JF Exclusive: CAG Report on IPTL/Tegeta Escrow Account

JF Exclusive: CAG Report on IPTL/Tegeta Escrow Account

Mkuu,

Pumzika; lengo si kuvuruga mwenendo wa Bunge bali kuwafanya wanaojaribu kufanya upotoshaji wafahamu kuwa nyaraka nzima ya ripoti ipo tayari kwetu raia na waache michezo yao.

Wawajibishane, kila mtu aubebe mzigo wake. Wanaowajibika na wawajibike; usanii wowote katika hili utachafua hali ya hewa pasi na ulazima wa kufikia huko.

Nadhani tusiendelee, tuliachie Bunge lifanye kazi yake

nina mashaka na haya maelezo yako!
 
mkuu Invisible pls kwa hali ilivyo sasa nadhani hujuma kubwa zaidi zinaweza fanyika hata kukata mawasiliano ya mkongo wa taifa wa mawasilino, au hujuma nyingine zozote zitakazokwamisha mawasiliano.

Ni bora umalizie tu mkuu. Hali ishachafuka sana. Kuna uharamia wa miundo mbinu unaweza fanyika tutashanaana hapa mkuu. mi silali naisubiri kwa kweli. hizo page ulizoweka hazisisimui kabisa, wakati bado mnashauriana weka kwanza zile page zenye majina ya Payees.

Heee wewe unajua maana ya huo mkongo wa taifa au naww ndi GT wa JF? Unajua system ya mawasiliano ya internet? Zantel unajua wanamiliki nn?
 
Last edited by a moderator:
Hawa jamaa "wajanja" wamepima upepo kiwango cha original report kusambaa......hiyo kunyofoa ni ili wenye original wasimame sasa wajulikane ni "wafunge kazi" ......ila kauli ya Invisible kuwa ipo "mawinguni" maana yake kwa muda uliosalia "wameshafeli"

Sidhani kuwa invisible alimaanisha hivyo. Nnavyoelewa mawinguni alimaanisha cloudy storage, akimaanisha Report ya CAG iko stored huko, hivyo hakuna namna yeyote inaweza kuchakachuliwa!!!
 
Last edited by a moderator:
Hii si ripoti ya mtu, ni ya watu. Utahonga wangapi? Kama kuna jumla ya watu takribani 60 wanayo, utaanza na nani umalize na nani?

Narudia, moto huu hauzimiki kwa kuumwagia petroli!

What if wakisema kuwa report inayowasilishwa ni ile iliyopelekwa kwa Spika ambayo imenyofolewa hizo kurasa huku wakiwa wameshawabana wale wabunge wao waliopo kwenye Kamati na wale wa upinzani wameshashikishwa ndefu? I'm thinking loud...
 
Kijana mbona unakurupuka, na wewe umeingia mkenge kwa uzushi wa mitaani kuwa ripoti eti imenyofolewa kurasa?

Hizo zilizowekwa hapa ni nini?

Na sijaona chochote cha kuonesha wizi wowote kati ya hizi kurasa zilizowekwa hapa.

Nashindwa hata kuwafikiria mkoje, yaani ni zaidi ya misukule.

We maza huwa unajitahidi sana kufanya watu wajinga?? umesoma bandiko zima LA Invisible kwani kasema ndio hizo tuu?? tuliomuelewa kasema nyingine anazo na ikibidi ataziweka, ila katoa onto kwa hao wanaodhani kunyofoa kurasa no ujanja. Binge lifanye kazi yake. Endelea kupiga kimya tu kwenye hili, subiri mengine utaendelea tu kuonyesha umahiri wako. Au kama huna kazi uwe unatusahihishia kiswahili chetu tunapokosea.
 
What if wakisema kuwa report inayowasilishwa ni ile iliyopelekwa kwa Spika ambayo imenyofolewa hizo kurasa huku wakiwa wameshawabana wale wabunge wao waliopo kwenye Kamati na wale wa upinzani wameshashikishwa ndefu? I'm thinking loud...
Manake tulio mtaani tutamwaga ugali.

Naeleweka? Na asipoweka "Invisible" basi "Karumekenge" ataweka. Bahati hatuna zaidi ya siku nyingi kuona Bunge linasemaje.
 
Tafadhari tunaomba haraka hiyo report iwekwe hapa tena ikiwa imekamilika. Mitaani tayari report ipo tena ikiwa imenyofolewa kurasa muhimu, sasa JF tunangoja nini?

Weka mzigo hapa critical thinker tuijadili, mbichi na mbivu zifahamike.
Hapa JF zimekuwa zikiwekwa nyaraka za siri nzito nzito sembuse hii report ambayo nasikia hata Chief Kiumbe anayo na huko Dodoma imetapakaa.

Mkuu Invisible tutendee haki kwa kuiweka humu report yote ili nasi tuone hicho kilichomo. Manake kwenye hizo page sioni kitu chenye mashiko
 
Last edited by a moderator:
It's a little hard to offer anything further without knowing the full context of my maxim!

Common sense is not so common-Voltaire

Sorry!
You better be sorry!!!!
Any wise man who knows the fundamentals of context will never expect common sense to be common!!
Impotent maxims derived from a sheer wish will never stand to be an authority leave alone the emic-etic phases of thesis-antithesis-synthesis flow of events!!!!

The pompous and pretenders will never shine above the power of knowledge and respect to human dignity!!!
 
Sidhani kuwa invisible alimaanisha hivyo. Nnavyoelewa mawinguni alimaanisha cloudy storage, akimaanisha Report ya CAG iko stored huko, hivyo hakuna namna yeyote inaweza kuchakachuliwa!!!

Nimemuelewa Invisible kama ulivyomuelewa ndio maana nikasema kwa kauli hiyo hata wakiwajua wenye original copy wote bado "watafeli" maana iko "mawinguni" ......
 
Last edited by a moderator:
Sasa kama mambo ni mepesi jinsi unavyoyaona wewe bibie,hizo sarakasi za kunyofoa hizo kurasa ni za nini? Hivi unadhani hao Magamba wenzio wangekuwa wanaona kama unavyoona wewe kungekuwa na sarakasi zote hizi?
Poleni kwa kukesha bure,mbona mpaka niko page ya 9 sioni kitu ama huku last page ndo kuna data?
 
Wee ajuza sheria za kodi zipo categorically nani apewe exemption kwa kitu gani na nani asipewe. Iwe ni tanesco wameengineer au mtu mwingine, mamlaka husika ya kusaheme hiyo kodi haikushirikishwa. Subiri report halisi watu tunayo. Acheni wizi halafu mnakuja kuongea upuuzi hapa.

Wewe wacha porojo, unajuwa kuwa IPTL wana exemption ya tax? Katika report ulizonazo limo hilo?
 
Ukiamua kuheshimu utu na nafsi yako PESA haitokupa shida kukufanya utende usiyopenda....

Wiki ilopita nilipotoa msimamo Mkali juu ya hili nilipigiwa SIMU za vitisho na hongo eti tu nitetee ujinga....

Ktk maisha nilishachora mstari kuwa hela haiwezi nunua fikra zangu....

CCM ilishajiandaa kwa hili ndio maana wakati JK anaenda US nilisema hapa anaondoka kutuachia uwanja tucheze vizuri ngoma ya ESCROW nafikiri BAK anakumbuka....

kwa hiyo mkuu lusungu,hata maradhi ya tezi dume ya mkulu ilikuwa ni mpango maalumu uliopangwa ukapangika.aisee jk noma.nimemvulia kofia kwa hilo.round hii kila "ntu" huko "silikalini" ajibebee zigo lake mwenyewe.
 
Last edited by a moderator:
Kwanini kurasa hizo zinyofolewe? Mbona sijaona ubaya wake kwa upande wowote?
Mkuu hata mimi nashangaa kwa sababu hayo ni maelezo tu na sioni kama yana impact yoyote, sasa kwa nini hizo zinyofolewe. Tick tack ni kubwa hapa
 
Back
Top Bottom