Usimpe mtu connection ya kazi ni Bora uiuze kwa gharama

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,339
51,883
Kwema Wakuu!

Namna Bora ya ku-deal na vijana wa sasa ambao Asilimia 90% ni Vijana wa hovyo ni kuwa na roho ngumu tuu. Kama unahitaji mahusiano mazuri yenye furaha na vijana hawa na hautaki kuumia basi nakushauri kuwa na roho ngumu.

Kama sio mtoto wako uliyemzaa basi usimpe connection ya kazi, au usimpe mchongo wa pesa. Ni akheri umuuzie hiyo connection.
Kwa wale wasiojua ni kuwa siku hizi kupata kazi ni mpaka uwe na pesa, hiyo ni biashara inayoendelea mjini. Na haijaanza Leo wala jana. Hilo watoto wa mjini wanalifahamu vizuri tuu.

Kuuza connection ya kazi ni Sawa na kuuza ramani ya nyumba. Hakuna kitu cha Bure. Mwambie mtu Kama unataka kazi nipe kiasi kadhaa nikupe kazi.
Mfano; kazi hii Mshahara wake Kwa mwezi ni Tsh Milioni moja hivyo ili nikupe hii kazi nipe 1M nikupe connection, hataki muache apite kushoto.

Au kijana anahangaika anatafuta kibarua chochote anakulilia shida, wewe usimuonee huruma machozi yake au anavyolalama. Mwambie kuna kazi ya laki tano, nipe laki tano nikupe connection ukafanye kazi. Masuala ya burebure mwambie huna.

Unajua KAZI Kama haujaitolea jasho kuitafuta huwezi kuithamini.

Uza kazi
Uza michongo
Uza ramani ya maadili
Hakuna kutoa burebure. Utanishukuru na hata unayempa hiyo connection atakushukuru.

Kijana ukimpa kazi anadhani uliipata kirahisi. Hiyo ndio mindset ya Vijana wengi ilivyo.
Kwanza kijana akikuambia umtafutie kazi ukamkubalia Kwa akili yake ameshachora Aina ya kazi na Mshahara ambao anautaka. Hivyo kitendo cha kumuambia umepata kazi roho yake itafurahi lakini utakapomuambia kazi gani na Mshahara wake wengi hunyong'onyea.
Na wengi wanaweza kukubali kishingo upande.
Elewa kuwa wakati huyo kijana unayemtafutia kazi hiyo akinyong'onyea Kwa kutoridhishwa na kazi na Mshahara huo, kuna kijana mwingine ambaye hamna mahusiano ya karibu anayekuambia umpe kazi hiyo na yupo tayari kukupa hata PESA Kwa ajili ya kazi hiyo.
Wewe Kwa vile unampenda nduguyo unaacha pesa unampa kazi alafu baada ya mwezi Kuisha anakuambia au unasikia ameacha kazi.
Hiyo inaitwa Shukrani ya Punda

Hajui anapoacha kazi anavunja uaminifu wako na boss wa hiyo Ofisi au Kampuni.
Yeye hajui na hataki kujua na anahaki ya kufanya hivyo Kwa sababu kila binadamu yupo Kwa ajili yake mwenyewe. Wewe ndio ulikosea kumpa kazi na connection mtu ambaye hanamsaada wowote na wewe. Ni Bora ungemuuzia hiyo kazi ili hata akiacha kazi basi uwe umepata chochote.

Haya unakuta mtu hajasoma lakini anchagua kazi, anataka kazi ya ofisini au Hotelini. Unamuambia hizo kazi zinahitaji vyeti yaani waliosomea, anajisikia vibaya.
Sasa unahitaji kazi nzuri na haujasoma unaakili Kweli?
KAZI nzuri zinahitaji walau elimu ya Diploma au Shahada.

Haya imetokea KAZI ya ofisini au hotelini umeunganishiwa lakini unaambiwa Kwa vile wewe haujasomea hayo mambo na hauna taaluma hiyo utalipwa nusu ya Mshahara wa waliosomea. Ati unajisikia vibaya.
Elimu inaongeza value ya mtu mahali pa kazi.
Hata kama utafanya majukumu yaleyale kama afanyavyo mwenye elimu lakini kamwe hamuwezi kulingana.

Kwa hasira unaacha kazi, unamgharimu aliyekutafutia na kuonekana anaakili za kipuuzi kama zako.

Taikon huwaga nashauri, hakikisha mtu anagharamia Kwa jasho na damu kupata nafasi unayoenda kumpa. Hiyo inajenga nidhamu na heshima ya kazi.
Lakini ukimpa kirahisi rahisi naye atafanya na kuacha kirahisi rahisi.

Hata Mungu ndivyo afanyavyo, hawezi kukupa kitu kirahisi rahisi ili ukidharau na kukiona hakina thamani.

Kijana akikuambia umtafutie kazi labda Kwa vile anakuona upo katika nafasi Fulani au Kampuni Fulani mwambie hakuna nafasi na huna huo muda wa kutafutia watu kazi.
Ila Kama itatokea utamuambia. Ikitokea mwambie akupe pesa kiasi Fulani umuunganishe, kama Hana mwambie huna msaada wowote kwake.
Uza kwingine.

Hivyo ndivyo Dunia ya sasa ilipofikia, na hivyo ndivyo tunapaswa kuishi.
Elewa mambo haya,
Wewe sio mungu wao, na wewe sio Baba Yao uliyewazaa hivyo hakuna popote utakapolaumiwa.

Watu tujifunze kujipigania, tujifunze kupambana wenyewe bila kumtegemea yeyote.

Ogopa watu wanaolialia wakiomba msaada. Ni hatari Sana.
Ogopa watu wenye lawama. Hao ndio hatari zaidi.

Mfano mzuri ni kijana Jackson majaliwa, alijitoa mhanga kuokoa Maisha ya watu wengine kwenye Ndege, sio Taaluma yake kuokoa watu lakini alifanya tuu bila kutegemea chochote, lakini hiyo ndio gharama aliyolipia na anachokipata ni sehemu ya malipo.
Unamtafutia mtu kazi mtu anayelala nyumbani anaangalia Series za kikorea au anayecheza PS unategemea nini?
Ni Bora umpe Bodaboda au anayeuza machungwa ambaye amekuomba.
Hawa vijana wanaochagua kazi ni wakuwakimbia au kuwafanyia biashara tuu

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Kwema Wakuu!

Namna Bora ya ku-deal na vijana wa sasa ambao Asilimia 90% ni Vijana wa hovyo ni kuwa na roho ngumu tuu. Kama unahitaji mahusiano mazuri yenye furaha na vijana hawa na hautaki kuumia basi nakushauri kuwa na roho ngumu.

Kama sio mtoto wako uliyemzaa basi usimpe connection ya kazi, au usimpe mchongo wa pesa. Ni akheri umuuzie hiyo connection.


Kwa sasa Dar es salaam
Utabaki na umaskini wako wa roho mbaya hivyo hivyo
 
👍Nakubali taikon WA fasihi. Tena sisi tuliokulia dar es salaam hayo mambo ya kumpa MTU connection ya kazi yametutokea Sana puani. ( Ila juzi kwenye makala Yako ya Quran na bibilia zikipelekwa mahakamani Quran itashwindwa. NAPINGA %💯)

😀😀😀😀
Lazima ikutokee puani, lazima.
Maana kijana anakuambia umpe kazi nzuri asijue wewe ulianza Kwa Mshahara wa Mbuzi au vibarua.
Sasa akikuona mambo Safi anadhani mambo yako yalianza hivyohivyo
 
Wape vijana Kaz acha hzo ,au wew Ni wale jamaa unachukua hela na Kaz ujatoa nitakuuaa mzee wa fasii

Vijana wanazingua.

Embu assume wewe unakampuni yako, ikatokea nafasi ya kazi Hapo kazini, katika kupiga Stori na Mimi ukanigusia hiyo fursa,
Mimi kusikia hivyo nikamkumbuka ndugu yangu Hana kazi.
Nikakuomba hiyo nafasi umpatie ndugu yangu, ukaniambia lakini KAZI hiyo inahitaji mtu aliyesomea na ndugu yangu hajasomea, nikakusihi Sana.
Kwa vile unaniheshimu ukakubali.
Ukasema aripoti kazini siku Fulani kwaajili ya kuanza kazi.

Ndugu yangu anakuja ofisini anaboronga ikiwezekana anaiba kabisa, au kuacha kazi bila sababu ya maana.

Hivi wewe utanichukuliaje Mimi?
Kumbuka ulikuwa unaniona kama mtu makini na mtu wa maana. Na nilikuhakikishia kuwa ndugu yangu atafanya kazi vizuri
 
Nimeona hii thread nikakumbuka hii

 
Niuzieni connection ya kazi Nina bachelor ya lishe, pia ninauzoefu wa sales and marketing
 
Siri ya mafanikio ni kunyanyua wengine pale unapokuwa na nafasi hiyo. Kuna nguvu tusizozielewa kwenye hii dunia, unapofanya wema somehow somewhere wema unakurudia. Wema ni mtaji usioonekana.

Msaada unakanuni zake.
Sio kila mtu ni wakusaidiwa, kasome vizuri maandiko au visa vya wahenga.

Kuna watu ukiwasaidia amini amini nakuambia umejitia kitanzi mwenyewe.
Ni kumuomba Mungu macho akuonyeshe
 
Kuna kijana niliona kaandika uzi anataka kuacha kazi aliyotafutiwa kisa ni haendani nayo, nikasema huyu atakua kula kulala maana angekaza huku anafanya hiyo kazi kwa bidii na juhudi na kujituma sana huku akiwa mwaminifu, palepale angekua promoted mapema au wakati huo anakua anatafuta kazi nyingine sehemu nyingine na hata akiondoka pale anaaga kwa amani kwa kueleza nawashukuru naona nikajaribu maisha mengine nipate uzoefu mwingine, kijana anataka aajiriwe mwezi mmoja atembelee subaru hiyo haipo
 
Kuna kijana niliona kaandika uzi anataka kuacha kazi aliyotafutiwa kisa ni haendani nayo, nikasema huyu atakua kula kulala maana angekaza huku anafanya hiyo kazi kwa bidii na juhudi na kujituma sana huku akiwa mwaminifu, palepale angekua promoted mapema au wakati huo anakua anatafuta kazi nyingine sehemu nyingine na hata akiondoka pale anaaga kwa amani kwa kueleza nawashukuru naona nikajaribu maisha mengine nipate uzoefu mwingine, kijana anataka aajiriwe mwezi mmoja atembelee subaru hiyo haipo

Hakuna Kaka ambaye anapenda aone mdogo au ndugu yake anafanya kazi yenye kipato duni.
Kinachofanyika ni kumpa mtu Ile fursa iliyombele yetu ili ajishikize Kwa Muda.
Sasa mtu unampa fursa anaacha alafu baada ya mwezi anakuja kuomba umtafutie kazi nyingine
 
Kwema Wakuu!

Namna Bora ya ku-deal na vijana wa sasa ambao Asilimia 90% ni Vijana wa hovyo ni kuwa na roho ngumu tuu. Kama unahitaji mahusiano mazuri yenye furaha na vijana hawa na hautaki kuumia basi nakushauri kuwa na roho ngumu.
Katika hii Dunia ukitegemea kuwa mtu wa kulipwa kila kitu utajikuta unalipa kila kitu. Tenda wema nenda zako. Mungu ameona wema wako. Yatakayo tokea ni historia. Acha roho mbaya
 
Na kubali Kweli Hakuna Kaz za bure connect inamata na yupi akupe hyo kazi

Iko HV Kuna jmaaa alichukuwa hell zangu akiniahidi kunipa kazi bonite ya area sales manager akanipanga nikapangika ajabu hela kala Hakuna pesa nikaona huyu anannichezeaa nikamtokeaa asbh sna analeta ujinga nikamtokeaa usku Tena akaleta ujinga nikaona huyo anannichezeaa siku mojaa nikamuibukiaa usku nikamuambia leo tutalal na mkeo na na Kama hell zipati Basi tutagawwna majengo ya serekali mbna walipa changu
 
Mtoa mada uko sahihi. Kwa upande wangu ni bora uniuzie kazi hata mil 2... Kuliko unipe mchongo wa kazi kwa kunisaidia zen uanze kunipiga mizinga isoisha miaka na miaka. Yaani kila changamoto ukipata unaleta kwangu kisa ulinipa kazi, so ni bora uniuzie kazi tumalizane kabisa, libaki suala la unirani/udugu mwema.

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom