HABARI YOTE WALIYOANDIKA ILIKUWA NI
YA KUSIKIA TU!
— Maana hakuna hata mmoja wao aliyekuwa hapo kushuhudia kwa macho kile kilichokuwa kikimtokea Yesu pale Golgotha.
Katika wakati muhimu kabisa wa maisha ya Yesu:
"...WOTE WALIMWACHA NA KUKIMBIA." (BIBLIA TAKATIFU) Marko 14:50
- "Alisulubiwa": Baadaye, hoja ya “ALISULUBIWA AU ALISULUBISHWA KWA KUIGIZWA” itajadiliwa. Waandishi wa Injili hawakujua matumizi ya alama za nukuu kuonesha kuwa hiki ndicho wengine wanasema, au hiki ndicho “kinachodaiwa”.
- Wazi zaidi ni Mathayo: "...Kisha wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia." (Mathayo 26:56)
WALE WANAFUNZI WA KWELI
Marko anazungumzia wale "kumi na wawili" waliochaguliwa. Sio kuhusu wale wa siri waliompenda Yesu kwa dhati kama yule Yohana mwingine aliyemchukua Mariamu mama yake Yesu nyumbani, na Nikodemo pamoja na Yosefu wa Arimathaya na wengine kama hao.
Kwa kuzingatia usaliti mbaya wa wale "kumi na wawili" wengine, ninasitasita kuwaita hawa "wanaume" wanafunzi.
Au je, Marko alikuwa anadanganya? Aliposema “wote,” je, hakumaanisha
“wote”?
Hakukuwa na kurejea tena kwa mashujaa hawa.
Mwandishi wa Injili ya nne anataja idadi ya wanawake waliokuwa katika msafara wa Yesu. Miongoni mwao walikuwemo Maria watatu,
“na yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu.”
Anarudia msemo huu mara kadhaa bila kumtaja waziwazi kuwa ni YOHANA — msaidizi wao kule Yerusalemu.
Kwa nini?
Kama huyo Yohana ndiye mwandishi mwenyewe wa Injili ya nne, basi kwa nini hajisema wazi?
Kwa nini aogope?
Hakuwa na haya alipomwomba Yesu awape yeye na nduguye viti:
“Mmoja mkono wa kuume, na mwingine mkono wa kushoto katika Ufalme wako.” (Marko 10:37)
Sababu ya unyamavu wake ni kuwa
"mwanafunzi mpendwa" ni mtu mwenye jina sawa naye — yaani
pia anaitwa Yohana! Wale wanafunzi wengine hawakuwapo kabisa wakati ambao Yesu aliwahitaji zaidi. Kama Marko asemavyo:
"wote walimwacha na kukimbia!" — (Marko 14:50)