Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal

Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal

Mgoyangi,
Kwa muda mrefu tumenyamaza kila swala la udhaifu wa vyama unapotajwa. Nadhani ni vema at some stage analysts wakatusaidia kujua sababu za msingi kwanini vyama viko dhaifu. Ziko nyingi kwa mtazamo wangu:-
........

wafanyi kazi kwenye viwanda na sekta mbalimbali wanadai haki zao. Kila moja akifika mahali anapiga kelele mabadiliko yatatokea. Kumbukeni Suharto "alipinduliwa" na wanafunzi kwa kuandamana tu mitaani kwa wiki moja hivi.

Dr. Slaa,

Kwa nini mapaka sasa hivi hamjafanya maandamano nchi nzima kupinga huu uhalifu unaofanywa na Serikali na CCM? Je, mtaungana na CUF kwenye maandamano waliyopanga, na pengine mtoe hotuba?

Tatizo nini? Mbona wafadhili wengi wako tayari kuwasaidieni.
 
Ningekuwa na uwezo ningekwenda niwaombe madaktari wapime Ubongo wa viongozi wa CCM,usikute hamna kitu.Tukawa tunawalaumu bure.
...Teh! teh! tehhhhhh!! Malila, sisi tunawaita Hamnazo hawa"
 
Gazeti letu mahili la mwanahalisi limedokeza hivi:

YUSUF MANJI ndiye mmiliki wa Kagoda agriculture ltd iliyochotewa tsh 30.8 b za EPA. Hii inanikumbusha kauli aliyowahi kutoa Mzee Mengi kwamba "Manji kiburi anakitoa wapi" leo nimepata jibu.Kiburi anakitoa kwa viongozi wa ngazi za juu ikulu/serikali ambao wanamkumbatia kwa kuwa kala nao hela ya EPA.
Nimetoa machozi kupata taarifa za kilichojadiliwa dodoma na CCM nec.
Namalizia kwa ku-quote alichosema mjumbe wa mkutano huo aliyesema:

"mkutano ulikuwa hauna ajenda, ulikuwa sawa mkutano wa hadhara, inasikitisha kwamba wabunge machachari wa ccm badala ya kupongezwa, wanadharauliwa na kutishwa,hakuna lolote la maana pale zaidi ya kikwete kumsafisha lowasa na wenzake"..
Kama unataka kutoa machozi kama mimi soma magazeti ya leo ya mwanahalisi na raia mwema.
Naweka kituo kwa kutamka
"uongozi wa juu wa ccm na serikali wamepoteza mwelekeo".Natamani niende rwanda nimlete kagame aongoze tanzania.


Mara Manji, mara Rostam sasa mtatupoteza kabisa maboya. Serikali na iseme sasa au ikae kimya milele kwani kama tume imeundwa kama uchunguzi umefanyika, kama ripoti imetolewa sasa kwa nini inatuweka kiaina namna hii.

Ungozi wa nchi uangalie sana nyakati. Hizi ni nyakati ambazo watu walio wengi wanathamini sana manufaa ya jumla na sii binafsi na nyakati hizi wameongeza uelewa. Wanajua udanganyifu na hata usanii katika maswala nyeti ya nchi. Pls pls jamani viongozi fanyeni maamuzi sahihi muda muafaka wananchi wanavunjika moyo sana huku chini.
 
Mkuu Dr Slaa, Nikushukuru kwa namna ya kipekee kabisa ktk kuwatetea, kuwahurumia na pia kuwaelimisha Watanzania... Mungu akulinde na abariki kazi za mikono yako till the end of time inshaallah.
Mahali ambapo nchi yetu imefikia ni patamu sana na inahitajika force kubwa zaidi kuweza ku-break-even! ama kwa hakika wapambanaji mmefanyakazi kubwa sana!... mchango wangu mdogo sana ni kwa wana JF wote wenye uwezo wa kuchapisha na kusambaza leaflets zenye kueleza uozo wa ufisadi uliotopea wa viongozi na mafisadi wote na kusambaza ktk kila pembe ya jamhuri yetu hii yenye utajiri lukuki ilihali tu- masikini fukara wa kunuka...
Nina uhakika vijarida vikisambazwa kwa wingi hadi shule za chekechea, pasi na shaka watanzania wataamka kutoka ktk usingizi mzito wa unyonge waliopuliziwa miaka lukuki...
 
Dr. Slaa,

Kwa nini mapaka sasa hivi hamjafanya maandamano nchi nzima kupinga huu uhalifu unaofanywa na Serikali na CCM? Je, mtaungana na CUF kwenye maandamano waliyopanga, na pengine mtoe hotuba?

Tatizo nini? Mbona wafadhili wengi wako tayari kuwasaidieni.

MiratKad,

Naomba unieleweshe. Hao wafadhili wengi ni wakinanani?
 
Mgoyangi,
Kwa muda mrefu tumenyamaza kila swala la udhaifu wa vyama unapotajwa. Nadhani ni vema at some stage analysts wakatusaidia kujua sababu za msingi kwanini vyama viko dhaifu. Ziko nyingi kwa mtazamo wangu:-
a) Vyama dodoki, vilivyoanzishwa kwa lengo la ku destabilize vyama makini. Mifano sasa tunayo mingi. Hutapata muungano au hata ushirikiano wa vyama katika mazingira ya divide and rule iwapo ni dhahiri kuna vyama vimeanzishwa kwa kazi hiyo tu.
ii) Kuna vyama vinatumika na vyombo vya dola hasa usalama wa taifa, kulinda maslahi ya ccm, officially or unfofficially. Inawezekana kabisa kinacholindwa ni maslahi ya watu binafsi ndani ya usalama, na au ni official na hivyo dola yenyewe inavitumia. Siku hizi kumezuka wana usalama wanaoitwa "Kanjanja" kama mmumewasikia. Hawa ndio wanaotumika sana na CCM, kama ilivyofanyika kwenye uchaguzi mdogo wa Kiteto.
iii) Kuna vyama viongozi wakishakatiwa mshiko ndio kazi yao imemalizika.
Katika mazingira haya, wakati umefika sasa Watanzania waelewe kuwa inawezekana kabisa swala la kudai mwungano wa vyama ni swala linalopandikizwa ili ukombozi ushindikane. Katika mazingira hayo, vyama serious au vitashindwa kuungana au hata kufanya siasa kama chama mmoja mmoja. Hata ulichokiita Chama makini kingelianzishwa leo, kama dynamics ya vyama vya siasa katika nchi iliyojaa ufisadi/umafia isipofanyiwa utafiti wa kina na kidhibiti mbinu hizo chafu yote yataishia katika ndoto na au matumaini yasiyotekelezeka.
Nina amini wote wenye mapenzi mema, na watanzania watakapoendelea kuelewa dynamics za siasa na uhusiano wa siasa na maisha yao ya kila siku, siasa vs umaskini/ujinga na maradhi wakapiga kelele za kutaka haki yao. Siku hiyo CCM haitakuwa na lake tena. Siku hizo haziko mbali Wazee wa EAC wanalala kwenye viwanja vya ikulu, wastaafu wa Idara mbalimbali Serikali nao wameanza kulala kwenye viwanja vya ikulu, waalimu ambao siku zote wamekuwa docile wamefika Dar kwa malori na wameanza kudai haki zao, wafanyi kazi kwenye viwanda na sekta mbalimbali wanadai haki zao. Kila moja akifika mahali anapiga kelele mabadiliko yatatokea. Kumbukeni Suharto "alipinduliwa" na wanafunzi kwa kuandamana tu mitaani kwa wiki moja hivi.

Dr.W.Slaa nashkuru kwa mchango wako..ni vema pia ukaweka wazi iman yako juu ya vyama unavyohisi ni Pandikizi..."Kuuficha ni sehem ya ufisadi"..kwani watanzania wanatakiwa wajue ni chama gani ktk vyama Upinzani ni Dodoki au Pandikizi....Uvijataje hivi vyama kama ulivyotaja list ya Mafisadi...ili Watz wajue Moja...Bahati mbaya kila ukikutana na Mpinzani au kiongozi wa Upinzani anasema maneno hayohayo...
 
Hivi hawa wahindi mbona katika kila ufisadi wapo,hawafikishwi mahakamani wanalindwa na viongozi wa chama na serekali kwa kutumia kodi zetu.Hii maana yake nini !.
Ukugusa EPA,Radar,Richmond ni wahindi wametamalaki.

Tusitafute visingizio. Ni "wamatumbi" wenzetu ndio ambao wanafungua milango yote hiyo. Walaumiwe wanaowalinda.
 
Hivi nani alituchagulia jina TANGANYIKA na ni nini maana yake? Inawezekana tumelaanika kuanzia jina hadi matendo...! TANGANYIKA = DANGANYIKA.
 
MiratKad,

Naomba unieleweshe. Hao wafadhili wengi ni wakinanani?

Wapo watu ambao hata si wabongo lakini wanahuzunishwa na tabia za wazi za viongozi wa serikali ambao ni wahuni wakisiasa. Wangependa kusaidia lakini wanashindwa pa kuanzia na wanataka wananchi wenyewe waanze na watake mabadiliko kwa vitendo.

Ndio maana nikauliza tatizo haswa ni nini?? Kwa nini wameshindwa hata kuandaa maandamano ya Kupinga vitendo hivyo vya wizi na uhalifu wa wazi?

.........Kwa hisani ya Ole L, (Kutoka T Daima).....

Maandamano haya ni nyeti na kila Mtanzania anayeipenda nchi yetu anatakiwa atoe mchango wake wa kuandamana.Hakuna aliyeambiwa atoe pesa zake.Fungeni biashara kwa masaa mawili kudai haki zenu. Kufunga biashara kwa lisaa limoja mawili haisababishi wewe kulala njaa lakini ukiwapuuza viongozi wenye kuipenda nchi yako usijekushangaa siku moja unachapwa bakora ndio upate huduma.Ninachoomba tu haya maandamano yasiitwe ya CUF kwa vile kuna migogoro mingo inayohusisha uongozi wa nchi hii na chama cha CUF.Utashangaa watabadili kuyaita maandamano ya kupindua nchi. Mimi nawajuwa viongozi wa CCM na Serekali hii ya Tanzania ni watu wa hila.Wameiga tabia za Wazungu wao waliowawekeza.Wazungu ni watu wa hila na wameshawaambukiza kina Makamba hadi hawakumbuki hata wananchi waliowapatia kura kule mbalamo.Mimi sikuamini kuwa Mwalimu akifariki ndio tutafanyiwa mambo ya aibu namna hii.Nashauri kila Mtanzania awe mtoto wa Shule,Mfanyakazi wa Serekali,Mkulima,Mchimba madini,Muongoza watalii,Taxi dereva,Mchuuzi wa soko,muuza nyama,Dereva wa mabasi ya abiria atoke kushiriki maandamano.Kila mtu na bango lake.
Mfano mabango yaandikwe hivi.
1.WATOTO WA SHULE - Fedha za mafisadi zimerudisha elimu nyuma.
2.WAKULIMA - Fedha za mafisadi zimepandisha bei za pembejeo.
3.MADINI - Fedha za mafisadi zimemaliza madini yetu bila tija.
4.WAONGOZA WATALII - Fedha za mafisadi zinamaliza wanyama pori wetu bila faida.
5.WACHUUZI SOKONI - Fedha za mafisadi zimetuulia biashara ya ndani.
6.MADEREVA - Fedha za mafisadi zimepandisha bei za nauli.
7.WAFANYAKAZI - Fedha za mafisadi zimepunguza ari ya utumishi kazini.nk
 
Toka vita vikali vya Richimonduli vilipofikia kumpumzisha Waziri Mkuu Lowassa, kulikuwa na swali kubwa sana of what Rostam played, Rostam alijua kuwa baada ya Lowassa pressure itakuwa kwake, kwa hiyo alichofanya ni kuyahamisha makampuni yake yote kwenye mikono ya Manji ambaye ni patner wake sana in crime,

Baaada ya kumaliza uhamishaji ndio akaanza kupiga makelele kuwa yuko clean, na mpaka akamtwanga Mtikila na akajaribu kila njia kumpaka Spika, na moja ya mashirika yake Rostam aliyompa Manji ni Kagoda, na pia hata Ze-Comedy walinunua pamoja kumzuia Mengi na makali ya Ze - Comedy na mafisadi.
 
vyama pandikizii alivyosema dr slaa ni kama ifuatavyo


1. NCCR MAGEUZI YA JAMES MBATIA NA AKINA SUNGURA

2. KILE CHAMA CHA MTU ANAITWA PAUL KYARA

3.
4.
5
PIA KUNA NGO FEKI NA PANDIKIZI KAMA

1. CEGODETA LILE LA THOMAS NGAWAIYA LA KUJIKOMBA KWA CCM
2.
3

ENDELEA KUJAZA LIST
 
Gazeti la Mwanahalisi la leo limeandika habari inayomhusisha RA na fedha nyingine za EPA kiasi kwa kutumia majina ya wafanyakazi wake. Kampuni iliyotumika ya Afritainer inatumia contact sawa na Kagoda na hiyo ndio inamuunganisha RA moja kwa moja na Kagoda.
attachment.php
 

Attachments

  • RostamTena.jpg
    RostamTena.jpg
    37.1 KB · Views: 273
Last edited by a moderator:
JK anasubiri Yesu aje amuhakikishie kuwa RA ni fisadi.

Yebo Yebo,

JK anajua kwamba RA kachota hizo pesa maana ilikuwa mipango yao wote. Labda alichozidiwa JK ni kwamba RA alichota nyingi zaidi na kuziingiza kwenye biashara zake na kuwagawia chache CCM.

Mimi niko convinced JK anajua hilo suala ndani mpaka nje. Huu ni ujambazi wa mchana
uliofanywa na CCM na serikali yao. Kilichofanyika ni sawa na baba kuiba uji wa mtoto wake, hivi kweli hii mijitu ina akili?
 
Back
Top Bottom