Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,760
Siamini kama Tanzania inaendeshwa na Katiba na Sheria ,naona ni vurugu mechi tu ,maana haiwezekani sheria iwe inahusu upande mmoja tu ,waislamu wanapotoa madai inabidi iangaliwe sheria,wanachama wapinzani wanapojiandikisha inabidi wafuate sheria,vyama vya upinzani vinapofanya mikutano inabidi viangalie sheria ,mgombea waupinzani anaposhindwa inabidi ifuatwe sheria ,tume ya uchaguzi inapotangaza matokeo ya ushindi wa wizi inabidi ifuatwe sheria ,mapapa na manyangumi wanapoiibia serikali inabidi ifuatwe sheria na kama haitoshi iundwe tume na kamati kuchunguza wizi huo ,ila wahujumu uchumi wengine wao wanatakiwa wafuate sheria ya papo kwa papo.Mkuu nchi inaongozwa kwa katiba na sheria.
Hivi ni sheria gani na katiba gani unayoizungumzia wewe ,vipimo vingi hivyo hapo juu inaonywesha sheria haifuatwi ila kwa wachache ?