Kagame tells Kikwete "I will hit you......"

Kagame tells Kikwete "I will hit you......"

Status
Not open for further replies.
Tanzania inabidi isitishe mahusiano yote ya kibalozi na Rwanda mpaka maelezo yatakapotolewa kuwa Rais wao alikuwa na maana gani aliposema ujinga huu. Kagame owe us an apology.
 
Nadhani hayo maneno siyo ya kagame kuna wahuni ambao wameyaweka, km ni ya kagame naona umefika muda muafaka wa kumuondoa madarakani kama tulivyomuondoa idi amin
 
Watch out Kagame your words are so insultful to our President,and you should apologize for this,otherwise we will not tolerate any more
 
Siku zote ukiona mtu mzima anaongea upumbavu mbele ya media au watu dhidi ya kiongozi mwenzake ujue ana matatizo.
Yupi alianza kumuongelea mwenzake? kama siyo baba Mwanaisha, Poor mwenyekiti
 
Mkuu Viper hiki ndicho nilichokuwa nakitafakari.Kuna ushirikiano wa nchi zinazopakana na nchi yetu dhidi ya maslahi ya kiuchumi,kisiasa,kijeshi na diplomasia ya kimataifa.Mambo haya hayajotekea kwa bahati mbaya bali udhaifu ambao umekuwa ukifanywa na serekali ya JK wa kuupuza ushauri wa vyombo vyake vya ulinzi na usalama.

Rwanda inamtusi Rais wa JMT mchana kweupe bila uoga kwasababu anajua waTanzania si wamoja tena wamegawanyika kwa misingi ya ukanda,ukabila na udini.Kwasababu anajua Tanzania ile aliyoicha Mwalimu Nyerere imetekwa na kikundi kidogo kinachouza rasilimali za nchi huku wananchi wakibaki katika hali ya umasikini mkubwa.Kwasababu anajua vita ikianza watakaofaidi tenda za ununuzi wa vifaa feki kwa bei ya kubambikiza ni kundi la mafisadi.

Nachukia Rais wangu akitukanwa,nachukia Rais wangu akikebeiwa lakini nifanyaje ?Hii hali ya kudhalilishwa tumejitakia wenyewe.Siku TISS itajikita kutafuta majibu ya kweli ya usalama wa taifa letu kamwe hatotokea kiongozi wa nchi jirani atakayethubutu kutudharau.



Tanzania Nchi yangu imekuwa kama ISRAEL... Majirani wote wanatutolea macho ....


MALAWI - bibie joyce banda anatuchokoza

KENYA- wanaitamani ardhi yetu ..

UGANDA- wamejitolea kabisa eneo la kikao na kuunda umoja wao KKK

KAGAME - ameanza vitisho...


HIVI HAWA WOTE WAKITUINGILIA KWA PAMOJA TUTAPONA KWELI....? INABIDI TUANZE USHIRIKIANO WA KIJESHI NA NCHI ZA KUSINI .....
 
Last edited by a moderator:
akili yako inatosha kwenye kifuniko cha soda tu wala huyajui mambo mengi ya vyombo vyetu vya dola unaongea bila hata ya fact na ukiona mtu anaizalau mpaka nchi yake anachuki binafsi na watu walioko madarakani wala huna lolote.
Umempasha sana huyu --------! Anadhani anaweza akajua mambo ya ndani ya vyombo vyetu vya ulinzi!..
 
Weak Leadership! Tanzanians we are very sorry kwa kweli and no wonder tukasambaratishwa kwasababu heshima ya TZ sasa imeshuka sana katika jumuia ya kimataifa huku ndani CDM wametushinda, Malawi wanakuja juu and ths has been there for a long but wameona ndo wakati sahihi kupigania ziwa lao, Kagame bila aibu anatishia kwa upande mwingine,EAC Kenya ,Uganda wanafanya ya kwao wamechoka, USA wanataka na ni sasa hivi no discusion na sasa usalama wetu upo UCHI system nzima ya ulinzi ilitekwa hili halifanyiki kwenye taifa lolote lililohuru, Wachina wanataka na sasa hivi msishangae RED BRIGED wafadhili ndo haohao tuchapane wachote mali zetu.Hatuna viongozi nchi imesambaratishwa watz tusimame imara tuipiganie nchi yetu Hatuna UONGOZI.Verry Sorry!
 
Kagame amepata kichwa baada ya kusikia kauli ya Mnyika Bungeni.Mnyika ndo amezalisha yote haya ya Rais wetu kudharauliwa.

kikwete anatoa ushauri wakati wanajeshi wake wanabaka huko mtwara na polisi wanawarushia mabomu na kuwauwa kwa risasi wananchi wasio na hatia..
 
Hili liwe fundisho JK usiwe unaandikiwa kila kitu, wewe huwa unasema akili ya kwaambiwa changanya na yako. we kila unachoambiwa na kuandikiwa unakubali tu, Hongera sana Kagame.

Inawezekana wewe ukawa ni Mnyarwanda, lakini ujue sisi WaTz hata kama tuna malumbano yetu ya vyama au na Rais wetu, ujue linapokuja tishio kwa usalama wa nchi yetu kutoka nje, basi ujue utaifa wetu huja kwanza. Kiburi anachokionesha Kagame kinafanana na kile cha Iddi Amin wa Uganda na Adolf Hitler wa Ujerumani. Asithubutu kutuchezea kama anavyoichezea Congo!
 
Amechelewa sana kutuma "Hitman" kuja ku-deal na huyu JK...

JK ni mnafiki, metally retarded, trouble-maker, problematic, weak person etc. JK anatakiwa adili na mambo ya wananchi wake na sio kurukia mambo ya wanaume wezanke.. Kilichotokea hapa ni kuleta tabia zake za kizaramo kwenye International affairs.

Kagame, just hit this kifafa boy....
 
Sana sana ninachokiona kutoka kwa Kagame ni kama anatafuta Bifu! JK aliongea, akayaacha lakini huyu jamaa bado tu; anataka nini kama sio ana-force bifu? Haki ya mungu sifai kuwa Rais manake kwa kauli za kipumbavu kama hizi ingekuwa tayari nishaanza kutafuta sababu muafaka za kumchapa! Hapa jukwaani nilishawahi kutoa HINT za namna gani mtu kama huyu unaweza kumtafutia sababu za kumtandika; sababu ambazo zinaweza kabisa kukubalika kimataifa! Huyu mtu anapaswa kumaliza muda wake na kuondoka (kama kweli ataondoka) coz' hii nchi ikija kupata mtu mwenye kuthamini utu, wallah, atatutafutia majanga!!
 
Kuna wakati mwingine viongozi wa nchi wanapozungumza, hawazungumzi kwa niaba ya wananchi wao bali huwa yanakuwa mawazo yao binafsi!!! Wananchi wa Rwanda hawana matatizo na wananchi wa Tanzania!!!
 
Ninaamini ukimya wa Tanzania dhidi ya huyu kiumbe anayeitwa kagame utakuwa na mshindo mkubwa. Ngoja tusubiri. Haitashangaza tukisikia kesho hayupo madarakani.

Hiyo ni Tanzania ya Nyerere na labda Mkapa kidogo waliokua wanasikiliza na kufanyia kazi kwa vitendo ushauri wa MI na TISS.
 
Inawezekana wewe ukawa ni Mnyarwanda, lakini ujue sisi WaTz hata kama tuna malumbano yetu ya vyama au na Rais wetu, ujue linapokuja tishio kwa usalama wa nchi yetu kutoka nje, basi ujue utaifa wetu huja kwanza. Kiburi anachokionesha Kagame kinafanana na kile cha Iddi Amin wa Uganda na Adolf Hitler wa Ujerumani. Asithubutu kutuchezea kama anavyoichezea Congo!
Yaani mkuu wangu hapa jukwani kuna watu wanatia kinyaa hadi kutapisha! Yaani walivyo wapuuzi wanazani political interests zao zitakuja kumalizwa na watu wa nje!! Uunapokutana na Thread kama hii ndipo unaweza kufahamu mpinzani wa kweli ni nani na mamluki ni nani! Hawa mamluki wapo tayari hata kutumika just for the sake of their political interests!
 
Look at this fool.Ajaribu aone jinsi watanzania tutakavyoungana kumfunza adabu and dump him huko lake Tanganyika.Na sisi tumekua wapole mno maana mimi ningemuonyesha cha moto.Hakuna cha intetnational community!

ccm na serikali yake wameishindwa cdm, watamuweza Kagame kweli?? Au chadema ni tough kuliko Kagame?
 
Kuna baadhi ya watu wanaamini kwamba haya yanayotokea yanatokana na kushuka kwa heshima ya nchi huku wakisahau kwamba unapokutana na viongozi wendawazimu na wa hovyo hovyo kama Kagame hakuna cha nchi kushuka heshima wala nini! Wanapoona umeingilia interest zao(hata kama ni personal interests)huwa hawana haya wala aibu kuongea lolote! Turejee kauli za Idd Amin dhidi ya Mwalimu Nyerere! Amin alikuwa anatoa kauli chafu, kashfa na za kishenzi dhidi Nyerere tena pengine kuliko huyo Kagame! Iddy Amini alishawahi kutamka kwamba anamtaka Nyerere kwenye ulingo wa masumbwi ili akamchakaze!!Sasa je, ndo kusema hata heshima ya Nyerere nayo ilikuwa imeshuka? Ni uendawazimu tu, tuache siasa zetu za ndani tunapokutana na washenzi kama Kagame!! Wala mzidhani eti siku mathalani CHADEMA wameingia madarakani Kagame anaweza kuwa na adabu unless CHADEMA wasiingilie interest zake hata kama interest hizo zina maafa kwa Tanzania!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom