Kagame tells Kikwete "I will hit you......"

Kagame tells Kikwete "I will hit you......"

Status
Not open for further replies.
Acheni umbumbumbu watanzania wenzangu mnaosema eti tutaipiga rwanda kisa ni ndogo kijokrafia, ni nani aliwafundisha kuwa uimara wa jeshi ama wa taifa unapimwa kwa misingi ya ukubwa wa ardhi??? Pumbafu nyie hamjui historia mnaandika tuu....kama nchi kuwa kubwa ndiyo inakuwa na jeshi nzuri mbona tulitawaliwa na ujerumani ambao tunawapita mara tatu kiukubwa??? Pumbafu nyie... Israel ilifanya mashambulizi kule misri na syria kati mwaka 1964 na 67 kwa wakati mmoja na kuzima ubabe wa hizo nchi ilhali ndiyo nchi ndogo kuliko zote hizo. Hamjui historia nyie mawazo yenu yanaendeshwa na hisia ambazo chanzo chake ni kushindwa kufikiri na kuchambua mambo kwa kina. Tuhoji kwanza uzoefu wetu wakupigana tulinganishe na ule wa wanyaruanda, tukisikia mlio wa risasi si tunakimbiaga uvunguni mwa kitanda wote baba,mama na watoto?------- sana
Teh teh teh!mkuu mbavu zangu!Inanikumbushia Uganda ilikuwa mtu akiacha briefcase yake mahali unattented wananchi wanatimkia mbali kabisa na mahali ilipo briefcase hiyo...Maana wameshadeal na mabomu ya briefcase.

Kwa bongo ukiacha briefcase somewhere watu wanalamba kumbe ndo wanalipuliwa.Ni kweli hatujazoea vita.Kwa wenzetu waliozoea vita, ukisikia mlipuko,unakimbilia mbali.Ila nakumbuka wakati wa ule mlipuko wa ubalozi wa marekani,nilikuwepo jijini Dar,watu walikuwa wakikimbilia eneo hilo,kwahiyo kama kungekuwa na a second explosion,basi maafa yangekuwa makubwa zaidi.Sasa mkuu umenichekesha sana uliposema baba,mama,na watoto wote uvunguni mwa kitanda!
 
Cuba ni nchi ndogo sana kushinda Miami, na iko karibu kabisa na USA.... lakini hawajawahi kupigana vita. na kila mtu anajua kabisa kwamba USA ina uwezo mkubwa.
na viongozi wa nchi hizo wanatofautiana sana kabisa kuliko huyo Rais Kikwette na Rais Kagame.Tena uhasama wao ni mkubwa na wa kihistoria....Cuba/Soviet

Je wantanzania mko tayari kwenda vitani eti kwasababu JK na Kagame wanachukiana? au wanakashifiana?
what will be the case for war ?

swala la Malawi ni hivyo hivyo tayari manawaza vita....tangia lini tatizo la mpaka likatatuliwa na vita?
jirani yako akiongeza hatua kadhaa kiwanjani kwako, je wewe utakuja na panga na bastola? au utakuja na vielelezo na ramani kutoka mamlaka husika?
tuondokane na maujinga.

Tuondokane na mawazo ya vita, vita ni garama kubwa mno, maisha na mali. na Tanzania ni maskini mno.
 
You are right! Mazingira ya sasa si kama yale ya Nyerere kabisa. Wakati ule mtu alikuwa anajivunia kuitwa mtanzania na alikuwa yupo tayari kufa kwa ajili ya nchi yake. Hivi leo hii yule aliyefiwa na ndugu zake kutokana kupigwa risasi na polisi unafikiri ataweza wapi kuitetea Tanzania? Atatamani majeshi ya kigeni yashinde ili utawala dhalimu uondolewe. Yaani tukiingia vitani sasa hivi tutapigwa kama alivyopigwa Iddi Amin. nawashangaa sana wanaosupport vita kwenye nchi iliyosambaratika kama hii.

Siyo tu kwamba tulijivunia kuwa Watanzania lakini tukiwa na Jeshi lenye nidhamu ya hali ya juu,jeshi la Ukombozi,jeshi lililokuwa likiendesha Operesheni kubwa za kijeshi kusini mwa Afrika! Wenye akili tunajua kwamba jeshi letu la sasa halina sifa hata nusu ya JWTZ ya wakati huo,ndio maana hata hivi vinchi vidogo vinatudharau sasa!
 
Rwanda kwa eneo lake ni ndogo kuliko mkoa wa Kilimanjaro ambao ni mdogo kuliko mikoa yote Tanzania. Tutamkanyaga kama kifaranga cha kuku akithubutu! Asidhani kuwa Tanzania ni kama Congo!

....daudi & goliathi
 
Achana na hao watoto wa CCM ambao hata JKT hawakuenda. Wanatambia tundege twa jeshi ambato tumechoka twa Kichina na Silaha ambazo huwa zijalipukia tu zenyewe kwenye maghala. Too sad. Acha Kagame aje waanze kusikia zile story za Wahaya zisemazo:

Mhaya: Askari wa Amini waliniwowa, na mke wangu wakamuwowa, ila binti yangu walimuwowa zaidi.
Mtangazaji: Una maanisha nini kusema walikuwowa Mzee?
Mhaya: Huelewi nini ndugu Mtangazaji? Warinisw**** ahhhhhh Wahaya bado wako macho na watoto wao!!!

Mkuu nimecheka sana,ingawa umeeleza kama utani lakini kuna ukweli. Mkazi wa Kagera ambaye aliona vita ya Kagera na baadaye akashuhudia uharibifu wa miundombinu na umasikini baada ya vita hawawezi shabikia ujinga wa vita ya kipuuzi eti rais ametukanwa!
 
"NASUBIRI WAKATI MWAFAKA WA KUMUONYESHA KIKWETE YA KWAMBA MIMI NI NANI".....HILI NI TISHIO LA KIHUNI LA RAISI KAGAME KWA RAIS KIKWETE

Nikiwa katika upekuzi wangu, nimeshtushwa sana na kauli za KIHUNI za Rais Paul Kagame dhidi ya Rais wetu Kikwete na nchi yetu kwa ujumla....


Rais Kikwete ameepuka malumbano na Kagame kwa kukaa kimya , lakini inaelekea Kagame anadhani ukimya wa Kikwete ni uoga kwake au labda anatafsiri kuwa anadharauliwa.....

Nadhani huu ni wakati mwafaka kwetu sisi watanzania kuungana na kumuunga mkono rais wetu juu ya huu UPUMBAVU wa Kagame....

Kagame ni lazima atambue kwamba watanzania tupo tayari kuilinda nchi yetu kwa gharama yoyote na kamwe hatuwezi kuwa VIBARKA wa Rwanda...

Ifuatayo ni Kauli ya Kihuni aliyoitoa Rais Kagame Kwa Taifa letu:
-------------------------------------------------------------

....."Those people [Tanzanian President Jakaya Kikwete] you just heard siding with Interahamwe and FDLR and urging negotiations… negotiations?


Me, I do not even discuss this topic, because I will just wait for you [Tanzanian President Jakaya Kikwete] at the right place and I will hit you! He[Tanzanian President Jakaya Kikwete] did not deserve my answer.


I did not waste my time answering him…It is well known. There is a line you cannot cross, there is a line, a line that you should never cross. It is impossible…""


It is in these ominous terms that the Rwandan dictator General Paul Kagame threatened to get even with Tanzanian President Jakaya Kikwete, while addressing Rwandan Youth on June 30, 2013 during a summit called "Youth Konnect"", sponsored by his wife, Janet Kagame.


Relations between Tanzanian President Jakaya Kikwete and Rwandan leaders have soured in the last weeks. On several occasions Rwandan leaders called the Tanzanian President "a genocide and terrorist sympathizer", "ignorant", "arrogant", and "mediocre leader".

The relations have deteriorated following the recommendation by President Jakaya Kikwete of open negotiations between Rwandan, Ugandan and Congolese leaders and their respective armed opposition in order to bring durable peace and security in the African Great Lakes region....


source..I will Just Wait For You At the Right Place And I will Hit You, Rwandan General Paul Kagame Threatens Tanzanian Jakaya Kikwete

 
Siyo tu kwamba tulijivunia kuwa Watanzania lakini tukiwa na Jeshi lenye nidhamu ya hali ya juu,jeshi la Ukombozi,jeshi lililokuwa likiendesha Operesheni kubwa za kijeshi kusini mwa Afrika! Wenye akili tunajua kwamba jeshi letu la sasa halina sifa hata nusu ya JWTZ ya wakati huo,ndio maana hata hivi vinchi vidogo vinatudharau sasa!

Mkuu vita ya Kagera vijana walikuwa wanakamtwa na kupewa mafunzo ya kushoot,kulenga shabaha na ukakamavu kwaharakaharaka.Na wengine wanafanywa mgambo.Sasa hivi hawawezi fanya hivyo dunia iko kama kijiji.Kuna kitu kinaitwa draft,ila ikifikia hapo,ni lazima serikali husika iwe inapendwa na wananchi vya kutosha.
 
Mkuu vita ya Kagera vijana walikuwa wanakamtwa na kupewa mafunzo ya kushoot,kulenga shabaha na ukakamavu kwaharakaharaka.Na wengine wanafanywa mgambo.Sasa hivi hawawezi fanya hivyo dunia iko kama kijiji.Kuna kitu kinaitwa draft,ila ikifikia hapo,ni lazima serikali husika iwe inapendwa na wananchi vya kutosha.

Mkuu nakubaliana nawe lakini wengi wa hawa ambao hawakua na mafunzo walipelekwa mbele kama chambo,jeshi letu lilikua na wapiganaji waliokua wameiva kivita kutokana na kushiriki ktk operations nyingi za kivita ktk nchi za kusini.
Siku hizi jamaa zetu wanafuga vitambi na kufyeka nyasi wakati wenzao kila siku wako misituni wanapigana,na wenzao wengine wakilinda amani maeneo hatarishi ambayo watawala wetu wanaogopa kupeleka jeshi letu!
 
Heri JK apigwe apate akili. Usanii kwa kila kitu me kananiboa ka JK.

I have a feeling there is more to this story. Inawezekana Kagame amemshtukia JK ni msanii(anang'ata na kupuliza) ili aonekane mzuri kwa Kagame na vilevile mzuri kwa waasi. Kagame ni straight talker; na hapa anaonyesha jinsi alivyona msimamo kwenye kile anachokisimamia (whether he is right or wrong). JK sidhani kama anamsimamo kwenye kitu chochote; yeye anaangalia tu upepo. Soon tutasikia amebadilisha mwelekeo. Nafikiri huu ugomvi ni wa JK na Kagame; and not Tanzania na Rwanda. Hata kama Rwanda ni ndogo tusiingie kichwa kichwa kama nchi wakati hatujui who are the people/power behind Kagame. Tukubali tu nchi yetu haina leadership. Uongozi huu unategemea na upepo unaelekea wapi na wakati gani. Wacha wachapane/waviziane wenyewe, atakayepigwa atapata akili. Inawezekana kabisa JK amepeleka usanii kwenye mambo sensitive akidhani yatapita kama anavyochezea watanzania. There must be more to this story that we do not know.
 
I have a feeling there is more to this story. Inawezekana Kagame amemshtukia JK ni msanii(anang'ata na kupuliza) ili aonekane mzuri kwa Kagame na vilevile mzuri kwa waasi. Kagame ni straight talker; na hapa anaonyesha jinsi alivyona msimamo kwenye kile anachokisimamia (whether he is right or wrong). JK sidhani kama anamsimamo kwenye kitu chochote; yeye anaangalia tu upepo. Soon tutasikia amebadilisha mwelekeo. Nafikiri huu ugomvi ni wa JK na Kagame; and not Tanzania na Rwanda. Hata kama Rwanda ni ndogo tusiingie kichwa kichwa kama nchi wakati hatujui who are the people/power behind Kagame. Tukubali tu nchi yetu haina leadership. Uongozi huu unategemea na upepo unaelekea wapi na wakati gani. Wacha wachapane/waviziane wenyewe, atakayepigwa atapata akili. Inawezekana kabisa JK amepeleka usanii kwenye mambo sensitive akidhani yatapita kama anavyochezea watanzania. There must be more to this story that we do not know.
Ni kweli mkuu,but there's a very thin line btn ugomvi binafsi wa marais vs nchi zao.Nadhani unakumbuka bifu la saddam na bush.
 
Unataka ushahidi kuwa dada yako alikuwa kwangu? Wee kijana unataka laana sasa. Ila usinilaumu.

Namsifu sister wako kwa usafi na ubunifu maana kwa mara ya kwanza, niliona kwa macho yangu C-String kama chupi.

Ilibidi niipige picha na kubaki na ukumbusho. Namsifu kwa ubunifu na ucheshi wake. Kweli amelelewa vema sana.

c-string-leopard.jpg

Weka ushahidi hapa usifikirie hiyo rangi nyekundu inanipa mashaka. Njia ya mwongo ni fupi. Umezoea vya kunyonga ..... ..... ...... Isije ikawa na wewe unaishi kama mkimbizi halafu unasingizia mambo ya Mirambo. Tutapekua makabrasha hapa na kuanika ulivyokua mnyenyekevu pale alifu. Wacha fujo!
 
Mkuu, hiki kituo haki ya nani mwenyewe nimekisikia kwa masikio yangu nikiwa mdogo sana Radioni.

Siyo rahisi mtu kuamini ila ni kweli huyo Mzee, Mkewe na Mwanaye walibakwa na Askari wa Amini. Enzi hizo unapewa live na Ben Kiko, kijana mkorofi wa RTD enzi hizo akitokea Sikonge na jina hasa ni Kikoroma.
Mkuu nimecheka sana,ingawa umeeleza kama utani lakini kuna ukweli. Mkazi wa Kagera ambaye aliona vita ya Kagera na baadaye akashuhudia uharibifu wa miundombinu na umasikini baada ya vita hawawezi shabikia ujinga wa vita ya kipuuzi eti rais ametukanwa!
 
Kaka wanaosema jeshi letu lina nguvu wana refer kipindi tofauti kabisa na wanaosema nchi yetu kubwa nao pia ni wafinyu wa mawazo, ukubwa wa nchi sio kushinda vita. Kumbuka Tony Blair ndiye mshauri wa Rwanda na ana reputation kubwa sana yule mzee na ushawishi mkubwa na anaheshimiana na Kagame kwa sababu kagame anatumia ushauri wa yule mzee. Hawa wanaotaka kutupiga ni wazungu tu walitaka kupitia ziwa nyasa wameona wanachelewa sasa hivi wanapitia Rwanda. Vita ni mbaya, hivi kabla ya vita tuko taabani je tukiingoia vitani mnadhani itakuwaje??? Baba Mwanaisha anahamisha familia yake yote na ndio itakayokuwa nafasi ya mafisadi kuba zaidi. Tukiingia vitani umaskini hautakuja ututoke kwa miaka mingi sana

so whats your point??? Kuna watu wako so useless in this country and you are one of them. Wewe raisi wako anatukanwa unakubali kuogopa adui?? sijui unamiaka mingapi but shame on you.
 
I have a feeling there is more to this story. Inawezekana Kagame amemshtukia JK ni msanii(anang'ata na kupuliza) ili aonekane mzuri kwa Kagame na vilevile mzuri kwa waasi. Kagame ni straight talker; na hapa anaonyesha jinsi alivyona msimamo kwenye kile anachokisimamia (whether he is right or wrong). JK sidhani kama anamsimamo kwenye kitu chochote; yeye anaangalia tu upepo. Soon tutasikia amebadilisha mwelekeo. Nafikiri huu ugomvi ni wa JK na Kagame; and not Tanzania na Rwanda. Hata kama Rwanda ni ndogo tusiingie kichwa kichwa kama nchi wakati hatujui who are the people/power behind Kagame. Tukubali tu nchi yetu haina leadership. Uongozi huu unategemea na upepo unaelekea wapi na wakati gani. Wacha wachapane/waviziane wenyewe, atakayepigwa atapata akili. Inawezekana kabisa JK amepeleka usanii kwenye mambo sensitive akidhani yatapita kama anavyochezea watanzania. There must be more to this story that we do not know.
Nakubaliana nawe mkuu:' there must be more to this story than meet the eyes? Haiwezekani mtu innocently kutaka suluhu ya amani akaishia kutukanwa namna hii. Mimi pia ni katika wale wasiopenda uongozi wa JK (kama tutauita uongozi, naona ni kuburuzwa tu). JK pia si mtu serious, challenged mentally na kusema kweli ni mzuri kwa Watanzaniaa tu. Kma alikuwa kweli na imani hiyo angemfahamisha kwanza mwenziwe kwa faragha badala ya kwenda kuonesha u star.
Kuna watu wanaojifutua hapa na kusema tutampiga aakicheza!Thubutu, hawa hawasomi alama za nyakati. Jeshi laa Tanzania la sasa si kama la miaka ya 70, halina imaani, sera wala uzaalendo baada ya kuona mijitu inaharibu nchi naa wao hawapatilizwi. I am sure hakuna mtu atakayepigaana kwa ajili ya magamba. Wee wadhania kinachoishinda DRC ni nini? Si ukosefu wa silaha wala wanajeshi....ni kuwa jeshi halina imani. Wakati huo huo wanapigana na jeshi la Rwanda ambalo, kama Israel, lina itikadi na nidhamu ya hali ya juu. Huwezi kulishinda kipuuzi jeshi kama hilo, uliza Uganda kule Kisangani!
 
Dictator mwingine huyu black Jews JK Akikutaka nusu saa hufikishi upo Mabwe pande we piga kelele usifikiri Sisi ni Wapaka Mkorogo mliozoea kuwachezea Akili
 
Rwanda kwa eneo lake ni ndogo kuliko mkoa wa Kilimanjaro ambao ni mdogo kuliko mikoa yote Tanzania. Tutamkanyaga kama kifaranga cha kuku akithubutu! Asidhani kuwa Tanzania ni kama Congo!

Kwa nini Tanzania si kama Congo? Ni kama na zaidi!
Ah, ngoja tumwone JK apeleke watu wake huko wakauwe, tumechoka kuuawa wenzetu Watanzania kisa wana mawazo tofauti na magamba. Kama ni bingwa kweli wa kuuwa, nafasi hiyo, aende huko.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom