Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,515
- 52,169
Kwema Wakuu!
Kuna watu hata uwape majibu ya mtihani bado Watafeli pakubwa, alafu watakuwa wakwanza kulalamika.
Taikon ni mtu wakuwapeni Magaka/majibu ya mitihani kabla ya kuingia Chumba cha mitihani. Ukiona Jambo nimeliandika ujue tayari nishalifanyia uchunguzi wa kina, na Kwa vile sio hulka yangu kuwa mchoyo au mbinafsi ndio maana nawapeni majibu.
Niliwahi andika hapa,👉👉Usisaidie masikini, acha wafe
Hapa nilieleza namna Bora ya kumsaidia masikini ni kumpiga mshindo mzito, kumdhulumu ili akili yake imkae Sawa. Umasikini WA Mtu unaanzia kwenye Akili yake. Hivyo namna Bora ya kumfanya mtu awe na Akili sio kumpeleka shule pekee Bali kumpiga na vitu vizito mpaka akili ifanye kazi.
Niliandika hapa pia kuhusu wawekezaji, nikasema Kama unataka kuwekeza basi wekeza Kwa watu wajinga na Masikini, utapiga pesa mpaka ulie. Alafu haohao masikini watakuabudu kama mungu wao. Niliandika hapa👉👉Tanzania ukitaka kutajirika wekeza kwa wajinga na masikini
Vijana wa sasa eleweni kuwa kwenye haya maisha hakuna mtu aliyekwaajili yako.
Eleweni kuwa Maisha ni Ligi kuu ya mabingwa hayana shortcut, na yanahitaji mtu jasiri, Mwerevu, na mtu wa timing
Eleweni kuwa hakuna atakayekusaidia kama huna utakachompatia. Na Kwa nature ya binadamu mtu hawezi kukusaidia ili umzidi Ila atakusaidia ili aendelee kukuzidi, yaani anakupa 10 alafu yeye anapata 1000. Hiyo ndio kanuni ya kupata, ambayo ili upate itakupasa utoe. Na ili ukose itakupasa upokee.
Hata katika uchumi, nchi ijayo export zaidi ndio hutajirika kuliko Ile inayo-import. Bado hujaelewa tuu!
Kijana elewa kuwa hakuna kitu cha Bure dunia ingalipo binadamu akiwepo.
Kuna watu wanawasema watu Fulani ni wakarimu na wanatoa misaada Sana. L😂😂 Hakuna mtu anayefanya hivyo pasipo Hesabu ndefu ambayo wajinga hawaioni.
Wanasiasa wao wanaelewa zaidi, ukitaka kujua Hilo, jaribu hapo kwenye jamii yako kujifanya unatoa misaada mikubwa mikubwa utaona Serikali na wakubwa wa hapo wakikuzuia kufanya hivyo hata kama utasema kuwa unatoa bure na hauna agenda yoyote. Watakuambia Kama hauna agenda yoyote basi wape wao hiyo misaada alafu wao ndio wakatoe😂😂.
Masikini na wajinga utamu wao ni kuwapa vitu rahisi ili uendelee kuwpiga Kwa vitu vizito ambavyo wao hawavioni.
Hivi Kwa mtu mwenye akili na mfanyabiashara utawezaje kumshawishi akupe milioni moja alafu ndani ya wiki moja umrejeshee milioni mbili. Kwa biashara ipi? Kwa namna ipi?
Yaani akupe milioni mbili naye hapohapo awe amepata faida😂😂 uliona wapi mambo ya hivyo ndugu yangu.
Serikali isiwafungulie watu wa namna hiyo mashtaka hasa kama wakiwa Watanzania, lakini kama sio Watanzania wafunguliwe mashtaka kwani watakuwa wametudhalilisha na kutuona taifa letu ni watu wajinga wasio na Akili.
Wasalamu
Kuna watu hata uwape majibu ya mtihani bado Watafeli pakubwa, alafu watakuwa wakwanza kulalamika.
Taikon ni mtu wakuwapeni Magaka/majibu ya mitihani kabla ya kuingia Chumba cha mitihani. Ukiona Jambo nimeliandika ujue tayari nishalifanyia uchunguzi wa kina, na Kwa vile sio hulka yangu kuwa mchoyo au mbinafsi ndio maana nawapeni majibu.
Niliwahi andika hapa,👉👉Usisaidie masikini, acha wafe
Hapa nilieleza namna Bora ya kumsaidia masikini ni kumpiga mshindo mzito, kumdhulumu ili akili yake imkae Sawa. Umasikini WA Mtu unaanzia kwenye Akili yake. Hivyo namna Bora ya kumfanya mtu awe na Akili sio kumpeleka shule pekee Bali kumpiga na vitu vizito mpaka akili ifanye kazi.
Niliandika hapa pia kuhusu wawekezaji, nikasema Kama unataka kuwekeza basi wekeza Kwa watu wajinga na Masikini, utapiga pesa mpaka ulie. Alafu haohao masikini watakuabudu kama mungu wao. Niliandika hapa👉👉Tanzania ukitaka kutajirika wekeza kwa wajinga na masikini
Vijana wa sasa eleweni kuwa kwenye haya maisha hakuna mtu aliyekwaajili yako.
Eleweni kuwa Maisha ni Ligi kuu ya mabingwa hayana shortcut, na yanahitaji mtu jasiri, Mwerevu, na mtu wa timing
Eleweni kuwa hakuna atakayekusaidia kama huna utakachompatia. Na Kwa nature ya binadamu mtu hawezi kukusaidia ili umzidi Ila atakusaidia ili aendelee kukuzidi, yaani anakupa 10 alafu yeye anapata 1000. Hiyo ndio kanuni ya kupata, ambayo ili upate itakupasa utoe. Na ili ukose itakupasa upokee.
Hata katika uchumi, nchi ijayo export zaidi ndio hutajirika kuliko Ile inayo-import. Bado hujaelewa tuu!
Kijana elewa kuwa hakuna kitu cha Bure dunia ingalipo binadamu akiwepo.
Kuna watu wanawasema watu Fulani ni wakarimu na wanatoa misaada Sana. L😂😂 Hakuna mtu anayefanya hivyo pasipo Hesabu ndefu ambayo wajinga hawaioni.
Wanasiasa wao wanaelewa zaidi, ukitaka kujua Hilo, jaribu hapo kwenye jamii yako kujifanya unatoa misaada mikubwa mikubwa utaona Serikali na wakubwa wa hapo wakikuzuia kufanya hivyo hata kama utasema kuwa unatoa bure na hauna agenda yoyote. Watakuambia Kama hauna agenda yoyote basi wape wao hiyo misaada alafu wao ndio wakatoe😂😂.
Masikini na wajinga utamu wao ni kuwapa vitu rahisi ili uendelee kuwpiga Kwa vitu vizito ambavyo wao hawavioni.
Hivi Kwa mtu mwenye akili na mfanyabiashara utawezaje kumshawishi akupe milioni moja alafu ndani ya wiki moja umrejeshee milioni mbili. Kwa biashara ipi? Kwa namna ipi?
Yaani akupe milioni mbili naye hapohapo awe amepata faida😂😂 uliona wapi mambo ya hivyo ndugu yangu.
Serikali isiwafungulie watu wa namna hiyo mashtaka hasa kama wakiwa Watanzania, lakini kama sio Watanzania wafunguliwe mashtaka kwani watakuwa wametudhalilisha na kutuona taifa letu ni watu wajinga wasio na Akili.
Wasalamu