Jinsi uchumi wa nchi unavyoathiriwa na biashara ya bodaboda

ankol

JF-Expert Member
Aug 21, 2012
2,113
3,484
Salaam wadau.

Leo ningependa kuelezea jinsi gani uchumi wa nchi unavyo/takavyoathiriwa na biashara ya bodaboda.

Biashara hii inayokua kwa kasi kila uchao imekua ni kimbilio la vijana wengi wanaotafuta maisha hasa kutokana na ukweli kua ni biashara rahisi isiyohitaji mtaji na nguvu kazi kubwa kuifanya.

Yaani ukiweza tu kuendesha you are good to go.

Biashara hii ina impact ya moja kwa moja na uchumi wa nchi kwani inawashirikisha vijana ambao ndio nguvu kazi ya taifa. Wanashindwa kufanya ubunifu na kuliingizia taifa kipato badala yake wamekua wakingangania vijiweni kutokana na uwingi wao wamekua wakigombaniana abiria wachache na kuambulia kichache na kuridhika na maisha.

Kiuhalisia vijana hawa wanashindwa kuwa productive kwa taifa na badala yake ni suala la muda tu athari zake zitakuja jitokeza.

Nashauri serikali i-control biashara hii ya bodaboda kwa kuweka kodi kubwa kwa wafanya biashara hizo ili kunusuru vijana wengi kukimbilia huko kabla hali haijawa mbaya.
 
Salaam wadau.
Leo ningependa kuelezea jinsi gani uchumi wa nchi unavyo/takavyo athiriwa na biashara ya bodaboda.
Athari kubwa ya Boda ni kwa waendesha Boda ajali ni nyingi sana na mwisho wa siku ki-afya impact yake ni negative, lakini short term sio kama ulivyosema wewe isingekuwa Boda fahamu kwamba vijana na watu hao ndio either wangekuwa machinga au vibaka as well as usafiri from point A to B isingekuwa rahisi hivyo

Badala ya kulaumu watu ambao wamekwenda huko sio kwa kupenda bali mkono uende kinywani laumu serikali ambayo ina sera mbovu hence watu kukosa ajira zenye ujira
Biashara hii inayokua kwa kasi kila uchao imekua ni kimbilio la vijana wengi wanaotafuta maisha hasa kutokana na ukweli kua ni biashara rahisi isiyohitaji mtaji na nguvu kazi kubwa kuifanya.
Kwamba haiitaji mtaji ? Unajua bei ya Boda ? Unaweza kulinganisha na kupika vitumbua au uchuuzi wowote wa aina nyingine ? Ukiona hivyo gundua kwamba huenda huko angalau ndio kuna ujira
Yaani ukiweza tu kuendesha you are good to go.
Biashara hii Ina impact ya moja kwa moja na uchumi wa nchi kwani inawashirikisha vijana ambao ndio nguvu kazi ya taifa.
Sasa kama sera ya serikali haitumii nguvu kazi hio unategemea wafanye nini kutembeza bahasha kuomba kazi zilizopo au kufanya vitu ambavyo nchi hii ni betting to say the least na ukijitahidi kufanya huenda ni kuingia kwenye madeni ya vicoba
Wanashindwa kufanya ubunifu na kuliingizia taifa kipato badala yake wamekua wakingangania vijiweni kutokana na uwingi wao wamekua wakigombaniana abiria wachache na kuambulia kichache na kuridhika na maisha.
Hivi wewe unaishi kwenye hii nchi kweli ? Ulitaka wabuni nini unaweza kunipa mfano ? Niambie ni kitu gani kwenye hii nchi unpredictable ambacho kina guarantee ya ujira (kwanini wewe usibuni alafu uwaambie wafanye) Issue watu hawana disposable income hata ukifanya mazuri wanunuzi sio wengi hence kila sekta ni kugawana umasikini (middle income is shrinking)
Kiuhalisia vijana hawa wanashindwa kuwa productive kwa taifa na badala yake ni suala la muda tu athari zake zitakuja jitokeza.
Ni kazi ya vijana au ya nani serikali imetangaza watu waende sehemu fulani wakagoma kwenda ? Bora ungesema haya enzi zile watu wanazurura wanabebwa na kupelekwa kulima au kurudishwa vijijini walime leo hii watu wanajipeleka wanavuna masoko hayapo zaidi ya ngonjera za kuuza au kutokuuza nje
Nashauri serikali I control biashara hii ya bodaboda kwa kuweka kodi kubwa kwa wafanya biashara hizo ili kunusuru vijana wengi kukimbilia huko kabla hali haijawa mbaya.
Ili vijana hawa waamie kwenye wizi au wafanye nini ? walime ambapo soko halina guarantee; unaona nchi mpaka wazee wa miaka 60 ni walinzi; watu wanamaliza chuo wanatembeza uji ikitokea nafasi moja ya kazi wanakwenda watu 1000 bado tu haujajua tatizo lipo wapi?

Kweli wanasiasa wamewa-brainwash kwamba hili tatizo sio lao bali ni la uzembe wa hawa wabangaizaji wenyewe kwa kukosa ubunifu na uvivu (yaani kama mchawi anakupa masharti ukifanikiwa ni yeye ukishindwa hukufuata masharti)
 
Una hoja mkuu, kilimo kilifaa kuwa kimbilio kubwa na rahisi kwa nguvu kazi ya taifa letu, ikifuatiwa na mifugo (Tz ni moja ya taifa lenye ngo'mbe wengi Africa).

Bado kuna kazi kubwa ya kutengeneza na kuwekeza zaidi kwenye sekta za kilimo, ufugaji ili kuvutia nguvu kazi huko kuliko kuzalisha wachuuzi wadogo wadogo.
 
Vijana sahvi wamejitumbukiza
Kwenye bodaboda, betting, kukata msuno(usanii)
Hayo ndiyo mambo wanaona yanawafaa

Ova
 
Una hoja mkuu, kilimo kilifaa kuwa kimbilio kubwa na rahisi kwa nguvu kazi ya taifa letu, ikifuatiwa na mifugo (Tz ni moja ya taifa lenye ngo'mbe wengi Africa)....

Bado kuna kazi kubwa ya kutengeneza na kuwekeza zaidi kwenye sekta za kilimo, ufugaji ili kuvutia nguvu kazi huko kuliko kuzalisha wachuuzi wadogo wadogo.
Vijana wa sasa sio wavivu kama soko likiwa guarantee utaona watu watakavyomiminika; mfano mdogo tu vilimo vinavyoanza na kufa vitunguu mara matikiti mara miti, mara miwa mara kilimo cha drip irrigation; mara watu wanaenda kulima soko wanakosa basi ni shida tu

Vitu ni interconnected na bila ku-solve matatizo haya kwa ujumla wake wachache watapiga pesa kwa kuleta solutions ambazo ni unsustainable, short term na za kulighai watu; ila ukweli ni kwamba things are falling apart...
 
Salaam wadau.
Leo ningependa kuelezea jinsi gani uchumi wa nchi unavyo/takavyo athiriwa na biashara ya bodaboda.
Biashara hii inayokua kwa kasi kila uchao imekua ni kimbilio la vijana wengi wanaotafuta maisha hasa kutokana na ukweli kua ni biashara rahisi isiyohitaji mtaji na nguvu kazi kubwa kuifanya...
Nilitamani kutukana,lakini nimejizuia.
Mambo ya kuongea bila utafiti yanaleta hoja za ajabu sana.

Wakati unafikiria wapandushiwe kodi unadhani anayeathirika ni nani?

Watu mnaishi Dar usafiri wa umma upo wa kutosha,mnashindwa kufikiria watu wa mikoani ambao hawana njia nyingine zaidi ya hizo boda boda na mikoa mingine baiskeli.

Huo ubunifu unaotaka vijana wafanye ni upi iwapo serikali inatoa pesa nyingi za uwekezaji kwenye elimu ya hovyo ya kukariri mambo waliyofanya wazungu miaka ya 1800?Elimu inayotoa degree za kutambia mtaani na sio maarifa ya kazi!

Natamani niongee sana lakini sijui uelewa wako ukoje
 
Acha hizo Muhimu wamejiajiri hawaibi Wanafanya Kazi halali inayoendesha maisha yao hayo mambo ya ubunifu Tumuachie Mtengenez jezi za Yanga
 
Write your reply...ukilima unaambiwa hakuna kuuza nje nchi ina njaa.uza kwa 30alfu gunia.bora tu waendeshe bodaboda.kazi ya kulisha serikali ngumu mtu analipwa mamilion kwa mwez bdo anataka auziwe mahndi alfu30 kwa gunia
 
Back
Top Bottom