Makucha
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 258
- 35
Ndg. Mdondoaji, ukwleli suala la mahakama ya kadhi inatokana na dini ya Kiislamu na wafuasi wake na kwahiyo ni kwa ajili ya waumini wa dini hiyo. Katika nchi ambayo haina dini lakini yenye uhuru wa kuabudu itakuwa makosa kupinga mahakama ya kadhi ndani yao ya Kiislamu na kwahiyo hata nguvu ya uwekwaji na utekelezaji wake sharti utoke ndani dini ya Kiislamu. Kwa mfano, wakristu wanaamini mume mmoja mke mmoja tofauti na waislamu na utekelezaji wake unaishia ndani ya dini husika. Hivyo, mke anapopinga mume wake kuoa mke wa pili tu sheria za dini huzingatiwa na mlalamikaji huelekezwa wasuluhishwe kidini. Mawazo hapa ni woga kuwa dini inaweza kuamua kosa amabalo si la jinai na bado serikali ikahoji ni vipi uamuzi huo ukafanywa. Hapa ni statement tu pengine angefafanua kwa mfano. Ukweli ni kwamba tanzania inatambua uwepo wa dini mbali mbali na imani zao na hivyo uamuzi uliozingatia misingi ya kidini hauna tatizo na serikali. lakini mwanya huo ukitumika kumnyima haki raia ni sharti mahakama ya serikali iingilie kati. Na hata hizo mahakama za kadhi kama hazina rufaa kuna uwezekano wa kuwa na harufu ya uonevu maana zinaamriwa na binadamu na anaweza kukosea katika uelewa wa kunukuu ibara fulani, kutenda haki (chuki yeye kama binadamu kutokana na mahusiano mengine kati yao, nk.) na hapa ndipo umuhimu wa rufaa unakuja kudumisha haki na imani kwa mahakama.
Lakini tofauti na nchi inayoendeshwa kwa misingi ya dini, nchi isiyo ya kiislamu haiwezi kulaumiwa kwa kukosa mahakama ya kadhi. Tuzungumuzie precedence hii kwa Tanzania. Tanzania tuna dini na madhehebu mengi sana ya dini ambazo zinaongezeka kila kukicha na ukiruhusu mahakama ya kadhi utazuiaje dini zingine kuja na madai ya mahakama zao na kama utaruhusu tutakuwa na mahakama ngapi na kwa umuhimu gani gharama hizo? Ni dhahiri kutakuwa na tatizo la mwingiliano na udhibiti wa mwenendo na uendeshaji wa mahakama hizi za dini. Gharama za shughuli ya dini hugharimikiwa na waumini wake ikiwa ni pamoja na misaada ya hiari tu.
Kwa kifupi tukumbuke, msingi wa dini ni imani (na mkataba wa dini na mfuasi wa dini ni imani tu) kwa muda wote ni hiari na hudumu kwa nguvu ya imani ambapo wakati wowote mtu anaweza kubadili bila masharti pindi apatapo ufunuo mpya katika imani yake, mara nyingi kuhusu maisha baada ya kifo au chanzo cha kuwapo tunavyoviona na kuvihisi (uumbaji).
Mimi baada ya kusema hayo, bado sijajua waislamu watakosa haki gani katika hali ya sasa na shria zake kuhusu hayo wanayoyataka katika mahakama ya kadhi wakati serikali imeruhusu mahakama ya kadhi ndani ya dini kwa ajili ya waumini wao na kwa gharama ya waumini wao na zaidi kuwa wakitaka kuomba msaada wa serikali kifedha ruksa kutegemea maamuzi na uwezo wa serikali. Hapa nini zaidi. Wawe wawazi kama ni gharama waseme na kama ni kutaka mahakama hiyo iendeshwe ki-imra waseme pia, yote haya yanazungumzika. Kwahiyo haya ni maoni yangu kwa sasa kuhusu pro and cons yaani sipingi ila kwanza nielemishwe.
Lakini tofauti na nchi inayoendeshwa kwa misingi ya dini, nchi isiyo ya kiislamu haiwezi kulaumiwa kwa kukosa mahakama ya kadhi. Tuzungumuzie precedence hii kwa Tanzania. Tanzania tuna dini na madhehebu mengi sana ya dini ambazo zinaongezeka kila kukicha na ukiruhusu mahakama ya kadhi utazuiaje dini zingine kuja na madai ya mahakama zao na kama utaruhusu tutakuwa na mahakama ngapi na kwa umuhimu gani gharama hizo? Ni dhahiri kutakuwa na tatizo la mwingiliano na udhibiti wa mwenendo na uendeshaji wa mahakama hizi za dini. Gharama za shughuli ya dini hugharimikiwa na waumini wake ikiwa ni pamoja na misaada ya hiari tu.
Kwa kifupi tukumbuke, msingi wa dini ni imani (na mkataba wa dini na mfuasi wa dini ni imani tu) kwa muda wote ni hiari na hudumu kwa nguvu ya imani ambapo wakati wowote mtu anaweza kubadili bila masharti pindi apatapo ufunuo mpya katika imani yake, mara nyingi kuhusu maisha baada ya kifo au chanzo cha kuwapo tunavyoviona na kuvihisi (uumbaji).
Mimi baada ya kusema hayo, bado sijajua waislamu watakosa haki gani katika hali ya sasa na shria zake kuhusu hayo wanayoyataka katika mahakama ya kadhi wakati serikali imeruhusu mahakama ya kadhi ndani ya dini kwa ajili ya waumini wao na kwa gharama ya waumini wao na zaidi kuwa wakitaka kuomba msaada wa serikali kifedha ruksa kutegemea maamuzi na uwezo wa serikali. Hapa nini zaidi. Wawe wawazi kama ni gharama waseme na kama ni kutaka mahakama hiyo iendeshwe ki-imra waseme pia, yote haya yanazungumzika. Kwahiyo haya ni maoni yangu kwa sasa kuhusu pro and cons yaani sipingi ila kwanza nielemishwe.