Kampeni ya kuikataa Vodacom

Kampeni ya kuikataa Vodacom

Nami natangaza rasmi kuachana na voda leo nishavunja line yao nabaki na tigo na airtel,pumbavu zao wanatudukua sisi.
 
kisa nini, mbona hakuna maelezo ya kutosheleza
 
Voda wametufelisha big time... Ulikuwa ni mtandao wa kuaminika sana na kinara hapa nchini ila siku za hivi karibuni wameanza kubweteka baada ya kujizolea wateja wa kutosha. Kwanza wameanza kwa kupandisha gharama za bundles zao even mpesa charges na PILI kuna hili ambalo ndio linakuna vichwa vyetu la privacy. Wamekuwa wakishirikiana na mamlaka kutoa credential zetu bila order ya mahakama wao wakidai wanacomply na policies zilizowekwa!
Kwa hayo yote ni big disappointment kwa wateja wao.
 
Si walisema ilikuwa ya ccm... .
Inawezekana kabisa kuwa bado ina miiko ya ccm.
Watu walishachoka kila kitu kinachohusu ccm.
Yaani Jana kanijia mtu wa Siku nyingi ambaye tunajuana sana kahitaji msaada mmoja ila kavaa kofia ya kijani imeandikwa Chagua CCM.
Sina hakika kama atakuja ivaa tena, maana msaada alikosa na hotuba kali aliipokea.
 
Kwa heri Vodacom

Karibu Halotel

Voda mbaki salama na udukuzi wenu na policccm
 
Ili kuonyesha kwa vitendo mjikusanye hata watu mia mrudishe line zao muambatane na vyombo vya habari hii itakuwa na impact kubwa sana.
 
Kwepeni zote.

Hakuna kampuni ambayo wateja wake hawarekodiwi.
Msipotoshe,issue sio kurekodiwa,issue ni kutoa/kuvujisha mawasiliano ya wateja kinyume na sheria taratibu tena kwa masilahi yenye mwelekeo wa kisiasa.

CCM bakini na voda yenu kwa masilahi yenu.
 
Sijawahi kuwa Vodacom tokea mobitel zianze. Nilianza kuwa na kampuni ya kwanza Tanzania "Mobitel "mpaka leo Tigo.
 
Hapo serikali ikisema mtandao ufutwe nchini sababu za udukuzi hawa hawa wanaonadi kususia voda watakuja na kusema mnajua ni watu wangapi wanakosa ajira kwa maamuzi hayo?
 
Wafanyakazi wa mitandao mingine punguzeni makeke..voda mtandao Bora Tena wamashua..boys and girls tigo
 
Hakuna mwenye ubavu wakukimbia mtandao kama voda watu wanaongea tu lakini sio rahisi hivyo mpesa haikwepeki lakini pia kabla mtu hajakutumia atahitaji kuongea na wewe kwanza
Mkuu, usemalo ni kweli but fanya utafiti upya, airtel money inakua kwa kasi ya ajabu sana sasa hivi; binafsi nina mwezi 2 hu sinunui kabisa vocha zao hawa jamaa, sababu yangu ilikua ni wizi, lilipo ibuka suala la udukuzi ndio kabisaaa, nimewafutilia mbali. Mke wangu mwenyewe nae nimemnunulia line ya airtel, Maisha yanasonga
 
*149*03# utapata southern offer unakula GB 1.2 kwa 1500 tu kwa week kwangu voda ni mteremko kama kitongaaa
 
Back
Top Bottom