Je, umeshawahi pitia maisha magumu?

Je, umeshawahi pitia maisha magumu?

Ndugu, ni vigumu sana kuelewa ninayopitia. Na kile ninachopata baada ya maombi.

Bila kufanya hivi , tayari ningekuwa nimeishajinyonga zamani au kufa.

Last week nilipata attack nikiwa bafuni naoga, nilianguka ghafla...damu zilitoka nyingi sana... ( nakumbuka , mchana yake kuna mtu alinitamkia atanifanya kitu kibaya - jioni nikapatwa na hali hii)
ecc23a8c060db886933b6764fb298519.jpg


Ni watu wachache sana wakianguka bafuni kama nilivyoanguka wanapona. Mara nyingi huwa wanapata stroke au kufa.

Nimenusurika kufa mara nyingi sana Ndugu. Huwezi kunielewa kwa kusoma hapa.
Jamani pole kaka..ee Mungu hebu sikia shida za huyu ndugu umtue mzigo mzito aloubeba naamini kwa jina lako utatenda juu yake baba amina..pole pole sana mpaka umepata hadi stroke Mungu akuponye
 
Maisha yanachangamoto zake hata mimi hali ninayoipitia mungu kwa kweli anaijua naona hata uvivu kuisimulia lakini naamini siku njema yaja yote hayo tutayasahau wakuu,tuwe na imani
Neno La Mungu > Amani >Furaha
 
Yan hizo zote nimeshazipitia siwez kuja kusahau kwenye maisha yangu kabisa nilala chin kwa kulalia nguo zangu na kula mkate kama chakula kwa muda wa wiki nzima. Kuna wakati nilitaman kujiua niliumwa vibaya sana halafu hakuna mtu sio rafik wala ndugu anayekupa ushirikiano wa dhati. Oh MGD sitak kukumbuka kabisa.
pole JIKESHUPA,salam kwa MZIWANDA N.
 
Hapa duniani nimepitia mengi sana magumu kwa upande wangu ila siwezi kuyalinganisha kwa namna yoyote na ya wengine.
Kupitia matatizo nimejifunza kuwa always there is an alternative way kwa tatizo lolote,unachotakiwa kufanya ni kupanua ubongo wako kwa hatua 1 then you will find a way ktk tatizo lako
 
Yesu Kristo mwenyewe alitumia muda mwingi sana kuwa karibu na Mungu katika mapito yake.

Wakati mwingine alijitenga na watu na kwenda mlimani kusali Usiku kucha.

fe04c2564bb69be251b526d3b18687fc.jpg
Naam... Paulo anasema na Wafilipi.

"Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo nayo.
12 Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.
13 Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
 
Maisha yanachangamoto zake hata mimi hali ninayoipitia mungu kwa kweli anaijua naona hata uvivu kuisimulia lakini naamini siku njema yaja yote hayo tutayasahau wakuu,tuwe na imani
Hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea mkuu,naamini unakopita sasa yatakufanya kua imara zaidi...
 
"Tutawajaribun kwa matatizo na mabalaa" "Matatzo yakshazd ndo tunakumbukaga dua"
Nashukuru sote tuna mkumbuka Mungu na tunakir uwepo wa Mungu kwenye matatzo, shda, misukosuko,taabu n.k. Tusiache pia kumkumbuka na kumtaja kwenye RAHA, FURAHA.
 
Back
Top Bottom