Kama unasumbuliwa na panya pitia hapa

Kama unasumbuliwa na panya pitia hapa

Mkuu katika wanyama wabishi na wenye akili paka hawezi kukosa, paka ni mjanja sana unaweza ukamtegea sumu lakini ataenda atainusa na kuiacha kama ulivyoweka watu wanasema paka ana tabia ya kunusa ndipo uanza kula na iwapo utatega sumu basi utakuta kama ulivyoweka
Ila mkuu hapa hoja iliyopo ni kuua panya na siyo kuua paka.
 
Hiyo Indocid ndugu utawapata wawili au watatu wa mwanzo tu, wakishajua umewatega hawalii! Ukitaka kuwakomoa vizuri wewe mwaga Ugoro tu kwenye njia yao au hata Nyoka kama wanakutembelea sana. Mwaga Ugoro tu uone kimbembe chake, panya, nyoka hawana Chafya.
 
Hivi kwa mtu asiye na mapenzi na paka na asiyehitaji kuongeza bajeti ya kumhudumia paka huyo kwa nini aangaike na kumfuga wakati kunapotokea uhitaji wa kuwaua panya anatumia gharama ndogo tu kununua dawa kama hizo indocin, piriton na valium?
Hiyo ya kuwategea dawa/sumu ni zoezi la kudumu pia, kila baada ya muda fulani utalazimika kutega tena.

Lakini pia panya sio wajinga kihivyo, ni wepesi sana kujifunza, baada ya muda utakua unatega sumu yako lakini wao hawagusi mtego wako.

Fuga paka, mnyama rafiki wa binadamu, atakula kile mtakacho kula nyumbani.
 
Labda mapanya ya Dar yaliyozoea kula kitimoto na mapaka kwenye bar.

Yale majanja hayalagi nyama zilizotegwa. Yatafanya kila yawezalo hata ikibidi kufungua friji na kula vilivyomo.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my Infinix X5515 using JamiiForums mobile app
 
Last week nimewekea panya sumu. Naamka asubuhi si dada wankazi kafungulia kuku. Nikakuta panya na kuku wawili wa kienyeji wamekwenda na maji....
Panya shenzi kabsa....
Usirudie huo mchezo mkuu.

Ukiweka dawa ya panya hom usifanye siri watangazie kila mtu ajue na uweke wewe mwenyewe na uwahi kuamka asubuhi kutoa mabaki wewe mwenyewe.

Kumbuka hiyo ni sumu. Siku ingine utawamaliza binadam wenzio.
 
Mimi alikaa kwenye sofa, anatoka usiku mchana anakausha unamsikia anavyohangaika.

Muda ukaenda akatanuka nakuongezeka size..... Kunasiku anatembea kwenye sofa namsikia anavyojipenyeza..... Aiseee nilipiga ngumi, vipepsi na mateke lile eneo alipo hadi akaanza kupiga ukunga....

Aisee nilitandika ngumi za maana hadi akatulia baada ya siku mbili nikaanza kusikia harufu ya mzoga nikajua tayari....
[emoji3]
 
Panya ni kero sana, wamekata nyanya za music system nina hasira nao, Leo inabidi ninunue piriton halafu mchana sisikii kabisa movement za panya.
 
Kuna vile visumu vinauzwa barabarani vina pakti la rangi ya kijani, kimoja buku

Njoo home kata nyanya vipande vinne nyunyizia halafu vipange kila pembe, siku hiyo utasikia kitu kinajirusha na kujipigiza chini[emoji1787][emoji28]Mi nimemuua mmoja mkubwa huyo last month

NB hakikisha hizo procedure unavyozifanya hakuoni, akikuona hali ng'oo
[emoji33]

Seriously! Kwamba akikuona unaandaa anajua unataka kumuuwa?
 
Hiyo Indocid ndugu utawapata wawili au watatu wa mwanzo tu, wakishajua umewatega hawalii! Ukitaka kuwakomoa vizuri wewe mwaga Ugoro tu kwenye njia yao au hata Nyoka kama wanakutembelea sana. Mwaga Ugoro tu uone kimbembe chake, panya, nyoka hawana Chafya.
[emoji3]
Ugoro unawafanya nini hawa viumbe wasumbufu mkuu?
 
Ahhh aseeh kwenye sabufa yangu pale kweny lile tobo aliingia nikiwa namuona kabisa ilikuwa mchana basi ilikuwa on nikaweka bluetooth nikatafuta nyimbo yenye mdundo wa maana alafu nikaongezaaaa sauti volume hadi mwisho nikapita kinyuma nyuma nikaziba kwa haraka lile tundu na nguo kisha nika play [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nilimchangamsha niliplay nyimbo tano zenye mdungo mkubwa kisha nikatoa tambara alitoka anatembea kama mlevi nikamalizia kuua saafi
 
Je umekuwa ukisumbuliwa na panya sana?

Je umetumia pesa sana kununua sumu za panya bila mafanikio?

Kama jibu ni ndiyo basi soma na ufanye hivi;

Nenda duka la dawa nunua dawa inaitwa INDOCID (indomethacin 25 mg capsules) halafu katege kama unavyotegaga sumu nyingine za unga za panya. Baada ya siku 4-5 matokeo utakayoyapata naamini mwenyewe utaleta mrejesho

Dawa hii hutumiwa na binadamu kama dawa zingine tu ila kwa panya ni sumu kwani wakishakula utaona siku ya nne panya wanakufa na wengine wanashindwa kutembea kwa kusagika sagika mifupa

Kama una jirani yako mshauri naye atumie maana muda mwingine waweza kuta unahangaika kumbe wanahamia kutoka nyumba ya pili

Dawa hii inaepusha gharama kwani pakiti ya buku (tembe 10) unaweza tega mara kadhaa bila kuimaliza pia ni salama kabisa wakati wa kutega kwani siyo sumu kwa binadamu
Nami natumia hii kwa muda sasa, ni komesha ya panya.
 
Ahhh aseeh kwenye sabufa yangu pale kweny lile tobo aliingia nikiwa namuona kabisa ilikuwa mchana basi ilikuwa on nikaweka bluetooth nikatafuta nyimbo yenye mdundo wa maana alafu nikaongezaaaa sauti volume hadi mwisho nikapita kinyuma nyuma nikaziba kwa haraka lile tundu na nguo kisha nika play [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nilimchangamsha niliplay nyimbo tano zenye mdungo mkubwa kisha nikatoa tambara alitoka anatembea kama mlevi nikamalizia kuua saafi

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom