Kampeni ya kuikataa Vodacom

halafu mpaka wasomi kabisa na akili zao, eti....wanaacha kutumia VODA!!! wakati ni mitambo ya TCRA na makampuni yote wanafanya hivyo

Hapo kwenye mitambo ya TCRA sijakuelewa unamaanisha nini. Ujumbe upi ulitaka kuufikisha? TCRA wana mtambo upi huo?
 
Vodacom wamevimbiwa pesa zetu wanazo tulangua ktk huduma zao uchwara wameona haitoshi wanashirikiana Majini, mashetani na vibaraka wote wa uovu kumwaga Damu za wa Tanzania. Vodacom ikataliwe na kilapenda Haki, amani na umoja hapa nchini? Voda ni janga la kitaifa?
 
Mkuu hapo kwenye nyumbu namaanisha wabongo wengi wasahaulifu,
Vodacom wakitoa ofa mfululizo kama 2 au 3 hivi watarudi tu wapenda dezo,ila wachache watakomaa
 
Kweli hawawezi kukataa, fikiria sakala lile la vigogo wakuu wa Voda kuswekwa ndani kwa Uhujumu uchumi, je wangekataa vipi?
Ila mi binafsi nilishaachana nao mwaka 2014 baada ya kukaa nao miaka miaka saba. Walisepa na vijisenti vyangu nikaachana nao mpaka leo naona maisha yanaendelea kwingineko
 
Chochote nisichokusudia kisikiwe na MTU asiyetarajiwa nami ni siri yangu bila kujali mtazamo wako ndugu
 
Mitandao yote ipo chini ya TCRA na sheria ya mawasiliano ,sasa mtahamia mtandao gani ambao TCRA na sheria hazifanyi kazi!?
 
Hadi sasa mzee anapata taabu sana kutawala analazimika kudukua kuteka kupiga risasi kuua kufanya chochote kwa hata anayetoa mawazo guru kikatiba lakini hola he akikaa miaka 10 ataua wangapi?
Kuhoji uraia, kupiga marufuku mikutano halali ya kisiasa.

Nchi inaendeshwa kwa uhuni wa kishamba sana.
 
Wabongo wameamua kususia kweli? Au stories za Twitter tu?
 
Kama wanajua sheria zinakataza kwa nini wakubali kutoa siri za watu,kwani wao hawawezi kutumia sheria zilizopo,huoni utetezi rahisi kabisa,kama kuna mitandao mingine itabainika nayo tutaipigia kelele kama Vodacom.
 
Safi sana..
 
Badala ya kuwachukia wabunge waliopitisha sheria, mnawachukia Voda wanaotii sheria zilizotungwa na bunge lenu ajabu...
 
Voda wameshajipambanua tayari, hayo makampuni mengine wakifanya hivyo, tutajua namna ya kupambana nao.

Vv
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…