Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal

Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal

Uko sahihi ndio maana hata hapa JF watu wamechoka, hawaoni hata sababu ya kuchangia kama ushahidi wa wazi upo na hakuna hatua

Vijana msilalee lale lalee vijana msilalee.. X2 Bado mapambano...
 
Don't just sit there, do something! Ukikaa pembeni gari la madiliko linaloshika kasi litakubeba vile ulivyo na kondakta atakutafutia sehemu nzuri ya kukaa



WE DONT SAY GOODBYE BUT SEE YOU LATER- Denzil Washington
 
Nadhani sasa tunahitaji kuamka watanzania tuanze maandamano kuishinikiza serikali katika masuala ya ufisadi. Nadhani yale maandamano yaliyokuwa yameandaliwa na kikundi kisichokuwa cha kushinikiza kutajwa mafisadi wa EPA na kuwafikishwa mahakamani kinatakiwa kianzie pale tulipokomea. Ni haki yetu ya kikatiba kuwakamata na kuwafikisha kwenye sheria wale wote wanaohujumu nchi. Ni kosa kufahamu kosa limetendeka na usichukue hatua
 
Vigogo wa Kagoda, Jeetu Patel waogopwa

Mwandishi Wetu Oktoba 29, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

Yadaiwa ushahidi dhidi yao 'dhaifu'

'Kondoo wa kafara' ndiyo watakaoshitakiwa

ZIKIWA zimebakia siku mbili kwisha kwa muda uliotolewa kwa timu ya Rais iliyokabidhiwa jukumu la kuchunguza wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania, watuhumiwa wakuu watatu wa wizi huo wanaelekea kuumiza vichwa vya viongozi na watendaji wakuu serikalini na ndani ya chama tawala cha CCM kutokana na nguvu kubwa waliyonayo.

Wanaoteswa na jinsi ya kuwashughulikia watuhumiwa hao ni pamoja na Rais Jakaya Kikwete, aliyeunda timu na baadaye kuiongezea muda huku akitoa kauli zinazopishana kuhusu hatua za kuchukua ikiwa ni pamoja na kuwashitaki waliohusika na jinai hiyo na ile kauli ya kuwa wasiolipa fedha ndio watakaofikishwa mahakamani.

Habari za uhakika kutoka serikalini zinaeleza kwamba, suala la kuwachukulia ama kutowachukulia hatua watuhumiwa hao wakuu limekuwa likiisumbua timu ya Rais inayoongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, kutokana na kile kinachoelezwa kwamba watuhumiwa hao wakuu walikuwa "makini" katika kuchukua fedha za EPA na hata wakati wa urejeshaji wake.

Ofisa Mwandamizi wa serikali ameliambia RAIA MWEMA kwamba watuhumiwa wakuu watatu ambao wananchi wengi wanataka wafikishwe mahakamani hawataguswa; angalau kwa sasa kutokana na watuhumiwa hao kuwa makini wakati wa mchakato wa kuchukua fedha za EPA na ndio pekee waliorejesha fedha zote walizochukua kwa wakati, ikiwa ni "kutimiza masharti yaliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete".

"Wakati wa mchakato wa kuchukua fedha za EPA watuhumiwa hao ambao watu wengi, vikiwamo vyombo vya habari, wanataka wachukuliwe hatua walikuwa makini mno kiasi cha kuwafanya wachunguzi wakose makosa ya kijinai ya kuweza kuwafikisha mahakamani na walipopewa muda wa kulipa walilipa kwa wakati na kwa uangalifu mkubwa kiasi cha kuwa vigumu kuwabana," alisema ofisa huyo.

"Hata hivyo, bado kuna mambo yanayoangaliwa ikiwa yatakamilika lolote linaweza kutokea; hasa ikiwa uongozi wa juu wa serikali utafanya maamuzi magumu kwa kuwa uamuzi wa kisiasa pia ni muhimu katika kufikia maamuzi katika suala la fedha za EPA kwa kuwa linaweza kusababisha mtikisiko mkubwa katika siasa za Tanzania," alisema Ofisa huyo ambaye hata hivyo anakiri udhaifu katika kuwashughulikia wahusika hao.

Uchunguzi wa RAIA MWEMA kwa muda mrefu sasa umebaini kuwapo kwa watuhumiwa ambao wanaweza kufanywa 'kondoo wa kafara' kutokana na msimamo wao katika kutoa maelezo kwenye timu iliyokabidhiwa jukumu la kuchunguza tuhuma hizo, na pia kwa kile kilichoelezwa "kiburi cha ajabu" walichoonyesha watuhumiwa hao.

Watuhumiwa wanaotarajiwa kufikishwa mahakamani ni wale ambao wanaelezwa wamegoma kutoa ushirikiano kwa Serikali ikiwa ni pamoja na kushindwa kulipa fedha na baadhi kukataa kutoa maelezo waliyotakiwa kuyatoa, na badala yake wamekuwa wakitoa maelezo kuonyesha kwamba wao walishiriki katika uchukuaji wa fedha za EPA kwa kufuata taratibu na sheria na baadhi walidai kupata fedha hizo kwa kazi walizofanya.

Utata mkubwa zaidi unaelezwa kutarajiwa kuibuka kuhusiana na fedha hizo kutumika katika uchaguzi wa mwaka 2005 hususan katika kukisaidia Chama cha Mapinduzi (CCM; huku baadhi wakitajwa kuwa na ushahidi wa jinsi fedha hizo zilivyotumika, jambo ambalo tayari limekwisha kukanushwa na viongozi wa chama hicho tawala.

Imeelezwa kwamba mmoja wa watuhumiwa, ambaye ni mfanyabiashara maarufu mwenye asili ya kiasia, ameelezwa kujitokeza kulipa fedha za kampuni ya Kagoda Agricultural Limited, kampuni iliyochota zaidi ya Shilingi bilioni 40, lakini pamoja na kujitokeza kwake, kumekuwa na kigugumizi cha kumuunganisha na makosa ya jinai yaliyofanywa wakati wa kuchukua fedha hizo.

"Unajua ni kichekesho, tunaambiwa wahusika wa Kagoda hawajulikani, lakini anakuja mtu analipa fedha za Kagoda na anajulikana kuwa analipa kwa niaba ya nani, halafu tunaendelea kusema hatuwafahamu wahusika wa kampuni hiyo ambayo imethibitika kufanya jinai. Kwa kweli inatuaibisha sana sisi tuliosomea kazi ya upelelezi wa mambo ya jinai na ni aibu pia kwa serikali nzima kuwaogopa watu," anasema ofisa mwingine mwandamizi wa serikali mwenye uzoefu na mambo ya upelelezi wa jinai.

Kampuni ya Kagoda imekuwa ikitajwa kutofahamika ofisi zake wala wahusika wake wakuu kutopatikana, lakini kitendo cha kujitokeza kwa mtu kulipa fedha za kampuni hiyo kwenye timu ya Rais, kimeelezwa kutokuwa na tofauti yoyote na watuhumiwa wengine wa wizi wanaokutwa na mali, hata wale walionunua mali hiyo kwa wezi.

"Kuna wafungwa wengi ambao wamefungwa kwa kukutwa na mali za wizi, baadhi hawakuhusika hata na wizi; bali walinunua mali hizo kwa watu wengine tena baadhi bila hata ya kujua kama ni mali za wizi, sasa mtu anakuja analipa fedha zilizoibwa unamwachia, si tungewaambia kina Kasusura (Justine) na wenzake walipe tu fedha walizoiba wakati ule badala ya kuwashitaki?" anasema ofisa huyo ndani ya serikali.

Habari zaidi zinaeleza kwamba miongoni mwa watuhumiwa ambao Serikali inapata kigugumizi kuwashitaki ni pamoja na mfanyabiashara Jeetu Patel na wenzake wanaofahamika ambao makampuni yao manane ni miongoni mwa makampuni yaliyochukua zaidi ya Shilingi bilioni 90 ambazo zimethibitika kupatikana kwa njia ya udanganyifu na kwa kutumia nyaraka za kughushi.

Imeelezwa kwamba, pamoja na kuwa katika orodha ya makampuni yaliyopata fedha za EPA kwa kughushi nyaraka, Jeetu Patel, anaelezwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa timu ya Rais, huku akiwa na kumbukumbu kubwa ya kuchangia kwa kiwango kikubwa kampeni za CCM za mwaka 2005, ikiwa ni pamoja na kuchangia ununuzi wa magari na misaada mingine, mambo ambayo yameelezwa kumpa kinga mfanyabiashara huyo.

Wanaotajwa kuwa wanaweza kufikishwa mahakamani, ni wale ambao kampuni zao zimo katika kampuni zilizochukua jumla ya Shilingi bilioni 44, fedha ambazo wakaguzi walisema wameshindwa kuthibitisha kuwapo kwa jinai na kupendekeza kufanyika kwa ukaguzi mpana zaidi wa kutumia kampuni za kimataifa zenye uzoefu katika uhakiki.

Imeelezwa kwamba kesi zitakazofunguliwa sasa zinalenga kushusha joto la kisiasa lililopanda kutokana na kuonekana kwamba watawala hawachukui hatua thabiti juu ya tuhuma za ufisadi zinazowakabili wanasiasa na matajiri kadhaa walio karibu na chama tawala wakati huu wa kuelekea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Kwa mujibu wa habari hizo, kesi hizo zinatakiwa ziendelee hadi hata baada ya 2010 ili kutoa picha kwamba utawala umedhamiria kupambana na ufisadi hata kama kesi hizo zitakuwa zikitajwa tu na watuhumiwa, hasa wale wa EPA wakiwa ndani chini ya tuhuma kama za hujuma ya uchumi, kughushi na kula njama kuiba.

Wanaotajwa kufikishwa mahakamani ni wamiliki wa kampuni za Changanyikeni Residential Complex Limited, Malegesi Law Chambers, G&T International Limited na Karnel Meals Holdings Ltd zinazomilikiwa na Jose Van de Merwe, Samson Mapunda na Charles Mabina, Beredy Maregesi, Octavio Timoth, Johnson Lukaza na Mwesigwa Rutakyamilwa Lukazas.

