Kabla hujaisema serikali kushindwa jiangalie wewe mwenyewe umeweza kuongoza Familia yako

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,900
Habari za Mwaka Mpya Wakuu!

Kuna Watu ni wepesi sana kutoa vibanzi katika macho ya wenzao ilhali wao wako na boriti.
Serikali imeshindwa!
Rais gani huyo!
Viongozi wa nchi hii ni wajinga sana!
Maneno ni mengi.

Sawa. Ni haki yao. Lakini Haki inapotea pale ambapo mtu hastahili kukosoa kile ambacho yeye mwenyewe kimemshinda.
Mwizi hana haki ya kumhukumu mwizi mwenzake. iko hivyo.
Kipofu hawezi kumwongoza kipofu mwenzake.

Kabla hujaanza kusema Wenzako waliobahatika kuwapata viongozi wa nchi. Wenyewe mnaita kuisema Serikali. Jitathmini, wewe umeweza kuongoza nini kwenye maisha yako? Kama hiyo haitoshi kama unafamilia, jiulize umefanikiwa kuweza kuongoza familia yako?

Familia ni serikali ndogo. Je sheria za familia yako ni za haki? Au ndio zile sheria za Baba hakosei, au mzazi hakosei?
Je unatimiza majukumu yako kama kiongozi ndani ya familia?
Je umeweza kuitiisha familia yako?
Je malengo uliyoyapanga katika familia yako yametimia?

Elewa kuwa, kama wewe katika level ya uongozi wa familia unachangamoto zinazokusibu mpaka kufikia kushindwa kuongoza familia yako ndio hivyohivyo katika level ya kitaifa nako kuna changamoto kubwa za kiwango cha kitaifa zinazoifanya serikali ishindwe kufanya mambo yake.

Kama wewe kwenye uongozi wako wa familia hakuna uaminifu baina yako na mkeo au watoto ndio hivyohivyo katika level ya serikali nako kuna Watu wasio waaminifu.

Kama kwenye familia yako hamna umoja na kila mtu ni mbinafsi. Yaani mkeo anajali maslahi yake na wewe unajali maslahi yako. Ndio hivyohivyo ndani ya serikali mambo yanavyoendelea. Kila kiongozi anajali maslahi yake na familia yake.

Elewa kuwa kama unaona serikali ndio kikwazo cha wewe kuongoza familia yako vizuri basi ndio hivyohivyo hiyo serikali yako nayo inawakubwa wake huko duniani wanayoifanya ishindwe kuongoza vizuri.

Kulaumu wengine kwa jambo lilelile unalolifanya hata kama ni kwa level ya chini ni dalili ya kutojitambua, ubinafsi na kiburi.

Elewa kuwa, viongozi wengi kabla ya kuingia madarakani hufikiria kuwa wakipata madaraka wataleta maendeleo na kufanya makubwa kwa nchi lakini wakiyapata hayo madaraka huona mambo tofauti kwa sababu kumbe kuna changamoto zinazolingana na ukubwa wa madaraka yao. Na wapo wakubwa huko duniani ambao nao wanamaslahi na nchi.

Kama wakati unaanzisha familia yako ulivyokuwa unandoto ya kuongoza familia nao kuipa furaha lakini mambo yanavyoendelea kwa sasa huamini kama kweli ni wewe ya mwingine. Ndio hivyo.

Hakuna cha kusema serikali sijui ina vyombo vya dola, sijui usalama wa taifa sijui nini.
Utawala unahusu zaidi Mtazamo, falsafa, ideology, maadili, Akili na maarifa, utayari, kujitoa, maono.

Hivyo kama ni maendeleo. Huanza katika ngazi ya familia.

Taikon acha apumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Tuseme ule ukweli tu bi mkubwa nchi imemshinda.
Unapokosea kuiongoza familia unakuwa responsible moja kwa moja kwa sababu ni familia yako, lakini kiongozi akikosea wanaoumia ni wananchi na hawi responsible zaidi ya chawa kupiga kelele na kumlinda.

Kingine kuongoza nchi unalipwa, je kuongoza familia unalipwa? unafanya kazi na kuihudumia familia, hakuna mfanano wa mambo mengi.
 
Kupanga ni kuchagua!
Lakini pia inategemea, mtu anaweza asiwe mzuri sana ktk kuongoza familia yake lakini akawa mzuri ktk kuongoza taasisi au organization Fulani kama vile Serikali. So, it depends.
 
Habari za Mwaka Mpya Wakuu!

Kuna Watu ni wepesi sana kutoa vibanzi katika macho ya wenzao ilhali wao wako na boriti.
Serikali imeshindwa!
Rais gani huyo!
Viongozi wa nchi hii ni wajinga sana!
Maneno ni mengi.

Sawa. Ni haki yao. Lakini Haki inapotea pale ambapo mtu hastahili kukosoa kile ambacho yeye mwenyewe kimemshinda.
Mwizi hana haki ya kumhukumu mwizi mwenzake. iko hivyo.
Kipofu hawezi kumwongoza kipofu mwenzake.

Kabla hujaanza kusema Wenzako waliobahatika kuwapata viongozi wa nchi. Wenyewe mnaita kuisema Serikali. Jitathmini, wewe umeweza kuongoza nini kwenye maisha yako? Kama hiyo haitoshi kama unafamilia, jiulize umefanikiwa kuweza kuongoza familia yako?

Familia ni serikali ndogo. Je sheria za familia yako ni za haki? Au ndio zile sheria za Baba hakosei, au mzazi hakosei?
Je unatimiza majukumu yako kama kiongozi ndani ya familia?
Je umeweza kuitiisha familia yako?
Je malengo uliyoyapanga katika familia yako yametimia?

Elewa kuwa, kama wewe katika level ya uongozi wa familia unachangamoto zinazokusibu mpaka kufikia kushindwa kuongoza familia yako ndio hivyohivyo katika level ya kitaifa nako kuna changamoto kubwa za kiwango cha kitaifa zinazoifanya serikali ishindwe kufanya mambo yake.

Kama wewe kwenye uongozi wako wa familia hakuna uaminifu baina yako na mkeo au watoto ndio hivyohivyo katika level ya serikali nako kuna Watu wasio waaminifu.

Kama kwenye familia yako hamna umoja na kila mtu ni mbinafsi. Yaani mkeo anajali maslahi yake na wewe unajali maslahi yako. Ndio hivyohivyo ndani ya serikali mambo yanavyoendelea. Kila kiongozi anajali maslahi yake na familia yake.

Elewa kuwa kama unaona serikali ndio kikwazo cha wewe kuongoza familia yako vizuri basi ndio hivyohivyo hiyo serikali yako nayo inawakubwa wake huko duniani wanayoifanya ishindwe kuongoza vizuri.

Kulaumu wengine kwa jambo lilelile unalolifanya hata kama ni kwa level ya chini ni dalili ya kutojitambua, ubinafsi na kiburi.

Elewa kuwa, viongozi wengi kabla ya kuingia madarakani hufikiria kuwa wakipata madaraka wataleta maendeleo na kufanya makubwa kwa nchi lakini wakiyapata hayo madaraka huona mambo tofauti kwa sababu kumbe kuna changamoto zinazolingana na ukubwa wa madaraka yao. Na wapo wakubwa huko duniani ambao nao wanamaslahi na nchi.

Kama wakati unaanzisha familia yako ulivyokuwa unandoto ya kuongoza familia nao kuipa furaha lakini mambo yanavyoendelea kwa sasa huamini kama kweli ni wewe ya mwingine. Ndio hivyo.

Hakuna cha kusema serikali sijui ina vyombo vya dola, sijui usalama wa taifa sijui nini.
Utawala unahusu zaidi Mtazamo, falsafa, ideology, maadili, Akili na maarifa, utayari, kujitoa, maono.

Hivyo kama ni maendeleo. Huanza katika ngazi ya familia.

Taikon acha apumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Huu ndo ukweli ulio wazi , hii ndo nilikuwa naamini kuwa nikifika ulaya utatuma Sana hela nyumbani na hautakuwa kama wengine lakini ukifika ulaya unashindwa kutuma hela Una Adapt itikadi za kibepari
 
Habari za Mwaka Mpya Wakuu!

Kuna Watu ni wepesi sana kutoa vibanzi katika macho ya wenzao ilhali wao wako na boriti.
Serikali imeshindwa!
Rais gani huyo!
Viongozi wa nchi hii ni wajinga sana!
Maneno ni mengi.

Sawa. Ni haki yao. Lakini Haki inapotea pale ambapo mtu hastahili kukosoa kile ambacho yeye mwenyewe kimemshinda.
Mwizi hana haki ya kumhukumu mwizi mwenzake. iko hivyo.
Kipofu hawezi kumwongoza kipofu mwenzake.

Kabla hujaanza kusema Wenzako waliobahatika kuwapata viongozi wa nchi. Wenyewe mnaita kuisema Serikali. Jitathmini, wewe umeweza kuongoza nini kwenye maisha yako? Kama hiyo haitoshi kama unafamilia, jiulize umefanikiwa kuweza kuongoza familia yako?

Familia ni serikali ndogo. Je sheria za familia yako ni za haki? Au ndio zile sheria za Baba hakosei, au mzazi hakosei?
Je unatimiza majukumu yako kama kiongozi ndani ya familia?
Je umeweza kuitiisha familia yako?
Je malengo uliyoyapanga katika familia yako yametimia?

Elewa kuwa, kama wewe katika level ya uongozi wa familia unachangamoto zinazokusibu mpaka kufikia kushindwa kuongoza familia yako ndio hivyohivyo katika level ya kitaifa nako kuna changamoto kubwa za kiwango cha kitaifa zinazoifanya serikali ishindwe kufanya mambo yake.

Kama wewe kwenye uongozi wako wa familia hakuna uaminifu baina yako na mkeo au watoto ndio hivyohivyo katika level ya serikali nako kuna Watu wasio waaminifu.

Kama kwenye familia yako hamna umoja na kila mtu ni mbinafsi. Yaani mkeo anajali maslahi yake na wewe unajali maslahi yako. Ndio hivyohivyo ndani ya serikali mambo yanavyoendelea. Kila kiongozi anajali maslahi yake na familia yake.

Elewa kuwa kama unaona serikali ndio kikwazo cha wewe kuongoza familia yako vizuri basi ndio hivyohivyo hiyo serikali yako nayo inawakubwa wake huko duniani wanayoifanya ishindwe kuongoza vizuri.

Kulaumu wengine kwa jambo lilelile unalolifanya hata kama ni kwa level ya chini ni dalili ya kutojitambua, ubinafsi na kiburi.

Elewa kuwa, viongozi wengi kabla ya kuingia madarakani hufikiria kuwa wakipata madaraka wataleta maendeleo na kufanya makubwa kwa nchi lakini wakiyapata hayo madaraka huona mambo tofauti kwa sababu kumbe kuna changamoto zinazolingana na ukubwa wa madaraka yao. Na wapo wakubwa huko duniani ambao nao wanamaslahi na nchi.

Kama wakati unaanzisha familia yako ulivyokuwa unandoto ya kuongoza familia nao kuipa furaha lakini mambo yanavyoendelea kwa sasa huamini kama kweli ni wewe ya mwingine. Ndio hivyo.

Hakuna cha kusema serikali sijui ina vyombo vya dola, sijui usalama wa taifa sijui nini.
Utawala unahusu zaidi Mtazamo, falsafa, ideology, maadili, Akili na maarifa, utayari, kujitoa, maono.

Hivyo kama ni maendeleo. Huanza katika ngazi ya familia.

Taikon acha apumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Mimi nimefanikiwa kwenye family lakini serikali hii ni ya matapeli tupu na yameshindwa na yatashindwa. Watanzania mpaka tuamke sote ndiyo tuyashinde
 
Nisiiseme serikali kisa nimekuwa failure kwenye mahusiano binafsi. Si ukichaa huo

Unadhani serikali inapata wapi pesa kama sio kwenye direct and indirect taxes ninazotoa

Unadhani madeni wanayokopa nchi za nje atalipa nani??...

Unadhani failure za mifumo au maamuzi wanayotoa leo ni nani atakaeathirika nayo??....

Halafu familia na uzazi ni kitu social and biological. Si kitu mtu lazma uwe professionally, mentally or financially qualified maana ni msingi wa kila kitu na muendelezo wa vizazi

ila uongozi ni karama maana sio kila mtu anayo ndio maana si kitu ambacho kila mtu anaweza kufanya au apitie,

ni ile ari, uwezo, passion na vision ya mtu binafsi hadi akaamua aingie. Uongozi wa watu ni utumishi maana wao ndio wanakulipa ukawaongelee na ukawasimamie

mwananchi ni boss wa kiongozi maana kama unaelewa mfumo wa uchumi, pesa inatoka kwa watu hivyo, boss akimlaumu au kumfokea mtumishi wake pale anapokuwa anakosea ni tatizo???...

ndio maana nchi za wenzetu viongozi hujiudhuru pale wanaposhindwa kazi kwa sababu wao ni watumishi wa wananchi. Unless huelewi uongozi wa nchi na familia ni vitu viwili tofauti bhasi utakuwa na hakikata ya kuandika ulichokiandika
 
Sijasoma ansiko lako.

Lakini maadui hawa waliotangazwa 1961.
Ujinga , umasikini na maradhi wanazidi kuongezeka kwa kasi sana.

Vipi vitendo vya Kifisadi na mikataba Tata.
Wezi wa viongozi na mashirika.
Fuatilia pia Report ya CAG.

Kinachofanywa na selikali ndio kina reflect maisha ya kawaida mtaani hadi ngazibya Familia.
 
Back
Top Bottom