JF Exclusive: CAG Report on IPTL/Tegeta Escrow Account

JF Exclusive: CAG Report on IPTL/Tegeta Escrow Account

Yes,

Ndo maana inabidi tuhimizane UZALENDO na kusisitiza zaidi watu kusahau tofauti zao za dini, vyama n,k na tukawa wamoja kuwakataa wanaolizamisha Taifa letu.

Wabunge watusaidie kusimama kuhesabiwa; waweke Taifa mbele lakini asionewe mtu wala asilindwe mtu!
Busara tupu.
 
CCM wanaipeleka nchi pabaya, soon tutaanza kuchinjana

Kwa lipi?

Nakushauri subiri ripoti kamii, sikioni cha maana katika hizi kurasa zilizobandikwa hapa. Bali naona TANESCO inadaiwa na inajaribu kupunguza deni kwa kukaa chini na wadai wake.
 
Asante Invisible!

Watabakia kujificha uso huku viuno vikionekana. Mchezo wa kitoto ktk nchi ya watu wazima!

Nasubilia hatua zitakazochukuliwa na hivyo vyombo vya 'ulinzi na usalama'!

Ati document zimeandikwa confidential.....siri za serikali.....kumbe hizo ndo huwa siri za serikali? ......wizi ni siri ya serikali?

TISS ni chombo cha 'siri' za serikali.....?

Nasubili kuona uzalendo wa nchi yetu.....I am already at the crossing line.....mwenye kuanzisha uzi aanzishe tu-confirm wangapi tupo hapo na nini tuko tayari kufsnya dhidi ya hao wezi!

Msomw vizuri Invisible ameandika maneno ya busara wacha kukurupuka na kushutumu watu wakati hauna ushahidi.
Invisible ameandika "asionewe mtu wala asilindwe mtu".

Mpaka sasa naona makurupuka na kuonea watu kuwaita ni wezi ilhali hizi kurasa chache zzilizowekwa humu hakuna implication yoyote ya huo wizi? kulikoni?

Nilisema, ripoti ikitoka watu watabadili nyimbo na bado nnaendelea kusema hivyo hivyo.
 
Last edited by a moderator:
Tunataka pesa zirudishwe na adhabu za sheria za mahakama ya kijeshi dhidi ya wezi zichukuliwe. Si adhabu za kisheria ya mahakama ya jaji Chande No!....majaji wanahusika.....sina imani na mahakama zetu.....mahakama imehusika ktk wizi huuuuu...No sitaki kusikia kesi hiko mahakamani....watatuzuia kusikia, kuona na kujadili mwenendo wa kesi....

Nataka mahakama za kijeshi...kuanzia tar 27 pindi tu baada ya mjadara wa bunge na concl zake.

Tutafatilia pia mjadara wa bunge...nao ukiwa kama wa katiba pendekezwa tutawafuata hapo kabla ya kufunga bunge.
 
Kwa lipi?

Nakushauri subiri ripoti kamii, sikioni cha maana katika hizi kurasa zilizobandikwa hapa. Bali naona TANESCO inadaiwa na inajaribu kupunguza deni kwa kukaa chini na wadai wake.

Sasa kama mambo ni mepesi jinsi unavyoyaona wewe bibie,hizo sarakasi za kunyofoa hizo kurasa ni za nini? Hivi unadhani hao Magamba wenzio wangekuwa wanaona kama unavyoona wewe kungekuwa na sarakasi zote hizi?
 
Kwanini kurasa hizo zinyofolewe? Mbona sijaona ubaya wake kwa upande wowote?
Kuna viashiria kuwa watu walionywa au walikuwa na uhakika kuwa malipo sio sahihi ila yamefanyika!!!
Pia kuna wingu la kodi hapo, sijui maindocument imeainishaje hili.
 
Invisible nakushangaa unaposema "taarifa za kuanza kunyofolewa kurasa za ripoti hii", unajishusha hadhi yako. Ripoti za mitaani kuchomolewa kurasa wewe au mwingine yeyote wa karne hii zinamstuwa?

Ripoti kamili na rasmi zipo, na wala hizo za mitaani zisikufanye ukakurupuka. Ngoja Zitto aziwasilishe kwa mujibu wa kanuni na sheria za bunge, kama zitakuwa mbadala na zile za CAG na PCCB hapo ndipo utakuwa na la kusema, kwa sasa chunga hadhi yako usiingizwe mkenge ukawa biased.
 
Nasikia hata hii page imenyofolewa, basi inawekwa public...

attachment.php
Naona Invisible unamwaga Mboga na maji ya kunawa kabisa,:becky::becky::becky::becky::glasses-nerdy::msela::msela:
"Laus Jamiiforums"
 
Last edited by a moderator:
mkuu Invisible pls kwa hali ilivyo sasa nadhani hujuma kubwa zaidi zinaweza fanyika hata kukata mawasiliano ya mkongo wa taifa wa mawasilino, au hujuma nyingine zozote zitakazokwamisha mawasiliano.

