Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 8,848
- 15,253
Hapa Umeeleza vizuri lakini Kiranga atakuambia ulikuwa unaumwa ukaona maruwe ruwesababu ya kiwasha ganja kabla sijalianza pori la ushirombo.
ilikuwa mwezi wa ramadhani mwaka 2013 mida ya saa 11 jion na siku hiyo kulikuwa na mvua ya rasha rasha, nilikuwa naendesha pulling ya kampuni moja ya mafuta na hilo gari sikuwa nimekabithiwa mimi dereva wake alipata udhuru ambaye pia ni mjomba wangu na kwa kuwa yeye ndiye aliyenifundisha gari akachukua chuma akaja nayo mpaka river side akanikabithi gari yeye akaenda kwenye mambo yake, mimi nikashobokea dundo nikaomba dua mdogomdogo, ikumbukwe hata lesen yangu wakati huo haikuwa ikiruhusu nikokote lile gari ni ubishi tu wa kibongo, basi kufika mji mmoja unaitwa masumbwe ile gari ikaanza mapicha picha inachemsha hatari, nikawa nalikokota hivyo hivyo temp ikishuka safar inaendelea, sasa ktk lile pori chuma ikaanza kuchemka tena, nikashuka chini nikawa naisubiria ipoe niwahi runzewe nikafturu nilikuwa nimefunga ila ni zile funga za masela c unajua tena? sasa nimemaliza kujaza maji nikasema ngoja nichungulie feni nikakuta chuma inataka kuanguka, na pale porin nikaona hapa nikijikokota nafika runzewe, naingia ndani ya gari fresh ile chuma inaanza ondoka dah naona mdada anatokea nyuma ya kitanda, nilistuka nusu niruke sasa akili ingine ikanikatalia kufanya hivyo, nikamuuliza we umeingia saa ngapi humu? huku sasa napaki gari pemben akaniambia ukipaki tu hii gar inawaka moto, ****** alafu mle ndani ya gari harufu imebadilika kuna marashi yanakera ndani ya pua zangu, sasa kuna jambo liliniponza mimi dini yetu inasema wakati wa mwez mtukufu viumbe vya ajabu vinafungiwa huyu katoka wapi? katoroka? nikakumbuka nna ganja tena ishanyongwa nilikuwa nasubiri nifungulie niilipue, ikabidi nifuturu bangi nikapandisha vioo ananiangalia tu ananichekea mm jasho linanitoka na vile sikula tangu asubuhi na mwili nauhisi unaisha nguvu akasema we mtoto usiwashe hayo majani mimi nikabana usukani na goti nikawasha alafu nikampulizia ule moshi, hamkuwepo ila nahisi nilikuwa na malaika maana mle katika cabin ulitanda moshi mzito na kelele ambazo sijui mpaka leo niseme ni za mnyama gani, hapo chuma inatembea maana nilihisi giza likiingia niko ma lile dubwana basi ndio kifochangu baada ya ule moshi kutanda mm nilichochora, chuma ikatoka nje ya barabara lakini nashukuru sikuingia kule kwenye ule msitu, wakati gari imesimama mle ndani moshi umejaa kama cabin inaungua, nikashuka nikaacha mlango wangu wazi ule moshi ukawa unatoka hapo natetemeka sasa nikakimbilia barabarani, chuma nimeiacha kule ktk njia ambayo ilikuwa diversion zaman, nimesimama pale kama dakika kumi hakuna gari hata moja kupita, hapo ganja yangu imebak kikucha, nikasema ngoja niende ktk gari nikaangalie yupo? hapo eneo lile lishaanza kuingiwa na ukimya na giza, narudi kule sikumkuta, hali ipo shwari kabisa, nikaizunguka gari kuikagua kama kuna janga lolote nimesababisha hamna, nikapanda nikaihakiki gar yote na nikaridhia niko mwenyewe chuma ikatoka huyoo mpaka runzewe nimeingia pale kama saa moja na robo sasa kilichonifanya niandike hapa ni hiki wakat nimefika runzewe nikapaki jiran ya mzee mmoja anauza kahawa, maana bado nilikuwa na wasiwasi nilitaka niwahadithie lile tukio nijue yule ni jini ama wenge la lile gari kabla sijashuka namuona yule mwanamke upande wa pili anaomba lifti katika gari ya Azam ambayo inarudi kule kule tulipotoka alaf tayar giza limetanda, nilipiga honi nikamwambia kaka usimpakie huyo mwanamke jini huku nashuka basi yule dada hata sijui alipoteaje lakini baada ya mm kuvuka nikamuambia kaka ungempakia yule mwanamke yangekukuta makubwa ananiuliza mwanamke gani? jaman si huyo ulikuwa unaongea nae hapa anakuomba lift? jamaa akasema yeye hajaongea na mtu katoka kula anaondoka zake nikamwambia basi kaka we lala hapa ondoka asubui hapa leo kuna jinni kisirani sio bure, ndio baada ya kuwahadithia wenyeji wakasema nyie mnabahati sana, kuna mwanamke jinn hapo ktk hilo pori, nikauliza lakin mwezi huu wanafungiwa wenyeji wakaishia kucheka tu.