Joseph Mbilinyi 'Sugu' amlipua Zitto Kabwe

Joseph Mbilinyi 'Sugu' amlipua Zitto Kabwe

Tuwekeni siasa kando na tufanye kazi. Tumesikia upande mmoja wa shilingi tusubiri Zitto nae aseme upande wake ili tulinganishe na tutoe hukumu kwani Chadema kwa chuki yao juu ya Zitto wanaweza ongea lolote lile.
Afu pia wao kina Sugu walipata wapi hizo documents kama wao nao sio wadau?

Hili povu lako ni kali sana ..
 
Ccm wanamuharibia Zito. Why kila Zito akishutumiwa au kutuhumiwa,watu wa ccm ndio huwa fasta kumtetea. Mfano Lizaboni na Msalani humu jf. Why?

siyo jf tu hata bungeni WANACCM NDIYO WALIO UPANDE WAKE !
 
Nadhani mbilinyi amenunuliwa ili kuweka chunvi ktk kidonda. Kwani kwa kauli hiyo mbilinyi hajengi bali anabomoa. Anaonyesha wazi kwamba hata upinzani nao kumbe wanapiga dili. Hivyo kelele zao ni sababu hawajahusishwa. Na wakihusishwa ni washiki wazuri. Haya yetu macho

kwani zitto ni mpinzani?
 
ww unafikir Zuber kabwe anataka nin? tena fedha anayo tena mingi!!umaarufu wa kutosha.wewe piga ZOGO mtandaoni.kesho utamkuta MJOMBA SUGU yuko ndan ya ACT lissu na mnyika hawa watarudi lumumba2

Ndoto nazo ruksa katika uhai wa mwanadamu mkuu
 
Mkuu.
MSALANI na Lizaboni ni wapuuzi wachimia tumbo wasiojitambua.
Pamoja nao kuna ifweero Ruttashobolwa utaifakwanza na Simiyu Yetu.
Hawa tulishawapuuza kitambo sana hapa jukwaani.

Hawa ni sehemu ya Dola!
Ukitaka ufahamu vizuri angalaia Mama yake Zitto Kabwe anavyohudumiwa na Dola ndani na nje ya nchi!!
Wakati mama Zitto Kabwe akiwa ICU taarifa hizo zimesitua watawala hadi kwenda haraka kwenda kumuona kuliko hata Vicky Kamata ambaye ni danguro lao!
Zitto Kabwe na Mama Zitto Kabwe ni sehemu ya watawala wa sasa hata Mungu akiamua utaona huko Kigoma
Utanikumbuka!!
 
Uongo Wa mchana kweupe

Mkuu kwa nini nidanganye???@Zitto alilkuwa anapita kwenye mastudio anawahamasisha wasanii kukataaa kupeleka nyimbo zao kwenye kampuni za miito ya simu mpaka atakaporudi na jibu la kueleweka eti ataenda kuwatetea bungeni....cha kusikitisha na kilichowastua ni yeye kupeleka nyimbo ya kigoma all stars kwenye kampuni ya miito ya simu Pera Africa baada ya kuhaidiwa pesa nzuri na mmiliki wa kampuni swahiba wake ndugu Ruge Mutahaba...Waulize wasanii wa Leka Tutigite waliambulia nini?kama sio Mwasiti kuambuliwa kuchapwa nao na Zitto kisha akamtelekeza.....


Mh Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kwenye picha na Mh Mbunge wa Mbeya Mjini ambaye ni moja kati ya wasanii wenye mchango mkubwa kwenye muziki wa kizazi kipya,Sugu(Joseph Mbilinyi).


PENDEKEZO BINAFSI LA MBUNGE KUHUSU KUZUIA UNYONYAJI DHIDI YA WASANII WA TANZANIA KATIKA BIASHARA YA MIITO (RING BACK TONES)

Kwenda kwa: DR ABDALLAH KIGODA, Waziri wa Viwanda na Biashara

Kuhusu: BIASHARA YA MIITO YA SIMU (RINGBACK TONES)

Kumekuwa na malalamiko makubwa sana kuhusu biashara ya mauzo ya nyimbo kama miito kwenye simu. Malalamiko haya yalianzia kwa wasanii wenyewe na baadaye mimi binafsi niliwasilisha hoja zao Bungeni mwaka 2012. Hata hivyo, hadi sasa malalamiko haya bado hayajapatiwa ufumbuzi na hivyo wasanii kuendelea kunyonywa. Tatizo kubwa katika biashara hii ni USIRI na UNYONYAJI kwa wasanii wa Tanzania. Suala la USIRI lipo Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia. Suala la Unyonyaji lipo Wizara ya Viwanda na Biashara.

