Kwanza wanatuambia dunia ni duara, pili tunaambiwa tupo nje ya dunia na sio ndani ndio sababu tunaliona jua, duh. Sasa mi najiulizaga, hivi ingekuwa dunia ni duara, si kungekuwa na miteremko kila upande wa huo mduara, bahari zingekaaje, kuna ziwa, mito. Maji yote yangeshamwagika. Kaazi kwelikweli. Halafu inawezekanaje dunia ikawa inazunguuka, halafu mtu kama umezaliwa Arusha, unaishi hadi unazeeka, upo palepale. Mzunguko haukuhamishi, mfano mkoa upo mashariki, ukizunguka si utaenda labda kusini, basi ulione jua kwa upande huo. Lakini wapi. Endeleeni kutudanganya wasomi. Tunaambiwa kuna sayari, nazo ni kubwa kweli kweli, hatuzioni. Na hatutaziona hadi mwisho wa dunia.