Kampeni ya kuikataa Vodacom

Kampeni ya kuikataa Vodacom

Mi nawaomba kwa umoja kabisa tuanze kampeni hii ya kukataa kutumia vodacom labda akili itawarejea, haiwezekani sisi kama wateja siri zetu zinatolewa pasipo ruhusa ya mteja na kama haitoshi unafungiwa kupiga simu pasipo kutaarifiwa na kubwa zaidi tabia yao ya kupunguza vifurushi. Tuseme sasa inatosha voda wameota mapembe wakati sisi ndo tumewafikisha hapo.
# TuikataeVoda
# HawatufaiVoda
Nakuunga Mkono

Vodacom wamekuwa wezi sana

Halafu hivi vifurushi vya cheka na kaskazini ofa vikoje? Wenzangu wakitoa 1500 wanapata dakika za kutosha za wiki nzima, lakini kwangu ni dakika 70 tu

Kulikuwa na huduma ya Jimwage na cheka huku Mwanga KLM, sasahv wameondoa na kuwafanya watu warudi tigo na line zingine

KWANINI WANATOFAUTISHA HUDUMA KWA WATEJA?

Tangu mwezi wa 6 mwanzoni nimekuwa nikitumia tigo zaidi.

Nitawahama hawa Voda wallah.
 
halotel hawana 4g mkuu, speed yao ina-range kwenye 7Mbps akati voda wanacheza na 50+ Mbps. Mbabe ni mbabe tu
Same shaking tibia kilimanjaro, waweke usawa kwny huduma na warudishe huduma kama jimwage na cheka
 
Mi nawaomba kwa umoja kabisa tuanze kampeni hii ya kukataa kutumia vodacom labda akili itawarejea, haiwezekani sisi kama wateja siri zetu zinatolewa pasipo ruhusa ya mteja na kama haitoshi unafungiwa kupiga simu pasipo kutaarifiwa na kubwa zaidi tabia yao ya kupunguza vifurushi. Tuseme sasa inatosha voda wameota mapembe wakati sisi ndo tumewafikisha hapo.
# TuikataeVoda
# HawatufaiVoda

Tatizo voda ni serikali unakataa voda unatumia mtandao gani ttcl ahahahaha yani ndo utakua punguani kabs labda ukatae voda uamie safaricom kenya ila sio mtandao wa hapa tz kama voda amefata sheria ya tcra ni mtandao gani unadhani utakua na kiburi ili uitwe wa kibeberu alafu tena utaitwa na serikali pamoja na mwananchi huyu huyu anaesema haya leo wakati sheria inatungwa na kupitishwa wengi walifurahi hadi wasanii wengi wa bongo walifurahi sana wakijua ni sheria kwaajili ya taifa kumbe ni seeikali dhidi ya raia wake ndani ukaletwa mtambo toka sijui korea watu wakasema ndio mitandao mwisho wa kutuibia sasa ngoja tuone sarakasi hii tutulie dawa ituingie bora voda amewapa taarifa wateja kuwa ni sheria nenda ttcl ndo kwao tena hata taarifa upati loudspeaker iko gogoni na bando wamewashushia yani kama kumkamata njiwa weka mtama mwingi wataingia mtegoni c tunajulikana tena tunaambiana na wengine wanajua nn kinaendelea wanatuswaga tu msingi turudi tu kwenye tamaduni zetu tukutane mbichi mbichi tupeane taarifa au whatsapp na social media nyingine basi ndo mana mkuu anajua awezi pata kitu huko ndo mana anachukia sana mitandao ya kijamii sana anatamani afanye kama china
 
Naanza na TTCL then Voda na wengine!

Makampuni ya kipumbavu sana!

Eti TCRA wamesema tufungie simu yako,yaani Vodacom inaongea hivi kabisa mbele ya mteja anaeenda kutekwa na regime hiyo hiyo!?

Yaani kampuni inasaidia utekaji??!

Kuna makampuni pia yalimsaidia Hitler,hii dunia tunaenda wapi?!

Tatizo ni serikali yetu sio kampuni mkuu mbona we ukikamatwa na askari unatulia na kutii sheria nini voda wenye nchi wakitaka yao we huna say na ndo mana una fake id mkuu
 
Kusema ukweli mpenzi wa mungu toka zianze kusikika tetesi za kuwa chama tawala kina hisa na kampuni yasimu yavodacom tanzania baadhi yawadau tumetokea kutokuikubali kampuni hii kwa gharama na kuvujisha privacyza watu
Naombeni ushauri kwa wadau tusio penda siasa na gharama za matumizi ya bandle na mengineyo upi nimtandao sahihi wakutumia ??
LISEMWALO LIPO
Kama sio mtumiaji sana wa internet, yani wewe haujali sana Internet kuwa slow tafuta laini ya chuo ya Airtel itakusaidia sana ila kama una matumizi makubwa ya internet jaribu tigo ndio naona at least internet yake ipo strong.

