Je tuhahitaji tena Ze Utamu?

Je tuhahitaji tena Ze Utamu?

Status
Not open for further replies.
Hata thread zetu nyingi hapa JF kwa tabaka kubwa tu la waTZ zinaonekana ni za uchochezi na zilizovuka mipaka, Muulize Dr. Nchimbi, Mh. Masha, n.k. JF Nayo Ifungwe?
Alafu ukiangalie trend ya ze Utamu ilikuwa inajikusanyia mashabiki na walikuwa wanatengeneza pass wafike golini, na golini ndio huyo waliyemfikia leo. Nasita kusema zeUtamu watakuwa na ufadhiri wa maadui zake mkuu wa kaya kisiasa, waliorecruit vijana wenye vipaji na akili kwa ajili ya kuwaisaidia kuelekea 2010. Ngoja tuone.
Juzi Juzi hapa ilipotolewa picha ya Kagisi wengi hapa mkajifanya mna data za kutuaminisha kuwa mwisho wa ile web umefika, matokeo yake imeboreshwa mara dufu, hata sisi tuwe makini kabla hatujatoa utabiri wetu tunapoteza credibility zetu.
 
Kwa hiyo kwa mujibu wako wewe unaona kuwa utu na heshima ya raisi vina thamani zaidi ya Nsia kwa vile tu raisi kachaguliwa na watu wengi?

Well, mimi kama Ngabu ninastahili heshima kama binadamu mwingine yeyote yule regardless ya cheo au nafasi yoyote aliyonayo mtu mwingine. Heshima yangu, utu, na ubinadamu wangu ni sawasawa kabia na ule wa Kikwete, Obama, Malkia Elizabeth, Nsia, Aunty Mudy, Masanilo, Juma Kilaza na wengineo. I am not above or under anyone.

All Animals are equal but there are some that are more equal than Others!

Utamu Ipatiwe suluhisho la kudumu ili kupunguza Machungu ambayo yameshawapata wana wa Tanzania wengi
 
Kinachoniudhi mimi ni hii outrage wanayoionyesha baadhi ya watu humu kwa vile tu aliyefanyiwa mbaya ni raisi. Ebo! Vipi leo muonyeshe kukasirishwa hivi wakati kila siku raia wa kawaida wanabandikwa huko utamu.

Inakuwa kama vile heshima ya raisi ni bora zaidi kuliko heshima ya watu wengine. Watu mbona hamuwaki hivi muonapo picha za akina Nsia na wengineo? Acheni unafiki wenu bana.

Nsia na JK wote ni binadamu sawa lakini Jk ni kiongozi wa nchi tena ni alama ya taifa letu, mara kadhaa huwakilisha taifa letu kwenye mikutano ya dunia sijasikia nsia akifanya hivyo, hata hivyo kuna heshima anapewa rais hata katika sheria hawezi kufunguliwa mashtaka ya jinai akiwa bado ni rais. Sifurahishwi na kitendo cha kubandikwa picha za nsia lakini naogopa inapofikia zinabandikwa picha za rais.
 
what is going on here? kwa nini watu mnaenda utamu? I have perused the blog, is dirty,haina maadili na sidhani kama mtanzania wa kaiwadia anatakiwa apitie kule.

au ni zile hadithi za mkuu wa mkoa? kukamata machangudoa na sio wateja?? HII BLOG, IKIKOSA WATEMBELEAJI BASI ITAKUFA NATURALY, MBAYA ZAIDI KUANZISHA THREAD KAMA HII NDIYO KUMPA KICHWA NA ATAENDELEA NA UPUMBAVU WAKE!

Kuna watu amepinda, hi issues tumezipigia kelele sana, tumeruhusu haya mmabo yasmwe na watu, kwenye magazetui kuna vituko, watu wengi wanatolewa na kila siku.

