Kama dunia inazunguka kwanini hatumwagiki?

Kama dunia inazunguka kwanini hatumwagiki?

Swali hili linahitaji utulivu kidogo.
Mwalimu alisema
Dunia inajizungusha yenyewe na hapo hapo inalizunguka Jua katika mhimili wake.
Hivyo ina mizungiko miwili kwa wakati mmoja.
Ivi ukiwa kwenye Dunia imbayo inajizungusha na kuuzunguka mhimili wake utalionaje Jua ambalo tunaambiwa limesimama tuli kabisa ?
Halafu mwalimu anasema dunia ni ya mvilingo kama mpira au chungwa na hatudondoki eti kuna ka nguvu ka Gravity.
Hapo kuna ukweli wa kweli ?
Ivi upepo unapovuma na kutulia dunia inakuwa imesimama ?
Mbona matone ya mvua huwa yanadondoka huku yamenyooka kabisa toka mawinguni Juu ?
Hapo dunia huwa imesimama ?
Kwenye mtihani nilijibu kama mwalimu alivosema ili kupata vema.
Lakini mimi bado sijashawishika na hii Nadhalia ya Dunia ya mvilingo kujizungusha na kuzunguka Jua kwa wakati mmoja, bila sisi wanadamu kupata misukosuko.
Naomba kipimo cha kuthibitisha haya madai.

Sidanganyiki
Speed ya dunia ni kubwa lakini pia ni constant ndo maana huwezi kuhisi hiyo motion mfano ni kama gari lipo kwenye Barbara nzuri halafu linakimbia speed kubwa kama halijabadili gia unaweza hisi kama haliendi vile ni kwa sababu na ww unatembea na gari katika same speed au ukiwa kwenye lift huwezi hisi motion mpaka lifti ikisimama
 
Dunia inazunguka pamoja na atmosphere yake kwa spidi ile ile. Kwa hivyo kama unataka kuona spidi yake lazima utoke kwenye hii atmosphere uende kwenye utupu anga za mbali ( in space)
Siyo atmosphere Bali orbit yake mpaka utoke ndani ya hiyo orbit
 
Hatumwagiki kwa sababu Dunia haijafunga breki! 😀😀.
Siku Dunia ikifunga breki tutarushwa hukoo, sijui tutaenda kutulia wapi, labda kwenye sayari ya Mars. Dunia kwa sasa inakimbia kwa zaidi ya km 110,000 kwa saa huku ikilizunguka jua. Kumbuka, gari inayokimbia sana mpaka unaona kufa kufa kwa hapa Bongo wala hata haizidi km 180 kwa saa!
Najuta kufungua huu uzi, maana mbavu zangu ziko hoi kwa kicheko. Dah! Kweli jf ni kiboko
 
Speed ya dunia ni kubwa lakini pia ni constant ndo maana huwezi kuhisi hiyo motion mfano ni kama gari lipo kwenye Barbara nzuri halafu linakimbia speed kubwa kama halijabadili gia unaweza hisi kama haliendi vile ni kwa sababu na ww unatembea na gari katika same speed au ukiwa kwenye lift huwezi hisi motion mpaka lifti ikisimama
Kwahiyo dunia haisimami siyo km ni hivyo mbna kunakuwa na Giza? Nilijua wakati wa Giza inasimama....kuna MTU pia aliniambia Yale mawimbi baharini inaonesha namna dunia inavyo tikisika
 
Kuna uzi nyingi zipo juu ya hilo seals
Mtafute Tanzania Nationalist
 
Kwahiyo dunia haisimami siyo km ni hivyo mbna kunakuwa na Giza? Nilijua wakati wa Giza inasimama....kuna MTU pia aliniambia Yale mawimbi baharini inaonesha namna dunia inavyo tikisika
Waves ni disturbances kweli au forces that affect the earth
 
"Nakumbuka shuleni tulisoma dunia inajizungusha" bwana we mtaongezea maneno siunajua enzi zetu divison5 @ naomba msaada kwa nini hatuhisi kuzunguka?
Kwa nini maji hayamwagiki baharini?
Kwanini hatujikuta tuko ulaya tule maisha maana uwezo wa kupata viza sijui passport maana sielewi hata...
Wataalamu nipeni elimu
Nimependa ulivyo mkweli sijui umeweka huu uzi ili watu wacheke.

Kinachotufanya tusianguke ni force if gravity, hii hata unapoinua mzigo mzigo inakuwa kiunoni na unakuta balance.

Unappona msimu wa kiangazi na kipupwe ndiyo uhakisia wa mzunguko. Kiangazi tunakuwa tumelitazama jua.

Hatuwezi kwenda ulaya kwakuwa dunia ni kama chungwa kwenye mhimili wake.
 
"Nakumbuka shuleni tulisoma dunia inajizungusha" bwana we mtaongezea maneno siunajua enzi zetu divison5 @ naomba msaada kwa nini hatuhisi kuzunguka?
Kwa nini maji hayamwagiki baharini?
Kwanini hatujikuta tuko ulaya tule maisha maana uwezo wa kupata viza sijui passport maana sielewi hata...
Wataalamu nipeni elimu

ukijua kitu kina itwa gravity
gravity ndio sehemu kubwa ya kusaidia wewe na vitu vyote unavyo viona kuanzia binadamu,maji,sayari,anga na n.k
ili uweze kutembea kusimama,kuruka hata dunia basi kuzunguka ukajiona hupo kama mwengine aliye kuwa kwenye mduara huu ni mvutano baina pande mbili mfano wewe na dunia.
soma physics
 
Dunia inazunguka pamoja na atmosphere yake kwa spidi ile ile. Kwa hivyo kama unataka kuona spidi yake lazima utoke kwenye hii atmosphere uende kwenye utupu anga za mbali ( in space)
Ukikaa ndani ya meli inayotembea kwa ndani wakati hakuna mawimbi huwezi jua kama meli ipo kwenye mwendo.
Lakini ukiangalia nje unaona miti majumba na uoto wa asili unatembea.
Mbona sisi tunaokaa ndani ya dunia inayokimbia hatuoni nyota ambazo haziko ndani ya hiyo Atmosphere zikitembea kama tunavyoona kwenye meli inayotembea ?
Mi najua kuwa Nyota na Jua havipo ktk Atmosphere ya Dunia.
Lakini cha ajabu Jua na Mwezi tunaona vinatembea, lakini Nyota hazitembei.
Kwanini Jua na mwezi vitembee, ila Nyota zibaki bila kutembea ?
Wakati zote zipo nje ya Atmosphere ya Dunia ?
 
Ushahidi wa dunia kuzunguka ni MAJI KUPWA NA KUJAA,,, USIKU NA MCHANA,,, NA MABADILIKO YA MAJIRA YA MWAKA,,, KIPUPWE,, MVUA,, JUA KALI,, BARIDI,,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom