hawa wanafunzi kudai wakopeshwe 100% hatulilalamikii, maana ni haki yao kudai na kulalama, na nnaomba wapewe. ila huu usulubu mie ndio nnaopingana nao.
sisi watu wazima tumeambiwa hata 40% pacenti hatupewi, kwani sisi si watanzania? jee hatulalamiki? tunalalamika.
mkuu wa chuo aliwaambia warejee madarasani na kunasihiwa kuwa mambo yao yanashughulikiwa, ikiwa mkuu wa chuo anasema hivyo una wasi wasi wa nini kuhusu field? si yakiwa hayajawa mnarudi kwake na kumwambia tumefata nasaha zako mlezi wetu na ndio mambo hayajawa, na wazee wetu hawana uwezo halafu tuangalie nini kitatokea kwa nini tuharakishe mambo?
halafu baya zaidi kuzarau kauli za walimu wao, za serikali na kujitia undava pahala pasipostahiki.
wangesubiri, mie hata ule mkutano pia walifanya vizuri just kupressurelize lkn kuzidi ule mstari hawa watoto hawajipendi.
ushauri wanafunzi wakuwe na mazingira, hawa ndio viongozi wa kesho, na hawa viongozi waliokuwepo leo walikuwa wanafunzi wa jana na wengine walishagoma kama wao na wanajua machungu yake.
nnashauri wanafunzi waombe kurejea chuoni na kutubu kwa utovu wa nidhamu, pia serikali iliangalie hili suala kwa umakini.
serikali kabla ya kuandaa sera au kukopia huko kwa wenzetu tuangalie na mazingira yetu.
mshahara anaolipwa mtanzania kwa sasa jee unaweza kuchangia 40%, jee mtu akiwa na watoto watatu fanya mmoja yuko chuoni na wengine wako sekondari na chukulia ni mtu wa kipato cha laki tatu(ambacho hadi sasa ni watanzania wachache wanamiliki) vipi ataweza kuwasomesha watoto hao na kuweza kulipia 40% na kulipia gharama nyengine ambazo nazo zinapanda kama umeme, maji na mengineyo, nimesikia tungule moja (wenzetu mnaita nyanya) ni sh 100. hapa waandaa sera jitahidini kuja na mchanganuo ambao utawasaidia watanzania na kuweza kufanikisha suala hjili la elimu.
]
imani yangu kuu serikali itatumia busara zake kuhakikisha inalinda eshima ya taifa letu na wananchi wake.
pia kwa vile tunajiandaa na ushindani wa soko huria tunahitaji kuandaa mazingira mazuri ya kielimu, nnakiri kuubeba mzigo huu wote serikali ni kazi ila ijaribu kuandaa mazingira na ufafanuzi ambao utawakinaisha watanzania wengi.
nnaomba kuwasilisha