Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Swali langu ni dogo tu. Wakristu na wengine wataathirika vipi kama tukijiunga na O.I.C?

Kwa kupinga tu kwa vile kinahusu waislamu kunawapa upenyo wenye nia mbaya kupenyeza suala la Mahakama ya Kadhi. Hawa wanawaambia wenzao, wakristu watapinga chochote chenye manufaa kwa WAISLAMU na haya mahakama wanayapinga kwa sababu tu yatawafaidia waislamu kama wanavyopinga OIC! Kwangu mimi hayo Mahakama ya Kadhi kwa muundo wanaopendekeza hayana tija kwa taifa letu, wakristu, waislamu na wengine. Kwa kuyaingiza katika katiba tutakuwa tumekubali system mbili tofauti za haki ziende sambamba. Hii ni hatari sana na inastahili kupingwa na kila mwenye nia njema na nchi yetu.
 
images

Field Marshall Al Haj Dr. Idi Amin Dada
Aliingiza Uganda OIC.


images

Colonel Al Haj Mrisho Jakaya Kikwete
Ataiingiza Tanzania OIC.

Masikini Tanzania - Uganda wanafikiria kujitoa, Tanzania wanajitayarisha kuingia.
 
..hivyo hivyo Fundi Mchundo umekuwa ukiunga mkono Tanzania kujiunga na OIC. nipe kauli/nasaha utakazotumia kuwatuliza wale wanaokuunga mkono ikiwa serikali itachukua uamuzi tofauti na matakwa yao.

JokaKuu! Sidhani kuwa ni nafasi yangu mimi kumtuliza yeyote atakayeudhika na uamuzi wowote utakaochukuliwa na serikali. Nilishaonya hapo mwanzoni kuwa kwa kutanguliza kwanza udini, kwa pande zote mbili, ndiko kutakakotuletea matatizo hapo mbeleni. Wakristu kwa kusema waziwazi na kwa majigambo kuwa ni jukumu lao kama wakristu kulipinga suala hili ni dalili mbaya. Kwa waislamu nao kudai kuwa kujiunga huku ni haki yao kama waislamu (si watanzania) nako kutatupeleka huko huko. Inabidi pande zote mbili iweke pembeni udini wao na kutanguliza maslahi ya taifa letu kwanza. Kwangu mimi chombo chochote kitakachomletea maendeleo yeyote katika jamii yetu awe muislamu, mkristu, aliye na ulemavu, mwanamke n.k. kinaleta maendeleo kwa taifa. Kuwepo kwa uhusiano huo haunipunguzii au kuniondolea haki zangu za kikatiba za kuabudu nitakavyo, kwenda nitakako, kutafuta elimu ninakotaka n.k. Ndio maana mimi kama mkristu sioni tatizo kwetu sisi kujiunga na chombo hiki. Lakini kama baada ya majadiliano na uchunguzi wa kina na wazi, ikionekana kuwa hakitufai, basi kama raia wa nchi yangu ni lazima nikubaliane na maamuzi ya wale niliowachagua kuniwakilisha. Hata kama hayanifuraishi. Hao wanaoleta vitisho ni wapuuzi. Hakuna mtu anayejiita moderate atakaekubali amani katika nchi yake ivunjwe kwa sababu yeyote. Tunaamini katika kuvumiliana katika tofauti zetu. Na si vinginevyo.

Amandla.........
 
Kati ya masuala yote yanayolikabili Taifa leo hii, suala la OIC ndilo rahisi zaidi kulishughulikia na pande zote zinakuwa na furaha.
 
mnazunguka tuuu mkidhani nchi yenu wakati hata Uhuru wenyewe mmedandia jahazi!


Well, ITAWEZEKANA na Waislaam watabakia BARA labda itakuwa vizuri kama Wakristu wakiondoka wasogee huko Kongo na Burundi..


mkandara kati ya watu ninaowaheshimu hapa forum ,,,,..ni wewe ..nakuchukulia kama intellectual na mawazo yako huwa nayatafakari kwa kina ..nakuchukulia kama ninavyowaheshimu wanaforum wote akiwemo FMES,MWANAKIJIJI,A.MOSHI,REV,JASUSI...ET AL.....

LAKINI SIAMINI KAMA UNAWEZA KUWA NA MAWAZO FINYU KAMA HAYA.....PLEASE YO CAN DO BETTER THAN THIS!!!

...HISTORIA YA UHURU WA NCHI HII HAIPINGIKI...LAKINI MNATAKIWA MJUWE KUWA TULIKUWA HATUTAFUTI UHURU WA MZIZIMA..TULIKUWA TUNATAFUTA UHURU WA TANGANYIKA............HESHIMA KUBWA NAWAPA WAZEE WA MZIZIMA ...LAKINI HAWAKUWA NA MAWAZO YA KUENEZA CHAMA BEYOND ILALA......CHAMA KILIJIKITA ZAIDI KWENYE SIASA ZA MJINI...chama kilianza kuenezwa tanganyika nzima baada ya kuwakaribisha WAMLIMA...[WATU WA BARA]....NDIO HAPO JUHUDI ZA KUDAI UHURU ZIKAUNGANISHWA...

LA SIVYO leo tungekuwa na MZIZIMA huru,....LAKE VICTORIA nao wangedai uhuru kivyao,KUSINI NA NYANDA ZA JUU[HIGHLANDS],kivyao..na OFFCOURSE juhudi pia za kudai uhuru kama NORTH zilikuwa wazi......

kimsingi tunawashukuru veterans wa BURMA..WW2 kwa kuanzisha vuguvugu...lakini si halali kubeza UMOJA WA KITAIFA......NA NI TUSI KUSEMA KUWA WATU WA MIKOANI WALIDANDIA JAHAZI......

MKANDARA NADHANI HUFANANI NA SIASA ZA UTENGANO..kama tumeishi kwa umoja na amani miaka yote hiyo bila OIC wala KADHI[na ieleweke hatupingi hii mahakama ILA TUNATAKA HII MAHAKAMA IWE NI CHOMBO CHA WAISLAMU WENYEWE ...pasipo kugharamiwa na serikali...mkandara unafikiri ni vema kodi zetu zigharamie kadhi...]///MAHAKAMA IS WELLCOME ANYTIME!!!

LAKINI OIC ...NO...TUULINDE UMOJA WETU PLEASE..KWA NINI TUNATAKA KULETA KITU KITACHOWAACHA SECTION YA NCHI YETU KUBWA HII IKIWA NA MAJOZI.....tukiamua KUPIGANA HAPA WOTE TUTATOKA DAMU...HAKUNA ANAYEVUJA MAJI ....!!
 
Na ajabu anashambuliwa kama mkristu aliyepotea kiasi kwamba ni dini tupu inayoongoza hoja za hapa. Trust me hili swala halitakwisha kwa amani na inatisha sana!

Kwamba Membe ana kichwa sana, hapana Membe ni opportunist kama all politicians, alikuwa rafiki wa Kitine, lakini ilipofikia kuchagua between power na urafiki wao akamsaliti na kuchagua power,

majuzi baada ya kugundua kua amekurupuka, amewatafuta maaskofu kwa siri na kujaribu kuwaomba msamaha na kwamba sio yeye chanzo cha hili sagga,

Off course ukiwaambia wananchi wowote duniani ambao taifa lao sio la Kiisilamu, wajiunge na shirika la Kiisialmu, lazima kutakua na mfarakano tena mkubwa sana, hapa tatizo ni incompetence ya viongozi wetu wa sasa, sio wananchi, katiba za OIC ziko wazi sasa hawa viongozi vilaza wanakuja na hizi nyepesi nyepesi hatuwezi kuwakubalia, maana maovu waliyokwisha tufanyia hili taifa yanatosha tayari.

Mimi msimamo wangu bdo uko pale pale na not only that naomba niwe mkweli kwamba toka Membe aseme hizi pumba I have been working around the clock ku-rewach out wanaoshusika na maamuzi ya mwisho on this ishu kwamba wananchi wengi hatukubaliani kabisa na haya maneno ya kujiunga na OIC, na sababu yangu muhimu ni moja tu kwamba hilo shirika la OIC ni la Waisilamu na sisi Tanzania sio taifa la wasiilamu, zaidi ya hapo siamini kwamba kuna maelezo zaidi wala apologies kwa anybody.
 
Mimi naomba nipate ufafanuzi kabala sijaingia ndani zaidi katika mada hii.Kuna nchi wanachama wa OIC kama Benin,Burkina Faso,Cameroon,Chad,Cote D'Voir,Gabon,Gambia,Guinea,Guinea Bissau,Mozambique,Niger,Nigeria,Senegal,Togo na Uganda.

Kuna mjadala wa kitaifa uliowahi kufanyika katika nchi tajwa kabala ya kuijiunga na OIC?Kama hakuna ni kitu gani ambacho wale wanaopinga Tanzania kujiunga na shirika hili kinachowatia hofu?

Baada ya kujiunga kwa nchi tajwa hapo juu kuna faida au hasara gani walizozipata baada ya kujiunga?

Kuna nchi iliyojivua uanachama kutokana na sababu zozote zile?
 
Mimi msimamo wangu bdo uko pale pale na not only that naomba niwe mkweli kwamba toka Membe aseme hizi pumba I have been working around the clock ku-rewach out wanaoshusika na maamuzi ya mwisho on this ishu kwamba wananchi wengi hatukubaliani kabisa na haya maneno ya kujiunga na OIC, na sababu yangu muhimu ni moja tu kwamba hilo shirika la OIC ni la Waisilamu na sisi Tanzania sio taifa la wasiilamu, zaidi ya hapo siamini kwamba kuna maelezo zaidi wala apologies kwa anybody.

Na usiuache msimamo huo.
Membe anatakiwa kufafanua baadhi ya mambo aliyoyasema. Aliposema kuwa SERIKALI imefanya utafiti, ebu atueleze huyo SERIKALI ni nani hasa? Anaposema NCHI inaweza kujiunga OIC na hakutakuwa na madhara, huyu NCHI anayemtaja ni nani hasa. Inakuwaje SERIKALI ifanye utafiti wa suala hili na aonyeshe mwelekea wa NCHI kutaka kujiunga bila utafiti huo kuwahusisha WANANCHI ambao ndio wenye NCHI inayotakiwa kujiunga huko OIC?
Kama anamaanisha kuwa Baraza la Mawaziri (kwa maana ya serikali) ndilo lililofanya utafiti huo, afahamu kuwa huo ni utafiti finyu kwa sababu NCHI hii ni zaidi sana ya Baraza la Mawaziri.
Imefika wakati sasa wakae chini na kuanza kuwasikiliza WANANCHI wanasema nini
 
Kati ya masuala yote yanayolikabili Taifa leo hii, suala la OIC ndilo rahisi zaidi kulishughulikia na pande zote zinakuwa na furaha.
Nakubakiana na kauli hii. Hivyo Maaskofu full-stop. Masheikh full-stop. Wapenzi na washabiki wa siasa full-stop, Maamuma full stop. Tuiachie Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mhe. Membe ifanye kazi yake. Tutafikia pahala na naamini -pande zote zinakuwa na furaha.
 
Nakubakiana na kauli hii. Hivyo Maaskofu full-stop. Masheikh full-stop. Wapenzi na washabiki wa siasa full-stop, Maamuma full stop. Tuiachie Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mhe. Membe ifanye kazi yake. Tutafikia pahala na naamini -pande zote zinakuwa na furaha.
We acha hiyo!
Huu msururu wa mambo tunayoyalalamikia leo hii umefanywa na nani, si serikali hii hii!. Mbona basi hatuna furaha?, la msingi hapa ni kupiga kelele mpaka wakose raha. Natukose yote lakini amani ibaki.
 
We acha hiyo!
Huu msururu wa mambo tunayoyalalamikia leo hii umefanywa na nani, si serikali hii hii!. Mbona basi hatuna furaha?, la msingi hapa ni kupiga kelele mpaka wakose raha. Natukose yote lakini amani ibaki.
Amani utaipata wapi yakhe!!! kama utakuwa unakosa uadilifu wa kuwaridhisha wadau wako wote sawia.
 
PM: narudia you are just a paper tiger!

Wewe na jopo lenu la maaskofu hamuwezi kuziwia maamuzi yasifanyike.

Wenye utaifa ni wale walio wakaribisheni mjini na makaputura na leo mnawatukana.

Nyinginezo ni ngonjera na chuki mlizopandikizwa.

NN.
 

Tanzania sio taifa la wasiilamu, zaidi ya hapo siamini kwamba kuna maelezo zaidi wala apologies kwa anybody.
Lakini Kuna waislamu humu - Ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Na naamini kuwa Taifa ni watu-sio mbuga za wanyama , migodi ya dhahabu au miti ya mikarafuu. Kama ni Taifa kwa nini lisijali maslahi ya watu wenye hilo Taifa?
 
Imani jamani imani. Kama kuna sehemu nyeti za kuchezea maisha ya watu basi ni pamoja na kuchezea imani zao katika maisha. Watu wako tayari kwenda an extra mile to defend what they believe in. No question about that. Aidha wewe ni muislam au mkristo, basi lazima ungefanya juhudi zozote zile pale unapohisi mtu anajaribu kuyumbisha/kuchezea imani yako. Suala la OIC na ofisi ya kadhi pamoja na mahakama ya kadhi, linaweza kuwa sio kubwa kama tunavyolitafsiri wakristo. Suala naloliona hapa ni ukosefu wa elimu husika. Miongoni mwa waislamu pia kumekuwa na ushabiki tu bila kujua faida za kujiunga na OIC au kuwa na mahakama ya kadhi. Serikali ingetumia busara na kutoa elimu kwa wakristo na waislam juu ya faida na hasara za kujiunga na OIC au kuwa na ofisi ya kadhi na kuwa na mahakama ya kadhi.

Kwa wale wenzangu na mimi tuliojaribu kufanya utafiti kidogo kuhusu haya masuala, nadhani wengi watakubaliana na mimi kwamba hakuna kinachotisha hapa. Hoja kubwa na ya msingi kwa upande wa ofisi ya kadhi ni funding. Kwamba hii isiwe taasisi ya kiserikali na wala isiendeshwe kwa kodi za wananchi. Lakini hoja la kuwa na hiyo ofisi na mahakama ya kadhi, sidhani kama inahusiana na ukristo au dini nyingine yoyote.
 
Tanzania ni nchi huru na kila mwananchi anaabudu anavyotaka bila ya kuzuiwa na serikali kwani katiba ya nchi haiingilii dini yoyote. Kama serikali ikiamua kujiunga na OIC watakofanikiwa si waislamu bali ni watanzania wote kwa mujibu wa katiba ya OIC.
Kama wakristo pia nao watakuwa na mahakama yao pia si vibaya. Itabidi kwamba Waislamu wahukumiwa na mahakama ya Kadhi na Wakristo nao wahukumiwe na Mahakama ya Padre , na whindu nao wahukuwiwe na mahakama yao na Wayahudi nao pia wahukumiwe na mahakama ya Kijahudi.

Kusema kweli kelele za bure tu kwani Usislamu, na Ukristo na Uyahudi zote ni Dini moja tu. Ndio maana kwenye Qur’ani imeandikwa kwamba TAFAUTI ZENU (za kidini) MUNDU ATAWAELEZA SIKU YA KIYAMA.

Hapa Duniani mnasumbuana bure tu.
 
PM: narudia you are just a paper tiger!

Wewe na jopo lenu la maaskofu hamuwezi kuziwia maamuzi yasifanyike.

Wenye utaifa ni wale walio wakaribisheni mjini na makaputura na leo mnawatukana.

Nyinginezo ni ngonjera na chuki mlizopandikizwa.

NN.

Mtu mzima unatoa kauli kama hizi ..mtoto naye afanyeje?

Ndo maana nilipendekeza 'nchi iuzwe, na kila raia apewe chake' ili wanaotaka kujiunga na OIC, kuanzisha sharia etc sio tu wafanye hivyo bali hata wamwite kabisa Sultan toka Oman aje awatawale..

Hii nchi coexistance nadhani imeshafikia ukomo..

Hio naona itakuwa tiba ya kudumu.
 
pm: Narudia you are just a paper tiger!

Wewe na jopo lenu la maaskofu hamuwezi kuziwia maamuzi yasifanyike.

Wenye utaifa ni wale walio wakaribisheni mjini na makaputura na leo mnawatukana.

Nyinginezo ni ngonjera na chuki mlizopandikizwa.

Nn.


.....nungunungu wewe nakujuwa...nilikuwa najaribu kujibu hoja za mkandara.....i cant believe kama hoja zako zina uzito wa za mkandara ...or vice versa.... As i said i respect him.....

Ingekuwa wewe ndio umetowa hiyo hoja nisingeshangaa......

...lakini napenda kukukumbusha ..kuwa uhuru ulikuwa hautafutwi wa mzizima....bali wa tanganyika...,nakubali kuwa wazee waliotoka burma walikuja na vuguvugu kubwa na hawa walienea nchi yote......dar es salaam kama ilivyoleo ilikuwa na nguvu ya mawasiliano....lakini lazima ujuwe kulikuwa na kazi kubwa ya kuitoa taa au tanu kutoka kwenye urban influence hadi kuifanya national party ......sio mambo ya kubeza kaputula...wakati kaptula lilikuwa vazi la wasomi........

..tambueni kuwa vugu vugu la kudai uhuru lilikuwa nchi nzima......kuanzia bukoba ....hadi mbeya....
Maeneo kama kaskazini walishakuwa hadi na bendera....mwanza tayaru walikuwa mbali na nyanza yao........sasa unafikiri kazi ya kufanya kuunganisha nguvu ya wapigania uhuru ingefanikiwa bila kupeleka chama mikoani,,,,

....ukijaribu kuliangalia hili la kufanya chama kiwe cha kitaifa ..utaona tatizo linalokumba vyama vya upinzani leo hii vinavyofikiri chama ni kukaa dar es salaam...vingi vinakufa,vitakavyowafuata wenye nchi mikoani vitabakia.......

.....naomba tuondokane na fikra potofu ya kubeza juhudi zilizofanywa na wana vuguvugu la uhuru la mikoani.......kumbukeni watu kama kina japhet kiliro....,na wengine wengi ..juhudi zao zilishafika ...hadi kuhutubia un..........bila kuunganisha nguvu ....hii nchi ingekuwa na free states nyingi sana......
 
Tanzania ni nchi huru na kila mwananchi anaabudu anavyotaka bila ya kuzuiwa na serikali kwani katiba ya nchi haiingilii dini yoyote. Kama serikali ikiamua kujiunga na OIC watakofanikiwa si waislamu bali ni watanzania wote kwa mujibu wa katiba ya OIC.
Kama wakristo pia nao watakuwa na mahakama yao pia si vibaya. Itabidi kwamba Waislamu wahukumiwa na mahakama ya Kadhi na Wakristo nao wahukumiwe na Mahakama ya Padre , na whindu nao wahukuwiwe na mahakama yao na Wayahudi nao pia wahukumiwe na mahakama ya Kijahudi.

Kusema kweli kelele za bure tu kwani Usislamu, na Ukristo na Uyahudi zote ni Dini moja tu. Ndio maana kwenye Qur’ani imeandikwa kwamba TAFAUTI ZENU (za kidini) MUNDU ATAWAELEZA SIKU YA KIYAMA.

Hapa Duniani mnasumbuana bure tu.

kWA NINI NI SISI Wa-Afrika ndiyo tunalumbana sana kuhusu Uislamu na ukristo? Why only us in Africa/Tanzania? We have our own land, culture, freedom, sea, natural resources and our own people! Why we are bothered by issues like IOCs and religions? I am afraid we are wrong somewhere, IQ? Difficult to say! What is our priority as a nation? We are the poorest of the poors; we cannot eat enough food, we are living in shelterless shelters; we are technically backward; still we are not taking our own priorities as serious issues: Agriculture, Education, medicare, housing, infrastructure etc.

