri machinjio ya kiembe mbuzi leo hii tena angeshuhudia fujo,vipigo mabomu sijui mtoto huyu akili yake itakuwa na kumbukumbu gani????.....
Naandika hapa kwa uchungu sana jamani mlionyuma ya haya mambo tunawaomba sana muache tuishi kwa amani
nashukuru viongozi wenyewe wanalijua hili kuwa wanatumiwa kisiasa
please muache na nyie waislamu amkeni mnatumiwa tu mwisho wa siku hakuna mnachopata zaidi ya kupigwa,kudhalilishwa na kupotezewa mda tu
wenzenu wapo majumbani mwao wanawaangalia kupitia channel ten miguu juu
 
Haki gani akosayo muislamu akapata mkristo? Wote tunataabika na maisha, akili yako na busara tu ndo vinaweza kukusaidia kupata haki duniani.... Wala si vurugu.... Wahuni wachache wasivuruge amani yetu

Mungu saidia TZ

Hata shule za kikristo wanapeleka watoto wao, hebu wewe peleka mwanao kwenye shule zao..
 
Sio kweli,mkapa alipeleka majeshi mwembechai,na hata vifaru alipeleka ktk uchaguzi zenj,mkapa aliua watu kama kuku,jk hajaua watu ktk maandamano,jk ana imani sana.

kaua sana Arusha,Morogoro,Iringa na Migodi Musoma.
 
Tanzania imepoteza amani kwa kuichezea amani. Tunamsubiri mkuu wa kaya anene.Ila ninashakia,maana si mwepesi kuingilia kati mambo yakiharibika.Naona anaogopa kuchukua uamuzi mgumu. Uongozi siyo kutafuta kumfurahisha kila mtu.
 
Waislamu mnaonewa????? angalia list hii

1) President
2) VP
3) IGP
4) director was TISS
5) Judge mkuu
6) Judge kiongozi

Mungu awape nini???? wakristo wamekaa kimya kabisa, ila ingekuwa opposite ungeona moto wake.

Usisahau RPC wa Dsm pia
 
haitakuwa na faida. Lkn najua endapo nchi ikachafuka, halafu maamuzi yakija kwamba waislam na wakiristo na wislam wagawane madaraka ndani ya nchi itakuwa pigo kwa wakiristo ambao kwa sasa kitu kama hicho hawataki kukisikia

Vp kuhusu hindus, baniani, freemasons na atheist nao wagawiwe madaraka pia. Tuna dini nyingi Tz hivyo ni ubinafsi kujifikiria wenyewe.
Kibaya ni kuwa mkimaliza kugawana kidini itafuata kikabila, kijimbo, kiukoo kabla hujajua tutakuwa tumekwisha.
 
Matokeo ya kucheka na kima tunaelekea kuvuna mabua...Walikuja mambo ya ndani mkawapokea kwa nderemo na bashasha, mkatekeleza madai yao tena kwa kukiuka utaratibu wa kisheria....wakaandamana kumn'goa ndalichako na mufti dhaifu kakaa kimya yuko busy kupanda vibaiskeli vya kukokotwa na kupiga picha na masupa staa sasa wanakuja ikulu...safi sana. wenye akili za kutosha tuliona haya na tukaasa! Very guuud nendeni ikulu....

Wamefikia hatua ya juu kabisa ya ujinga wao. Kama wanamtaka Ponda Issa Ponda, nani kawaambia kuwa yuko Ikulu?
 
Back
Top Bottom