Ashampoo burning
JF-Expert Member
- May 12, 2023
- 420
- 1,582
Basi tulivyokuwa wadogo enzi mwaka 1996 nikiwa zangu mgeni kabisa iringa mafinga ndo mara kwanza niliwaona hawa wana kamati ya nidhamu(nyigu)...
Hawa wanakamati ya nidhamu(nyigu) mara nyingi walipenda sana kujenga nyumba zao vibarazani hasa karibu na meter za umeme sasa tukiwa wadogo tulipenda sana kupiga nyumba zao mawe zinabomoka wakitoka tunakimbia ..
Hawachoki wanajenga tena kama kawaida yetu watoto wa mtaa ule tulikuwa tunapenda kuchezea sana nyumba zao kwa kuzibomoa sasa kumbe wanakamati wanatusoma tu jinsi gani ya kututia adabu
Sasa siku moja tukiwa kuna mtoto mmoja mtaani alirusha jiwe kwenye nyumba ya wanakamati haikubomoka ...asee walitoka kama 30...kwa hasira walimfanyia operation ya kichwa aasee alivimbaaa kichwa macho akawa kama mchina mimi nilipona siku hiyo maana tulikimbia mno ....yule mtoto aliyefanyie operation ya kichwa alikuwa jiran yetu alipelekwa hospital mafinga na kulazwa... nyigu ni mdudu balaaa wana hasira sana yaani kukufanyia open surgery dakika mbili
Baaada ya wiki kupita tukawa tuna cheza cheza tuko na kakangu mmoja sasa hivi anafanya kazi njombe huko.... sasa tukamuona mwanakamati ya maadili katua kwenye maua tukamua kwa hasira kulipa kisasi ....sasa mwanakamati aka nyigu hata ukimua ule mkia wake bado unakuwa unafanya kazi
Kiutani yule kaka angu akachukua ule mkia akijua amekufa si akaniweke ndani ya sweater maeneo ya kifuani asee nilifanyiwa operation ya kifua fasta nilipiga yowe sito sahau kifua kilivimba balaaa ......aseee nililiia balaaaa nilitoka naruka ruka nimeshika kifua hadi nyumbani kwa maza mungu amrehemu akaninipooza akanishauri nikiiona nyigu nikae pembeni hadi leo nikiwaona sina hamu nao
Walinipa nidhamu hadi leo sina hamu nao
Andika kisa chako ni hii kamati ya nidhamu aKA nyigu