Kamati Teule ya Richmond ilitumia sh 400 milioni?!!

Teh teh teh!! Mafisadi bwana. We do not compromise with you fisadiz.

Kwa vyovyote vile, kuleta kioja kama hicho ili tujadili ni kutudhalilisha kiaina. Msomi kama Kitila ndugu yangu vipi tena umenasa kirahisi namna hii.

Nyie mafisadi tunao tu mpaka tuone mwisho wake.
 
Nawapongeza wana JF wenzangu wengi ambao mmegundua hila na udanganyifu wa mafisadi... msikubali kupotoshwa kwa mada .... si tunasubiri mjadala wa Richmond, hili la Mwakyembe na posho zake tumekiweka kiporo..... hehehe....
 
Hahahaaa, Shalom.
Habari za siku Mkuu? Nilifikiri mama Kubwa kakuzua kuingia JF maana ulikuwa umeadimika kama Makalio ya Nyoka haahaha!! Mnyakyusa wangu.

Hii vita niko upande wa Mkwanyembe na wa TAKURURU. Hatimaye UFISADI utaanza kupigwa vita kwa nguvu zote. SI unasikia Sendeka anasema "na yeye atafichua siri?" Mwakyembe alisema "na yeye atamwaga mtama ..." Sasa maadamu wamebanwa kama mjusi kwenye Mlango, itabidi waseme yote. Vinginevyo wangeliendelea kupeta.

Shalom hata wewe nafahamu ndani ya Moyo unaamini kabisa kuwa "Mwakyembe si smart....." Mbona Dr. Slaa alishawashtukia CCM na kuwaasa wabunge wake wasipokee posho mara mbili? Yeye Mwakyembe na usomi wake wote huo alikuwa anakomba hadi posho ya Malazi, na tena kutoka TAKURURU na wakati huo mkutano umefanyika DAR na yeye kwake Kunduchi? Yeye anapokea tu kumbe wenzake wanamuingiza Mkenge..... Hapa lazima ukiri kuwa Ngosha Hosea kichwa kipo na ndugu yenu Mwakyembe ana vi-element vya Lowassa.

Anyway, acha WAPIGANE wenyewe kwa wenyewe na sisi PANZI tufaidike.

Msimamo wangu: Mie Nampinga Mwanzilishi thread kwa kesi ya 400mls Tsh. Ni hela ndogo kwa mafanikio yale.

Sikonge

Mimi mbona nipo tu niende wapi na mimi nalelewa tu na lijimama la kizungu? Sema tu nillikuwa natumia name yangu nyingine ya Masanilo.

Mimi naamini kuwa Mwakyembe ni smart vimtegovya posho haviwezi kumfanya asiwe smart, wewe subiri waendelee na huo ujinga wao wa posho wataumbuka siku si nyingi. Jamaa ni smart to msijipe moyo mwambie mwakalinga akaze boot na awaambie sponsor waongeze fungu hasa kuweza kujibu tuhuma za SUA, kuiba mtihani ni criminal offence
 
Jamani tunatakiwa kuwa makini sana na hawa mafisadi mana kila wakati wakipata muda wanatafuta jinsi ya kutuharibia watanzania.sijaona tatizo kubwa kwa kiasi cha fedha kilichotumiwa na kamati.ikumbukwe hii kamati imetusaidia sana maana wengine tusingejua kama hao richmond walikuwa wakilipwa haya mamilion ya sh kwa siku jamani.mi naomba niipongeze hii kamati kwa ujasiri ingawa kuna kitu walituficha.
 
Sikonge

Mimi mbona nipo tu niende wapi na mimi nalelewa tu na lijimama la kizungu? Sema tu nillikuwa natumia name yangu nyingine ya Masanilo.

Mimi naamini kuwa Mwakyembe ni smart vimtegovya posho haviwezi kumfanya asiwe smart, wewe subiri waendelee na huo ujinga wao wa posho wataumbuka siku si nyingi. Jamaa ni smart to msijipe moyo mwambie mwakalinga akaze boot na awaambie sponsor waongeze fungu hasa kuweza kujibu tuhuma za SUA, kuiba mtihani ni criminal offence

Watu wanashau jamaa amebobea kwenye sheria....

