Wazalendo halis
Member
- Oct 30, 2009
- 13
- 0
Tanzania ni Nchi na sio NGO
Kamati ya bunge ya kuchunguza kampuni ya kufua umeme, Richmond, ilitumia kiasi cha shillingi za Tanzania zisizopungua millioni 400.
Vyanzo vya uhakika kutoka hazina vimethibitisha kuwa, kiasi hicho kikubwa cha pesa za wakipa kodi zilitumika kwa kusudi la kuwezesha uchunguzi makini na kamilifu ili haki iweze kutendeka.
Baadhi ya maofisa wa serikali wamesema wanashangazwa sana na habari kuwa, baada ya kutumia pesa hizo zote, kamati hiyo ilishindwa kukabidhi vithibitisho kamili kwa wakati mmoja na badala yake, wanasema leo kuwa walificha vielelezo ambavyo wameanza kutoa katika vyombo vya habari.
Wataalamu wanasema, hatua hii ni kinyume cha sheria kwa sababu vithibitisho vyote ni mali ya bunge iliyoagiza uchunguzi huo, na kwa wanakamati kutokabidhi nyaraka zote ni ishara kuwa walishindwa kukamilisha kazi waliopewa.
Pia, hatua hizi zinaonyesha kuwa, wanakamati walikuwa na agenda binafsi kwa kuchagua kipi cha kuorodhesha na kipi cha kuficha.
"Duniani sehemu zote, ukikabidhiwa kazi ya uchunguzi wowote na kilipwa kwa kazi hiyo, unatakiwa kukabidhi yote uliyoyathibitisha. Kushikilia vielelezo kadhaa ili uje kuyatoa kwa sababu zako binafsi ni kosa kubwa na kamwe haiwezi kuhalalishwa kwa kigezo cha maslahi ya umma," alieleza mtaalamu na kuongeza kuwa, kama maslahi ya umma yangezingatiwa, basi ripoti kamili ingetolewa wakati huwo wa kuwasilisha ili maamuzi kamili yachukuliwe.
Malumbano ambayo hayana tija kuhusu suala la Richmond na ambayo yanaendelea kupoteza wakati na akili za watanzania leo yamekithiri katika vyombo vya habari. Wakati nchi inaelekea uchaguzi, badala ya kuweka kipaumbele kuzungumzia habari zinazowasumbua wananchi kama huduma za elimu, afya n.k, vyombo vya habari vinaendeleza poroja za wanakamati wa Richmond.
Wanakamati hao wanatakiwa kushtakiwa kwa kushindwa kukabidhi vielelezo vyote vya uchunguzi walioufanya kwa pesa za wananchi. Kwanza, hawakuwatendea haki wananchi kwa kutumia hela hizo zote na kutokamilisha ripoti yao. Pia, eti walishikilia vielelezo hivyo ili waje watoe baadae. Je sababu ni nini? Ili kuwasaidia kisiasa? Hapo hawajawatendea haki wananchi.
Pia, kuzitoa habari walizopata kwa kutumia pesa za umma kwa vyombo binanfsi vya habari ni kosa la jinai.
Wasomi wanasema milioni hizo 400 zingeweza kununua genereta na wananchi wasingeendelea kuwa gizani leo. Kwa uzembe wa kamati hiyo, wananchi wako gizani kwa kutokuwa na umeme leo, na pia wako gizani kwa kutojua ukweli kamili wa waliyojia katika ufatiliaje kamili wa Richmond.
Kamati ya bunge ya kuchunguza kampuni ya kufua umeme, Richmond, ilitumia kiasi cha shillingi za Tanzania zisizopungua millioni 400.
Vyanzo vya uhakika kutoka hazina vimethibitisha kuwa, kiasi hicho kikubwa cha pesa za wakipa kodi zilitumika kwa kusudi la kuwezesha uchunguzi makini na kamilifu ili haki iweze kutendeka.
Baadhi ya maofisa wa serikali wamesema wanashangazwa sana na habari kuwa, baada ya kutumia pesa hizo zote, kamati hiyo ilishindwa kukabidhi vithibitisho kamili kwa wakati mmoja na badala yake, wanasema leo kuwa walificha vielelezo ambavyo wameanza kutoa katika vyombo vya habari.
Wataalamu wanasema, hatua hii ni kinyume cha sheria kwa sababu vithibitisho vyote ni mali ya bunge iliyoagiza uchunguzi huo, na kwa wanakamati kutokabidhi nyaraka zote ni ishara kuwa walishindwa kukamilisha kazi waliopewa.
Pia, hatua hizi zinaonyesha kuwa, wanakamati walikuwa na agenda binafsi kwa kuchagua kipi cha kuorodhesha na kipi cha kuficha.
"Duniani sehemu zote, ukikabidhiwa kazi ya uchunguzi wowote na kilipwa kwa kazi hiyo, unatakiwa kukabidhi yote uliyoyathibitisha. Kushikilia vielelezo kadhaa ili uje kuyatoa kwa sababu zako binafsi ni kosa kubwa na kamwe haiwezi kuhalalishwa kwa kigezo cha maslahi ya umma," alieleza mtaalamu na kuongeza kuwa, kama maslahi ya umma yangezingatiwa, basi ripoti kamili ingetolewa wakati huwo wa kuwasilisha ili maamuzi kamili yachukuliwe.
Malumbano ambayo hayana tija kuhusu suala la Richmond na ambayo yanaendelea kupoteza wakati na akili za watanzania leo yamekithiri katika vyombo vya habari. Wakati nchi inaelekea uchaguzi, badala ya kuweka kipaumbele kuzungumzia habari zinazowasumbua wananchi kama huduma za elimu, afya n.k, vyombo vya habari vinaendeleza poroja za wanakamati wa Richmond.
Wanakamati hao wanatakiwa kushtakiwa kwa kushindwa kukabidhi vielelezo vyote vya uchunguzi walioufanya kwa pesa za wananchi. Kwanza, hawakuwatendea haki wananchi kwa kutumia hela hizo zote na kutokamilisha ripoti yao. Pia, eti walishikilia vielelezo hivyo ili waje watoe baadae. Je sababu ni nini? Ili kuwasaidia kisiasa? Hapo hawajawatendea haki wananchi.
Pia, kuzitoa habari walizopata kwa kutumia pesa za umma kwa vyombo binanfsi vya habari ni kosa la jinai.
Wasomi wanasema milioni hizo 400 zingeweza kununua genereta na wananchi wasingeendelea kuwa gizani leo. Kwa uzembe wa kamati hiyo, wananchi wako gizani kwa kutokuwa na umeme leo, na pia wako gizani kwa kutojua ukweli kamili wa waliyojia katika ufatiliaje kamili wa Richmond.