olimpio
JF-Expert Member
- Apr 5, 2023
- 402
- 834
Nimewaza sana baada ya kuona bunge la umoja wa nchi za ulaya umepiga kura kwa wingi kabisa kulaani serikali ya Tanzania kuwaondoa kwa hiari wamaasai Ngorongoro .
Hamaki yangu kubwa ilisimamia hapa
1. Je, ni kweli wanatupenda sana hawa wazungu kuliko ndugu zao wanaoteseka huko Ukraine ?
Nchi kibao haziwa support ukraine lakini ziko tayari kuwa support wamaasai , huu ni upendo wa agape kwa wamaasai wa ukweli?
2. Wazungu wanapeleka silaha kali za kuangamiza ndugu zetu katika imani na wapigania uhuru wao huko Gaza
,watu wanakufa maelfu kwa maelfu , lakini hawaizuii Israel kuua watu , je wamaasai ni watu bora sana kuliko wanaokufa huko gaza?
Ngoro ngoro wamekufa wamaasai wangapi? Israel imeua wapalestina wangapi?
kwa nini Tanzania?
3. Wazungu waliua babu zetu na kuwatumikisha kwa dharau na mpaka leo hawajawahi kuomba radhi kwa ufedhuli waliotufanyia, leo hii mapenzi ya dhati ya kuwatetea wamaasai yako yametoka wapi?
4. Wazungu walitukataza tusijenge bwawa la mwalimu nyerere la kufua umeme ,wakisema tutafukuza vyura adimu duniani,yaani wanajali zaidi vyura kuliko maisha ya watanzania , leo wanapata wapi nguvu ya kuendelea kuwa remote ya maamuzi yetu?
Hawa wameua babu zetu ,wamemuua Mkwawa , wameua viongozi wetu wa kale wengi sana , na bado wamekua remote za maamuzi yetu , ni lini Tanzania itakua nchi huru? ni lini tutafanya mambo yetu bila hawa wanaojiita wapigania haki kutuingilia?
wanafiki wakubwa , wameruhusu ushoga kwenye nchi zao , wanatupa misaada ya masharti mabaya na magumu , wanatupeleka kuzimu hawa.
Hamaki yangu kubwa ilisimamia hapa
1. Je, ni kweli wanatupenda sana hawa wazungu kuliko ndugu zao wanaoteseka huko Ukraine ?
Nchi kibao haziwa support ukraine lakini ziko tayari kuwa support wamaasai , huu ni upendo wa agape kwa wamaasai wa ukweli?
2. Wazungu wanapeleka silaha kali za kuangamiza ndugu zetu katika imani na wapigania uhuru wao huko Gaza
,watu wanakufa maelfu kwa maelfu , lakini hawaizuii Israel kuua watu , je wamaasai ni watu bora sana kuliko wanaokufa huko gaza?
Ngoro ngoro wamekufa wamaasai wangapi? Israel imeua wapalestina wangapi?
kwa nini Tanzania?
3. Wazungu waliua babu zetu na kuwatumikisha kwa dharau na mpaka leo hawajawahi kuomba radhi kwa ufedhuli waliotufanyia, leo hii mapenzi ya dhati ya kuwatetea wamaasai yako yametoka wapi?
4. Wazungu walitukataza tusijenge bwawa la mwalimu nyerere la kufua umeme ,wakisema tutafukuza vyura adimu duniani,yaani wanajali zaidi vyura kuliko maisha ya watanzania , leo wanapata wapi nguvu ya kuendelea kuwa remote ya maamuzi yetu?
Hawa wameua babu zetu ,wamemuua Mkwawa , wameua viongozi wetu wa kale wengi sana , na bado wamekua remote za maamuzi yetu , ni lini Tanzania itakua nchi huru? ni lini tutafanya mambo yetu bila hawa wanaojiita wapigania haki kutuingilia?
wanafiki wakubwa , wameruhusu ushoga kwenye nchi zao , wanatupa misaada ya masharti mabaya na magumu , wanatupeleka kuzimu hawa.