Sidhani kama ni JK tu dunia hii, almost all leaders suffres the same problem.Kwa TANZANIA haikutakiwa tufike huko!!! ila tumeruhusu vidogovidogo kila kona, leo inapofikia hapa watu wanapiga kelele!

watu wanasema ushoga is Ok, usagaji is ok here In Tz! unafikri wao ukiwawekea picha kama hii watahuzunika kama sisi?


Nchi amelalamikiwa kuwa haina ulinzi, ulinzi sio tu kuishia kushika bunduki, ulinzi ni kuwa na watu vichwa wa kuweza kufunga mitandao kama hii, HII INAWEZEKANA! WATU WAPO! UWT amkeni!

CCM KAMA MNATAKA KUNDAMANA BASI THIS IS RIGHT REASON, SIO MNAANDAMANA MTU AKITOA HOTUBA ZA UTUMBO, kundaman kuwe

1.Kufungia magazeti yote yenye mlengo wa kingono
2. Night club zote zinazohamasisha haya mambo
3.Vyumba au vituo vya kuonesha video za utupu zilizozagaa kila kona DSM!
4.TUPIGE KELELE TURUDI ENZI ZILE,.... inawezekana!

!
 
Sitaki ligi lakini nadhani hapo tutakubaliana kupingana bila kupigana. Heshima ya mwenye mamlaka ya madaraka haiizidi heshima yangu mimi kama raia wa kawaida ninayestahili kutendewa kwa heshima na kuwatendea kwa heshima binadamu wengine kama mimi.

wee rudi kwenu "Nyarugusu" ndio utajua tofauti yako na "Rais".....kwi kwi kwi kwi....
 
Please close th e blog outright. Hata kama ungekuwa ukweli haingii akilini kwa mtu mwenye akili timamu kupiga au kuonyesha uozo wa nanmna hii. HUYU ZEUTAMU ACHUKULIWE HATUA ZA KISHERIA MARA MOJA. hivi hamna IT wa kuiblock nchi hii??
 
Hata thread zetu nyingi hapa JF kwa tabaka kubwa tu la waTZ zinaonekana ni za uchochezi na zilizovuka mipaka, Muulize Dr. Nchimbi, Mh. Masha, n.k. JF Nayo Ifungwe?
Alafu ukiangalie trend ya ze Utamu ilikuwa inajikusanyia mashabiki na walikuwa wanatengeneza pass wafike golini, na golini ndio huyo waliyemfikia leo. Nasita kusema zeUtamu watakuwa na ufadhiri wa maadui zake mkuu wa kaya kisiasa, waliorecruit vijana wenye vipaji na akili kwa ajili ya kuwaisaidia kuelekea 2010. Ngoja tuone.
Juzi Juzi hapa ilipotolewa picha ya Kagisi wengi hapa mkajifanya mna data za kutuaminisha kuwa mwisho wa ile web umefika, matokeo yake imeboreshwa mara dufu, hata sisi tuwe makini kabla hatujatoa utabiri wetu tunapoteza credibility zetu.

dada umeongea vizuri kama sura yako....point tupu.
 
website inaitwa zeutamu kwa hiyo ukienda kwenye hiyo website uwezi ukakuta jukwaa la siasa utakuta zeutamu......

lazima ukubali website mbalimbali zenye maudhui mbalimbali...

kwa huku UK kunawasomaji wa news of the world/ the sun ni tofauti na FT
ukisoma hello/ok ni tofauti na ukisoma FT or The Economist
 
Kabisa kabisa Raisi ni mamlaka mazee, huwezi linganisha NN na JK labda kama unataka ligi!

Mamlaka ameyatoa wapi, siamepata toka kwa watanzania..........sasa kwa nini tuwe na double standards? kama watz wengine walishadhalilishwa in the same way, na hakuna voice zilizotolewa na mamlaka husika zaidi kuchekelea tu mauchafu hayo, kwa nini leo huyu aliyepewa mamlaka na wananchi yanapomtokea haya kwake tuone kama ni big issue, kama si unafiki ni nini? endeleeni kuchekelea na leo why panic?
 
Nsia na JK wote ni binadamu sawa lakini Jk ni kiongozi wa nchi tena ni alama ya taifa letu, mara kadhaa huwakilisha taifa letu kwenye mikutano ya dunia sijasikia nsia akifanya hivyo, hata hivyo kuna heshima anapewa rais hata katika sheria hawezi kufunguliwa mashtaka ya jinai akiwa bado ni rais. Sifurahishwi na kitendo cha kubandikwa picha za nsia lakini naogopa inapofikia zinabandikwa picha za rais.

Nimeshaona picha ya Bush akimdinya Osama. Nimeshaona picha ya Mama Clinton akiigiza kwenye porno. Bill Clinton ndio usiseme kabisaaa. Sarah Palin tayari watu wameshamtengenea porno. Hawa nao wote ni viongozi wanaowakilisha taifa lao.

Kutengeneza picha kama hiyo si kazi ngumu kama unajua kutumia photoshop. Hata mimi ninaweza kuzitengeneza picha kama hizo halafu nikazisambaza kwenye barua pepe.

Kinachonichukiza mimi ni huu unafiki wa kuthamini watu wengine na kutowathamini wengine. Sikatai kuwa hiyo picha ni repulsive lakini kwa mtu yeyote mwenye akili atagundua kuwa ni ya kutengeneza.

Acheni double standards na karibuni ktk karne ya 21!
 
Nimepata picha zake, nimejua alisoma wapi na lini na kwa sasa anafanya kazi. Sina sababu ya kutishia sababu sioni sababu ya kufanya hivyo. Nimeomba aache upuzi wake vinginevyo nitamweka wazi hapa jf sina utani na uchafu kwani siwezi kukubali uchafu.

Siamini, then you are extremely far worst person than Utamu!
 
Kinachoniudhi mimi ni hii outrage wanayoionyesha baadhi ya watu humu kwa vile tu aliyefanyiwa mbaya ni raisi. Ebo! Vipi leo muonyeshe kukasirishwa hivi wakati kila siku raia wa kawaida wanabandikwa huko utamu.

Inakuwa kama vile heshima ya raisi ni bora zaidi kuliko heshima ya watu wengine. Watu mbona hamuwaki hivi muonapo picha za akina Nsia na wengineo? Acheni unafiki wenu bana.

Nakupa big up NN;
Kila cku nasema cc WaTZ 2wanafiki sana na ni ndumilakuwili. Likimfika mtu ni la kwake hilo, lakini cku ya cku likikutokea wewe unataka watu woote wakuonee huruma.

Kama kitu hakifai kiwe hakifai tu, heshma ni kitu cha bure na kila mtu hata mtoto mdogo aliezaliwa leo anastahili heshma yake kutoka kwa mwengine.

Tulikosea tangu tulipoikaribisha teknolojia; Nawashauri watu wa IS (najua wapo humo jamvini) wawasiliane na wenzao wa CHINA au CUBA kujua waliwezaje ku-block site zote zisizotakiwa nchini mwao.

Vinginevyo ni lutwanga maji ktk kinu tuu
 
Kinachonichukiza mimi ni huu unafiki wa kuthamini watu wengine na kutowathamini wengine. Sikatai kuwa hiyo picha ni repulsive lakini kwa mtu yeyote mwenye akili atagundua kuwa ni ya kutengeneza.

Acheni double standards na karibuni ktk karne ya 21!

NN,

Watu wanakimbia ukweli huu sielewi kwa nini! Watz kibao wameshakuwa victim wa hii kitu......mijitu ikajikausha huku kimyakimya ikivisit ile site na kuchekelea, leo mkuu wa kaya kanaswa.....midomo juu, why?

Wengine (e.g Gembe & Co) eti wanakimbilia mpaka kwa Mwanakijiji na Robot eti wasaidie kufind a way ya kuimaliza Ze utama....mlikuwa wapi?

