JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Akizungumza na waandishi wa habari Machi 04, 2024, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Benjamin Kuzaga katika hafla fupi ya mapokezi ya magari na Pikipiki ameishukuru Kamati ya Usalama barabarani Mkoa wa Mbeya kwa msaada wa magari na Pikipiki hizo kwani zitasaidia sana katika kufanikisha kutekeleza majukumu kwa ufanisi na haraka.
Naye, Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama barabarani Mkoa wa Mbeya Mhandisi Rajabu Ghuliku ameeleza kuwa "Kamati imeona vema kutoa msaada wa pikipiki na magari kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya ili kuongeza ufanisi katika kutekeleza majukumu katika Kikosi cha Usalama barabarani Mkoani Mbeya"
Jumla ya magari mawili na pikipiki mbili yenye thamani zaidi shilingi Milioni 31 yamekabidhiwa katika hafla hiyo.