USIRI
Biashara hii ya “Ring Back Tones” (RBT) hufanywa na Kampuni za simu (Network providers) kwa kununua maudhui kutoka wachuuzi (Content Providers) ambao nao huingia mikataba na Wasanii (Content Creators).
Hakuna sheria yoyote au Kanuni hapa nchini inayoongoza biashara hii na hivyo “Network providers” na “Content Providers” kuwa watu pekee wenye taarifa zote za biashara hii. Kampuni za simu hujumuisha mapato ya biashara hii na mapato yake mengine (Not Ringfenced), hawatoi taarifa za manunuzi ya nyimbo (au ‘content’ nyingine yeyote) kwa wadau na hasa wasanii. Wachuuzi (Content Providers) nao hawatoi taarifa za mauzo kwa wasanii na wanatumia uelewa mdogo wa wasanii kuwasainisha mikataba inayowanyonya. Matokeo yake ni kwamba msanii hupata kiasi cha asilimia mbili tu (2.5%) ya mapato ghafi ya kazi yake. Hivi sasa biashara hii inathamani (turnover) ya takribani shilingi 44 bilioni kwa mwaka.

Suluhisho:
Serikali kupitia Wizara ya Mawasiliano iandike kanuni (regulations) zitakazolazimisha makampuni ya simu kuweka wazi mapato yatokanayo na biashara ya RBT (Miito ya simu) kila baada ya miezi 4 (disclosure rules). Kanuni hizi zielekeze makampuni kutoa taarifa za mauzo kwa kila kazi (nyimbo/vichekesho etc.)

UNYONYAJI
Kutokana na usiri ulioelezwa hapo juu, wasanii wamekuwa wakinyonywa kimapato. Kwa mfano Msanii hulipwa mapato yatokanayo na ununuzi wa awali wa kazi yake (wimbo) katika mwezi (downloads).

Lakini mapato yatokanayo na “subscriptions” ambapo mlaji hukatwa shilingi 30 kila siku msanii hapati chochote. Hivyo katika mapato ya sh. 1,300 kila mwezi kwa kila mteja kwa kila wimbo, msanii hupata mgawo wake kutoka shilingi 400 tu za ‘downloads’ na ndio maana wasanii wote nchini hupata 2.5% ya shilingi 44 bilioni zinazokusanywa na Kampuni za Simu.

Nchini Marekani biashara ya miito ya simu (RBT) imetafsiriwa kama maonyesho (Public Performances) na hivyo “copyright Association” ya Marekani imeweka kiwango cha chini cha mrahaba (royalty) ambacho msanii hulipwa. Marekani msanii hulipwa asilimia 10 ya patoghafi linalozalishwa na kazi yake kama muito wa simu.

SULUHISHO
Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara iandike kanuni kwamba mauzo ya kazi za wasanii kama miito ya simu inachukuliwa kama ‘performance’ na kwamba Kampuni za simu zitalipa sio chini ya asilimia 12 (12%) ya mapato ghafi, ambapo asimilia 10% itakwenda kwa msanii na asilimia 2% COSOTA kwa ajili ya usimamizi na Ulinzi wa kazi za Wasanii.

HITIMISHO
Kanuni za Uwazi (disclosure rules) katika biashara hii ya ‘Ring Back Tones’ na mgawo wa haki wa mapato (fair and just revenue share) ndio suluhisho endelevu na litakaloleta tija kwa wasanii wa Tanzania na hata Serikali kukusanya mapato stahili. Kanuni (Regulations) zinazopendekezwa zianze kutumika kuanzia tarehe 1/7/2013

Kabwe Z. Zitto, Mb
Kigoma Kaskazini

Dodoma, 13 Mei 2013
 
Kama kapotea iweje muendelee kumsakama? CHADEMA hata aibu hawana. Mwenzao anaugulwa na mama yake mzazi, wao kazi ya kumsakama

si bora yeye anauguliwa , mimi nimefiwa na MAMA MZAZI hata hivyo siwezi kuvumilia huku nchi ikitafunwa kirahisi namna hii .
 
Back
Top Bottom