BWT...ile signature yako mbona umebadili....thread hii ni mahala pake ''Miafrika ndivyo tulivyo'' best say, Mitanzania ndivyo tulivyo!
 
Nimeshaona picha ya Bush akimdinya Osama. Nimeshaona picha ya Mama Clinton akiigiza kwenye porno. Bill Clinton ndio usiseme kabisaaa. Sarah Palin tayari watu wameshamtengenea porno. Hawa nao wote ni viongozi wanaowakilisha taifa lao.

Kutengeneza picha kama hiyo si kazi ngumu kama unajua kutumia photoshop. Hata mimi ninaweza kuzitengeneza picha kama hizo halafu nikazisambaza kwenye barua pepe.

Kinachonichukiza mimi ni huu unafiki wa kuthamini watu wengine na kutowathamini wengine. Sikatai kuwa hiyo picha ni repulsive lakini kwa mtu yeyote mwenye akili atagundua kuwa ni ya kutengeneza.

Acheni double standards na karibuni ktk karne ya 21!

Sio kuthamini watu wengine tu, la kushtuka wakati is too late! nasema haya mambo tumeyalea wenyewe! wengine wanapopiga kelele wanaonekana aidha walokole au wajinga, au hawaendi na wakati! we are to be blamed of this current situation.

Watanzania tunaona mtu wa kuchukua hatua fulani ni mwingine na si wewe! thye utamau ataendela kuwepo tu kama kuna watembeleaji kweye hiyo tovuti!

Huyu mtu emelelewa na watanzania watembeleaji katika hiyo tovuti! INAPOFIKIA HUYU SHETANI ANAKUWA MKUBWA TUNASEMA NO, ENDELEA KUWA SHETANI MDOGO HAPA UMEVUKA MPAKA!, TUNASAHU SHETANI NI SHETANI ANAWEZA KUFANYA LOLOTE, UTAMU HATAONA AIBU MPAKA KUWEKA PICHA YA UTUPU YA MAMA YAKE!

HE IS DEVIL! NA MAEKUWA HIVI SIKU NYINGI!

Tumezoa kuremedy matatizo yakishatokea na ndivyo tulivyo, KILA SIKU TUNAWALAUMU VIONGOZI KUTOZUIA MATATIZO, LAKINI INAONEKANA NI TABIA YETU, TUMERUHUSU VITABIA VYA AJABU AJABU kila kona ktk nchi yetu!

solution sio kufuta utamu tu NO.

1, Video za x kila kona DSM
2. mAGAZETI YA NGONO, yakiwemo ya shigongo
3. kuna baadhi ya miziki ina promote hii tabia
4. Kuna night clubs na casino kibao kila kona
5. tovuti mbali na utamu ziko nyingi na hazijapigwa marufuku Tz
6. Just go to internet cafe, watoto wanashinda huko!

do i need to say more?

Hii ya JK iendane na waziri mmoja kuwajibika, utaona hata kama watalisemea hili swala!

kesho zamu ya wewe! watachukua picha yako na kuitengeneza hivyo, kwa sababu wewe sio rais utaona.............kama watu watapiga kelele.
 
lakini ni watu wengi sana ambao wamekuwa ma victims wa hiyo site since ianzishwe, lakini si unajua tena mambo ya mkuki kwa .....,kwa binadamu unauma....!!!
ni mara ngapi watu wamekuwa wakilalamikia kuhusu hii site na serikali ilikuwa imekaa kimya tu..leo imewageukia wao..naona wanaanza ku_act mara moja!!!
hilo ndio tatizo kubwa tulilonalo sisi waafrika,people dont care about others!!
kama siku zote ingekuwaga inarusha hewani mambo kama hayo toka mwanzo, nadhani isingeweza kufika hii leo,lkn kwa vile ni watu wengine ambao ni wa kawaida,haikuwa issue...
... anyway...
 
Please close th e blog outright. Hata kama ungekuwa ukweli haingii akilini kwa mtu mwenye akili timamu kupiga au kuonyesha uozo wa nanmna hii. HUYU ZEUTAMU ACHUKULIWE HATUA ZA KISHERIA MARA MOJA. hivi hamna IT wa kuiblock nchi hii??

Ku-block website kwa nchi yetu ni ngumu kidogo kwa sababu gateways zipo tofauti,(ofisi kama ofisi inaweza lakini si kwa nchi) kitu rahisi ni ku-hack na kama wapo hackers wazuri.

Usishangae sn ndugu maana HATA ILE WEBSITE YETU YA TAIFA WATU WALII-HACK NA KUWEKA PICHA CHAFU, TULISHINDWA KUIREKEBISHA, HADI WATAALAMU WA KI-JAPAN WAKAITANZUAN 😕



Labda tuwaambie ISP wote TZ na Duniani kwa ujumla 🙄
 
Linapokuja suala la faragha and heshima ya mtu, ibara ya 16 ya katiba yetu inasema hivi:


16.-(1) Kila mtu anastahili kuheshimiwa na kupata hifadhi kwa nafsi yake, maisha yake binafsi na familia yake na unyumba wake, na pia heshima na hifadhi ya maskani yake na mawasiliano yake ya binafsi.
(2) Kwa madhumuni ya kuhifadhi haki ya mtu kwa mujibu wa ibara hii, Mamlaka ya Nchi itaweka utaratibu wa sheria kuhusu hali, namna na kiasi ambacho haki ya mtu ya faragha na ya usalama na nafsi yake, mali yake na maskani yake, yaweza kuingiliwa bila ya kuathiri ibara hii.

Haki haianzii kwa Rais pekee. Hata wale wadogo wanastahili haki ya faragha kama ilivyo kwa Rais.Hivyo ndivyo katiba inavyotaka!
 
naikumbuka ile mwanakijiji na mwafrika wa kike walisema wana picha ya namna hio.....ndio maana nasema tuanze sisis wenyewe hapa JF......

Ahaaaa, sasa napata picha kwa nini Mwanakijiji na Mwafrika wa kike walijishaua kipindi kileeeee, kwamba wameahirisha kuziweka picha hadharani.

Mwanakijiji it's pity kwamba i have to connect you with this scandal kwa 95% you know why? Kwanza una chuki binafsi na CCM, na vile JK ni CCM, na kila siku hapa unamchafua mara kumuita fisadi, terrorist na kadhalika, bado umeona haitoshi. Ukijua wazi 2010 ndiyo hiyoooo, umeamua kumdhalilisha Baba wa watu kwa hizi picha ulizotengeneza na kuzitunza tangu kipindi kileee, ili kumchafua kwamba muoneni Raisi wenu! Ukoje lakini wewe Mwanakijiji jamani?

Kila siku kujifanya wewe unauchungu sana na Tanzania kuliko wengine, Bongo yenyewe huji kuona iko vipi tangu uondoke miaka ileee, kulalamika tu CCM, sijui nani na nani, as if wewe uko safi.

Sijapenda ulivyofanya. You really need to convice me kwamba huhusiki which I won't buy it anyway. Kwa nini hukuitoa kipindi kile, eti mwenyewe ukaitunza kufikiri tumesahau, leo na wewe unajishaua. Grrrrrrrr. Unafiki mbaya sana.

Nenda bana kaitoe hiyo picha. Ni wewe umezituma kwa zeUtamu, zile ulizozitunza kipindi kileee, nitajaribu kuzitafuta Post zenu na Mwanamke wa kike sijui wa kiafrika, whatever the name. You didnot play smart this time Mwanakijiji.

Eti na wewe upo hapa kuchangia kulaani, come on old man! You lost big time kupigia Kampeni JF.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom