JWTZ Wakanusha taarifa za kuibiwa Kifaru

JWTZ Wakanusha taarifa za kuibiwa Kifaru

Nilijua tu hii habari lazima Ikanushwe, ila ni vema wangekanusha halafu watupe Ukweli halisi wa jinsi ilivyo maana kwa wengi haituingii akilini.
Ukweli upi unaotaka kuambiwa?? Hao Dira ndo wapeleke reliable source ya habari yao na ushahidi la sivyo wapigwe ban tu, hamna namna!
 
Inawezekana hakikuibwa ila kilisahaulika kwa bahati mbaya nje ya nyumba ya mwanakijii mmoja, wakati wakufanya stock wakagundua kimoja kina misi.
inasemekana pia yy mwandshi kapata hio habari mahakaman...............
 
.hawawezi kukubari ushawai.sikia wanatangaza idadi ya watu wanaokufa mafuntoni
 
Hapo Kauli Sahihi ilikuwa Ni "Mahakama iombe radhi Kwa Jeshi la Wananchi" na si Gazeti Kwani Mwandishi wa Gazeti Ameinukuu Mahakama!!
Lakini Kwa Jeshi Kuibiwa Kifaru Kiuhalisia ni Aibu Kuliko Lugumi, Kwahiyo lazima Wakatae.
Mlinzi wa Nchi kaibiwa!! Aisee......
 
Halafu wapuuzi kama hawa CHADEMA na UKAWA inajitokeza kuwatetea. Tutasikia watachanga fedha kumlipia fidia. Pambafu kweli
Wanawachangia wahalifu tu, yule binti kipepeo wa Mzumbe University aliyepofuka wameshindwa kumchangia hata sh mia ili aende India, lakini wahalifu wanawachangia!!
 
Hivi kama kesi ipo mahakamani na jeshi limekanusha si tayari watuhumiwa wanakuwa huru? Maana inakuwa ni kesi hewa.Kesi ya kubambikiwa
ace0f02b254537533b193804b305fa55.jpg
 
Mambo mengine ukiyafikiria unaweza kupasuka kichwa bure sasa hao wananchi 20 kesi yao inahusu Kifaru yule mnyama?
 
Wakidhibitiwa hawa makanjanja utasikia oooh wanarudisha nyuma demokrasia,uhuru wa vyombo vya habari na majungu mengi sasa mukipewa uhuru ndio kuandika utumbo.
Ombi langu kwa serikali vyombo vyote vya habari vitoe taarifa zao kutoka katika vyanzo vya vyombo vya Serikali na sio kujitafutia habari zao za uzushi.
unawaza kwa kutumia kiungo gani cha mwili mkuu?
 
Kitu ajibu hapo. Jeshi ni aibu na sio rahisi kupataga habari kutoka huko. Na vile vile sio sehemu nzuri kwa waadishi wa habari kupachukulia poah hawawezi kukurupuka. Kukanusha panahitajika ili tusiaibike
 
Ila hapo panawezekana walikamatwa wana kijiji kwa udhibitisho upi na kwa kosa lipi? Naomba jibu.[emoji850][emoji40]
 
Halafu wapuuzi kama hawa CHADEMA na UKAWA inajitokeza kuwatetea. Tutasikia watachanga fedha kumlipia fidia. Pambafu kweli
Mkuu, mwandishi ana shida gani? ameripoti kutoka mahakamani, amemnukuu hakimu.
Je hiyo kesi haipo mahakamani? hakuna shitaka? nilitarajia great thinker kama wewe uende mbali zaidi.
 
kwa porojo za magazeti utasikia kesi ni kwamba jamaa alitaka kuiba kifaru, ila wao wameripoti kifaru kimeibiwa, hv hicho kifaru ni peni labda hao wezi walikiweka mfukoni wakapita getini bila kuonekana nacho? wakifungiwa oooh hakuna uhuru wa habari, kwa habari kama hzi bora uo uhuru wa habari ucwepo
Ndiyo hapo Mkuu ujiulize Serikali yako je inaongozwa na Musukule??
Coz Mwandishi Kaishuhudia Kesi Mahakamani Kuwa Wananchi 20 wameshikiliwa Na Jeshi la Polisi na Kufikishwa Mahakamani Kwa Kosa la Kuiba Kifaru cha JWTZ, sasa Kama Jeshi Linakataa Je, Wakuchukuliwa Hatua ni Nani! Mwandishi au Mahakama??

Na Je Kwanini Hao Wananchi Waliopo Mahakamani Hawaachiwi Huru na Kufutiwa Mashtaka Yao kwasababu Kutokana na Kuwa Jeshi Limeshakataa Kuwa Halijaibiwa, Kwa maana hiyo itakuwa Wamebambikiziwa Kesi?

Mkuu mimi nahisi JWTZ linakimbia aibu tu kwasababu Kuibiwa Kifaru ni Kosa Kubwa Kiusalama.
 
Back
Top Bottom