Wiki iliyopita muhubiri maarufu wa dini ya kiisilamu nchini She yahaya aliingilia suala la kadhi mkuu , huyu yeye akawa anateta hoja ya waisilamu kuwa na kadhi wa kwa ajili ya kuwatetea katika mambo yao
Hoja alizozitoa ni pamoja na kwamba eti , waisilamu wamegawanyika sana , kutokana na kuwa na misikiti mingi na madhehebu mengi kwahiyo mahakama ya kadhi itawaunganisha na kuwa na chombo chao sababu nyingine ni kwamba huu mgawanyiko unaifanya bakwata isiwe na nguvu katika maamuzi kwa waisilamu wengine kwa kuwa kuna baadhi ya watu hawaitambui bakwata .
Pia alisema mahakama za kawaida zinashindwa kutatua matatizo mengine ya waisilamu mahakama ya kadhi ndio inatosha kwa zote hizi , mimi tangia nimezaliwa miaka 24 sijawahi kusikia kwamba mahakama imeshindwa kutoa hukumu kwa mtu wowote yule kwa misingi ya dini ?
Kabla ya huyu pia siku chache mzee mwinyi nae alikuja na hoja za ukadhi , naye alitetea ukadhi , sasa najiuliza kwanini huyu mwinyi hakuleta ukadhi wakati yeye akiwa kiongozi wan chi enzi hizo alikuwa anamuogopa nani kwanini hakujadili enzi zake anazileta sasa hivi kama sio kuletea shida wengine ?
Napenda kuwasihi vijana wa kiisililamu na waisilamu wote popote walipo wasigubali kutumiwa kisiasa na watu ambao wameshashiba mamlaka wameshaishiba hii dunia hawajali wanachosema wanasema tu ilimradi waonekane wameongea lakini kuongea kwao hakuna chachu yoyote katika maendeleo ya nchi hii na watu wake .
Lazima mambo ya dini yaondolewe katika maisha ya kawaida ya mwadanamu haswa mtanzania kwanza hizi dini ni za kuja sio za asili yetu kwanini tunazingangania tangia zimeingia tumepata shida sana , tabu na majuto mengi na sasa hii mahakama ya kadhi inataka kutetenga watanzania .
Viongozi wa dini nyingi walivyosema mahakama ya kadhi haitakiwi kujadiliwa hawakua wajinga na sio mbumbumbu wanajua ubaya wa mahakama hizo na wanajua kwa mifano kwa nchi zingine , hivi mfano waikrito nao wakiamua kuwa na kadhi wao itakuwaje ? wahindu nao je ?? kuna maana gani ya kuwa na katiba ya nchi kama watu wengine wataanzisha mahakama zao ?
Inasemekana hizi mahakama zitakuwa zinapewa ruzuku na serikali kwasababu ni ilani ya CCM tangia wakati wa uchaguzi mkuu wamwaka jana , nashangaa hawa CCM nani alitengeneza ILani yao ? hii ni ilani ya kutupagawisha watanzania na kutugawa mafungu kama kule Sudan , kwanini katika Ilani kuwe na hoja kama hizo za kadhi ??
Basi tuna haki ya kusema kwamba CCM ni chama cha kidini , kwa sababu katika Ilani zao za uchaguzi zina hiyo ishu ya kadhi , kadhi ni kuingilia masuala ya ndani ya dini ingine kuichokonoa .
Kikwete alivyosema kutenganisha dini na siasa basi yeye awe muazo wa kubadilisha hivyo , Aondoe ilani ya ukadhi ndani ya katika ya CCM kisha tumuelewe , na pia atoa tamke rasmi kuhusu kadhi , sisi kaama wananchi tumuelewe sio anakimbia hoja hii
Tumekuwa na malalamiko mengi kuhusu Udini katika Nchi hii watu wananyamaza sasa hivi limekuja suala la ukadhi watu wananyamaza pia tena inahusiana na siasa iko katika Ilani ya CCM taifa
Tutambue kwamba nchi yetu ni nzuri na inapendeza kwa watu wake na mambo yake sasa haya mambo yasiharibu watu na kuwagawanyisha
Hii maana yake nini kama sio kututenganisha watanzania ??