Ni bora umalizie tu mkuu. Hali ishachafuka sana. Kuna uharamia wa miundo mbinu unaweza fanyika tutashanaana hapa mkuu. mi silali naisubiri kwa kweli. hizo page ulizoweka hazisisimui kabisa, wakati bado mnashauriana weka kwanza zile page zenye majina ya Payees.

Usiwe na wasiwasi,mkongo sio kama Tanesco wamemonopoly kila kitu,kuna mikongo mitatu hawawezi kukata yote at the same time,kuna mkongo wa taifa,ttcl,eassy,seacom.
~Invisible weka pages zenye majina tuzisave kabisa,maana Mwenyekti na makamu wake wapo kigoma wanaweza wasirudi maana yanaweza yakatokea ya kina Ntayamira na abelliymana.
 
Last edited by a moderator:
Kwanini kurasa hizo zinyofolewe? Mbona sijaona ubaya wake kwa upande wowote?

Utaona kuwa kuna watu humu huwa hawafikiri hata kidogo, hizo kurasa zilichomolewa kwenye kompyuta? wanataka ripoti iliyovuja mitaani zaidi ya iliyopo kihalali kwa PAC?

Hata mimi sikioni ni nini kikubwa kwenye hizi kurasa zilizowekwa hapa mpaka watu waongee hovyo.
 
Kwa lugha nyepesi ni kuwa hawa "nguruwe"(CCM) walizidiana ulafi na kuanza "kudhulumiana"..Sasa kuna kundi jingine la nguruwe baada ya kuona "wamedhulumiwa sana" wakaamua sasa watamwaga ugali..na nguruwe wengine nao wanadai watamwaga mboga…Siku ya kumwaga ugali na mboga ni jumatatu…kwa hiyo mkuu jumatatu tembea na TV yako…
Ndio kusema upinzani walipewa tu hizo datazi kutoka kwa nguruwe"wazalendo"..Wapinzani wakazimwagwa data uwanjani... na huyu mmwaga data mpaka sasa analindwa na hao nguruwe "wazalendo"
Ninavyojua mimi tushukuru huko "kudhulumiana" kwao ndo tumepata hizo data…
We mkuu hujaona swala la katiba lilikuwaje!!!upinzani, wamelia wee lakini hawajasikilizwa na swala la katiba ndio muhimu zaidi lakini magamba wakalidharau..lakini hili la mkwanja wamejitokeza…hawa magamba sio wakuwaamini mkuu..
Likiisha hili kuna jingine limeshaanza kufumuka..hili ni la ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara…hapo napo kuna hela ya kufa mtu, hii hela ya Singa wenyewe wanaiita hela ya ugoro…hapa ndio CCM itakuwa ni kitimtimu maana hawa watakaojeruhiwa jumatatu lazima wafe na wale wa gesi…
Kakobe atakumbukwa...

Tuombe Mungu hawa Nguruwe waendelee kudhulumiana...Maana bila kudhulumiana wananchi tutaendelea kunyanyasika
 
mkuu Invisible pls kwa hali ilivyo sasa nadhani hujuma kubwa zaidi zinaweza fanyika hata kukata mawasiliano ya mkongo wa taifa wa mawasilino, au hujuma nyingine zozote zitakazokwamisha mawasiliano.

Ni bora umalizie tu mkuu. Hali ishachafuka sana. Kuna uharamia wa miundo mbinu unaweza fanyika tutashanaana hapa mkuu. mi silali naisubiri kwa kweli. hizo page ulizoweka hazisisimui kabisa, wakati bado mnashauriana weka kwanza zile page zenye majina ya Payees.

Sasa hizo page zinazosemekana zimenyofolewa zimesha kuwa "hazisisimui", unafikiri hizo zilizopo mitaani ndio zitakusisimua?

Mmeshakuwa disappointed mapema hii? mmejazana uongo humu, sasa subirini Zitto awasilishe ripoti yake rasmi muone mlivyo danganywa.
 
Invisible nakushangaa unaposema "taarifa za kuanza kunyofolewa kurasa za ripoti hii", unajishusha hadhi yako. Ripoti za mitaani kuchomolewa kurasa wewe au mwingine yeyote wa karne hii zinamstuwa?

Ripoti kamili na rasmi zipo, na wala hizo za mitaani zisikufanye ukakurupuka. Ngoja Zitto aziwasilishe ka mujibu wa kanuni na sheia za bunge, kama zitakuwa mbadala na zile za CG na PCCB hapo ndipo utakuwa na la kusema, kwa sasa chunga hadhi yako usiingizwe mkenge ukawa biased.

Tuliza papa hilo, wajanja wa ccm wapo kwenye hiyo list.......wewe mtoka povu kazi yako ni kushabikia wenzio watengeneze neema zao.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom