Consigliere
Platinum Member
- Sep 9, 2010
- 12,690
- 26,567
Leo mapema tu nikiwa natoka zangu Nakuru to Nairobi along the A104 highway (Nairobi-Nakuru Highway), nilipofika pale Kayole pande za Naivasha nikaona ninunue some drink and bites za kunipa company kwenye kasafi hako ambako si karefu ni kama Kanakaribia umbali wa Dar mpaka Moro.
Nikaingia shopping center inaitwa Safari center, nilipokosa nilichohitaji ikabidi nielekee Buffalo Mall, nikiwa Buffallo Mall nikawasikia jamaa wawili na msichana mmoja wakiwa na maongezi serious huku wakiendelea kufanya shopping. Waliponikaribia ndiyo nikaelewa mjadala wao unahusiana vita ya maneno kati ya viongozi wa Tanzania na Gen Z wa Kenya (so embarrassing ). Katika maongezi hayo nikasikia wakisema inabidi Gen Z wa apologize kwa Watanzania na bunge lao (kwa kweli sikuelewa), nikapata nilichoenda kununua, nikaendelea na safari yangu.
Nikaingia Nairobi baada ya misele kadhaa nikawa nimeenda Kitisuru kukutana na jamaa fulani, baadaye ya nikawa naelekea Muthaiga, kwenye gari wakaongezeka watu watatu tukawa wanne, tukiwa humo nikasikia tena jamaa wakianzisha maongezi ya Gen Z kuwaomba msamaha watanzania na Bunge lao (Ninafahamiana nao kwa zaidi ya Mwaka lakini hawakuwahi kufahamu wala kuhisi kuwa mimi ni Mtanzania), nikawauliza wana maanisha nini, kuomba msambaha? Ndipo mmoja akafunguka kwamba siyo swala la Gen Zee pekee bali la wakenya wote sababu wamekuja kugundua kuwa Tanzania haina bunge, walichokiona ni Kanisa lenye waumini wanaoingia kwa kupigiwa kura na Wananchi, na kile kinachoonekana kama bunge kiuhalisia ni Kanisa kwa ajili ya kusifu na kuabudu. Jamaa mwingine aladakia kwamba pia wamekuja kugundua Tanzania haina rais bali ina Mungu, wakadai rais Samia ni Mungu nchini Tanzania na wao walidhani wanamshambulia rais kumbe ni Mungu, na si lengo lao kudharirisha imani za watu, hivyo wanajipanga waombe msamaha kwa kile walichomfanyia Mungu wa Tanzania na Kanisa lao (Bunge).
Kufikia hapo nikawa nimechoka hoi, kwa kweli nikaona ni bora waendelee na chochote wanachokifanya huko mitandaoni kuliko kutukashifu kiasi hiki.
Nikajikuta nawaambia "Brush it off."
Nikaingia shopping center inaitwa Safari center, nilipokosa nilichohitaji ikabidi nielekee Buffalo Mall, nikiwa Buffallo Mall nikawasikia jamaa wawili na msichana mmoja wakiwa na maongezi serious huku wakiendelea kufanya shopping. Waliponikaribia ndiyo nikaelewa mjadala wao unahusiana vita ya maneno kati ya viongozi wa Tanzania na Gen Z wa Kenya (so embarrassing ). Katika maongezi hayo nikasikia wakisema inabidi Gen Z wa apologize kwa Watanzania na bunge lao (kwa kweli sikuelewa), nikapata nilichoenda kununua, nikaendelea na safari yangu.
Nikaingia Nairobi baada ya misele kadhaa nikawa nimeenda Kitisuru kukutana na jamaa fulani, baadaye ya nikawa naelekea Muthaiga, kwenye gari wakaongezeka watu watatu tukawa wanne, tukiwa humo nikasikia tena jamaa wakianzisha maongezi ya Gen Z kuwaomba msamaha watanzania na Bunge lao (Ninafahamiana nao kwa zaidi ya Mwaka lakini hawakuwahi kufahamu wala kuhisi kuwa mimi ni Mtanzania), nikawauliza wana maanisha nini, kuomba msambaha? Ndipo mmoja akafunguka kwamba siyo swala la Gen Zee pekee bali la wakenya wote sababu wamekuja kugundua kuwa Tanzania haina bunge, walichokiona ni Kanisa lenye waumini wanaoingia kwa kupigiwa kura na Wananchi, na kile kinachoonekana kama bunge kiuhalisia ni Kanisa kwa ajili ya kusifu na kuabudu. Jamaa mwingine aladakia kwamba pia wamekuja kugundua Tanzania haina rais bali ina Mungu, wakadai rais Samia ni Mungu nchini Tanzania na wao walidhani wanamshambulia rais kumbe ni Mungu, na si lengo lao kudharirisha imani za watu, hivyo wanajipanga waombe msamaha kwa kile walichomfanyia Mungu wa Tanzania na Kanisa lao (Bunge).
Kufikia hapo nikawa nimechoka hoi, kwa kweli nikaona ni bora waendelee na chochote wanachokifanya huko mitandaoni kuliko kutukashifu kiasi hiki.
Nikajikuta nawaambia "Brush it off."