Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,900
Kwema Waheshimiwa!
Kwanza sijajua maandamano haya ni endelevu au ni ya siku moja tuu. Maandamano ya amani ni nini hasa? Huwezi ita maandamano ya amani wakati muda huohuo ni kudai haki Fulani. Hakuna maandamano ya hivyo.
Kudai haki zipo njia nyingi kama kukaa mezani, lakini yakishakuwa maandamano hii inamaanisha njia ya amani yaani ya kukaa mezani imeshindikana.
Maandamano ya Amani mara nyingi huhusu kumpongeza mtu fulani, kusherehekea jambo fulani, kushangilia ushindi fulani nk, lakini kukishakuwa na madai ya haki fulani hayawezi kuwa maandamano ya Amani.
Sio ajabu Màandamano ya Amani yoyote duniani yenye lengo la kudai haki utakuta vyombo vya dola vikiyazuia kwa namna mbalimbali ikiwemo Nguvu.
Watu wanaofanya maandamano ya Amani ya kusherehekea, kupongeza au kushangilia jambo fulani hata uwape Bunduki au mabomu hawawezi kuleta madhara.
Lakini maandamano ya kudai Haki ambayo hayawezi itwa maandamano ya amani huwezi wapa Watu hao bunduki au mabomu kwani kitakachotokea kinajulikana.
Swali ni je, ikiwa maandamano ya Kenya ambayo nayo yaliitwa ya Amani yalishindwa, nini tutegemee kwenye maandamano yetu?
Je, Wapinzani wanataka kupima kiwango cha ushawishi wao kwa wananchi dhidi ya serikali? Ni hakika kuwa Wito wa maandamano kwa wanasiasa pia huchukulia kama kipimo cha nguvu ya ushawishi kwa Wananchi.
Nitakuwepo Route ya Mbezi ya Kimara.
Nawatakia Jumatatu njema.
Kwanza sijajua maandamano haya ni endelevu au ni ya siku moja tuu. Maandamano ya amani ni nini hasa? Huwezi ita maandamano ya amani wakati muda huohuo ni kudai haki Fulani. Hakuna maandamano ya hivyo.
Kudai haki zipo njia nyingi kama kukaa mezani, lakini yakishakuwa maandamano hii inamaanisha njia ya amani yaani ya kukaa mezani imeshindikana.
Maandamano ya Amani mara nyingi huhusu kumpongeza mtu fulani, kusherehekea jambo fulani, kushangilia ushindi fulani nk, lakini kukishakuwa na madai ya haki fulani hayawezi kuwa maandamano ya Amani.
Sio ajabu Màandamano ya Amani yoyote duniani yenye lengo la kudai haki utakuta vyombo vya dola vikiyazuia kwa namna mbalimbali ikiwemo Nguvu.
Watu wanaofanya maandamano ya Amani ya kusherehekea, kupongeza au kushangilia jambo fulani hata uwape Bunduki au mabomu hawawezi kuleta madhara.
Lakini maandamano ya kudai Haki ambayo hayawezi itwa maandamano ya amani huwezi wapa Watu hao bunduki au mabomu kwani kitakachotokea kinajulikana.
Swali ni je, ikiwa maandamano ya Kenya ambayo nayo yaliitwa ya Amani yalishindwa, nini tutegemee kwenye maandamano yetu?
Je, Wapinzani wanataka kupima kiwango cha ushawishi wao kwa wananchi dhidi ya serikali? Ni hakika kuwa Wito wa maandamano kwa wanasiasa pia huchukulia kama kipimo cha nguvu ya ushawishi kwa Wananchi.
Nitakuwepo Route ya Mbezi ya Kimara.
Nawatakia Jumatatu njema.