·1999 2002 University of Dar es Salaam Head of Department - Constitutional Admin.
·Law 1998 2005 University of Dar es Salaam Senior Lecturer in Law
·1997 1999 University of Dar es Salaam Head of Department - International Law
·1996 2005 UHURU Publications UPL Managing Director
·1992 1995 PhD Student at University of Hamburg (Law)
·1991 1997 University of Dar es Salaam Lecturer in Law
·1990 1991 Postgraduate Student - LLM Law - University of Hamburg
·1986 1991 University of Dar es Salaam Assistant Lecturer in Law
·1984 1986 University of Dar es Salaam Tutorial Assistant in Law
·1984 1986 University of Dar es Salaam Postgraduate Student - LLM Law
·1980 1983 University of Dar es Salaam Undergraduate Student - LLB Law
Hata kama anamapungufu yake lakini sifa zake tumpe!

Masanilo aka Shalom
 
- Shillingi Millioni 400, the results Waziri Mkuu amejiuzulu, mawaziri wawili wametoka naye, malipo ya dola 154,000 kwa mwezi kwa Richimonduli yakasimamishwa, Rostam akaanza kuuza makampuni yake ya kifisadi na kujificha ficha, kwa mara ya kwanza taifa zima tukagundua kuwa kumbe tuna kundi la Mafisadi, na wao officially na kwa mara ya kwanza wakaanza ku-operate wazi wazi bila kujificha na wote sasa tunawajua, Ika m-cost Lowassa umakamu wa CCM, na kumkosesha kabisa kiu yake ya urais, eti it was not worthy?

- Mnasema ilikuwa sawa Shillingi Millioni 100 kutumika na kesi ya Malima VS Mengi? Kamati ya kurekebisha Muungano ilitumia hela ngapi na matokeo ni nini? Kamati ya kina Mwema ilitumia hela ngapi na matokeo yalikuwa ni nini? Kamati ya Bomani ilitumia ngapi na matokeo yalikuwa ni nini hasa? Kamati ya Warioba ilitumia hela ngapi na matokeo yako wapi jamani?

- Tunazidi kuliua taifa tunapojaribu kuingiza siasa kwenye kila ishu hata zisizohusika, sasa mnasema nini bila ya kutumia hizo Shillingi Millioni 400, tungeishia kuwalipa hela ngapi hawa kina Lowassa, Rostam na Richimonduli? Hawa mafisadi sasa wanatapa tapa baada ya NEC na Sitta, walifikiri nini kwamba wana nguvu sana kwa sababu wana hela zetu walizotuibia?

- Hivi ni lini tutaambiwa hasa madhambi ya kweli ya Mwakyembe kiuongozi na kisiasa badala ya hizi ngonjera zisizokwisha na batili? Mbona hawakupata tabu kummaliza Mtikila, ushahidi ulikuwa wazi na mweupe, sasa Mwakyembe mbona anawasumbua sana na ushahidi wa kweli kuhusu madhambi yake?

Respect.

FMEs!

FMEs, I respect u.
Kuna mambo yamefunuliwa katka ufahamu wa Watanzania baada ya report ya Mwakyembe na ninauhakika hata wanaobeza wanajua hilo,si rahisi kwa kila Mtanzania kujua/kuwa alijua jinsi ufisadi ulivyokuwa unaitafuna hii nchi.
Nimejaribu kuangalia yafuatayo kuonyesha ninini kilifanyika katika fikra za Watanzania kwa wengi wao.
  1. Ufahamu wa watanzania umefunguka sana baada ya report ya Mwakyembe kuhusu mikataba mbalimbali iliyoingia nchi yetu.
  2. Tumejua kuwatafsiri watu wanaoiyumbisha hii nchi kwa kiwango kikubwa
  3. Tumejua viongozi bora na wapambe kupitia/baada ya report ya Mwakyembe
  4. Uchambuzi/mijadala ihusuyo maslahi ya nchi imekuwa na mwonekano wa kueleweka hakuna kudanganyana tena
  5. Taasisi za serikali mfano TAKUKURU zimesomeka vyema kiutendaji nadhani hata wao wanajua kuwa Watanzania sasa sio majuha.
  6. Viongozi wanapotoa taarifa/kuhutubia wamekuwa makini wakijua kuwa watanzania wanajua mambo mengi kuliko siri walizonazo
  7. Tunajua Viongozi wajao 2010 ni wanamna gani,hatudanganyiki tena.
  8. Tunajua mambo mazuri yana gharama,bora kupata ufahamu wa kujua nini kinatakiwa kifanywe kwa ghrama kubwa kuliko kuibiwa mabilioni hata ufahamu sina,nani alijua 152m inaondoka kila siku? ni wachache walijua.Sasa tunajua,mmekamatwa pabaya.
  9. Tumejua hata hao walitafiti ufisadi yamkini nao wana madhaifu yao,kama hizo posho nk,wajisafishe.
  10. Tumejua,Jamii forum ingekuwa ni gazeti lakila siku,wengi wangefunuliwa fahamu zao lakini si wengi wanapata taarifa hizi,Tuseme hivi,Kilichofanyika na Kamati ya Mwakyembe Kimetusaidia sana.
Ndaga.
 
Sikonge

Mimi mbona nipo tu niende wapi na mimi nalelewa tu na lijimama la kizungu? Sema tu nillikuwa natumia name yangu nyingine ya Masanilo.

Mimi naamini kuwa Mwakyembe ni smart vimtegovya posho haviwezi kumfanya asiwe smart, wewe subiri waendelee na huo ujinga wao wa posho wataumbuka siku si nyingi. Jamaa ni smart to msijipe moyo mwambie mwakalinga akaze boot na awaambie sponsor waongeze fungu hasa kuweza kujibu tuhuma za SUA, kuiba mtihani ni criminal offence

Mkuu,

Naona unanichanganya na Engineer. Masanilo kwa taarifa yako nawasiliana naye moja kwa moja. Yaani tukipata muda tunatwangiana simu nyumbani. Sasa ukisema wewe ni Masanilo, huoni aibu? Yaani unanidanganya waziwazi Mkuu? Lete nyingine mkuu. Hata Mhandisi nilimwambia kuwa Masanilo yuko Mwanza akijiandaa kugombea Ubunge. Wewe si uko Texas kwa mama wa Kizungu (Somehow mie ni Mpinzani wa neno Mzungu. Sasa utachukia watu wakimwambia mkeo "your nigger husband").

Kurudi kwa Mwakyembe, mkuu mie yote sawa. Kama inabidi Mwakyembe abanwe ndiyo aropoke basi let it be. Hawa wabunge wakiishi kwa kuoneana haya na aibu sisi ndiyo twaumia. Sasa hivi Mwakyembe kama si Mwakalinga, si ajabu hasa huo Mzunguko aliufanya mwaka huu usingelifanyika. Wee mwenyewe wafahamu kuwa "wa mbili, havai moja". Mshindano wa Wabunge ni faraja ya Wananchi.

Kama Mwakalinga ataingia hapo na yeye aanze kuwa FISADI, basi itabidi niwe kama FMes vs Waziri Masha.

Sawa Mkuu kama kazi zinakuwa nyingi na unapotea, huna haja ya kusema wee ni Masanilo. Cha muhimu kwanza kuchunga familia kama imepata kikombe cha chai na ndipo jioni unakaa na kuchangia mawazo yako JF. Ukikwama basi hakijaharibika kitu. Tufike sehemu tupunguze viutani na viushabiki na tuangalie Mwananchi wa kawaida anafaidika au anaumizwa.

Bado tuna muda sana. Mwakani kikishapigwa kipenga, tutukanane saana sana. Tuulizane vyeti na sisi tutauliza mabaya ya Mwakyembe. Uchaguzi ukiisha, basi tushikane mikono na tuseme "Mshindi ni mwananchi wa Tanzania". Ila mkianza mapema, basi na sisi tunaanza na hapo ndiyo yanaanza maneno yasiyo na miguu wala kichwa. Hebu angalia kama hizi kesi:

1. Matokeo ya Mwakalinga SUA, wakati sasa Mwakalinga ana Masters ya Computer Science na MBA, yanasaidia nini Watanzania?

2. Shalom anatunzwa na limama la Kizungu, si UPUUZI wa hali ya juu. Hata kama anatunzwa na Sokwe mtu, si yeye? Sisi haituhusu.

3. Kumteka kijana Daniel Mwakalinga, si ujinga? Hii ilileta maendeleo gani kwa Wanyakyusa? .......... nk nk

Ukichunguza sana sana wakati mwingine tunayojadili, utaona kweli Nyani yuko sawa kabisa na maneno ya FMes nayo yako sawa kabisa kuwa "Viongozi wetu ni reflection yetu wenyewe".

Namalizia kwa kusema "Ushabiki usio na kichwa wala miguu, nitaanza kuukimbia". Ila kama ni JOKE, hapo nitakaa maana si JOKE? Na kama ntaandika upuuzi basi mwisho ntaandika kitu chochote kiashiriachi kuwa ni JOKE.
 
Milioni 400 kwa kazi waliyoifanya akina mwakyembe si nyingi sana ukulinganisha na shs milioni 152 walizokuwa wanakula Richmond bila kufanya kazi yoyote. Kumbuka bw Hosea alishabariki kuwa Richmond ni safi hivyo bila kuingia gharama kama hiyo ya milion 400 basi mpaka sasa tumgekuwa bado tunatoa milioni 152 kwa siku kwa hao mafisadi wa Richmond.

Mimi tatizo langu na Mwakyembe ni ile kukiri kuwa walificha baadhi ya mambo waliyoyagundua ili government isianguke! Hawakutumwa na bunge kuleta habari nusu nusu. Sababu ya kuficha mambo ndio maana mpaka leo Richmond bado ni kitendawili.
 
Tanzania ni Nchi na sio NGO

Kamati ya bunge ya kuchunguza kampuni ya kufua umeme, Richmond, ilitumia kiasi cha shillingi za Tanzania zisizopungua millioni 400.

Vyanzo vya uhakika kutoka hazina vimethibitisha kuwa, kiasi hicho kikubwa cha pesa za wakipa kodi zilitumika kwa kusudi la kuwezesha uchunguzi makini na kamilifu ili haki iweze kutendeka.

Baadhi ya maofisa wa serikali wamesema wanashangazwa sana na habari kuwa, baada ya kutumia pesa hizo zote, kamati hiyo ilishindwa kukabidhi vithibitisho kamili kwa wakati mmoja na badala yake, wanasema leo kuwa walificha vielelezo ambavyo wameanza kutoa katika vyombo vya habari.

Wataalamu wanasema, hatua hii ni kinyume cha sheria kwa sababu vithibitisho vyote ni mali ya bunge iliyoagiza uchunguzi huo, na kwa wanakamati kutokabidhi nyaraka zote ni ishara kuwa walishindwa kukamilisha kazi waliopewa.

Pia, hatua hizi zinaonyesha kuwa, wanakamati walikuwa na agenda binafsi kwa kuchagua kipi cha kuorodhesha na kipi cha kuficha.

"Duniani sehemu zote, ukikabidhiwa kazi ya uchunguzi wowote na kilipwa kwa kazi hiyo, unatakiwa kukabidhi yote uliyoyathibitisha. Kushikilia vielelezo kadhaa ili uje kuyatoa kwa sababu zako binafsi ni kosa kubwa na kamwe haiwezi kuhalalishwa kwa kigezo cha maslahi ya umma," alieleza mtaalamu na kuongeza kuwa, kama maslahi ya umma yangezingatiwa, basi ripoti kamili ingetolewa wakati huwo wa kuwasilisha ili maamuzi kamili yachukuliwe.

Malumbano ambayo hayana tija kuhusu suala la Richmond na ambayo yanaendelea kupoteza wakati na akili za watanzania leo yamekithiri katika vyombo vya habari. Wakati nchi inaelekea uchaguzi, badala ya kuweka kipaumbele kuzungumzia habari zinazowasumbua wananchi kama huduma za elimu, afya n.k, vyombo vya habari vinaendeleza poroja za wanakamati wa Richmond.

Wanakamati hao wanatakiwa kushtakiwa kwa kushindwa kukabidhi vielelezo vyote vya uchunguzi walioufanya kwa pesa za wananchi. Kwanza, hawakuwatendea haki wananchi kwa kutumia hela hizo zote na kutokamilisha ripoti yao. Pia, eti walishikilia vielelezo hivyo ili waje watoe baadae. Je sababu ni nini? Ili kuwasaidia kisiasa? Hapo hawajawatendea haki wananchi.

Pia, kuzitoa habari walizopata kwa kutumia pesa za umma kwa vyombo binanfsi vya habari ni kosa la jinai.

Wasomi wanasema milioni hizo 400 zingeweza kununua genereta na wananchi wasingeendelea kuwa gizani leo. Kwa uzembe wa kamati hiyo, wananchi wako gizani kwa kutokuwa na umeme leo, na pia wako gizani kwa kutojua ukweli kamili wa waliyojia katika ufatiliaje kamili wa Richmond.

Uchunguzi ni kazi endelevu with a series of reports kutegemena na swala linalochunguzwa...
 
400M kumwangusha kinara wa mafisadi mie naona inalipa.hayo ni malipo ya siku tatu aliyokuwa anapata richmond/dowarns kwenye mkataba wake wa kifisadi. kilichobaki serikali ijibu mapendekezo ya tume maana tumechoka na subirisubiri.
 
Maadam fedha hizo zimekuwa accounted for hakuna tatizo..Tujifunze kuelewa thamani ya mali au kazi na sio thamani ya fedha.
 
Mbona watu hamkumbushi kuwa ugomvi wa Mengi na Manji zilitumika 100 milioni wakati kamati ilikaa hapahapa nchini?
 
Tanzania ni Nchi na sio NGO

Kamati ya bunge ya kuchunguza kampuni ya kufua umeme, Richmond, ilitumia kiasi cha shillingi za Tanzania zisizopungua millioni 400.

Vyanzo vya uhakika kutoka hazina vimethibitisha kuwa, kiasi hicho kikubwa cha pesa za wakipa kodi zilitumika kwa kusudi la kuwezesha uchunguzi makini na kamilifu ili haki iweze kutendeka.

Baadhi ya maofisa wa serikali wamesema wanashangazwa sana na habari kuwa, baada ya kutumia pesa hizo zote, kamati hiyo ilishindwa kukabidhi vithibitisho kamili kwa wakati mmoja na badala yake, wanasema leo kuwa walificha vielelezo ambavyo wameanza kutoa katika vyombo vya habari.

Wataalamu wanasema, hatua hii ni kinyume cha sheria kwa sababu vithibitisho vyote ni mali ya bunge iliyoagiza uchunguzi huo, na kwa wanakamati kutokabidhi nyaraka zote ni ishara kuwa walishindwa kukamilisha kazi waliopewa.

Pia, hatua hizi zinaonyesha kuwa, wanakamati walikuwa na agenda binafsi kwa kuchagua kipi cha kuorodhesha na kipi cha kuficha.

"Duniani sehemu zote, ukikabidhiwa kazi ya uchunguzi wowote na kilipwa kwa kazi hiyo, unatakiwa kukabidhi yote uliyoyathibitisha. Kushikilia vielelezo kadhaa ili uje kuyatoa kwa sababu zako binafsi ni kosa kubwa na kamwe haiwezi kuhalalishwa kwa kigezo cha maslahi ya umma," alieleza mtaalamu na kuongeza kuwa, kama maslahi ya umma yangezingatiwa, basi ripoti kamili ingetolewa wakati huwo wa kuwasilisha ili maamuzi kamili yachukuliwe.

Malumbano ambayo hayana tija kuhusu suala la Richmond na ambayo yanaendelea kupoteza wakati na akili za watanzania leo yamekithiri katika vyombo vya habari. Wakati nchi inaelekea uchaguzi, badala ya kuweka kipaumbele kuzungumzia habari zinazowasumbua wananchi kama huduma za elimu, afya n.k, vyombo vya habari vinaendeleza poroja za wanakamati wa Richmond.

Wanakamati hao wanatakiwa kushtakiwa kwa kushindwa kukabidhi vielelezo vyote vya uchunguzi walioufanya kwa pesa za wananchi. Kwanza, hawakuwatendea haki wananchi kwa kutumia hela hizo zote na kutokamilisha ripoti yao. Pia, eti walishikilia vielelezo hivyo ili waje watoe baadae. Je sababu ni nini? Ili kuwasaidia kisiasa? Hapo hawajawatendea haki wananchi.

Pia, kuzitoa habari walizopata kwa kutumia pesa za umma kwa vyombo binanfsi vya habari ni kosa la jinai.

Wasomi wanasema milioni hizo 400 zingeweza kununua genereta na wananchi wasingeendelea kuwa gizani leo. Kwa uzembe wa kamati hiyo, wananchi wako gizani kwa kutokuwa na umeme leo, na pia wako gizani kwa kutojua ukweli kamili wa waliyojia katika ufatiliaje kamili wa Richmond.
'
NA HAKUNA KILICHOFANYIKA. MTUHUMIWA AKAGOMBEA URAIS, MPAKA SASA HATUJUWI NANI ALIWAIBIA WATANZANIA KATI YA HAWA MARAFIKI WAWILI. JUU YAKE MILLION 400 ZIKAYEYUKA. WANASIASA WANAJUWA KUCHEZA NA HAKIRI ZETU. NA ALIYE MADARAKANI AMEAHIDI ATAWAPROTECT KUTUMIA VYOMBO VYETU VYA USALAMA, HUU UMEKUWA NI MUCHEZO WA KAMALI. DEMOCRACY WILL NEVER WORK WHEN THE PEOPLE ARE SO POOR. OUR VOTES COULD BE EASILY BOUGHT FOR A LOF OF BREAD. TOO POOR TO PROTEST.
 
Back
Top Bottom