Raia Mwema limefahamishwa kwamba watakaofikishwa mahakamani kwanza ni Maregesi, Mapunda na Lukaza katika hatua inayozua minong'ono ya kuwa watuhumiwa wakubwa wa fedha za EPA wanakingiwa kifua kwa kuwa wana uhusiano wa karibu na chama tawala ama kuwapo kwa 'mikono michafu'.

"Ni kama sasa wanataka kutolewa kafara. Hata muda uliotolewa wa Oktoba 31 ni kama uliwalenga wao. Wamekuwa wakikataa kurudisha fedha wakidai kwamba wao walifanya kazi, walioiba ni hao ambao sasa wanaelezwa kwamba wamerudisha. Kwamba wao sasa wanataka kushitakiwa huku wakubwa wakiachwa maana yake kubwa ni kwamba watawala wanafunika kombe," alisema mmoja wa watu walio karibu na watuhumiwa hao.

Kampuni zilizokwiba fedha nyingi zaidi kutoka akaunti ya EPA na ambazo sasa kwa utaratibu huu wamiliki wake hawataguswa ni pamoja na ya Kagoda Agricultural Limited kampuni nane za Jeetu Patel.

Kwa mujibu wa wakaguzi, Kagoda ilighushi nyaraka zilizotumika kuchota zaidi ya Shilingi bilioni 40 wakati Jeetu Patel naye amechota zaidi ya nusu ya fedha zilizoibwa akitumia kampuni nane.

Maofisa wa Serikali hususan wale wa vyombo vya dola, wakiwamo wajumbe wa kikosi kazi (task force) kilichokabidhiwa kazi ya kuchunguza na kuchukua hatua dhidi ya wahusika waliochota fedha hizo, walipoulizwa kuhusu kushitakiwa kwa wachache tu katika wizi wa EPA wote walidai kwamba muda aliotoa Rais Jakaya Kikwete kukamilika kwa suala hilo haujakwisha na ni yeye mwenye kauli ya mwisho.

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai (DCI), Robert Manumba, ambaye alitajwa na vyanzo vya habari kwamba ofisi yake ndiyo inakamilisha taratibu za kuwashitaki wahusika aliiambia Raia Mwema wiki iliyopita kwamba hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kuwa msemaji wa kikosi kazi (task force) ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, ambaye naye amenukuliwa akisema suala hilo linapaswa kuzungumziwa na Rais ambaye ndiye aliyetoa muda wa ziada.

Kauli kama hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk. Edward Hosea ambaye naye hakuwa tayari kuzungumzia hatua ambayo wamefikia katika kuwashitaki wahusika, huku Ofisa Mwandamizi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, akisema kwamba kila kitu kitajulikana siku chache zijazo.

Hata hivyo, Raia Mwema limethibitishiwa kwamba Maregesi, Mapunda na Lukaza, wanatajwa kuwa watu watakaotolewa kafara kutokana na kile kilichoelezwa kwamba wamekuwa na "jeuri ya Kiafrika" kwa kukataa kulipa fedha wanazotuhumiwa kuzichota.

Imeelezwa kwamba tokea awali watuhumiwa hao wamekuwa wakigoma 'kutoa ushirikiano' jambo ambalo limeelezwa kuwakera baadhi ya wanasiasa na watendaji wa Serikali walioamua sasa kuwaburuza mahakamani.

Raia Mwema imethibitisha kwamba bado akaunti na hati za kusafiria za watuhumiwa hao zinaendelea kushikiliwa hata baada ya muda wa miezi sita kisheria kupita kwa maelekezo ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu.

Habari zinaeleza kwamba awali watuhumiwa hao walikuwa wafikishwe mahakamani sambamba na maofisa wa BoT waliohusika katika mchakato wa EPA, lakini uamuzi huo ulibadilishwa baada ya tishio kutoka kwa watumishi hao kwamba 'wataanika' kila kitu hadharani wakitolewa kafara.

"Baada ya watumishi hao wa BoT kutishia kumwaga kila kitu hadharani, mwelekeo umebadilika na sasa wataitwa kama mashahidi wa upande wa serikali kesi hizo zitakapofikishwa mahakamani, lakini bado wanaweza kuiharibia serikali watakapoamua kutaja watu ambao wamefichwa," anasema mtoa habari wetu aliye karibu na vyombo vya dola.

Raia Mwema imefahamishwa kwamba kesi hizo zinatarajiwa kutumika kama mwavuli wa kuivusha serikali kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, kukwepa wimbi la manung'uniko ya wazi kwamba serikali ya CCM imekuwa ikiwalea watuhumiwa wa ufisadi, wengi wakiwa ni wafadhili wa chama hicho.

Wakaguzi wa ndani na wale wa nje, walibaini kuwapo kwa wizi mkubwa wa fedha katika akaunti ya EPA katika kipindi cha mwaka mmoja pekee wa 2005/2006 ambako zilipotea zaidi ya Shilingi bilioni 133.

Wakaguzi hao walibaini kwamba kati ya fedha hizo shilingi bilioni 90 ni zile ambazo zimethibitika kuchotwa kwa kutumia nyaraka za kughushi, sehemu kubwa zikiwa zimekwenda kwa wafanyabiashara wawili, wamiliki halisi wa Kagoda Agricultural Limited na Jeetu Patel kupitia kampuni zake nane.

Ripoti ya Wakaguzi wa Kampuni ya Ernst and Young waliofanya kazi kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ilionyesha kwamba kiasi cha Shilingi 90,359,078,804.00 zililipwa kwa kampuni 13 ambazo zilitumia kumbukumbu, nyaraka na hati zilizo batili na za kugushi na kwamba kampuni hizo hazikustahili kulipwa chochote.

Wakaguzi hao na Ikulu, kupitia taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wake, Philemon Luhanjo, Januari 9, 2008, walipendekeza moja kwa moja bila kuuma maneno kwamba wahusika wa kampuni hizo 13 wachukuliwe hatua za kisheria mara moja, kauli ambayo Rais Kikwete aliirejea katika hotuba yake bungeni, lakini bila ukali tena.

Makampuni ambayo Jeetu Patel anahusika nayo na ambayo yamethibitika kughushi nyaraka na kuchota fedha BoT ni Navycut Tobacco (T) Limited, Ndovu Soaps Limited, Bina Resorts Limited, Bencon International Limited, Maltan Mining Company Limited, Bora Hotels & Apartments Limited, Venus Hotels Limited, and B.V. Holdings Limited.

Pamoja na kampuni hizo za Jeetu Patel, kampuni nyingine zilizohusika na jinai ya kughushi nyaraka ni pamoja na Kagoda Agriculture Limited ambayo wanaoonekana katika nyaraka ni John Kyomuhendo mwenye hisa 40 na Francis William anayemiliki hisa 60 katika kampuni hiyo.

Kampuni nyingine ni V.B & Associeties Company zinazomilikiwa na Devendra Patel na Jantkumar Chandubhai Patel na Changanyikeni Residential Complex Limited inayomilikiwa na Jose Van de Merwe, Samson Mapunda na Charles Mabina ikiwa na makao yake, Sinza, Kumekucha, Dar es Salaam.

Pia katika orodha hiyo ya kampuni 13 zilizoghushi nyaraka ambazo wahusika wake wamependekezwa kuchukuliwa hatua za kisheria mara moja ni Money Planners & Consultants inayomilikiwa na Paul Nyingo na Fundi Kitungi na kampuni ya Njake Hotel & Tours Limited inayomilikiwa Japhet Lema, Anna Lema, Abel Lema, Derick Lema na Benard Lema wa Arusha.

Jeetu Patel katika baadhi ya kampuni anashirikiana na wafanyabiashara wengine wa Dar es Salaam ambao wanatajwa kushiriana naye katika kuhamisha fedha hizo kwenda nje kwa kuzibadili kutoka shilingi za Kitanzania kwenda Dola za Merakani ama Euro bila kufuata mkondo halali wa fedha kinyume cha Sheria ya Udhibiti wa Fedha Haramu.

Miongoni mwa wanaotajwa kushirikiana na Jeetu Patel ni Sidik Yacoubu kupitia kampuni yao ya Ndovu Soap Limited ambayo kwa mujibu wa nyaraka za Wakala wa Leseni na Usajili wa Kampuni (BRELA), kampuni hiyo yenye namba ya usajili 20536 ya Februari 3, 1992, wamiliki wake ni Jayantulal Chandubhai Patel na Sidik Yacoubu.

Katika kampuni ya Bora Hotels and Apartments iliyosajiliwa Septemba 8, 2005 inaonyeshwa katika orodha ya BRELA kwamba wamiliki wake wamo Jayantkumar Chandubhai Patel na Devandra Patel wakati Bina Resort Limited iliyosajiliwa Machi 31, 2005, wamo Jayantikumar Chandubhai Patel na Devendra Patel.

Kampuni ya Maltan Mining Company iliyosajiliwa Machi 8, 1993 inamilikiwa na Jantkumar Chandubhai Patel na Hariharier Radhakrishna wakati Navy Cut Tobacco iliyosajiliwa Oktoba 12, mwaka 1995 inamilikiwa na Jantkumar Chandubhai Patel na Radakrishna.

Kampuni nyingine ni Bencon Limited, B.V Holdings, Venus Hotels na V.B & Associeties Company zinazomilikiwa na Devendra Patel na Jantkumar Chandubhai Patel, ambazo zote zilisajiliwa Aprili 4, 2005.

Katika orodha ya BRELA imo pia kampuni ya Excellent Service Limited inayomilikiwa na Emil Samanya, Peter Sabas na Elisifa Ngowi ambaye anatajwa kuwa ni Ofisa Mwandamizi wa Idara ya Usalama wa Taifa, ambaye yumo katika task force inayochunguza wizi huo. Kampuni hiyo ilisajiliwa Mei 13, 1992 na kupewa namba 26959.

Ngowi anahusishwa pia katika kampuni nyingine ya Clyton Marketing iliyosajiliwa Juni 6, 2005 akiwa na mwenzake Edwin Mtoi, ambaye haikuweza kufahamika mara moja anafanya shughuli gani zaidi ya kuwa katika kampuni hiyo.

Wamiliki wengine waliofahamika ni Rajabu Maranda na Thabit Katunda ambao wanatajwa kumiliki kampuni ya Liqiud Service Limited ambayo usajili wake ulifanyika Desemba 12, 2004 na kupewa namba 15007.

Wamiliki wengine waliofahamika ni Johnson Lukaza na Mwesigwa Rutakyamilwa Lukaza ambao wao wanamiliki kampuni ya Karnel Meals Holdings Ltd ambayo usajili wake ulipatikana Agosti 4, 1998, Mibale Farm iliyosajiliwa Septemba 2, 2005 na kupewa namba 154039 ambayo inamilikiwa na Kizza Selemani na Farijala Hussein, Malegesi Law Chambers inayomilikiwa na Beredy Malegesi ambayo ilisajiliwa Septemba 24, 2001.

Wamiliki wengine ni Paul Nyingo na Fundi Kitungi, wanaomiliki Kampuni ya Money Planners & Consultants iliyosajiliwa Machi 22, 2005 na Kiloloma & Bros Enterprises inayomilikiwa na Charies Kissa, ambayo ilisajiliwa Aprili 8, 2005.

Katika ukusanyaji wa fedha hizo, task force ya serikali inaelezwa kukusanya shilingi 53,738,835,392/= fedha ambazo Rais Kikwete ameagiza ziingizwe katika mfuko maalumu kwa ajili ya kusaidia sekta ya kilimo zikichanganywa na nyingine zinazotarajiwa kufikia shilingi 64,844,770,688/=
 
Wakuu naomba kuwakilisha hii makala ya Raia Mwema, kwa mtizamo wangu imechambuliwa vizuri sana ni muhimu kuisoma.

Vigogo wa Kagoda, Jeetu Patel waogopwa

Mwandishi Wetu Oktoba 29, 2008

Yadaiwa ushahidi dhidi yao 'dhaifu'

'Kondoo wa kafara' ndiyo watakaoshitakiwa

ZIKIWA zimebakia siku mbili kwisha kwa muda uliotolewa kwa timu ya Rais iliyokabidhiwa jukumu la kuchunguza wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania, watuhumiwa wakuu watatu wa wizi huo wanaelekea kuumiza vichwa vya viongozi na watendaji wakuu serikalini na ndani ya chama tawala cha CCM kutokana na nguvu kubwa waliyonayo.

Wanaoteswa na jinsi ya kuwashughulikia watuhumiwa hao ni pamoja na Rais Jakaya Kikwete, aliyeunda timu na baadaye kuiongezea muda huku akitoa kauli zinazopishana kuhusu hatua za kuchukua ikiwa ni pamoja na kuwashitaki waliohusika na jinai hiyo na ile kauli ya kuwa wasiolipa fedha ndio watakaofikishwa mahakamani.

Habari za uhakika kutoka serikalini zinaeleza kwamba, suala la kuwachukulia ama kutowachukulia hatua watuhumiwa hao wakuu limekuwa likiisumbua timu ya Rais inayoongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, kutokana na kile kinachoelezwa kwamba watuhumiwa hao wakuu walikuwa "makini" katika kuchukua fedha za EPA na hata wakati wa urejeshaji wake.

Ofisa Mwandamizi wa serikali ameliambia RAIA MWEMA kwamba watuhumiwa wakuu watatu ambao wananchi wengi wanataka wafikishwe mahakamani hawataguswa; angalau kwa sasa kutokana na watuhumiwa hao kuwa makini wakati wa mchakato wa kuchukua fedha za EPA na ndio pekee waliorejesha fedha zote walizochukua kwa wakati, ikiwa ni "kutimiza masharti yaliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete".

"Wakati wa mchakato wa kuchukua fedha za EPA watuhumiwa hao ambao watu wengi, vikiwamo vyombo vya habari, wanataka wachukuliwe hatua walikuwa makini mno kiasi cha kuwafanya wachunguzi wakose makosa ya kijinai ya kuweza kuwafikisha mahakamani na walipopewa muda wa kulipa walilipa kwa wakati na kwa uangalifu mkubwa kiasi cha kuwa vigumu kuwabana," alisema ofisa huyo.

"Hata hivyo, bado kuna mambo yanayoangaliwa ikiwa yatakamilika lolote linaweza kutokea; hasa ikiwa uongozi wa juu wa serikali utafanya maamuzi magumu kwa kuwa uamuzi wa kisiasa pia ni muhimu katika kufikia maamuzi katika suala la fedha za EPA kwa kuwa linaweza kusababisha mtikisiko mkubwa katika siasa za Tanzania," alisema Ofisa huyo ambaye hata hivyo anakiri udhaifu katika kuwashughulikia wahusika hao.

Uchunguzi wa RAIA MWEMA kwa muda mrefu sasa umebaini kuwapo kwa watuhumiwa ambao wanaweza kufanywa 'kondoo wa kafara' kutokana na msimamo wao katika kutoa maelezo kwenye timu iliyokabidhiwa jukumu la kuchunguza tuhuma hizo, na pia kwa kile kilichoelezwa "kiburi cha ajabu" walichoonyesha watuhumiwa hao.

Watuhumiwa wanaotarajiwa kufikishwa mahakamani ni wale ambao wanaelezwa wamegoma kutoa ushirikiano kwa Serikali ikiwa ni pamoja na kushindwa kulipa fedha na baadhi kukataa kutoa maelezo waliyotakiwa kuyatoa, na badala yake wamekuwa wakitoa maelezo kuonyesha kwamba wao walishiriki katika uchukuaji wa fedha za EPA kwa kufuata taratibu na sheria na baadhi walidai kupata fedha hizo kwa kazi walizofanya.

Utata mkubwa zaidi unaelezwa kutarajiwa kuibuka kuhusiana na fedha hizo kutumika katika uchaguzi wa mwaka 2005 hususan katika kukisaidia Chama cha Mapinduzi (CCM; huku baadhi wakitajwa kuwa na ushahidi wa jinsi fedha hizo zilivyotumika, jambo ambalo tayari limekwisha kukanushwa na viongozi wa chama hicho tawala.

Imeelezwa kwamba mmoja wa watuhumiwa, ambaye ni mfanyabiashara maarufu mwenye asili ya kiasia, ameelezwa kujitokeza kulipa fedha za kampuni ya Kagoda Agricultural Limited, kampuni iliyochota zaidi ya Shilingi bilioni 40, lakini pamoja na kujitokeza kwake, kumekuwa na kigugumizi cha kumuunganisha na makosa ya jinai yaliyofanywa wakati wa kuchukua fedha hizo.

"Unajua ni kichekesho, tunaambiwa wahusika wa Kagoda hawajulikani, lakini anakuja mtu analipa fedha za Kagoda na anajulikana kuwa analipa kwa niaba ya nani, halafu tunaendelea kusema hatuwafahamu wahusika wa kampuni hiyo ambayo imethibitika kufanya jinai. Kwa kweli inatuaibisha sana sisi tuliosomea kazi ya upelelezi wa mambo ya jinai na ni aibu pia kwa serikali nzima kuwaogopa watu," anasema ofisa mwingine mwandamizi wa serikali mwenye uzoefu na mambo ya upelelezi wa jinai.

Kampuni ya Kagoda imekuwa ikitajwa kutofahamika ofisi zake wala wahusika wake wakuu kutopatikana, lakini kitendo cha kujitokeza kwa mtu kulipa fedha za kampuni hiyo kwenye timu ya Rais, kimeelezwa kutokuwa na tofauti yoyote na watuhumiwa wengine wa wizi wanaokutwa na mali, hata wale walionunua mali hiyo kwa wezi.

"Kuna wafungwa wengi ambao wamefungwa kwa kukutwa na mali za wizi, baadhi hawakuhusika hata na wizi; bali walinunua mali hizo kwa watu wengine tena baadhi bila hata ya kujua kama ni mali za wizi, sasa mtu anakuja analipa fedha zilizoibwa unamwachia, si tungewaambia kina Kasusura (Justine) na wenzake walipe tu fedha walizoiba wakati ule badala ya kuwashitaki?" anasema ofisa huyo ndani ya serikali.

Habari zaidi zinaeleza kwamba miongoni mwa watuhumiwa ambao Serikali inapata kigugumizi kuwashitaki ni pamoja na mfanyabiashara Jeetu Patel na wenzake wanaofahamika ambao makampuni yao manane ni miongoni mwa makampuni yaliyochukua zaidi ya Shilingi bilioni 90 ambazo zimethibitika kupatikana kwa njia ya udanganyifu na kwa kutumia nyaraka za kughushi.

Imeelezwa kwamba, pamoja na kuwa katika orodha ya makampuni yaliyopata fedha za EPA kwa kughushi nyaraka, Jeetu Patel, anaelezwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa timu ya Rais, huku akiwa na kumbukumbu kubwa ya kuchangia kwa kiwango kikubwa kampeni za CCM za mwaka 2005, ikiwa ni pamoja na kuchangia ununuzi wa magari na misaada mingine, mambo ambayo yameelezwa kumpa kinga mfanyabiashara huyo.

Wanaotajwa kuwa wanaweza kufikishwa mahakamani, ni wale ambao kampuni zao zimo katika kampuni zilizochukua jumla ya Shilingi bilioni 44, fedha ambazo wakaguzi walisema wameshindwa kuthibitisha kuwapo kwa jinai na kupendekeza kufanyika kwa ukaguzi mpana zaidi wa kutumia kampuni za kimataifa zenye uzoefu katika uhakiki.

Imeelezwa kwamba kesi zitakazofunguliwa sasa zinalenga kushusha joto la kisiasa lililopanda kutokana na kuonekana kwamba watawala hawachukui hatua thabiti juu ya tuhuma za ufisadi zinazowakabili wanasiasa na matajiri kadhaa walio karibu na chama tawala wakati huu wa kuelekea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Kwa mujibu wa habari hizo, kesi hizo zinatakiwa ziendelee hadi hata baada ya 2010 ili kutoa picha kwamba utawala umedhamiria kupambana na ufisadi hata kama kesi hizo zitakuwa zikitajwa tu na watuhumiwa, hasa wale wa EPA wakiwa ndani chini ya tuhuma kama za hujuma ya uchumi, kughushi na kula njama kuiba.

Wanaotajwa kufikishwa mahakamani ni wamiliki wa kampuni za Changanyikeni Residential Complex Limited, Malegesi Law Chambers, G&T International Limited na Karnel Meals Holdings Ltd zinazomilikiwa na Jose Van de Merwe, Samson Mapunda na Charles Mabina, Beredy Maregesi, Octavio Timoth, Johnson Lukaza na Mwesigwa Rutakyamilwa Lukazas.

Raia Mwema limefahamishwa kwamba watakaofikishwa mahakamani kwanza ni Maregesi, Mapunda na Lukaza katika hatua inayozua minong'ono ya kuwa watuhumiwa wakubwa wa fedha za EPA wanakingiwa kifua kwa kuwa wana uhusiano wa karibu na chama tawala ama kuwapo kwa 'mikono michafu'.

"Ni kama sasa wanataka kutolewa kafara. Hata muda uliotolewa wa Oktoba 31 ni kama uliwalenga wao. Wamekuwa wakikataa kurudisha fedha wakidai kwamba wao walifanya kazi, walioiba ni hao ambao sasa wanaelezwa kwamba wamerudisha. Kwamba wao sasa wanataka kushitakiwa huku wakubwa wakiachwa maana yake kubwa ni kwamba watawala wanafunika kombe," alisema mmoja wa watu walio karibu na watuhumiwa hao.

Kampuni zilizokwiba fedha nyingi zaidi kutoka akaunti ya EPA na ambazo sasa kwa utaratibu huu wamiliki wake hawataguswa ni pamoja na ya Kagoda Agricultural Limited kampuni nane za Jeetu Patel.

Kwa mujibu wa wakaguzi, Kagoda ilighushi nyaraka zilizotumika kuchota zaidi ya Shilingi bilioni 40 wakati Jeetu Patel naye amechota zaidi ya nusu ya fedha zilizoibwa akitumia kampuni nane.

Maofisa wa Serikali hususan wale wa vyombo vya dola, wakiwamo wajumbe wa kikosi kazi (task force) kilichokabidhiwa kazi ya kuchunguza na kuchukua hatua dhidi ya wahusika waliochota fedha hizo, walipoulizwa kuhusu kushitakiwa kwa wachache tu katika wizi wa EPA wote walidai kwamba muda aliotoa Rais Jakaya Kikwete kukamilika kwa suala hilo haujakwisha na ni yeye mwenye kauli ya mwisho.

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai (DCI), Robert Manumba, ambaye alitajwa na vyanzo vya habari kwamba ofisi yake ndiyo inakamilisha taratibu za kuwashitaki wahusika aliiambia Raia Mwema wiki iliyopita kwamba hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kuwa msemaji wa kikosi kazi (task force) ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, ambaye naye amenukuliwa akisema suala hilo linapaswa kuzungumziwa na Rais ambaye ndiye aliyetoa muda wa ziada.

Kauli kama hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk. Edward Hosea ambaye naye hakuwa tayari kuzungumzia hatua ambayo wamefikia katika kuwashitaki wahusika, huku Ofisa Mwandamizi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, akisema kwamba kila kitu kitajulikana siku chache zijazo.

Hata hivyo, Raia Mwema limethibitishiwa kwamba Maregesi, Mapunda na Lukaza, wanatajwa kuwa watu watakaotolewa kafara kutokana na kile kilichoelezwa kwamba wamekuwa na "jeuri ya Kiafrika" kwa kukataa kulipa fedha wanazotuhumiwa kuzichota.

Imeelezwa kwamba tokea awali watuhumiwa hao wamekuwa wakigoma 'kutoa ushirikiano' jambo ambalo limeelezwa kuwakera baadhi ya wanasiasa na watendaji wa Serikali walioamua sasa kuwaburuza mahakamani.

Raia Mwema imethibitisha kwamba bado akaunti na hati za kusafiria za watuhumiwa hao zinaendelea kushikiliwa hata baada ya muda wa miezi sita kisheria kupita kwa maelekezo ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu.

Habari zinaeleza kwamba awali watuhumiwa hao walikuwa wafikishwe mahakamani sambamba na maofisa wa BoT waliohusika katika mchakato wa EPA, lakini uamuzi huo ulibadilishwa baada ya tishio kutoka kwa watumishi hao kwamba 'wataanika' kila kitu hadharani wakitolewa kafara.

"Baada ya watumishi hao wa BoT kutishia kumwaga kila kitu hadharani, mwelekeo umebadilika na sasa wataitwa kama mashahidi wa upande wa serikali kesi hizo zitakapofikishwa mahakamani, lakini bado wanaweza kuiharibia serikali watakapoamua kutaja watu ambao wamefichwa," anasema mtoa habari wetu aliye karibu na vyombo vya dola.

Raia Mwema imefahamishwa kwamba kesi hizo zinatarajiwa kutumika kama mwavuli wa kuivusha serikali kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, kukwepa wimbi la manung'uniko ya wazi kwamba serikali ya CCM imekuwa ikiwalea watuhumiwa wa ufisadi, wengi wakiwa ni wafadhili wa chama hicho.

Wakaguzi wa ndani na wale wa nje, walibaini kuwapo kwa wizi mkubwa wa fedha katika akaunti ya EPA katika kipindi cha mwaka mmoja pekee wa 2005/2006 ambako zilipotea zaidi ya Shilingi bilioni 133.

Wakaguzi hao walibaini kwamba kati ya fedha hizo shilingi bilioni 90 ni zile ambazo zimethibitika kuchotwa kwa kutumia nyaraka za kughushi, sehemu kubwa zikiwa zimekwenda kwa wafanyabiashara wawili, wamiliki halisi wa Kagoda Agricultural Limited na Jeetu Patel kupitia kampuni zake nane.

Ripoti ya Wakaguzi wa Kampuni ya Ernst and Young waliofanya kazi kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ilionyesha kwamba kiasi cha Shilingi 90,359,078,804.00 zililipwa kwa kampuni 13 ambazo zilitumia kumbukumbu, nyaraka na hati zilizo batili na za kugushi na kwamba kampuni hizo hazikustahili kulipwa chochote.

Wakaguzi hao na Ikulu, kupitia taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wake, Philemon Luhanjo, Januari 9, 2008, walipendekeza moja kwa moja bila kuuma maneno kwamba wahusika wa kampuni hizo 13 wachukuliwe hatua za kisheria mara moja, kauli ambayo Rais Kikwete aliirejea katika hotuba yake bungeni, lakini bila ukali tena.

Makampuni ambayo Jeetu Patel anahusika nayo na ambayo yamethibitika kughushi nyaraka na kuchota fedha BoT ni Navycut Tobacco (T) Limited, Ndovu Soaps Limited, Bina Resorts Limited, Bencon International Limited, Maltan Mining Company Limited, Bora Hotels & Apartments Limited, Venus Hotels Limited, and B.V. Holdings Limited.

Pamoja na kampuni hizo za Jeetu Patel, kampuni nyingine zilizohusika na jinai ya kughushi nyaraka ni pamoja na Kagoda Agriculture Limited ambayo wanaoonekana katika nyaraka ni John Kyomuhendo mwenye hisa 40 na Francis William anayemiliki hisa 60 katika kampuni hiyo.

Kampuni nyingine ni V.B & Associeties Company zinazomilikiwa na Devendra Patel na Jantkumar Chandubhai Patel na Changanyikeni Residential Complex Limited inayomilikiwa na Jose Van de Merwe, Samson Mapunda na Charles Mabina ikiwa na makao yake, Sinza, Kumekucha, Dar es Salaam.

Pia katika orodha hiyo ya kampuni 13 zilizoghushi nyaraka ambazo wahusika wake wamependekezwa kuchukuliwa hatua za kisheria mara moja ni Money Planners & Consultants inayomilikiwa na Paul Nyingo na Fundi Kitungi na kampuni ya Njake Hotel & Tours Limited inayomilikiwa Japhet Lema, Anna Lema, Abel Lema, Derick Lema na Benard Lema wa Arusha.

Jeetu Patel katika baadhi ya kampuni anashirikiana na wafanyabiashara wengine wa Dar es Salaam ambao wanatajwa kushiriana naye katika kuhamisha fedha hizo kwenda nje kwa kuzibadili kutoka shilingi za Kitanzania kwenda Dola za Merakani ama Euro bila kufuata mkondo halali wa fedha kinyume cha Sheria ya Udhibiti wa Fedha Haramu.

Miongoni mwa wanaotajwa kushirikiana na Jeetu Patel ni Sidik Yacoubu kupitia kampuni yao ya Ndovu Soap Limited ambayo kwa mujibu wa nyaraka za Wakala wa Leseni na Usajili wa Kampuni (BRELA), kampuni hiyo yenye namba ya usajili 20536 ya Februari 3, 1992, wamiliki wake ni Jayantulal Chandubhai Patel na Sidik Yacoubu.

Katika kampuni ya Bora Hotels and Apartments iliyosajiliwa Septemba 8, 2005 inaonyeshwa katika orodha ya BRELA kwamba wamiliki wake wamo Jayantkumar Chandubhai Patel na Devandra Patel wakati Bina Resort Limited iliyosajiliwa Machi 31, 2005, wamo Jayantikumar Chandubhai Patel na Devendra Patel.

Kampuni ya Maltan Mining Company iliyosajiliwa Machi 8, 1993 inamilikiwa na Jantkumar Chandubhai Patel na Hariharier Radhakrishna wakati Navy Cut Tobacco iliyosajiliwa Oktoba 12, mwaka 1995 inamilikiwa na Jantkumar Chandubhai Patel na Radakrishna.

Kampuni nyingine ni Bencon Limited, B.V Holdings, Venus Hotels na V.B & Associeties Company zinazomilikiwa na Devendra Patel na Jantkumar Chandubhai Patel, ambazo zote zilisajiliwa Aprili 4, 2005.

Katika orodha ya BRELA imo pia kampuni ya Excellent Service Limited inayomilikiwa na Emil Samanya, Peter Sabas na Elisifa Ngowi ambaye anatajwa kuwa ni Ofisa Mwandamizi wa Idara ya Usalama wa Taifa, ambaye yumo katika task force inayochunguza wizi huo. Kampuni hiyo ilisajiliwa Mei 13, 1992 na kupewa namba 26959.

Ngowi anahusishwa pia katika kampuni nyingine ya Clyton Marketing iliyosajiliwa Juni 6, 2005 akiwa na mwenzake Edwin Mtoi, ambaye haikuweza kufahamika mara moja anafanya shughuli gani zaidi ya kuwa katika kampuni hiyo.

Wamiliki wengine waliofahamika ni Rajabu Maranda na Thabit Katunda ambao wanatajwa kumiliki kampuni ya Liqiud Service Limited ambayo usajili wake ulifanyika Desemba 12, 2004 na kupewa namba 15007.

Wamiliki wengine waliofahamika ni Johnson Lukaza na Mwesigwa Rutakyamilwa Lukaza ambao wao wanamiliki kampuni ya Karnel Meals Holdings Ltd ambayo usajili wake ulipatikana Agosti 4, 1998, Mibale Farm iliyosajiliwa Septemba 2, 2005 na kupewa namba 154039 ambayo inamilikiwa na Kizza Selemani na Farijala Hussein, Malegesi Law Chambers inayomilikiwa na Beredy Malegesi ambayo ilisajiliwa Septemba 24, 2001.

Wamiliki wengine ni Paul Nyingo na Fundi Kitungi, wanaomiliki Kampuni ya Money Planners & Consultants iliyosajiliwa Machi 22, 2005 na Kiloloma & Bros Enterprises inayomilikiwa na Charies Kissa, ambayo ilisajiliwa Aprili 8, 2005.

Katika ukusanyaji wa fedha hizo, task force ya serikali inaelezwa kukusanya shilingi 53,738,835,392/= fedha ambazo Rais Kikwete ameagiza ziingizwe katika mfuko maalumu kwa ajili ya kusaidia sekta ya kilimo zikichanganywa na nyingine zinazotarajiwa kufikia shilingi 64,844,770,688/= .
 
Wakuu,

JK will be addressing the nation later today and (WE) hope all the HOT issues will be addressed effectively! I'm sure Kagoda will feature somewhere in that SPEECH!
 
Wakuu,

JK will be addressing the nation later today and (WE) hope all the HOT issues will be addressed effectively! I'm sure Kagoda will feature somewhere in that SPEECH!

Atasema ameombwa aongeze muda kwa timu ya EPA maana hadi sasa wamekusanya fedha zaidi.
 
Siri mpya ya EPA yaiumbua Kagoda

Mwandishi Wetu, Raia Mwema.
Novemba 12, 2008

WAKATI watuhumiwa 20 wakiwa, hadi juzi, wamekwisha kupandishwa kizimbani kwa tuhuma za kuhusika na wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu (BoT), ushahidi mpya umeibuliwa unaoonyesha kwamba kampuni ya Kagoda Agricultural Limited, ambayo wahusika wake bado hawajashitakiwa, ilikuwa ya kwanza kuchota mapesa hayo zaidi ya miaka minane iliyopita.

Uchunguzi wa muda mrefu wa Raia Mwema umethibitisha kuwapo kwa uhusiano mkubwa kati ya kampuni ya Afritainer (T) Limited na kampuni ya Kagoda Agricultural Limited ambayo hadi sasa wahusika wake na mahali ilipo ni kitendawili.

Kampuni ya Afritainer ilifanikiwa kuchota zaidi ya Shilingi bilioni 12 za EPA kwa kutumia nyaraka zilizosainiwa na watumishi wa kampuni moja maarufu ya Dar es Salaam (jina tunalo) wakidaiwa kuwa wakurugenzi wa kampuni hiyo kabla ya kufahamika kwamba hawakuwa wakurugenzi halali kisheria.

Kagoda, ambayo ilitumia nyaraka za kughushi, ilichotewa mabilioni hayo ya fedha kabla haijasajiliwa na katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2005. Hadi sasa hakuna taarifa rasmi zinazoonyesha watu waliorejesha fedha za EPA kwa jina la Kagoda pamoja na kuwapo taarifa za uhakika kuhusiana na wafanyabiashara wazito waliorejesha fedha hizo kwa nyakati tofauti kabla ya muda uliowekwa kwisha Oktoba 31, 2008.

Nyaraka zilizotumiwa na Afritainer kuchota mabilioni ya fedha za EPA mwaka 2000 zinaonyesha kwamba kampuni hiyo imetumia namba za simu 2861371 na 2861372 ambazo pia ndizo zimetumiwa na Kagoda katika kuchota fedha za EPA mwaka 2005. Namba hizo zinaonekana katika nyaraka za kampuni nyingine yenye uhusiano na wamiliki wa Afritainer.

Nyaraka kutoka Wakala wa Usajili wa Makampuni na Leseni (BRELA) zinaonyesha kwamba Tabu Omari Masula na Barati A. Goda, walidaiwa kuingizwa kuwa wakurugenzi wa kampuni hiyo Mei 15, 2000 kinyume cha sheria.

Barua ya BRELA ya Februarin 18, 2002, miaka miwili baada ya Tabu na Barati kuchota fedha za EPA, ilieleza kwamba wakurugenzi hao hawakuwa halali kutokana na kutokuwa na hisa katika kampuni ya Afritainer.

Kwa mujibu wa barua hiyo kwenda kwa kampuni ya mawakili ya M.A.Imail, Tabu na Barati walikiuka kifungu cha 50 cha hati ya usajili ya kampuni hiyo kinachomlazimu mkurugenzi kuwa na hisa katika kampuni kwanza ili aweze kuwa na maamuzi.

Waraka wa Afritainer uliowasilishwa BRELA Mei 15, 2000, ulieleza kwamba wakurugenzi pekee na waazilishi wa Afritainer ni Bahram Abdurasul Chakaar na Gulam Abdurasul Chakaar, wamejiuzulu ukurugenzi na kuwaachia Tabu na Barat.

Hata hivyo, BRELA katika barua ya Februari 18, 2002 iliyoandikwa na Msajili Msaidizi wa wakala huo, L. Kimaro, ilieleza wazi kwamba hadi wakati huo ubadilishaji wa wakurugenzi haukuwa umeidhinishwa kutokana na kutokufuata masharti ya usajili.

Tabu anatajwa kufanya kazi katika kampuni moja ya jijini Dar es Salaam yenye ofisi zake eneo la viwanda barabara ya Nyerere na Upanga.

Kwa mujibu wa habari ambazo Raia Mwema imezipata fedha hizo kiasi cha Sh. Bilioni 13 zilichukuliwa Agosti 2000 kabla ya uchaguzi wa pili wa vyama vingi ambao Benjamin Mkapa aligombea tena urais.

Waidhinishaji wakuu wa mikataba ya uchukuaji wa fedha hizo walikuwa ni mawakili maarufu wa kampuni ya uwakili ya Law Associates chini ya mkuu wake Dk. Ringo Tenga. Dk. Tenga sasa ni mwanasheria wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Nyaraka za uchukuaji wa fedha hizo mwaka 2000 zinaonyesha kwamba benki ya Akiba Bank ilitumika kupitishia fedha hizo kutokea BoT.


Haikuweza kufahamika mara moja kama vyombo vya dola vimefanikisha kupata nyaraka husika, pamoja na kuwapo taarifa kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ilikwishachunguza nyaraka hizo ikiwa ni pamoja na kuwahoji watumishi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kuhusiana na na matumizi ya namba za simu 2861372 na fax zilizotumiwa na kampuni ya Afritainer na Kagoda Agricultural.

Kwa sasa wafuatiliaji wa sakata la EPA wanasubiri wahusika wa kampuni ya Kagoda Agricultural Limited iliyochota Sh bilioni 40 kufikishwa mahakamani baada ya kufikishwa kwa watuhumiwa wengine 20 hadi sasa.

Tayari inafahamika kwamba kati ya shilingi bilioni 90 zilizoibwa katika akaunti ya EPA, sehemu kubwa ilichukuliwa na kampuni ya Kagoda Agricultural Limited ambayo hadi sasa wahusika wake hawajaguswa pamoja na kujitokeza kwa vigogo wawili kurejesha fedha zilizoibwa na kampuni hiyo.

Vyanzo vya uhakika vinaeleza kwamba sehemu kubwa ya Shilingi bilioni 90 zilizothibitika kuchukuliwa kihalifu zilichukuliwa na makundi mawili tu, kundi la kwanza likiwa chini ya Jeetu Patel na lingine likiwa chini ya usimamizi wa vigogo wawili waliotumia kampuni ya Kagoda.

Imefahamika kwamba kwa sasa kuna hekaheka kubwa za kutaka kuzuia kushitakiwa kwa wahusika wa Kagoda, lakini vyanzo vya ndani ya serikali vimeeleza kwamba kwa sasa serikali haitabiriki na lolote linaweza kutokea wakati wowote kabla ya mwisho wa mwaka.

Kumekuwa na utata kuhusiana na ilipo na umiliki wa Kagoda Agricultural Limited ambayo imethibitika kujichotea kiasi cha Dola za Marekani 30,732,658.82 (zaidi ya Sh Bilioni 40/-) kutoka akaunti ya EPA na hakuna anayeweza kubainisha hasa zilipo ofisi na wahusika wa kampuni hiyo tata.

Kumbukumbu za BRELA zinaonyesha kwamba ofisi zake zipo Kipawa Industrial Area Plot namba 87, Temeke, Dar es Salaam lakini eneo hilo lina makampuni tofauti jirani lakini namba iliyotajwa haionekani na badala yake eneo lenye ofisi na kampuni viwanja vyenye namba 77, 86 na 88 katika eneo hilo la viwanda.

Katika ukaguzi wake wa awali wa mkaguzi wa nje Samuel Sithole kutoka kampuni ya Kimataifa ya Deloitte & Touche yenye makao yake Afrika Kusini alionya kuhusu matendo ya kihalifu ndani ya Kagoda kabla ya kuandikiwa barua na Waziri wa Fedha, Zakia Meghji kwamba fedha hizo zilienda katika mambo "nyeti" ya kiusalama.

Hata hivyo siku nne baada ya kuandika barua hiyo, Meghji alifuta barua hiyo akielezea kupotoshwa na aliyekua Gavana, Dk. Daudi Ballali, uamuzi ambao ulimgharimu kwa kiasi kikubwa mwanamama huyo makini ambaye alijikuta akiachwa nje ya Baraza la Mawaziri.

Jamani tunaliwa na wenye meno !! Masikini Tanzania !! Je huyu ndiye Tenga wa Richmond AU ?
 
