Just in: UDSM wafukuzwa

Just in: UDSM wafukuzwa

Mzee Yakubu,

Heshima yako mkuu; ......nadhani iko pale pale

Hili jambo tuliwahi kuliongelea huko nyuma na kuwataka wale wote wanaotaka tujadili mada zilizo kwenye blog zao waziweke mada hizo hapa JamboForum badala ya kuweka title na link ya kutaka forumites tuende kwenye blogu zao. Majid Mjengwa hafanyi hivyo siku hizi, na ningekuomba hata wewe usifanye hivyo. Tafadhali kopi mada kutoka kwenye blogu yako uibadike hapa.
 
ahsante mkuu kwa maelekezo as asked:


MIGOMO CHUO KIKUU INAEPUKIKA

written by www.saidiyakubu.blospot.com

Chuo Kikuu cha Dar es salaam, katika siku za hivi karibuni kimekuwa katika chati kubwa sio kwa sababu zinazofurahisha, hivi niandikavyo Chuo hicho kimefungwa na wanafunzi wamewekewa masharti mazito wanayotakiwa kuyatimiza ili waweze kurejea. Kwa kadri nionavyo, kuna walakini mkubwa kwenye suala zima la mikopo ya wanafunzi. Kwa tafsiri na nadharia nyepesi, mkopo ni msaada anaopewa mtu kwa lengo la kuurudisha baadae lakini tunavyoona sasa hakuna mazingira kama hayo kwenye utaratibu wetu. Leo nimeona tujadili suala hili kwa kirefu ili kuweza kuishauri serikali ya sasa na kusaidia kuepuka migomo hii inayotokea mara kwa mara:

Vyuo vikuu duniani kote inafahamika ndio msingi mkuu wa uchumi wa nchi husika kwani kwa kiasi kikubwa wahitimu wa vyuo husika huingia katika uchumi wa nchi ama kwa ajira katika idara na makampuni au kujiajiri wenyewe.

Kwa mazingira ya sasa, takriban kila mwanafunzi aliesoma Chuo Kikuu cha Dar es salaam katika miaka ya hivi karibuni, historia yake ya chuo haiwezi kukamilika bila kukutajia ushiriki wake katika mgomo! Kwa asilimi kubwa mikopo na fedha za wanafunzi ndio imekuwa ni tatizo kuu.
Kama hatua madhubuti hazitachukuliwa, kuna hatari ya kuwa na wahitimu nusu nusu kutokana muda mwingi kupotea kwa wanafunzi kuwa katika migomo. Kwa vile tatizo ni mikopo nadhani ni bora kuangalia mfumo mzima kwa lengo la kuutafutia marekebisho maridhawa.

Wanafunzi wengi wamekuwa ''wakikopeshwa'' na serikali ili kumudu gharama za maisha wanapokuwa masomoni lakini kuna tatizo kubwa kwa vile hakuna utaratibu maalum au unaoeleweka wa kukusanya fedha za wanaohitimu, kwa kifupi hivi sasa mwanafunzi akimaliza shule basi ndio anapotea katika rekodi za chuo kwa vile hakuna mtandao wowote madhubuti wa kujua mhitimu husika yupo wapi seuze kumdai fedha alizokopeshwa.

Athari ya hii ni kuwa kumekuwa utumbukizwaji wa fedha za serikali bila ya kuwa na mfumo muafaka wa kukusanya fedha zilizotolewa huko nyuma, serikali zote zilizopita na hata hii ya sasa zimekuwa zikifadhili wanafunzi in disguise manake kama hakuna utaratibu wa kukusanya fedha zilizokwishatolewa huo tena si mkopo!

Kwa hiyo picha inayojitokeza ni kujikanganya kwa idara zinazohusika. Binafsi nikiangalia mfumo wa ukopeshaji wanafunzi hapa Uingereza napata picha kwamba mfumo wa mikopo kwa wanafunzi wa Vyuo vikuu Tanzania unahitaji mabadiliko makubwa sana.

Uingereza hapa mwanafunzi anakopeshwa fedha kwa ajili ya elimu ya juu kutokana na uwezo wake {income based assistance}, lazima mzazi wa mwanafunzi husika au mlezi kujaza fomu maalum akielezea kipato chake na kuna viwango maalum vimewekwa kuwa kwa mapato ya kila mwaka ya mzazi au mlezi husika basi mwanafunzi atapewa msaada kwa kiwango fulani. Kama mzazi wa mwanafunzi husika hana mapato yanayovuka kiwango cha chini kilochowekwa basi mwanafunzi atakopeshwa kwa asilimia mia moja.

Mkopo wenyewe mwanafunzi haanzi kulipia mpaka amemaliza masomo na kuanza kazi, kiwango cha kulipia ni kidogo sana, na si hivyo tu bali serikali kupitia mashirika yasiyo ya kiserikali inatambua hali ya maisha ilivyo hivyo mwanafunzi mpaka aanze kupata kiasi fulani ndio ataanza kulipa deni hilo, huwezi kumaliza chuo ukawa unapata malipo ya kima cha chini ukalazimishwa kulipia.

Deni la Chuo Kikuu Uingereza mwanafunzi hawezi kukwepa! Rekodi za deni husika zimeunganishwa na mamlaka ya kodi na kukatwa moja kwa moja kwa mwajiri kutokea Mamlaka ya kodi, kama kodi ya tatu anayolipa mdau husika. Hili linawezekana licha ya kuwa Uingereza bado hawajaanzisha utaratibu wa vitambulisho kwani wana kadi za bima zinazotumiwa katika kupata ajira.

Kwa Tanzania hili tunaliweza, wengi wa wafanyakazi wa Tanzania ni wahitimu wa vyuo vikuu vyetu vya pale pale nyumbani tunaweza kuwa na utaratibu wa revolving fund, yaani wanafunzi wanakopeshwa kulingana na uwezo na kisha wakiajiriwa hela zinakatwa kama inavyokatwa kodi ya mapato na mamlaka ya kodi Tanzania {TRA} inakuwa ikifanya kazi kwa karibu na mamlaka ya mikopo ya Elimu ya Juu ili kuweza kuwa na 'revolving fund' itakayotosheleza mahitaji ya wanafunzi wote.

Inaweza kusemwa kuwa ni vigumu kuwa na rekodi hizi, lakini mimi sifikiri hivyo kwani kila mwajiriwa hujaza fomu za maombi, hivyo kwa urahisi kabisa muomba kazi akiwa ni mhitimu chuo kikuu basi kuwe na kipengele maalum katika fomu hizo kwa mujibu wa sheria kukubali kukatwa fedha za kurejesha mkopo, kama waajiri wanaweza kulipia mifuko ya jamii na kodi za kichwa naamini wanaweza kusaidiwa na kushirikishwa katika ukusanyaji wa fedha husika na hivyo kiwango kikubwa zaidi kutumika kusaidia vijana na wasomi wetu.

Lakini hapa pia inabidi kuchangia kidogo kuhusu mchango wanaotakiwa kutoa wanafunzi wetu, kwa hivi sasa mwanafunzi anatakiwa kuchangia asilimia arobaini na serikali kumkopesha mwanafunzi husika asilimia sitini. Kwanza kabisa sijui ni vigezo gani vimetumiwa kufikia hiyo asilimia arobaini, kwa utafiti upi, na pili wanafunzi hawa wanatoka katika familia zenye vipato tofauti lakini kwenye kuchangia woote kwa pamoja wanatakiwa kuchangia asilimia arobaini, hii inamuumiza zaidi mwanafunzi anaetoka kwenye familia zenye vipato vya chini.

Hapa ipo haja ya kuiangalia upya sheria inayotaka wanafunzi kuchangia kiwango hicho, ingekuwa mzazi wa mwanafunzi anaepata kuanzia kiwango X kwenda juu anatakiwa kuchangia asilimia arobaini ingekuwa sawa lakini kuweka 'umbrella cap' kwa wote ni kuwanyanyasa zaidi wasio nacho ambao bila shaka ndio wanahitaji zaidi elimu kujikwamua kimaisha.

Njia nyingine ambayo nadhani tunaweza kujifunza kutoka Uingereza ni kuwa na misamaha ya kodi kwa kiwango fulani kwa mashirika na makampuni pale wanapofadhili wafanyakazi wao kusoma elimu ya juu. Hapa Uingereza shirika ambalo linahimiza wanafunzi wake kusoma elimu ya juu kwa kutoa ufadhili hupatiwa 'tax incentives' ambazo kwa hakika zinasaidia wadau wote, serikali kwa kuwa na mzigo mdogo wa kumsomesha mwanafunzi husika, mwanafunzi kwa kujua kampuni inamthamini na hivyo kuongeza ufanisi kazini, kampuni kwa kupata misamaha ya kodi.
Kama tumeweza kutoa misamaha ya kodi kwa makampuni yanayowekeza Tanzania tunaweza kusaidia makampuni ya nyumbani kufadhili wanafunzi kwa kuwapa misamaha hiyo. Huu naamini ndio UWEZESHAJI KWA WATANZANIA.

Nadhani kwa maoni yangu, migomo katika elimu ya juu inaepukika iwapo serikali itakuwa na sera madhubuti zinazoonekana kuwajali wananchi wake ambao wanafunzi ni sehemu muhimu sana. Tusipowathamini na kuwasaidia wanafunzi wawapo katika vituo vyao vya kusoma tutakuwa tunarudi nyuma badala ya kusonga mbele.


Naomba kutoa hoja, nakaribisha maoni kutoka kwa wadau...
 
Mada hii ya migomo na kufungwa kwa chuo kikuu ilichambuliwa na wanaforum hapa. Pamoja na mambo mengine, ilionekana kuwa wizara husika inafanya uzembe fulani na sehemu kubwa ya pesa za mikopo hupotezwa makusudi. Kuna taarifa kuwa serikali ilitoa mkopo wa jumla ya Tshs 111.3bn/- ambazo zingeweza kabisa kuwatosha wanafunzi wote walio vyuo vya serikali na vya binafsi kwa wastani wa Ths 3mil/- kila mwanafunzi. Lakini utaona kuwa wanafunzi wanaokopeshwa na serikali walipata sehemu ndogo sana ya pesa hizo na mpaka sasa haijulikani nyingine zilikwenda wapi.

Kuhusu serikali kukusanya madeni yake kweli ni jambo la muhimu, hata hivyo hiyo inahitaji serikali kuweka record zake sawasawa ikiwa ni pamoja na utaratibu wa kuwa na street address zinazoonyesha maskani ya watu badala ya P.O.Box.
 
Ifuatayo ni barua ya wanafunzi wa Vyuo Vikuu kuiomba radhi serikali ili waweze kurudishwa vyuoni. Picha zote na Issa Michuzi (www.issamichuzi.blogspot.com)

baruayawanafunzi1.jpg

baruayawanafunzi2.jpg


Na Maelezo ya uamuzi wao huo:

baruayawanafunzi3.jpg


Kwa wale ambao hawawezi kuona unaweza kufungua barua hizo kama attachment.

NB: Admn, unaweza kuiacha hapa kwa muda na baadaye kuiunganisha na ile ya migomo ya wanafunzi.
 

Attachments

  • baruayawanafunzi1.jpg
    baruayawanafunzi1.jpg
    185.8 KB · Views: 57
  • baruayawanafunzi2.jpg
    baruayawanafunzi2.jpg
    140 KB · Views: 77
  • baruayawanafunzi3.jpg
    baruayawanafunzi3.jpg
    203.2 KB · Views: 81
eeeh bwana wee, yamekuwa haya tena. Ndio leo kwenye article yangu nimeligusia hili.

Lakini sasa hwa wandugu watueleze kwanza wanaomba msamaha kwa kosa lipi hasa? Je, sasa tuseme madai yao ni batili na kwamba sasa wana uwezo wa kulipa ile 40%?

Je, hawa vijana wetu kweli huwa wana tafakari kabla ya kufanya vitendo? Again, we back to the poor state of our education system: inatoa watu woga, wasiojiamini, wasio na uwezo wa kujenga hoja!

Tuendelee kutafakari na kujadili
 
nadhani Utando wa Buibui.. umewagusa.. hasa baada ya wapinzani kuonesha kuwaunga mkono...
 
Mwanasiasa,

Hizi zote ni siasa za kupikwa. Kwa mtizamo wangu, masharti yaliyokuwa yametolewa awali na chuo kwa mwaka wa kwanza kurudi na laki tano, ikijumlisha matibabu na ada, wakati wengine wakitarajiwa kurudi na laki moja ya matibabu, halikuonekana kutimilika.

Nadhani marejesho ya barua za wanafunzi yalikuwa duni, uongozi wa chuo ukangamua hilo. Wiki ya mwisho ya April kukawa na vikao mbalimbali kati ya uongozi wa chuo na wanafunzi kama ilivyoripotiwa katika magazeti ya mwananchi na Tanzania daima. Nadhani Uongozi wa chuo ulitambua wazi, kwamba wanachuo watakaposhidwa kurudi shule kwa sababu ya ada zaga litageukia kwao, wakaamua kucheza siasa za kulegeza masharti iwapo wataombwa msamaha.

Serikali na chuo nadhani inatambua madai ya wanafunzi ni ya msingi, lakini mtu mzima anapokesea ni ngumu kuomba msamaha, basi mtoto unaparanganyika.

uparaganyikaji huu unatokana na mtizamo finyu wa wanafunzi ndio uliwafanya washidwe kukomalia madai yao. Laiti wangetambua, they had power of negotiation on their hands things will have been different. Nadhani hapa ndipo ushirikiano kati ya wanafunzi na other parties becomes critical.

Sasa siasa zetu zilivyo za ajabu, maongozi sasa hivi yatabadilisha muelekeo swala hititakuwa katika asilimia 40, litageuka kulipa fadhila kwa kulegezewa masharti.

Nabaki kutumaini kwamba wanafunzi wanaakili zaidi tuwafikiriavyo kwamba kuomba kwao msamaha wameahidiwa kutengeneza forum ya kujadili modalities ya kulipa hizo asilimia arobaini.
 
nadhani Utando wa Buibui.. umewagusa.. hasa baada ya wapinzani kuonesha kuwaunga mkono...


"Kamati ya Ufundi" imeshafanya vitu vyake.


mwanasiasa

Hili la elimu yetu kutoa wahitimu bomu tuliligusia kule kwenye "Lugha ya kufundishia iwe Ipi" kichwa cha habari kama hicho....yaani ni aibu tupu.

Enzi za Mwinyi kuna kiongozi mmoja wa wanafunzi (jina limenitoka) wa aliyekuwa anaongoza mgomo wakati ule ilimbidi akimbie nchi maana baada ya kuhitimu kila kazi aliyokuwa anapata alikuwa anafukuzwa within few months bila ya sababu za msingi...mwishowe akakimbilia either Zimbabwe au Botswana..nchi moja kusini mwa Africa.

Yangu macho hawa jamaa watarudishwa shuleni wiki ijayo au very soon.
 
Yebo Yebo
kwa msamaha huo wanafunzi lazima wanarudishwa shule katikati ya mei. Ukweli ni kwamba wanafunzi hawana hiyo pesa, na serikali ama chuo kama inamtizamo chanya haitakuwa tayari kusimamisha mafunzo kwa sababu ya ada hizo, it will be absurd and a political crisis. the goverment can not afford that so students will be back to the uni soon

Mwanasiasa
hili la kukaa na kusema wanafunzi ni woga, wasiojiamini, wasio na uwezo wa kujenga hoja! sidhani kama ni sahihi. Ukiangalia kwa makini vijana wa vyuo vikuu kwa kiasi kikubwa sana wamefanikiwa kupayuka kwero zao, na kuitikisa serikali kwa njia moja ama nyingine. Kumbe ni kweli wanafunzi wananguvu, swala la msingi ni vipi tunaunganisha mapambano ya vyuo vya juu na jamii. Ni jinsi gani tunaweza kutumia hii nguvu kupambanua hoja ama kusemea hoja za kitaifa.

Ni muunganiko tu, nchi hii inaweza kuchemka.
 
Yebo yeboNaomba nikukumbushe kiongozi wa wanafunzi, aliyeongoza mgomo UDSM enzi ya Rais Mwinyi aliyekimbilia kusini ni James Mbatia wa NCCR-Mageuzi.
 
Hiiii ni very interesting story, ni afadhali kuwasikiliza wachambuzi wa siasa humu ndani ya JF, maana mimi binafsi I am lost!
 
Yebo yebo hivi unajua hapa kwamba tunaongelea wanafunzi wanaosoma CHUO KIKUU ambao ni less than 1 percent ya watanzania?? I seriously doubt their intellectual standing! Sasa hawa kweli ukiwapa mamlaka ya kunegotiate mikataba na Bill Gates au Murdoch...si watatuuza na makaburi ya bibi zetu? Its very absurd! Imean hakuna kinachowaonyesha kwamba ni UNIVERSITY STUDENTS! Bali ni STUDENTS AT THE UNIVERSITY!
 
Usaniinaization unaendelea....Rais Muungwana mda si mrefu atatoka na kauli.."kwa kuwa yeye ni mzazi ameamua kuwasamee na watapewa mkopo 100%". Kwa hiyo ataonekana yeye ajachemka na ahadi yake hewa aliyowapa siku ya kuzaliwa kwa CCM,2007.

Tatizo linalotukabili sasa katika sector ya elimu Tanzania ni kugeuza elimu ni siasa na siasa ni elimu.Tunachezea maisha yetu yajayo bila kujua au kwa kujua ili mradi tutimize mahitaji ya kisiasa ya sasa.Waeboa sana,...wamewasumbua watu wa vyama vya upinzani kuwatetea na walimu wao chini ya UDASA waliwatetea kwa kuwa madai yao ni ya msingi.Leo wanaomba msamaa....kweli Afande Sele aliyesema "adui yako muombee njaa hawakukosea".Kwenye Njaa uwezo wa kufikiri upungua.Raisi na serikali yake waliyoiita serikali ya kisanii leo wanaiita serikali tukufu.
 
Yebo yeboNaomba nikukumbushe kiongozi wa wanafunzi, aliyeongoza mgomo UDSM enzi ya Rais Mwinyi aliyekimbilia kusini ni James Mbatia wa NCCR-Mageuzi.


Hapana hakuwa J. Mbatia. Nikipata jina lake nitaweka hapa (naogopa kuahidi maana ahadi ni deni..!!)...kuna mtu mwingine namfahamu alikuwa naye karibu zaidi nitamtafuta...huyu jamaa alipata shida sana baada kumaliza mlimani..kila alikokwenda watu wa system walikuwa wanamshughulikia.
 
Yebo yebo hivi unajua hapa kwamba tunaongelea wanafunzi wanaosoma CHUO KIKUU ambao ni less than 1 percent ya watanzania?? I seriously doubt their intellectual standing! Sasa hawa kweli ukiwapa mamlaka ya kunegotiate mikataba na Bill Gates au Murdoch...si watatuuza na makaburi ya bibi zetu? Its very absurd! Imean hakuna kinachowaonyesha kwamba ni UNIVERSITY STUDENTS! Bali ni STUDENTS AT THE UNIVERSITY!


mikuki

Sijajui hiyo 1% una maana gani?

Hawa viongozi hawana choice...system yetu ni mbovu from bottom to the top..mwanasiasa amegusia vizuri. Yaani hawana ujanja kabisa, serikali itaishia kuwa on-top na pengine hao viongozi wakuu watakuja kupata matatizo katika career zao huko mbeleni.

Mimi ingawaje nakubaliana na hoja yao ya kudai posho zao ila naona kugoma kunawapa hasara kubwa sana hivyo ningewashauri wafanye njia nyingine kama maandamo (na kuvumilia virungu vya FFU). Kukaa kimya isiwe option iko siku watapata support ya public.

Tatizo kubwa walilonalo hawa wanafunzi ni kuwa mpaka sasa mass public inaamini kulipiwa elimu chuo kikuu ni "wema au roho nzuri ya serikali".
 
Sasa nakupata..watanzania wengi wanaona kulipiwa University ni "roho nzuri ya serikali"..My point is..hawa wanafunzi walikuwa na hoja! Wangeamua kuziweka mezani bila mgomo, unajua bwana bureacrats wa TZ ni very shrewd! sasa usipojifunza namna ya kudeal nao...always watakuona ni hopeless! Nina imani we can do better! JK akiwarudisha..I tell you...watakuwa hawajapata ufumbuzi wa kudumu wa 40%. Unless unaniambia kwamba na wao wanaangalia short term goals zao wakiwa chuo, wakishamaliza watakao ingia nao watajijua!!!

Sasa kweli na kelele zooote..huu mgomo umeachieve nini??????? Ndo maana nilisema..vijana wajitahidi kutafuta njia mbadala za mtikila style..sasa si mara mia wangekwenda mahakamani, hata kama wangeshindwa wangeacha rekodi kwenye mafaili!!!! kuliko kugoma na kufukuzwa then kuomba msamaha?
 
Sasa nakupata..watanzania wengi wanaona kulipiwa University ni "roho nzuri ya serikali"..My point is..hawa wanafunzi walikuwa na hoja! Wangeamua kuziweka mezani bila mgomo, unajua bwana bureacrats wa TZ ni very shrewd! sasa usipojifunza namna ya kudeal nao...always watakuona ni hopeless! Nina imani we can do better! JK akiwarudisha..I tell you...watakuwa hawajapata ufumbuzi wa kudumu wa 40%. Unless unaniambia kwamba na wao wanaangalia short term goals zao wakiwa chuo, wakishamaliza watakao ingia nao watajijua!!!

Sasa kweli na kelele zooote..huu mgomo umeachieve nini??????? Ndo maana nilisema..vijana wajitahidi kutafuta njia mbadala za mtikila style..sasa si mara mia wangekwenda mahakamani, hata kama wangeshindwa wangeacha rekodi kwenye mafaili!!!! kuliko kugoma na kufukuzwa then kuomba msamaha?


Yup..ndio maana kila kitu wakihitaji kutoka kwa serikali wanasema "Tunaomba" serikali itufanyie hiki na kile...hata wabunge bungeni si unawasikia tunaomba serikali ijenge zahanati mahali fulani n.k Hakuna mtu wa kuikumbusha Serikali wajibu wake; si wabunge, si wananchi wala wasomi wa mlimani.

Huu mgomo umeacha mbegu ndugu yangu...tena mimi naona kuliko kwenda mahakamani kupoteza muda wao ni bora hata walivyogoma. Rekodi kwenye mafaili ambayo anasoma jaji na mawakili peke yao kwa Tanzania ni sawa na bure...bora hata ka-mgomo haka kalikowapa media attention na public imepata kuwasikia japo bila kuwapa support yoyote ya maana...ila wanasema haba na haba hujaza kibaba.
 
Sawa kaka nimekubali! Ila maisha yangu ya mlimani tuligoma kama mara tatu hivi! Na swala lilikuwa hilo hilo la PESA!!!!! Labda tujaribu njia nyingine wandugu! Maana itafika kipindi tutaonekana kama watu wasiojua wanataka nini...Si unajua mtoto akiwa anapenda kulia sana..ni rahisi mzazi kumuignore...kwamba ni kawaida yake...
 
Back
Top Bottom