Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,891
- 155,907
Weekend Kareem wapenzi wa JamiiForums popote mlipo. Naamini mu wazima wa siha muruwa kabisa huku mkifanya tathmini ya kile mlichokifanya kwa juma zima hili.
Leo nimeleta kwenu swali juu ya Idd Amini, sipendi kumwita Nduli ila tumuombe tu Mwenyezi Mungu aendelee kuipumzisha roho yake.
Idd Amini aliitwa majina yote mabaya na nchi za magharibi baada ya utiriri wa matukio ya wadhalilisha Wazungu na kuwatimua Wahindi ili Waganda wenyewe waendeshe shughuli zote za kiuchumi na kukuza uchumi wao.
Miongoni mwa visanga alivyo vifanya Idd Amini ni pamoja na:-
KUKAWA na maneno kati ya Mwalimu na Amini ambayo hayakuwa mazuri, hatimaye yakapelekea vita ya mataifa mawili haya.
Habari za Idd Amini kula nyama za watu, je ilikuwa uzushi ama propaganda?
Je habari za Amin kuwapasua wanawake wajawazito, ilikuwa ni kweli au uzushi?
Je habari za Amini kuwatupa mto Nile walemavu zina ukweli gani? Je kuna uhusiano gani na ule wimbo wa Mchakamchaka Idd Amini akifa siwezi kulia, nitamtupa Kagera awe chakula cha mamba?
Karibuni waungwana
Leo nimeleta kwenu swali juu ya Idd Amini, sipendi kumwita Nduli ila tumuombe tu Mwenyezi Mungu aendelee kuipumzisha roho yake.
Idd Amini aliitwa majina yote mabaya na nchi za magharibi baada ya utiriri wa matukio ya wadhalilisha Wazungu na kuwatimua Wahindi ili Waganda wenyewe waendeshe shughuli zote za kiuchumi na kukuza uchumi wao.
Miongoni mwa visanga alivyo vifanya Idd Amini ni pamoja na:-
- Kuwaamuru mabalozi wa nchi za Ulaya wambebe juu juu na kiti kisha kumzungusha mitaani huku wananchi wakishangalia. Alifanya hivi kulipa kisasi jinsi babu zetu walivyowabeba wazungù.
- Kuna wakati Amin aliomba msaada wa kifedha kwa Malkia Elizabeth, msaada ukachelewa, baada ya miezi kadhaa ndipo Amin akapewa hiyo pesa, kwa jeuri akamwambia sina shida na pesa yako, akairudisha. Malkia alikasirika sana.
- Idd Amini aliwatimua Waasia wote, Wahindi na Waarabu ili kupisha Waganda wenyewe wafanye biashara.
KUKAWA na maneno kati ya Mwalimu na Amini ambayo hayakuwa mazuri, hatimaye yakapelekea vita ya mataifa mawili haya.
Habari za Idd Amini kula nyama za watu, je ilikuwa uzushi ama propaganda?
Je habari za Amin kuwapasua wanawake wajawazito, ilikuwa ni kweli au uzushi?
Je habari za Amini kuwatupa mto Nile walemavu zina ukweli gani? Je kuna uhusiano gani na ule wimbo wa Mchakamchaka Idd Amini akifa siwezi kulia, nitamtupa Kagera awe chakula cha mamba?
Karibuni waungwana