Kwani Yona hakuendelea na uzima na uhai katika hali ngumu ?
😅😅😁 kuna kitu kidogo hujaelewa na hapa.
YESU KAMA YONA
Yesu pia, baada ya dhiki aliyodaiwa kupitia, alipaswa kufa. Kama alikufa, hilo halingekuwa muujiza. Lakini kama aliishi, kama alivyojitabiria mwenyewe, na kuthibitisha "kulingana na maandiko", hilo lingekuwa "ishara" — MUUJIZA! Na haya ndiyo maneno yake:
"... Kama Yona alivyo kuwa ..." (Kiingereza), "Want soos Jonah ..." (Kiafrikaans), "Ngokubanjengo Jonah ..." (Kizulu).
"Kama vile Yona alivyokaa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la samaki mkubwa, ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa ..."
— (Mathayo 12:40).
Je, Yona alikuwaje katika tumbo la samaki huyo kwa siku tatu mchana na usiku — Amefariki au Hai? Waislamu, Wakristo na Wayahudi wanatoa hukumu ya pamoja — A-L-I-K-U-W-A H-A-I!
Na Yesu je, alikuwaje kaburini kwa muda huo huo — Amefariki au Hai?
Zaidi ya Wakristo bilioni moja, kutoka katika kila dhehebu au madhehebu wanatoa hukumu ya pamoja — A-M-E-F-A!
Je, hilo ni sawa na Yona au TOFAUTI na Yona katika lugha yako?
Na kila mtu ambaye akili yake haijachanganyikiwa, atasema kuwa hilo ni TOFAUTI KABISA na Yona. Yesu alisema kuwa atakuwa
"KAMA YONA", lakini wafuasi wake waliovurugwa wanasema alikuwa
"TOFAUTI NA YONA!"
Nani anasema uongo — Yesu au wafuasi wake?
Nakuachia jibu wewe!
BIASHARA KUBWA
Lakini dini ni biashara nzuri. Kwa jina la Kristo wanapata pesa nyingi mno. Wainjilisti wanasema tumekosea kabisa. Wanasema lilikuwa ni jambo la muda ambalo Yesu alikuwa anatabiri, na siyo kama atakuwa Amefariki au Hai.
Wanasema, "Huwezi kuona kuwa alikuwa anasisitiza kipengele cha muda? Anarudia neno 'tatu' mara nne."
Hawa ni watu wanaozama wanaoshika majani; hata wanawake wanaozama hufanya hivyo hivyo!
Yesu alisema nini?
"Kama vile Yona alivyokaa siku TATU na usiku TATU katika tumbo la samaki; ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku TATU na usiku TATU katika moyo wa dunia."
(BIBLIA TAKATIFU) Mathayo 12:40
Yesu hakuwa karibu na "moyo wa dunia"; alisemekana kuwa katika kaburi, ambalo liko juu ya ardhi. Labda alikuwa anazungumza kwa mafumbo.
Tatu na tatu kwa hakika zimerudiwa mara nne, lakini hakuna cha kimiujiza kuhusu kipengele cha muda. Wayahudi walikuwa wanamwomba Yesu "ishara" — muujiza, na hakuna jambo la kimiujiza kuhusu siku TATU, au wiki TATU au miezi TATU.
Mara ya kwanza niliposafiri kutoka Durban kwenda Cape Town, miaka thelathini iliyopita, nilisafiri kwa treni, na treni ilichukua siku TATU na usiku TATU kufika huko.
Hoorey! Ni Muujiza!
Upuuzi, utasema, na nakubaliana nawe.
Lakini si rahisi kwa Mkristo kukubaliana kwa sababu wokovu wake unaning'inia kwa uzi mwembamba. Hivyo, analazimika kushikilia kwa nguvu.
Sisi tunaweza kumvumilia kwa wema. Hivyo, hebu tumfurahishe!
Basi, je ilikuwa ni kipengele cha muda ambacho Yesu alikusudia kutimiza?
"Ndiyo!" anasema Mkristo.
Yesu alisulubiwa lini?
Sehemu kubwa ya Ukristo inaamini kwamba ilikuwa ni Ijumaa jioni miaka elfu mbili iliyopita.