Tafakari yetu
JF-Expert Member
- Apr 19, 2021
- 1,502
- 4,408
CCM ikiwa na bahati ya kukuza na kutumia magwiji ya mikakati ya ushindi wa kisiasa hali hiyo imekuwa kinyume kwa vyama vya upinzani ambavyo havina hazina hiyo na matokeo yake kujiua vyenyewe. Chama chenye nia ya kushinda dola hakiwezi kuwa na mtendaji mkuu ambayo hana mbinu wala mikakati ya kushinda jimbo, ni aibu kubwa sana.
Kukosekana kwa falsafa kamili inayoweza kufundishwa na kuenezwa kupitia elimu imekuwa ni changamoto kwa vyama vya upinzani hususani CHADEMA katika suala la kushika dola. Watanzania wanataka kujua chama kinasimamia misingi ipi. Dola si kitu cha kusema kinaweza kuokotwa kama embe bovu, zinahitajika mbinu na mikakati ya ushindi kutoka kwa wabobezi na magwiji.
CHADEMA wajipange sana chini ya Mnyika kushindana na CCM .
Kukosekana kwa falsafa kamili inayoweza kufundishwa na kuenezwa kupitia elimu imekuwa ni changamoto kwa vyama vya upinzani hususani CHADEMA katika suala la kushika dola. Watanzania wanataka kujua chama kinasimamia misingi ipi. Dola si kitu cha kusema kinaweza kuokotwa kama embe bovu, zinahitajika mbinu na mikakati ya ushindi kutoka kwa wabobezi na magwiji.
CHADEMA wajipange sana chini ya Mnyika kushindana na CCM .