Gazeti letu mahili la mwanahalisi limedokeza hivi:
YUSUF MANJI ndiye mmiliki wa Kagoda agriculture ltd iliyochotewa tsh 30.8 b za EPA. Hii inanikumbusha kauli aliyowahi kutoa Mzee Mengi kwamba "Manji kiburi anakitoa wapi" leo nimepata jibu.Kiburi anakitoa kwa viongozi wa ngazi za juu ikulu/serikali ambao wanamkumbatia kwa kuwa kala nao hela ya EPA.
Nimetoa machozi kupata taarifa za kilichojadiliwa dodoma na CCM nec.
Namalizia kwa ku-quote alichosema mjumbe wa mkutano huo aliyesema:
"mkutano ulikuwa hauna ajenda, ulikuwa sawa mkutano wa hadhara, inasikitisha kwamba wabunge machachari wa ccm badala ya kupongezwa, wanadharauliwa na kutishwa,hakuna lolote la maana pale zaidi ya kikwete kumsafisha lowasa na wenzake"..
Kama unataka kutoa machozi kama mimi soma magazeti ya leo ya mwanahalisi na raia mwema.
Naweka kituo kwa kutamka
"uongozi wa juu wa ccm na serikali wamepoteza mwelekeo".Natamani niende rwanda nimlete kagame aongoze tanzania.
Wana JF,
Kwa kumbukumbu zote nilizonazo, Yusuf Manji ametumika tu kama camouflage. Mmiliki wa Kagoda,halisi ni lazima tuendelee kumsaka.
i) Aliyesajili Kagoda ni John Kyomuhendo, na ndiye aliyeweka saini yake kwenye nyaraka zote za Brela.
ii) Saini katika Barua iliyotoa fedha zote BOT ni ya Kyomuhendo, na ndiye pia aliyefungua akaunti CRDB. Ingelikuwa mwujiza kwa Yusuf Manji kumruhusu Kyomuhendo kuchukua hizo fedha zote, bila yeye mwenyewe kuonekana popote, mbona kwenye Akaunti zake nyingine zote yeye mwenyewe ndiye anayeshughulikia?
iii) Benki za Barclays na Kenya Commercial Bank walikataa kufungua akaunti za Kagoda kwa vile walitia mashaka na huyu mteja mpya ambaye ghafla anaweka mabilioni kwa mara moja. Ingelikuwa na Yusuf Manji kusingelikuwa na mshangao wa aina hii.
iv) Kumbukumbu zetu zinaonyesha aliyefuatilia fedha hizi BOT na negotiations zote zilikuwa zikifanywa na Rostam Aziz, wakati huo Mweka Hazina wa CCM. Memo zote zilizopelekwa kwa Balali zilikuwa zinapelekwa kwa Rostam Aziz. Manji hatajwi popote katika vimemo hivyo.
Nadhani, fumbo hili siku si nyingi litafumbuka. Nawapa hints
a) Serikali haina uchaguzi lazima iwaambie watanzania Kyomuhendo ni nani, na ushahidi wote unaonyesha alikuwa mfanyikazi wa Caspian ambayo ni ya Rostam Aziz. Ni kwanini huyu Bwana ametoweka tangu suala la Kagoda kulipuka?
b) Serikali kupitia Brella na BOT lazima watuambie Kyomuhendo ni nani, na kwanini ametoweka na kwanini Serikali haikuchukua hatua ya kumtafuta tangu alipotoweka, angalau kuweka Tangazo la kutoweka kwake? Mbona kwa matukio mengine hadi picha zinatawanywa katika jitihada za kumtafuta mhalifu? Inafichwa nini?
c) Rostam Aziz lazima aache sasa mchezo wa Mbuni awaambie Watanzania Kyoumuhendo ni nani, kwanini katoweka, na kwanini yeye binafsi alikuwa akienda BOT kufanya negotiation na Hazina ya kupata fedha hizo?
d) Malegesi, aliyetengeneza nyaraka za kugushi za makampuni ya nje ili Kagoda iweze kulipwa kwa niaba ya Makampuni hayo lazima awaambie watanzania Kyomuhendo ni nani. Haiwezekani Mwanasheria maarufu kama Malegesi na wenzake watengeneze nyaraka muhimu kiasi hicho bila kufahamu wanayemtengenezea nyaraka hizo.
e) Mwenye siri zote za EPA, hususan Kagoda ni aliyekuwa Gavana Balali. Serikali lazima ituambie Watanzania kwanini walikataa kata kata kumhoji Gavana Balali, hata kama alikuwa hospitalini. Mbona watuhumiwa wanahojiwa hata hospitalini kwa Balali nini kilikuwa kinakwepwa. Haya maswali yasipopata majibu Serikali daima ijue kuwa tutaiona kuwa imekuwa ikiwakingia kifua vigogo waliohusika kwa sababu zinazojulikana.
d)CRDB nayo inatakiwa sasa itoke hadharani kulinda image yake ya kwanini haikuweza kustuka mathalan 25 Billion zinachukuliwa siku moja kupitia matawi yake sita na kampuni ambayo haijulikani vizuri?