Jeshi la Polisi nchini, msimtishe Askofu Mwingira, bali zifanyieni kazi tuhuma nzito alizozitoa

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Jukumu namba moja la Jeshi la Polisi nchini, ni kuwalinda Raia na mali zao.

Katika mahubiri aliyoyatoa katika sikukuu ya Krismas, Askofu Mwingira wa kabisa la Efatha nchini, alitoa tuhuma nzito Sana kwa vyombo vya serikali, kuwa alinusurika kuuawa mara 3 na akaendelea kueleza kuwa hata yule dada ambaye alikuwa "informer" wake, aliuawa Katika mazingira ya kutatanisha, Katika Hoteli ya Rombo Green View, iliyoko Shekilango!

Pamoja na tuhuma hizo akaendelea kuelezea kuwa vyombo vya serikali viliharibu mali zake zilizoko shambani kwake zenye gharama ya mabilioni ya shilingi.

Sasa ni kwanini Jeshi la Polisi, badala ya kufanyia uchunguzi taarifa hizo, ambazo ziko wazi kabisa, badala yake, kamanda maalum wa Jeshi la Polisi, wa Dar, Jumanne Muliro, anampiga "mkwara" mzito Askofu Mwingira, ajitokeze Katika kituo cha Polisi, ndani ya masaa 24 kwa mahojiano na wameeleza kuwa kama madai yake yataonekana kuwa ni ya uongo, Jeshi la Polisi litamchukulia hatua na kumfungulia mashitaka?!

Hivi ni kitu gani alichoongea Askofu Mwingira, ni kigeni nchini mwetu?

Hivi kama kweli Jeshi la Polisi, liko "serious" na usalama wa Raia wake, hebu nijaribu tu kuwauliza, ni kitu gani kinachowafanya wao, waendelee kusuasua, kufanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa risasi, kwa aliyekuwa mbunge wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Tundu Lissu,zaidi ya miaka 4 iliyopita na hakuna hata mshukiwa mmoja aliyekamatwa Ili kuhojiwa, kutokana na tukio hilo la kutisha Sana?

Hivi Jeshi letu la Polisi, linaweza likaeleza walipo watu waliopotea zaidi ya miaka 4 iliyopita, kwa mfano Ben Saanane na mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Azory Gwanda?

Hivi Jeshi la Polisi linatufanya watanzania wote ni wajinga na linatofautiana Katika utendaji wake hata na Rais wa nchi, Samia Suluhu Hassan, ambaye alitamka wazi kuwa kuna watu wengi Sana walioumizwa, kutokana na vitendo vya kikatili, vilivyofanywa na serikali ya awamu ya 5 chini ya Mwendazake, Hayati John Magufuli?

Ni hayo tu ninayopenda Jeshi letu la Polisi iyatolee ufafanuzi.
 
Hakuna lolote la maana litakalofanyika, hapo jeshi la polisi linajitutumua tu ili lionekane lipo.

Uhuni wowote atakaofanyiwa raia wa nchi hii na kiongozi wa serikali ya CCM, jeshi la polisi haliwezi kuchukua hatua yoyote ya maana zaidi ya kuishia kutoa matamko ya kisiasa yasiyo na msaada wowote kwa waathirika.

Nashangaa wengi mpaka leo bado wanapiga kelele za ukatili wa awamu iliyopita, hawajui wengine bado wako wanatawala, wao wameamua kukomaa na past, badala ya kupoteza muda kuangalia way forward nini kifanyike ili ile hali isijekujirudia.

Hao jamaa hulindana.
 
Jiwe limetupwa gizani linagonga gonga waovu kelele lazima zisikike kwa sauti kuu
Huyo Askofu ameeleza hata mahali alipouliwa "informer" wake wa kike, kuwa ni Rombo Green View Hotel, ni kwanini Jeshi la Polisi halianzi kufanya uchunguzi huko, Ili libaini ukweli, badala ya kumpiga mkwara, Askofu Mwingira kuwa atafunguliwa mashitaka ya jinai, iwapo itagundulika kuwa tuhuma alizozitoa ni za uongo?
 
Nakubaliana na wewe kuwa baadhi ya Askari na maafisa wa jeshi la Polisi wanakosa weledi katika kazi zao na wanatumia mabavu sana kuwatisha watu. Ni wajibu wa Rais Samia anayekemea sana matumizi ya nguvu, kuanza kulisafisha jeshi la polisi. Itakuwa vizuri aanze kwa kujisafisha mwenyewe kwa kumwondoa Mbowe gerezani
 
Kwa hiyo bila yeye kwenda wakamhoji au bila kukamatwa hizo tuhuma watazifanyiaje kazi mkuu, au wawe wanampigia simu wanaandika maelezo?
 
Jukumu namba moja la Jeshi la Polisi nchini, ni kuwalinda Raia na mali zao.

Katika mahubiri aliyoyatoa katika sikukuu ya Krismas, Askofu Mwingira wa kabisa la Efatha nchini, alitoa tuhuma nzito Sana kwa vyombo vya serikali, kuwa alinusurika kuuawa mara 3 na akaendelea kueleza kuwa hata yule dada ambaye alikuwa "informer" wake, aliuawa Katika mazingira ya kutatanisha, Katika Hoteli ya Rombo Green View, iliyoko Shekilango!

Pamoja na tuhuma hizo akaendelea kuelezea kuwa vyombo vya serikali viliharibu mali zake zilizoko shambani kwake zenye gharama ya mabilioni ya shilingi.

Sasa ni kwanini Jeshi la Polisi, badala ya kufanyia uchunguzi taarifa hizo, ambazo ziko wazi kabisa, badala yake, kamanda maalum wa Jeshi la Polisi, wa Dar, Jumanne Muliro, anampiga "mkwara" mzito Askofu Mwingira, ajitokeze Katika kituo cha Polisi, ndani ya masaa 24 kwa mahojiano na wameeleza kuwa kama madai yake yataonekana kuwa ni ya uongo, Jeshi la Polisi litamchukulia hatua na kumfungulia mashitaka?!

Hivi ni kitu gani alichoongea Askofu Mwingira, ni kigeni nchini mwetu?

Hivi kama kweli Jeshi la Polisi, liko "serious" na usalama wa Raia wake, hebu nijaribu tu kuwauliza, ni kitu gani kinachowafanya wao, waendelee kusuasua, kufanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa risasi mfululizo, kwa aliyekuwa mbunge wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Tundu Lissu,zaidi ya miaka 4 iliyopita na hakuna hata mshukiwa mmoja aliyekamatwa Ili kuhojiwa, kutokana na tukio hilo la kutisha Sana?

Hivi Jeshi letu la Polisi, linaweza likaeleza walipo watu waliopotea zaidi ya miaka 4 iliyopita, kwa mfano Ben Saanane na mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Azory Agwanda?

Hivi Jeshi la Polisi linatufanya watanzania wote ni wajinga na linatofautiana Katika utendaji wake hata na Rais wa nchi, Samia Suluhu Hassan, ambaye alitamka wazi kuwa kuna watu wengi Sana walioumizwa, kutokana na vitendo vilivyofanywa na serikali ya awamu ya 5 chini ya Mwendazake, John Magufuli?

Ni hayo tu ninayopenda Jeshi letu la Polisi iyatolee ufafanuzi.
naunga mkono hoja
 
Kwa hiyo bila yeye kwenda wakamhoji au bila kukamatwa hizo tuhuma watazifanyiaje kazi mkuu, au wawe wanampigia simu wanaandika maelezo?
Hebu chukulia mfano wa tukio la Tundu Lissu, si wao wenyewe Polisi walikuwa wakituaminisha kuwa uchunguzi wao haujakamilika, kwa kuwa Tundu Lissu na dereva wake wamekimbia nchi?

Hebu jiulize mbona Tundu Lissu alirudi nchini wakati wa uchaguzi mkuu, kama ni kweli uchunguzi wao ulikwama kwa kuwa Tundu Lissu na dereva wake "wamekimbia" nchi, hiki kipindi walichorudi nchini, Polisi walifanya juhudi gani kuwahoji hao akina Tundu Lissu na dereva wake??
 
Hebu chukulia mfano wa tukio la Tundu Lissu, si wao wenyewe Polisi walikuwa wakituaminisha kuwa uchunguzi wao haujakamilika, kwa kuwa Tundu Lissu na dereva wake wamekimbia nchi?

Hebu jiulize mbona Tundu Lissu alirudi nchini wakati wa uchaguzi mkuu, kama ni kweli uchunguzi wao ulikwama kwa kuwa Tundu Lissu na dereva wake "wamekimbia" nchi, hiki kipindi walichorudi nchini, Polisi walifanya juhudi gani kuwahoji hao akina Tundu Lissu na dereva wake??
Aaa aaa! Lissu anaingiaje tena hapa! Hapo ndipo tunakuwa na mihemiko, tunaongelea Mwingira, ulitaka information wazipateje kma siyo kumuita na kuchukua maelezo yake na kujua pa kuanzia ni wapi?
 
Jukumu namba moja la Jeshi la Polisi nchini, ni kuwalinda Raia na mali zao.

Katika mahubiri aliyoyatoa katika sikukuu ya Krismas, Askofu Mwingira wa kabisa la Efatha nchini, alitoa tuhuma nzito Sana kwa vyombo vya serikali, kuwa alinusurika kuuawa mara 3 na akaendelea kueleza kuwa hata yule dada ambaye alikuwa "informer" wake, aliuawa Katika mazingira ya kutatanisha, Katika Hoteli ya Rombo Green View, iliyoko Shekilango!

Pamoja na tuhuma hizo akaendelea kuelezea kuwa vyombo vya serikali viliharibu mali zake zilizoko shambani kwake zenye gharama ya mabilioni ya shilingi.

Sasa ni kwanini Jeshi la Polisi, badala ya kufanyia uchunguzi taarifa hizo, ambazo ziko wazi kabisa, badala yake, kamanda maalum wa Jeshi la Polisi, wa Dar, Jumanne Muliro, anampiga "mkwara" mzito Askofu Mwingira, ajitokeze Katika kituo cha Polisi, ndani ya masaa 24 kwa mahojiano na wameeleza kuwa kama madai yake yataonekana kuwa ni ya uongo, Jeshi la Polisi litamchukulia hatua na kumfungulia mashitaka?!

Hivi ni kitu gani alichoongea Askofu Mwingira, ni kigeni nchini mwetu?

Hivi kama kweli Jeshi la Polisi, liko "serious" na usalama wa Raia wake, hebu nijaribu tu kuwauliza, ni kitu gani kinachowafanya wao, waendelee kusuasua, kufanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa risasi, kwa aliyekuwa mbunge wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Tundu Lissu,zaidi ya miaka 4 iliyopita na hakuna hata mshukiwa mmoja aliyekamatwa Ili kuhojiwa, kutokana na tukio hilo la kutisha Sana?

Hivi Jeshi letu la Polisi, linaweza likaeleza walipo watu waliopotea zaidi ya miaka 4 iliyopita, kwa mfano Ben Saanane na mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Azory Gwanda?

Hivi Jeshi la Polisi linatufanya watanzania wote ni wajinga na linatofautiana Katika utendaji wake hata na Rais wa nchi, Samia Suluhu Hassan, ambaye alitamka wazi kuwa kuna watu wengi Sana walioumizwa, kutokana na vitendo vilivyofanywa na serikali ya awamu ya 5 chini ya Mwendazake, Hayati John Magufuli?

Ni hayo tu ninayopenda Jeshi letu la Polisi iyatolee ufafanuzi.
Mwingira ukifanya mchezo yatakukuta ya BEN Ben Saanane: Ninatishwa kuuawa kwa kuikosoa Serikali
 
Aaa aaa! Lissu anaingiaje tena hapa! Hapo ndipo tunakuwa na mihemiko, tunaongelea Mwingira, ulitaka information wazipateje kma siyo kumuita na kuchukua maelezo yake na kujua pa kuanzia ni wapi?
Nimetoa mfano wa tukio la Tundu Lissu, Ili ijulikane namna Jeshi letu la Polisi linavyotumiwa na watawala wetu kwa manufaa ya kisiasa
 
Kwa mujibu wa kauli zake, Askofu Mwingira ni Muhanga/Victim wa jaribio la mauaji. Jeshi la polisi lenye weledi linapaswa kumtazama Askofu Mwingira kama Muhanga na kama shahidi. Awasaidie kutafuta taarifa za kuwafichua wahalifu - kama inawezekana.

Lakini kwakuwa polisi yetu ni chombo cha watawala kutawalia zaidi kuliko chombo cha kulinda raia na mali zao - hasa kunapozuka mgogoro kati ya serikali na raia, basi hutokea serikali inapotuhumiwa jeshi la polisi hugeuka kuwa wakili wa serikali. Sasa, eti Askofu Mwingira anatazamwa kama muhalifu. Ajabu na kweli.

Tuombe, kwamba siku moja nchi hii itakuwa na vyombo huru vya ulinzi na usalama...ili kwamba akitokea kiongozi wa kiserikali katili, mjinga, muuaji, muovu atadhibitiwa. Kwa sasa bado tupo kwenye nyakati za ujinga mwingi kwa kudhani viongozi wa nafasi za juu za uongozi ni miungu na wakamilifu - pamoja na ushahidi wa wazi tuliokwisha funuliwa.

Ni lini tutagundua kwamba, serikali inaundwa na watu ambao wanaweza kuwa wema au wabaya! werevu au mahambe?
FB_IMG_1640689220762.jpg
View attachment 2060515
 
Huyo Askofu ameeleza hata mahali alipouliwa "informer" wake wa kike, kuwa ni Rombo Green View Hotel, ni kwanini Jeshi la Polisi halianzi kufanya uchunguzi huko, Ili libaini ukweli, badala ya kumpiga mkwara, Askofu Mwingira kuwa atafunguliwa mashitaka ya jinai, iwapo itagundulika kuwa tuhuma alizozitoa ni za uongo?
Ili Jeshi lianze uchunguzi ni lazima muhusika apeleke malalamiko yake kituoni sio kusemea majukwaani. Kimsingi ni vigumu mno kufanyia kazi habari za majukwaani sasa kama mchungaji ni mwelewa akatoe ushirikiano ili jeshi la polisi lifanye kazi yake
 
NILIMSHANGAA Sana Simbachawene kushaangazwa na tuhuma za Mwingira! Kana kwamba haamini yule mtu alikuwa katili na mnyama?! Unafki ni kitu kibaya Sana.
 
Jukumu namba moja la Jeshi la Polisi nchini, ni kuwalinda Raia na mali zao.

Katika mahubiri aliyoyatoa katika sikukuu ya Krismas, Askofu Mwingira wa kabisa la Efatha nchini, alitoa tuhuma nzito Sana kwa vyombo vya serikali, kuwa alinusurika kuuawa mara 3 na akaendelea kueleza kuwa hata yule dada ambaye alikuwa "informer" wake, aliuawa Katika mazingira ya kutatanisha, Katika Hoteli ya Rombo Green View, iliyoko Shekilango!

Pamoja na tuhuma hizo akaendelea kuelezea kuwa vyombo vya serikali viliharibu mali zake zilizoko shambani kwake zenye gharama ya mabilioni ya shilingi.

Sasa ni kwanini Jeshi la Polisi, badala ya kufanyia uchunguzi taarifa hizo, ambazo ziko wazi kabisa, badala yake, kamanda maalum wa Jeshi la Polisi, wa Dar, Jumanne Muliro, anampiga "mkwara" mzito Askofu Mwingira, ajitokeze Katika kituo cha Polisi, ndani ya masaa 24 kwa mahojiano na wameeleza kuwa kama madai yake yataonekana kuwa ni ya uongo, Jeshi la Polisi litamchukulia hatua na kumfungulia mashitaka?!

Hivi ni kitu gani alichoongea Askofu Mwingira, ni kigeni nchini mwetu?

Hivi kama kweli Jeshi la Polisi, liko "serious" na usalama wa Raia wake, hebu nijaribu tu kuwauliza, ni kitu gani kinachowafanya wao, waendelee kusuasua, kufanya uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa risasi, kwa aliyekuwa mbunge wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Tundu Lissu,zaidi ya miaka 4 iliyopita na hakuna hata mshukiwa mmoja aliyekamatwa Ili kuhojiwa, kutokana na tukio hilo la kutisha Sana?

Hivi Jeshi letu la Polisi, linaweza likaeleza walipo watu waliopotea zaidi ya miaka 4 iliyopita, kwa mfano Ben Saanane na mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Azory Gwanda?

Hivi Jeshi la Polisi linatufanya watanzania wote ni wajinga na linatofautiana Katika utendaji wake hata na Rais wa nchi, Samia Suluhu Hassan, ambaye alitamka wazi kuwa kuna watu wengi Sana walioumizwa, kutokana na vitendo vya kikatili, vilivyofanywa na serikali ya awamu ya 5 chini ya Mwendazake, Hayati John Magufuli?

Ni hayo tu ninayopenda Jeshi letu la Polisi iyatolee ufafanuzi.
Vipi apewe kadi namba ngapi?
 
Back
Top Bottom