Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Mtu anayekataa kuundwa kwa mahakama ya kadhi lazima atakuwa na kasoro.Mahakama ya kadhi ni ibada kwa ndugu zangu waislamu.Tatizo linakuja pale watu wanapotaka kulazimisha mahakama ihudumiwe na serekali.Tangu lini serekali ikatumia kodi zake kuhudumia ibada za dini yoyote.

Mheshimiwa Pinda katoa ufafanuzi mzuri sana ndugu zangu waislamu tuwache kulalama tunatakiwa kuunda mahakama ya kadhi ndani ya taasisi zetu kama BAKWATA na taasisi nyingine zitakazoonekana zinafaa.

Tanzania inatakiwa kutumia muda na rasilimali zake kuondoa umaskini kwa wananchi wake mambo ya ibada yafanywe na taasisi za dini bila kuihusisha serekali.Serekali inaweza kusaidiana na madhehebu mbalimbali katika masuala kama elimu na afya.Baadhi ya wachangiaji wanashindwa kuona tofauti kati ya masuala yanayohusiana na imani na yale yanayosaidia jamii kama mahospital,shule na vyuo.
 
nadhani hata ile misamaha ya kodi iliofutwa irejeshwe kwani itasaidia kwa tz. makanisa yakubali kurejeshewa kodi

Mkubwa unaonekana unapenda kweli ligi za kidini, hivi unaelewa ile misamaha haikuwa kwa wakristu tu? Hivi unajua hata taasisi za kiislamu zinanufaika na misamaha hiyo? Unajua hata taasisi za kina Agakhan zinanufaika? Inabidi tufike mahali tukisikia kitu tujaribu kukiangalia in 3 dimensions kwanza, maana inavyoonekana ni kama wazee hatuangalii content ya kitu ila nani kasema au inahusu dini gani! Hiyo si sawa nadhani
 
Pinda amewapindisha hasa waislamu wasioelewa..kama mwataka mahakama ya kadhi nendeni mkawaombe hao waarabu wawapeni pesa za kuendesha mahakama zenu.
 
nijuwavyo mimi itawashinda tu!!!
kutokana na sheria zake,vingozi wenyewe zitawashinda.


MTOTO AKILIA WEMBE APEWE😕
 
Nisaidiwe statisticts ya wafungwa wangapi wa*s**m na wangapi wa***to in comparison with our population statistics,then we can deeply discuss it.
 
kutokana na mkataba kati ya makanisa na gov ndio maana wanavyanzo vingi. missada mingi kutoka Ulaya kwa ajili ya makanisa ndio chanzo, Ubalozi wa Vertican pia, waislam huewekewa vikwazo. sasa ikiwa mtoto mmoja unamsomesha ulaya na mwengine usimpe eLimu halafu akiwa mkubwa umsimange nani mkosa?

KAMA ELIMU YAKO ITAKUWA IMEZIDI DARASA LA SABA NITASHANGAA SANA. KAMA UMEMALIZA O-LEVEL BASI KATIKA SHULE ZA KIISLAMU.

The fact is , hata seminary na hospitali za kiislamu zinanufaika na msamaha wa kodi kwa taasisi za kidini, the problem is, waislamu wana shule na hospitali chache, so they dont feel the effect of tax exemptions to religious organizations. THINK BIG!! PERIOD!!!!!!!
 
kama inahudumia wote mbona makanisa yalikuwa mbele, nadhani irejeshwe tuone kama watz wataathirika

We mtu hatari sana - waweza kuonja sumu? Eti uone kama waTz wataathirika?
Sikutarajia kama kuna mtu makini anayeweza kuwa na mawazo ya namna hii.
Pili unapaswa kujua kuwa hata waislamu walilalamika!
 
Wakuu, kwa mujibu wa matangazo ya BBC yanayoendelea kusikika hivi sasa, Waziri mkuu Pinda ametoa update kwenye hii ishu ya mahakama ya kadhi

kwa jinsi nilivoweza kusikia,

Serikali haina tatizo na uanzishwaji wa mahakama hiyo, ila inachowaomba ni kuwa kwa kuwa suala hili lina sura ya kidini, kuuingiza dola italifanya lie na mtizamo wa kidola dola

kwa hiyo waangalie uwezekano wa kuianzisha ndani ya dini ya kiislamu ili isiwe na sura hiyo,

Nimeliona nilichomeke hapa kwa vile kuna wanaodhani kuwa serikali imekubali/kataa uanzishwaji wa mahakama hiyo kulingana na mijadala mbali mbali inayoendelea hapa

Kwa maoni yangu, nadhani waziri mkuu amechukua maoni ya wengi kuwa sawa, wawe na mahakama hii lakini sio kuihusisha serikali.

mlioko Dodoma mnaweza kutupa updates zaidi.
 
Tatizo ni kuwa kama msimamo ni huu, kwa nini kunakuwa na danadana ya kuanzishwa kwa mahakama hii? Labda sasa wanaohusika na uanzishwaji wake wataianzisha mara moja
 
Nadhani huo ndo uamuzi mzuri, inabidi tusichanganye dini na siasa. Kama kweli kadhi atasimamia sheria za kiislamu inabidi tuwaachie waislamu waianzishe bila mikono ya serikali kuingilia.
 
Tatizo ni kuwa kama msimamo ni huu, kwa nini kunakuwa na danadana ya kuanzishwa kwa mahakama hii? Labda sasa wanaohusika na uanzishwaji wake wataianzisha mara moja


Mkuu MN, nadhani hapo ndo tutajua mbivu na mbichi, wachangamke waanzishe tu na mjadala huu ufungwe wala usifike tena viwanja vya bunge!
 
1.Kama watu wanajua historia ya nchi hii ni kwamba hii mahakama ilikuwepo tangu kipindi cha ukoloni.
2.Kuhusu alichosema Pinda,angetakiwa kujiuliza awali hii mahakama ilikuwa inahudumiwa na nani?Lakini pia,angestahili kuchukua baadhi ya nchi ambako mahakama kama hii iko na inafanya kazi kama vile UK,Uganda nakadhalika halafu ndiyo atupatie jibu nani anastahili kuihudumia hii mahakama.Kwasababu kwa hii habari iliyoripotiwa hapa bado haina jibu la nani atakae hudumia!
Hata hivyo hizo mahakama nyingine zinahudumiwa na nani?Kama maamuzi yatabakia kama Pinda alivyosema basi ni full ubaguzi na siyo vinginevyo.
Hii ni sawa na mvulana kuingia choo cha kike and vice-versa is true.

Kama UK wanaruhusu ndoa za jinsia moja tukubaliane nao kama mfano? Wakoloni sera zao zilikuwa ni divide and rule, kwa hiyo mfano wao haufai hapa. Kwa upande wa Uganda hujatuambia kuwa Katiba yao inasemaje kuhusu mambo ya dini. Usituletee copy and paste ya mawazo yako!
 
Kwa nin watu hawaangalii hii ishu kwa mapana na marefu? Suala sio kukataa au serikali kugharamia. Nafikiri Waislam watakuwa na uwezo wa kuendesha hii mahakama.

Suala liko kwenye sheria nzima za nchi, na sijui tuanzie wapi. Kwa sasa, nafikiri mahakama ya nchi ina uwezo wa kurudisha baadhi ya kesi za ki-familia au jamii kwa wazee wa koo kwa usuluhisho wa hizo kesi. Kumbuka kesi kama hizi zinaanzia polisi (chombo halali cha dola)

Kuja kwenye mahakama ya kadhi, nani atakayekuwa anakamata wanaovunja sheria? Mimi nisipovaa HIJABU, ni askari yupi ataniuliza mbona sijavaa hijabu? Atajuaje mimi ni Muislamu au sio? Kama mimi ni Muislam na sikubaliani na baadhi ya sheria zake, rufaa yangu itasikilizwa wapi kama Mtanzania na raia wa kawaida? Serikali ina nafasi gani ya kuwalinda watu kama mimi? Sheria gani itabidi itungwe kutulinda? Kama mahakama ya kawaida itatumika kusikiliza rufaa yangu, je kutakuwa na ushahidi wowote? Je kutakuwa na POLISI WA KIISLAMU (Mzee Kifimbo-Cheza) kama Saudia?

Maswali li mengi sana. People need to analyze this issue as well as the government. It is not an overnight thing.

Goodluck!
 
Hilo sio tatizo litafanyiwa kazi na kwa kuwa serikali imesema lisihusishwe na dola halitahusishwa ,ila sio watu watakaa kimya ,bali ijulikane wazi kuwa na yale yote ambayo yanahudumiwa na dola kupitia dini zingine itabidi yasite mara moja , na vile vile Waislamu wanaweza kutazama ni kwa mtazamo gani wanaweza kujiunga na IOC,bila ya kujihusisha na dola.
 
Hilo sio tatizo litafanyiwa kazi na kwa kuwa serikali imesema lisihusishwe na dola halitahusishwa ,ila sio watu watakaa kimya ,bali ijulikane wazi kuwa na yale yote ambayo yanahudumiwa na dola kupitia dini zingine itabidi yasite mara moja , na vile vile Waislamu wanaweza kutazama ni kwa mtazamo gani wanaweza kujiunga na IOC,bila ya kujihusisha na dola.

Mkuu nchi inaongozwa kwa katiba na sheria.
 
Back
Top Bottom