30.jpg


Hivi Dr. Ringo Tenga ni nani Tanzania ??
 
Siri mpya ya EPA yaiumbua Kagoda

Mwandishi Wetu Novemba 12, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

WAKATI watuhumiwa 20 wakiwa, hadi juzi, wamekwisha kupandishwa kizimbani kwa tuhuma za kuhusika na wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu (BoT), ushahidi mpya umeibuliwa unaoonyesha kwamba kampuni ya Kagoda Agricultural Limited, ambayo wahusika wake bado hawajashitakiwa, ilikuwa ya kwanza kuchota mapesa hayo zaidi ya miaka minane iliyopita.

Uchunguzi wa muda mrefu wa Raia Mwema umethibitisha kuwapo kwa uhusiano mkubwa kati ya kampuni ya Afritainer (T) Limited na kampuni ya Kagoda Agricultural Limited ambayo hadi sasa wahusika wake na mahali ilipo ni kitendawili.

Kampuni ya Afritainer ilifanikiwa kuchota zaidi ya Shilingi bilioni 12 za EPA kwa kutumia nyaraka zilizosainiwa na watumishi wa kampuni moja maarufu ya Dar es Salaam (jina tunalo) wakidaiwa kuwa wakurugenzi wa kampuni hiyo kabla ya kufahamika kwamba hawakuwa wakurugenzi halali kisheria.

Kagoda, ambayo ilitumia nyaraka za kughushi, ilichotewa mabilioni hayo ya fedha kabla haijasajiliwa na katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2005. Hadi sasa hakuna taarifa rasmi zinazoonyesha watu waliorejesha fedha za EPA kwa jina la Kagoda pamoja na kuwapo taarifa za uhakika kuhusiana na wafanyabiashara wazito waliorejesha fedha hizo kwa nyakati tofauti kabla ya muda uliowekwa kwisha Oktoba 31, 2008.

Nyaraka zilizotumiwa na Afritainer kuchota mabilioni ya fedha za EPA mwaka 2000 zinaonyesha kwamba kampuni hiyo imetumia namba za simu 2861371 na 2861372 ambazo pia ndizo zimetumiwa na Kagoda katika kuchota fedha za EPA mwaka 2005. Namba hizo zinaonekana katika nyaraka za kampuni nyingine yenye uhusiano na wamiliki wa Afritainer.

Nyaraka kutoka Wakala wa Usajili wa Makampuni na Leseni (BRELA) zinaonyesha kwamba Tabu Omari Masula na Barati A. Goda, walidaiwa kuingizwa kuwa wakurugenzi wa kampuni hiyo Mei 15, 2000 kinyume cha sheria.

Barua ya BRELA ya Februarin 18, 2002, miaka miwili baada ya Tabu na Barati kuchota fedha za EPA, ilieleza kwamba wakurugenzi hao hawakuwa halali kutokana na kutokuwa na hisa katika kampuni ya Afritainer.

Kwa mujibu wa barua hiyo kwenda kwa kampuni ya mawakili ya M.A.Imail, Tabu na Barati walikiuka kifungu cha 50 cha hati ya usajili ya kampuni hiyo kinachomlazimu mkurugenzi kuwa na hisa katika kampuni kwanza ili aweze kuwa na maamuzi.

Waraka wa Afritainer uliowasilishwa BRELA Mei 15, 2000, ulieleza kwamba wakurugenzi pekee na waazilishi wa Afritainer ni Bahram Abdurasul Chakaar na Gulam Abdurasul Chakaar, wamejiuzulu ukurugenzi na kuwaachia Tabu na Barat.

Hata hivyo, BRELA katika barua ya Februari 18, 2002 iliyoandikwa na Msajili Msaidizi wa wakala huo, L. Kimaro, ilieleza wazi kwamba hadi wakati huo ubadilishaji wa wakurugenzi haukuwa umeidhinishwa kutokana na kutokufuata masharti ya usajili.

Tabu anatajwa kufanya kazi katika kampuni moja ya jijini Dar es Salaam yenye ofisi zake eneo la viwanda barabara ya Nyerere na Upanga.

Kwa mujibu wa habari ambazo Raia Mwema imezipata fedha hizo kiasi cha Sh. Bilioni 13 zilichukuliwa Agosti 2000 kabla ya uchaguzi wa pili wa vyama vingi ambao Benjamin Mkapa aligombea tena urais.

30.jpg

Dk. Ringo Tenga

Waidhinishaji wakuu wa mikataba ya uchukuaji wa fedha hizo walikuwa ni mawakili maarufu wa kampuni ya uwakili ya Law Associates chini ya mkuu wake Dk. Ringo Tenga. Dk. Tenga sasa ni mwanasheria wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Nyaraka za uchukuaji wa fedha hizo mwaka 2000 zinaonyesha kwamba benki ya Akiba Bank ilitumika kupitishia fedha hizo kutokea BoT.

Haikuweza kufahamika mara moja kama vyombo vya dola vimefanikisha kupata nyaraka husika, pamoja na kuwapo taarifa kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ilikwishachunguza nyaraka hizo ikiwa ni pamoja na kuwahoji watumishi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kuhusiana na na matumizi ya namba za simu 2861372 na fax zilizotumiwa na kampuni ya Afritainer na Kagoda Agricultural.

Kwa sasa wafuatiliaji wa sakata la EPA wanasubiri wahusika wa kampuni ya Kagoda Agricultural Limited iliyochota Sh bilioni 40 kufikishwa mahakamani baada ya kufikishwa kwa watuhumiwa wengine 20 hadi sasa.

Tayari inafahamika kwamba kati ya shilingi bilioni 90 zilizoibwa katika akaunti ya EPA, sehemu kubwa ilichukuliwa na kampuni ya Kagoda Agricultural Limited ambayo hadi sasa wahusika wake hawajaguswa pamoja na kujitokeza kwa vigogo wawili kurejesha fedha zilizoibwa na kampuni hiyo.

Vyanzo vya uhakika vinaeleza kwamba sehemu kubwa ya Shilingi bilioni 90 zilizothibitika kuchukuliwa kihalifu zilichukuliwa na makundi mawili tu, kundi la kwanza likiwa chini ya Jeetu Patel na lingine likiwa chini ya usimamizi wa vigogo wawili waliotumia kampuni ya Kagoda.

Imefahamika kwamba kwa sasa kuna hekaheka kubwa za kutaka kuzuia kushitakiwa kwa wahusika wa Kagoda, lakini vyanzo vya ndani ya serikali vimeeleza kwamba kwa sasa serikali haitabiriki na lolote linaweza kutokea wakati wowote kabla ya mwisho wa mwaka.

Kumekuwa na utata kuhusiana na ilipo na umiliki wa Kagoda Agricultural Limited ambayo imethibitika kujichotea kiasi cha Dola za Marekani 30,732,658.82 (zaidi ya Sh Bilioni 40/-) kutoka akaunti ya EPA na hakuna anayeweza kubainisha hasa zilipo ofisi na wahusika wa kampuni hiyo tata.

Kumbukumbu za BRELA zinaonyesha kwamba ofisi zake zipo Kipawa Industrial Area Plot namba 87, Temeke, Dar es Salaam lakini eneo hilo lina makampuni tofauti jirani lakini namba iliyotajwa haionekani na badala yake eneo lenye ofisi na kampuni viwanja vyenye namba 77, 86 na 88 katika eneo hilo la viwanda.

Katika ukaguzi wake wa awali wa mkaguzi wa nje Samuel Sithole kutoka kampuni ya Kimataifa ya Deloitte & Touche yenye makao yake Afrika Kusini alionya kuhusu matendo ya kihalifu ndani ya Kagoda kabla ya kuandikiwa barua na Waziri wa Fedha, Zakia Meghji kwamba fedha hizo zilienda katika mambo "nyeti" ya kiusalama.

Hata hivyo siku nne baada ya kuandika barua hiyo, Meghji alifuta barua hiyo akielezea kupotoshwa na aliyekua Gavana, Dk. Daudi Ballali, uamuzi ambao ulimgharimu kwa kiasi kikubwa mwanamama huyo makini ambaye alijikuta akiachwa nje ya Baraza la Mawaziri.

Wakati Rais Jakaya Kikwete akisema serikali yake haitomuingilia Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), watuhumiwa wengi walikamatwa na kufikishwa mahakamani walikuwa wamejiaminisha kuwa wamekwishapona na sasa waliobaki "hawalali" kuhofia kushitukizwa na kupandishwa kizimbani.

Tayari watu 20 wamekwisha kufikishwa mahakamani baada ya wafanyabiashara watatu kufikishwa mahakamani Jumatatu wiki hii wakitanguliwa na watuhumiwa wengine wakiwamo watumishi wa BoT waliohusika katika mchakato wa wizi huo.

Waliopandishwa kizimbani Jumatatu ni Ajay Somani na Jai Somani wanaodaiwa kula njama ya wizi wakiwa na watu wengine ambao hawajafahamika kuiibia BoT na kwamba Septemba 2, 2005 waliiba Sh. bilioni 5.9 mali ya benki hiyo.

Mtuhumiwa mwingine aliyefikishwa Jumatatu ni mfanyabiashara Mwesiga Lukaza, aliyepandishwa kizimbani akiunganishwa na mshtakiwa mwingine Johnson Lukaza, ambaye alishapandishwa kizimbani mapema wiki hii.

26.jpg

Watuhumiwa wa wizi wa EPA

Watuhumiwa wengine ambao tayari wamefikishwa mahakamani ni Farijala Hussein, Rajab Maranda, Japhet Lema, Bahati Mahenge, Davis Kamungu, Godfrey Mosha, Manase Mwakale na Eddah Mwakale, Devendra Vinodbhai Patel, Amit Nandy, Ketan Chohan, Jayantkumar Chandubahi Patel na Johnson Lukaza.

Wengine ni wafanyakazi wa BoT ambao ni Mkuu wa Idara ya Madeni ya Biashara, Iman David Mwakyosa, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Madeni, Ester Mary Komu na makaimu Katibu wa benki wawili ambao ni Bosco Ndimbo Kimela na Sofia Joseph Lakila.

Kati ya watuhumiwa hao, ni wawili tu ambao wako nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana hiyo ambao ni Godfrey Mosha na Davis Kamungu. Washitakiwa wengine licha ya dhamana zao kuwa wazi, wanaendelea kusota rumande kutokana na kushindwa kutimiza masharti.
 
Siri mpya ya EPA yaiumbua Kagoda

Mwandishi Wetu Novemba 12, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

WAKATI watuhumiwa 20 wakiwa, hadi juzi, wamekwisha kupandishwa kizimbani kwa tuhuma za kuhusika na wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu (BoT), ushahidi mpya umeibuliwa unaoonyesha kwamba kampuni ya Kagoda Agricultural Limited, ambayo wahusika wake bado hawajashitakiwa, ilikuwa ya kwanza kuchota mapesa hayo zaidi ya miaka minane iliyopita.

Uchunguzi wa muda mrefu wa Raia Mwema umethibitisha kuwapo kwa uhusiano mkubwa kati ya kampuni ya Afritainer (T) Limited na kampuni ya Kagoda Agricultural Limited ambayo hadi sasa wahusika wake na mahali ilipo ni kitendawili.

Kampuni ya Afritainer ilifanikiwa kuchota zaidi ya Shilingi bilioni 12 za EPA kwa kutumia nyaraka zilizosainiwa na watumishi wa kampuni moja maarufu ya Dar es Salaam (jina tunalo) wakidaiwa kuwa wakurugenzi wa kampuni hiyo kabla ya kufahamika kwamba hawakuwa wakurugenzi halali kisheria.

Kagoda, ambayo ilitumia nyaraka za kughushi, ilichotewa mabilioni hayo ya fedha kabla haijasajiliwa na katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2005. Hadi sasa hakuna taarifa rasmi zinazoonyesha watu waliorejesha fedha za EPA kwa jina la Kagoda pamoja na kuwapo taarifa za uhakika kuhusiana na wafanyabiashara wazito waliorejesha fedha hizo kwa nyakati tofauti kabla ya muda uliowekwa kwisha Oktoba 31, 2008.

Nyaraka zilizotumiwa na Afritainer kuchota mabilioni ya fedha za EPA mwaka 2000 zinaonyesha kwamba kampuni hiyo imetumia namba za simu 2861371 na 2861372 ambazo pia ndizo zimetumiwa na Kagoda katika kuchota fedha za EPA mwaka 2005. Namba hizo zinaonekana katika nyaraka za kampuni nyingine yenye uhusiano na wamiliki wa Afritainer.

Nyaraka kutoka Wakala wa Usajili wa Makampuni na Leseni (BRELA) zinaonyesha kwamba Tabu Omari Masula na Barati A. Goda, walidaiwa kuingizwa kuwa wakurugenzi wa kampuni hiyo Mei 15, 2000 kinyume cha sheria.

Barua ya BRELA ya Februarin 18, 2002, miaka miwili baada ya Tabu na Barati kuchota fedha za EPA, ilieleza kwamba wakurugenzi hao hawakuwa halali kutokana na kutokuwa na hisa katika kampuni ya Afritainer.

Kwa mujibu wa barua hiyo kwenda kwa kampuni ya mawakili ya M.A.Imail, Tabu na Barati walikiuka kifungu cha 50 cha hati ya usajili ya kampuni hiyo kinachomlazimu mkurugenzi kuwa na hisa katika kampuni kwanza ili aweze kuwa na maamuzi.

Waraka wa Afritainer uliowasilishwa BRELA Mei 15, 2000, ulieleza kwamba wakurugenzi pekee na waazilishi wa Afritainer ni Bahram Abdurasul Chakaar na Gulam Abdurasul Chakaar, wamejiuzulu ukurugenzi na kuwaachia Tabu na Barat.

Hata hivyo, BRELA katika barua ya Februari 18, 2002 iliyoandikwa na Msajili Msaidizi wa wakala huo, L. Kimaro, ilieleza wazi kwamba hadi wakati huo ubadilishaji wa wakurugenzi haukuwa umeidhinishwa kutokana na kutokufuata masharti ya usajili.

Tabu anatajwa kufanya kazi katika kampuni moja ya jijini Dar es Salaam yenye ofisi zake eneo la viwanda barabara ya Nyerere na Upanga.

Kwa mujibu wa habari ambazo Raia Mwema imezipata fedha hizo kiasi cha Sh. Bilioni 13 zilichukuliwa Agosti 2000 kabla ya uchaguzi wa pili wa vyama vingi ambao Benjamin Mkapa aligombea tena urais.

30.jpg

Dk. Ringo Tenga

Waidhinishaji wakuu wa mikataba ya uchukuaji wa fedha hizo walikuwa ni mawakili maarufu wa kampuni ya uwakili ya Law Associates chini ya mkuu wake Dk. Ringo Tenga. Dk. Tenga sasa ni mwanasheria wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Nyaraka za uchukuaji wa fedha hizo mwaka 2000 zinaonyesha kwamba benki ya Akiba Bank ilitumika kupitishia fedha hizo kutokea BoT.

Haikuweza kufahamika mara moja kama vyombo vya dola vimefanikisha kupata nyaraka husika, pamoja na kuwapo taarifa kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ilikwishachunguza nyaraka hizo ikiwa ni pamoja na kuwahoji watumishi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kuhusiana na na matumizi ya namba za simu 2861372 na fax zilizotumiwa na kampuni ya Afritainer na Kagoda Agricultural.

Kwa sasa wafuatiliaji wa sakata la EPA wanasubiri wahusika wa kampuni ya Kagoda Agricultural Limited iliyochota Sh bilioni 40 kufikishwa mahakamani baada ya kufikishwa kwa watuhumiwa wengine 20 hadi sasa.

Tayari inafahamika kwamba kati ya shilingi bilioni 90 zilizoibwa katika akaunti ya EPA, sehemu kubwa ilichukuliwa na kampuni ya Kagoda Agricultural Limited ambayo hadi sasa wahusika wake hawajaguswa pamoja na kujitokeza kwa vigogo wawili kurejesha fedha zilizoibwa na kampuni hiyo.

Vyanzo vya uhakika vinaeleza kwamba sehemu kubwa ya Shilingi bilioni 90 zilizothibitika kuchukuliwa kihalifu zilichukuliwa na makundi mawili tu, kundi la kwanza likiwa chini ya Jeetu Patel na lingine likiwa chini ya usimamizi wa vigogo wawili waliotumia kampuni ya Kagoda.

Imefahamika kwamba kwa sasa kuna hekaheka kubwa za kutaka kuzuia kushitakiwa kwa wahusika wa Kagoda, lakini vyanzo vya ndani ya serikali vimeeleza kwamba kwa sasa serikali haitabiriki na lolote linaweza kutokea wakati wowote kabla ya mwisho wa mwaka.

Kumekuwa na utata kuhusiana na ilipo na umiliki wa Kagoda Agricultural Limited ambayo imethibitika kujichotea kiasi cha Dola za Marekani 30,732,658.82 (zaidi ya Sh Bilioni 40/-) kutoka akaunti ya EPA na hakuna anayeweza kubainisha hasa zilipo ofisi na wahusika wa kampuni hiyo tata.

Kumbukumbu za BRELA zinaonyesha kwamba ofisi zake zipo Kipawa Industrial Area Plot namba 87, Temeke, Dar es Salaam lakini eneo hilo lina makampuni tofauti jirani lakini namba iliyotajwa haionekani na badala yake eneo lenye ofisi na kampuni viwanja vyenye namba 77, 86 na 88 katika eneo hilo la viwanda.

Katika ukaguzi wake wa awali wa mkaguzi wa nje Samuel Sithole kutoka kampuni ya Kimataifa ya Deloitte & Touche yenye makao yake Afrika Kusini alionya kuhusu matendo ya kihalifu ndani ya Kagoda kabla ya kuandikiwa barua na Waziri wa Fedha, Zakia Meghji kwamba fedha hizo zilienda katika mambo "nyeti" ya kiusalama.

Hata hivyo siku nne baada ya kuandika barua hiyo, Meghji alifuta barua hiyo akielezea kupotoshwa na aliyekua Gavana, Dk. Daudi Ballali, uamuzi ambao ulimgharimu kwa kiasi kikubwa mwanamama huyo makini ambaye alijikuta akiachwa nje ya Baraza la Mawaziri.

Wakati Rais Jakaya Kikwete akisema serikali yake haitomuingilia Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), watuhumiwa wengi walikamatwa na kufikishwa mahakamani walikuwa wamejiaminisha kuwa wamekwishapona na sasa waliobaki "hawalali" kuhofia kushitukizwa na kupandishwa kizimbani.

Tayari watu 20 wamekwisha kufikishwa mahakamani baada ya wafanyabiashara watatu kufikishwa mahakamani Jumatatu wiki hii wakitanguliwa na watuhumiwa wengine wakiwamo watumishi wa BoT waliohusika katika mchakato wa wizi huo.

Waliopandishwa kizimbani Jumatatu ni Ajay Somani na Jai Somani wanaodaiwa kula njama ya wizi wakiwa na watu wengine ambao hawajafahamika kuiibia BoT na kwamba Septemba 2, 2005 waliiba Sh. bilioni 5.9 mali ya benki hiyo.

Mtuhumiwa mwingine aliyefikishwa Jumatatu ni mfanyabiashara Mwesiga Lukaza, aliyepandishwa kizimbani akiunganishwa na mshtakiwa mwingine Johnson Lukaza, ambaye alishapandishwa kizimbani mapema wiki hii.

26.jpg

Watuhumiwa wa wizi wa EPA

Watuhumiwa wengine ambao tayari wamefikishwa mahakamani ni Farijala Hussein, Rajab Maranda, Japhet Lema, Bahati Mahenge, Davis Kamungu, Godfrey Mosha, Manase Mwakale na Eddah Mwakale, Devendra Vinodbhai Patel, Amit Nandy, Ketan Chohan, Jayantkumar Chandubahi Patel na Johnson Lukaza.

Wengine ni wafanyakazi wa BoT ambao ni Mkuu wa Idara ya Madeni ya Biashara, Iman David Mwakyosa, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Madeni, Ester Mary Komu na makaimu Katibu wa benki wawili ambao ni Bosco Ndimbo Kimela na Sofia Joseph Lakila.

Kati ya watuhumiwa hao, ni wawili tu ambao wako nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana hiyo ambao ni Godfrey Mosha na Davis Kamungu. Washitakiwa wengine licha ya dhamana zao kuwa wazi, wanaendelea kusota rumande kutokana na kushindwa kutimiza masharti.


Kazi kweli kweli. Sasa Mkono walimtoa kwa sababu ya harufu ya EPA mikononi mwake, sasa na huyu Dr. Tenga sijui itakuwaje? Hiyo Public Procurement ya kumpa mtu kandarasi ya kutoa huduma ya sheria huwa inatolewaje? make Public Procurement Act, inasema lazima itangazwe, Naomba nielimishwe kuhusu hili Je hawa 'jamaa' wa Benki Kuu huwa wanafuata sheria?

Yes we can ....
 
Hosea: Tukiwashtaki watuhumiwa wote wa ufisadi, nchi itayumba

MKURUGENZI wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah akizungumza jambo na waandishi wa habari ....

Exuper Kachenje

MKURUGENZI wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah, amesema kuwa kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wote wa ufisadi kwa pamoja kunaweza kusababisha nchi kuyumba.

Hoseah alisema hayo katika siku ambayo hakukuwa na mtuhumiwa yeyote katika sakata la wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) aliyefikishwa mahakamani baada ya wafanyabiashara 20 kupandishwa mfululizo kizimbani kuanzia Jumatano iliyopita hadi juzi.

Akitoa mada kwenye semina iliyohusisha vyuo vikuu tisa nchini iliyofanyika kwenye Hoteli ya Blue Pearl jijini, mkurugenzi huyo wa Takukuru alisema: "Tukiwapeleka wote mara moja mahakamani, nchi inaweza 'ikaparalyse' (ikapooza) ni lazima kuwe na 'stability' (kutoyumba), tufanye kwa kuwa ni sahihi," alisema Hoseah.

Akitoa mada katika semina hiyo iliyowahusisha wajumbe wa kamati za maadili kutoka vyuo hivyo, Hoseah alieleza kuwa, mapambano dhidi ya rushwa kubwa yanapaswa kufanyika kukiwa na utashi wenye nguvu wa kisiasa, mikakati sahihi ya kiuchumi pamoja na kuzuia rushwa.

Alisema kuwa watuhumiwa wa rushwa kubwa wana nguvu kutokana na fedha nyingi wanazomiliki, kiasi cha kuweza kuhatarisha usalama wa watu wengine kwa kutumia vibaya fedha zao.

Dk Hoseah ni kigogo wa tatu kuzungumzia uwezo wa mafisadi na hatari ya kuwashughulikia bila ya umakini baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kulieleza bunge kuwa, kushughulikia watu wenye uwezo wa kifedha ni kazi ngumu, kama ilivyoelezwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Ali Hassan Mwinyi kuwa mafisadi ni hatari.

Watuhumiwa katika kashfa hiyo ya EPA wanadaiwa kuchota fedha hizo katika kipindi cha mwaka 2005/06 wakisingizia kupewa au kulipa madeni na makampuni ya nje yaliyokuwa yakiidai serikali. Watuhumiwa hao wanadaiwa kuchota Sh133 bilioni.

Pamoja na kilio cha wananchi kuwa wote waliochota fedha hizo wapandishwe kizimbani, Rais Jakaya Kikwete alitoa maagizo kuwa wale ambao wangeshindwa kurejesha fedha walizochota kabla ya Oktoba 31, ndio waliotakiwa kufikishwa mahakamani.

Na watuhumiwa hao 20 waliofikishwa mahakamani hadi sasa wamekuwa wakipandishwa kizimbani kwa nyakati tofauti na wengi wameshtakiwa kwa makosa tofauti, wakipandishwa mmoja mmoja na wakati mwingine kuunganishwa na wenzao na kwa mahakimu tofauti.

Akitoa mada yake jana, Dk Hosea alisema Takukuru peke yake haiwezi kumaliza tatizo la rushwa nchini bila kuwepo ushirikiano kutoka kwa taasisi za elimu, mashirika mbalimbali na wananchi.

Aliongeza kuwa, mapambano dhidi ya rushwa, kubwa na ndogo yanapaswa kuwashirikisha wananchi wote, huku akielezea Watanzania kuwa ni waoga kutokana na kukosa ufahamu wa masuala mbalimbali yanayowahusu.

Hoseah alisema kuwa katika mapambano ya rushwa ni vema kuzuia rushwa na kwamba uadilifu ndiyo njia bora ya kulitokomeza tatizo hilo.

Alisema moja ya kasoro za Tanzania ni kuwa na taasisi nyingi dhaifu, zisizo na uwezo zinazofanya kazi zake bila ya uwazi, hali aliyoielezea kuwa inakaribisha rushwa.

"Moja ya kasoro za Tanzania ni kuwa na taasisi dhaifu, zisizo na uwazi... lazima tufanye kazi kuzipa nguvu kwa kurejesha maadili," alisema Hoseah.

Aliongeza kuwa, ndani ya serikali pia uadilifu upo chini na kueleza kuwa kuwa kutokana na hali hiyo ni vema wananchi wakaacha kulalamika badala yake kutafuta ufumbuzi wa tatizo kwa kushiriki kurejesha maadili na kupambana na rushwa.

Alisema kuwa Watanzania wengi wamekuwa wakilalamikia tatizo la rushwa huku wakishinikiza Takukuru ichukue hatua bila wao kushiriki katika mapambano hayo ambayo alisema kuwa ni ya kila mmoja.

Mkurugenzi huyo wa Takukuru alisema kuwa katika kutilia maanani umuhimu wa kuongeza jitihada za kuzuia na kupambana na rushwa nchini, wameanzisha mkakati maalumu wenye lengo la kurejesha uadilifu nchini.

"Tunataka kurejesha maadili, lengo ni kuzuia rushwa, jukumu letu ni kuwawezesha watu wafahamu na kushiriki katika mapambano hayo," alisema.

Kwenye Mahakama ya Kisutu, hali jana ilikuwa shwari baada ya siku nne za purukushani za kupandisha kizimbani watuhumiwa hao 20, ambao kati yao ni wawili tu waliopata dhamana kutokana na mahakama kuweka masharti magumu, anaripoti James Magai na Paulina Richard.

Hadi majira ya alasiri jana, hakuna mtuhumiwa hata mmoja mpya kwenye kesi hiyo ambaye alikuwa amefikishwa mahakamani hapo.

Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Inspekta Charles Kenyela, aliwaambia waandishi wa habari kuwa hadi mchana huo hakuwa na taarifa za kuwepo kwa watuhumiwa wengine ambao wangepandishwa kizimbani.

Mpaka sasa ni wamiliki wa kampuni 10 tu kati ya 22 zinazodaiwa kuchota fedha hizo ambao walikuwa wameshafikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, akiwemo mfanyabiashara maarufu mwenye asili ya Kiasia, Jayatkumar Chantubhai Patel, ambaye anajulikana zaidi kwa jina la Jeetu Patel.

Tofauti na siku nyingine jana hali ilionekana kuwa tulivu mahakamani hapo huku kukiwa na pilikapilika chache za baadhi ya ndugu wa watuhumiwa katika kashfa hiyo ya EPA ambao walikuwa wakishughulikia dhamana za watuhumiwa hao.

Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), Elieza Feleshi, hakutaka kuwaambia waandishi kama kuna watuhumiwa zaidi ambao wangefikishwa mahakamani jana na badala yake alisema aulizwe msemaji wa Wizara ya Sheria na Katiba.

Hata hivyo, msemaji huyo, Omega Ngole alijibu kwa ufupi kuwa hawawezi kusema ni lini watuhumiwa wanapelekwa mahakamani na badala yake taratibu zinapokamilika na DPP kujiridhisha, wahusika hufikishwa mahakamani.

“Hivyo ninachoweza kukuambia ni kwamba, tumwache DPP afanye kazi, kama kuna watu wa kuwapeleka mahakamani akishajiridhisha atawapeleka,” alisema Ngoe.

Wamiliki wa makampuni waliofikishwa mahakamani mpaka sasa ni Johnson na Mwesiga wanaomiliki kampuni ya Kernel, Ketan Chohan, Jeetu Patel na Amit Nandy (Bina Resort na Itoh), Bahati Mahenge, Manase Mwakale, Davis Kamungu, Godfrey Mosha na Edah Nkoma Mwakale (Changanyike Residential Compelex Ltd)

Wengine ni Rajabu Farijala, Japhet Lema na Rajabu Malanda (Mibale Farm), Rajabu Farijala na Rajabu Malanda (Money Planner), Japhet Lema (Njake Enterprises) na Ajay Somani na Jay Somani (Liquidity Services).

Wengine ni Jeetu Patel na ndugu zake wanaomiliki kampuni za Bencon International Ltd, Maltan Mining Ltd na Navy Cut Tobacco
(T) Ltd.
 
Nchi iyumbe mara ngapi, imeshayumba sana tu na inameshaonyesha kukosa mwelekeo kabisa. Hii inaaminisha kuwa wserikali haijui kusoma alama za nyakati, au kama inasoma haiendi into details.
 
Kazi kweli kweli, labda anashindwa kuelewa kuwa iliyashayumba na kupepesuka sasa inasubiri kuanguka tu.
 
Ni kauli ambayo haikupaswa kutolewa hadharani na mtu kama Hosea. Hii ni aibu kubwa sana kwa serikali ya Kikwete. Ni kuidhalilisha nchi na wananchi wote wa Tanzania! Huu ni unyonge na ulimbukeni ambao unatutia aibu Watanzania kila kona ya dunia. Inatia uchungu sana!
 
Kazi kweli kweli, labda anashindwa kuelewa kuwa iliyashayumba na kupepesuka sasa inasubiri kuanguka tu.

ha ha ha haa, God forbid isiyekuanguka maana sisi wananchi ndio tutakaokuwa victim wa vifusi vya huo mwanguko. Kinga ni bora kuliko tiba.
 
Selective prosecution! Hizi kesi zina hope kweli? Watuhumiwa wakitaka kuchunguza records itakuaje? Wakitaka kuwaita hao "untouchables" watoe ushahidi je?
 
Back
Top Bottom