Google wewe, bila Holy see hakuna nchi inayoitwa Vatican City, kifupi huwezi kuzitenganisha kwani hata rais wake yuko chini ya Papa. vatican kuna aina mbili ya mabalozi wapo wanaowakilisha nchi pekee na wapo wanaowakilisha nchi na Holy see, balozi wao Tanzania anawakilisha vyote.
Na tunabisha kitu gani haswa? ikiwa sisi wote tumeona jinsi Vatican ilivyoweza kuwasaidia Wakristu na hata mnajisifia kwa elimu, iweje iwe taabu sana kusikia kuna chombo cha Waislaam kinachotaka kuwasaidia kama nyie mnavyojivunia? au nchi yetu ina dini moja..Na kwa jinsi mnavyopinga yaonyesha wazi kuna jambo hapa hatulijui sisi tunaotazama sarufi kwa pande zote mbili..Yapo mabenki ya kikiristu lakini mkisikia ya Kiislaam haiwezekani hii sio nchi ya kiislaam..
Na hulka ya kibinadamu inatuumbua sote.. Jaribu kufikiria wewe mwenyewe ama fanya utafiti wako binafsi. Ni watoto wangapi wa Kikristu hujisikia huru studing at Muslim schools or Muslims at Catholic schools?.. ukweli ni kwamba kati ya 10 only few and could be none lakini kwa sababu hawana jinsi watasoma shule zinazoongozwa na dini nyingine.
Kama kweli nchi yetu haina dini basi shule, Hospital na huduma zote za kijamii zisiwe za kidini bali liwe ni jukumu la serikali iliyopo madarakani hapa tutaondoa matatizo mengi ya kidini ndani ya serikali, lakini kama dini zitaingilia kazi na huduma za serikali tutasemaje kwamba nchi yetu haina dini wakati dini ndizo zinatoa huduma?