Halotel sijawahi kutumia, TTCL nilitumia mwaka jana wako vizuri ila sio wa kuaminika sana kama mitandao ya tigo, airtel na voda ambao saiv it sucks!!
 
Shukrani sana Dr.@albaniemarcossy  Tafadhalini lengo letu ni kulinda faragha za .jpg


Hii ni hatari sana kibiashara , taarifa zinadokeza kwamba waliochukua hatua hii ni mamia kwa maelfu
 
Tatizo ni serikali yetu sio kampuni mkuu mbona we ukikamatwa na askari unatulia na kutii sheria nini voda wenye nchi wakitaka yao we huna say na ndo mana una fake id mkuu

Makampuni yapo kwenye position of power pia!

Yanatakiwa yakiona a bully anataka kuonea the powerless kabisa yasimamie haki ya the powerless!

Wewe na mimi ni wananchi wa chini kabisa tupo powerless kabisa,lijitu kama regime linataka kutuonea walao haya makampuni yasaidie haki!

Atleast hata kwa kukataa kutumiwa kufanya uonevu kwa niaba ya regime!

Mimi nikishikwa kwa chochote ni so powerless,walao makampuni yapo position of power zaidi yetu sisi!

Yasimame kwenye haki kwa mwananchi wa chini kabisa!

Usifananishe Vodacom na mtu powerless kama mimi na wewe!

Vodacom haiwezi onewa na serikali kiivyo,yana muscle kisheria na ki-connection ndani na nje ya nchi,maana sisi ndio wateja wao,tukifa wao watafeli!

Haki ni haki,na mnyonge wa chini ambao tupo wengi mwisho wa siku tuna-prevail!

Vodacom hata kama watu wataendelea kutumia kama ilivyo lakini mioyoni inachukiwa!Kuchukiwa mioyoni ni mbaya zaidi!Competitor anaweza capitalize hapo hapo Vodacom akawa number 2 in a minute!

Utawala huu utaondoka Vodacom itakauwepo,ila watu hawataisahau ilivyotumia unyama ku-act kama agent wa uonevu.

Wanachi hawasahau uonevu.Vodacom is evil kukubali hili hata kama kwa sheria!Wanadamu wana utashi,huyu Mu-Egypt angesimamia ubinadamu!

Tunajua regime ni evil,mbaya zaidi ni pale tunapoona tuliemuamini tukampa moyo wetu wa mawasiliano anashirikiana na the biggest evil kumfanyia kazi ya uonevu ina pain zaidi!

Sijui nani atatutetea kwenye hii prison country!

Sijui na sijui twende wapi!
 
Kwakweli sidhani kama hili ni jema kwa biashara ya hawa jamaa, jana tulikuwa tunajadili hili na rafiki zangu baada ya mmoja kutuambia na yeye kaachana na voda, nikawaza kwamba biashara ni ushindani, itakuwaje kama makampuni pinzani wakaingiza hela kinyemela kwa ajili ya kusapoti hii kampeni........
 
Si walisema ilikuwa ya ccm... .
Inawezekana kabisa kuwa bado ina miiko ya ccm.
Watu walishachoka kila kitu kinachohusu ccm.
 
Nimekumbuka somo la Kiswahili darasa la tatu. Nilikuwa nafurahi sana mwalimu akisema leo ni imla. Anasomaaa unaskia nukta, anasoma tena unasikia koma, halafu unasikia alama za kufungua semi, hivyo hivyo mpaka imla ya ukurasa mmoja inaisha anakusanya daftari.
 
View attachment 1167901

Hii ni hatari sana kibiashara , taarifa zinadokeza kwamba waliochukua hatua hii ni mamia kwa maelfu
Hii ya kukopa muda wa maongezi na kusepa inanikumbusha wakati ninasoma yalitokea maandamano ya wanafunzi wakidai kimenunuliwa chakula chenye sumu,mchele ndio unaopikwa shuleni.Lakini kitu cha ajabu wakati wa chakula wanafunzi wanagombania hicho chakula chenye sumu.Mimi ushauri wangu ni mngekopa pesa m-pawa ndio msepe!
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Hakuna mwenye ubavu wakukimbia mtandao kama voda watu wanaongea tu lakini sio rahisi hivyo mpesa haikwepeki lakini pia kabla mtu hajakutumia atahitaji kuongea na wewe kwanza
 
Mnawaonea voda, ikiwa maagizo yanatoka juu nani wa kupinga?
 
RIP Voda, ila utabaki nao Rostam na Fred maana hata watumishi was umma watakuwa TTCL
 
Back
Top Bottom