IOC or any organization will never benefit us if ourselves are not keen of our own problems; no one will come to solve our problems from IOC or anywhere. Even the rulers in our government are crazy taking issues for granted; they are the one to observe priorities. We have now replaced "begging" for hard work. Everybody in the government and in the general population is of the same opinion; thinking by joining IOC or such organization then wealth will come! Wealth comes by proper planning and hardwork NOT begging or fighting for hadouts from donors!! Work up cretins!
 
kWA NINI NI SISI Wa-Afrika ndiyo tunalumbana sana kuhusu Uislamu na ukristo? Why only us in Africa/Tanzania? We have our own land, culture, freedom, sea, natural resources and our own people! Why we are bothered by issues like IOCs and religions? I am afraid we are wrong somewhere, IQ? Difficult to say! What is our priority as a nation? We are the poorest of the poors; we cannot eat enough food, we are living in shelterless shelters; we are technically backward; still we are not taking our own priorities as serious issues: Agriculture, Education, medicare, housing, infrastructure etc.

IOC or any organization will never benefit us if ourselves are not keen of our own problems; no one will come to solve our problems from IOC or anywhere. Even the rulers in our government are crazy taking issues for granted; they are the one to observe priorities. We have now replaced "begging" for hard work. Everybody in the government and in the general population is of the same opinion; thinking by joining IOC or such organization then wealth will come! Wealth comes by proper planning and hardwork NOT begging or fighting for hadouts from donors!! Work up cretins!

Thank you very much sir/madam! Ujumbe murua kabisa kwa JK na kundi lake..
 
Imani jamani imani. Kama kuna sehemu nyeti za kuchezea maisha ya watu basi ni pamoja na kuchezea imani zao katika maisha. Watu wako tayari kwenda an extra mile to defend what they believe in. No question about that. Aidha wewe ni muislam au mkristo, basi lazima ungefanya juhudi zozote zile pale unapohisi mtu anajaribu kuyumbisha/kuchezea imani yako. Suala la OIC na ofisi ya kadhi pamoja na mahakama ya kadhi, linaweza kuwa sio kubwa kama tunavyolitafsiri wakristo. Suala naloliona hapa ni ukosefu wa elimu husika. Miongoni mwa waislamu pia kumekuwa na ushabiki tu bila kujua faida za kujiunga na OIC au kuwa na mahakama ya kadhi. Serikali ingetumia busara na kutoa elimu kwa wakristo na waislam juu ya faida na hasara za kujiunga na OIC au kuwa na ofisi ya kadhi na kuwa na mahakama ya kadhi.

Kwa wale wenzangu na mimi tuliojaribu kufanya utafiti kidogo kuhusu haya masuala, nadhani wengi watakubaliana na mimi kwamba hakuna kinachotisha hapa. Hoja kubwa na ya msingi kwa upande wa ofisi ya kadhi ni funding. Kwamba hii isiwe taasisi ya kiserikali na wala isiendeshwe kwa kodi za wananchi. Lakini hoja la kuwa na hiyo ofisi na mahakama ya kadhi, sidhani kama inahusiana na ukristo au dini nyingine yoyote.

Watatoa ELIMU gani wakati wao ni UPE wa Elimu hiyo! Kilichotufikisha hapa ni USHABIKI wa hao WASERIKALI! Historia inaonyesha kuna upande mmoja wa dini umekuwa na UVUMILIVU kiasi kwamba sasa UVUMILIVU umekwisha. Kama waswahili wanavyosema, WAMELIKOROGA NA SASA WANAPASWA KULINYWA! Membe alisema Wizara yake imeshafanya UTAFITI na kugundua kuwa HAKUNA tatizo TZ ikijiunga na OIC jana Mkulu anasema Wizara ya Mambo ya Nje bado inafanya UTAFITI! WATALINYWA!!???
 
Back
Top Bottom