Huihui2
JF-Expert Member
- Jan 5, 2012
- 5,277
- 7,996
Wakati wa mjadala mkali wa kashfa ya Richmond bungeni, huku tume iliyochunguza kashfa hiyo ikibanwa kuwa haikutoa nafasi kwa watuhumiwa hasa Lowassa kujitetea, aliibuka mwenyekiti wa tume ile Mwakyembe na kusema kuwa kama watu hawaridhiki waombe kanuni zitenguliwe ili aweze kuwasilisha upya ripoti yake ili aweze kusema hata siri waliyoificha ili kuikoa serikali isiporomoke yote.
Kwa maneno hayo mimi nilliewa kuwa kumbe tume ile iliwasilisha ukweli nusu na hivyo kumtoa kafara Lowassa na mawaziri wawili ili kumwokoa rais ambaye kwa maneno ya Mwakyembe kama wangeyasema yote, ingesababisha serikali yote kuporomoka.
Kwa ufupi nilivyoelewa ni kuwa taarifa ile ilikuwa inamgusa Rais moja kwa moja na kwa maana hiyo alipaswa kuondolewa madarakani lakini akaokolewa na tume kwa kuficha siri.
Hivyo kilichofanyika ilikuwa ni kukivunja kichwa (Lowassa) kwa kosa lililofanywa na ulimi (rais). Na ndio maana katika kikao kimojawapo cha chama Lowassa alimuhoji mwenyekiti kuwa ni jambo gani ambalo yeye aililifanya ambalo yeye hakujua au kumtuma?
Ni wazi Harrison Mwakyembe alitumika na Spika Sitta kumuumiza Lowassa kwa vile Sitta na Lowassa wote walikuwa wanautaka u PM kama build up ya U-Rais wa 2015
Kwa maneno hayo mimi nilliewa kuwa kumbe tume ile iliwasilisha ukweli nusu na hivyo kumtoa kafara Lowassa na mawaziri wawili ili kumwokoa rais ambaye kwa maneno ya Mwakyembe kama wangeyasema yote, ingesababisha serikali yote kuporomoka.
Kwa ufupi nilivyoelewa ni kuwa taarifa ile ilikuwa inamgusa Rais moja kwa moja na kwa maana hiyo alipaswa kuondolewa madarakani lakini akaokolewa na tume kwa kuficha siri.
Hivyo kilichofanyika ilikuwa ni kukivunja kichwa (Lowassa) kwa kosa lililofanywa na ulimi (rais). Na ndio maana katika kikao kimojawapo cha chama Lowassa alimuhoji mwenyekiti kuwa ni jambo gani ambalo yeye aililifanya ambalo yeye hakujua au kumtuma?
Ni wazi Harrison Mwakyembe alitumika na Spika Sitta kumuumiza Lowassa kwa vile Sitta na Lowassa wote walikuwa wanautaka u PM kama build up ya U-Rais wa 2015