Je, ni kwanini waajiri wengi hapa kwetu mishahara yao haiendani na uhalisia wa gharama za maisha, na Je, ni halali kubakia hivi miaka yote?

Heaven Seeker

JF-Expert Member
May 12, 2017
478
1,047
Si Serikali wala Sekta binafsi, ukiangalia, kwa uhalisia, kwa watu walio wengi, wanapata mishahara iliyo chini na uhalisia wa gharama za maisha. Mfano unakuta mwajiriwa wa Serikalini, graduate, kwa walio wengi, ukiachilia watu wachache sana waliopo kwenye sekta chache, wanalipwa kuanzia 750K- 950K kama basic salary. Ukiondoa makato yote mtu anajikuta anabakiza kama 500K hivi.

Katika hiyo 500K, unajikuta gharama za maisha kwa mwezi, yaani ulipie kodi ya nyumba, chakula, usafiri na bills nyinginezo ni karibu ya 1M kwa mwezi.

Ukienda kwa wenzetu nchi zilizoendelea, hata ufanye kazi ya kiwango kile cha chini kabisa kama usafi, warehouse assistance, food delivery, housekeeping, caretaker, huwezi kukuta mshahara wake ni chini ya gharama za maisha. Yaani wenzetu wame-standardize kwamba kiwango cha chini cha malipo kwa mtu kiwe sawa au juu kidogo ya gharama za kawaida za kuishi kwa mtu kwa mwezi. Yaani unakuta kwa mfano mtu anayefanya kazi ya usafi nchi zilizoendelea kama Sweden, UK, Uholanzi n.k analipwa average Euro 1800 - 2000 kwa mwezi, ila gharama za maisha kwa mwezi ni kama Euro 1500 hivi. Na kumbuka hapa ni kwa non-professional jobs.

Sasa swali langu ni kuwa, nyie wataalamu wa Uchumi na sheria hapa kwetu hebu tuambieni, Je ni kwa nini waajiri wengi hapa kwetu wanalipa mishahara chini ya gharama za kuishi zile za hali ya kawaida, mfano tuchukulie maisha ya kawaida mtu aishi angalau kwenye nyumba ambayo kodi ni 250K kwa mwezi, chakula na bills nyinginezo alipie angalau 600K kwa mwezi, jumla iwe angalau 850K.

Swali la pili, Je, ni hii ni haki au tunanyonywa?

Karibuni kwa mjadala.
 
Wewe unawaza kula tu au maisha ni kula tu? Vipi kusomesha, kujenga, nishati (umeme gesi )? Au huko ileje vyote hivi mnapewa bure? Jitahidi kufikilia nje ya box.
Nadhani hukumuelewa ndug.....ametumia kula na kusaza kama kuonesha kuwa mshahara huo unakidhi mahitaji yote ya msingi ikiwemo kula.......na kula ni moja hitaji la msingi la kwanza kwa kuwa ndio linebeba sababu ya kuishi........
 
hiyo ndio kitu inaitwa uchumi.

angalia bajeti ya mwaka mzima ya serikali na matumizi yake ndio utaelewa,yaani serikali tu inashindwa kujiendesha kwa kodi zake,wakati nchi nyingine bajeti ni 20-40% ya total revenue.ndio maana wanapata mahela mpaka ya kutukopesha hovyo.
wana uwezo wa kupandisha mishahara muda wowote wakitaka,kushape uchumi ukae wanavyotaka nk.
 
Nadhani hukumuelewa ndug.....ametumia kula na kusaza kama kuonesha kuwa mshahara huo unakidhi mahitaji yote ya msingi ikiwemo kula.......na kula ni moja hitaji la msingi la kwanza kwa kuwa ndio linebeba sababu ya kuishi........
mapanga3 kama ulishindwa kuelewa Ile comment nmekutafakari sana
 
Wewe una mfanyakazi wa ndani, shamba au msaidizi hapo kwako ?

Unamlipaje ? na hicho kipato kinatosha ?

Hizo Sekta Binafsi ushaangalia vitabu vyao ? wana-break even au wengi ni mwendo wa madeni na vikoba ?

Kabla haujaangalia mishahara angalia the whole system bora huyo anayepata 500K ana Security ukitaka kujua ugumu uliopo mwambia aache hio kazi aone wangapi wataiomba..., (In the meantime aishe within his/her means) sababu most are in a worse situation....

Hali sio hali na kuondoa hii shida we need to revamp the whole system; ila ndio hivyo supply and demand kama wengi wapo wanaoweza kuchukua pesa ndogo kwanini achukuliwe mwenye kutaka pesa kubwa na ukizingatia mishahara ni overheads zinazoongeza production costs, hence price ya product to eventually becoming less competitive within the market...

Na hapo sijaanza kuongelea automation.....
 
Hiki kitendawili kitakuja kujibiwa siku tutakapobadili mfumo wa kulipana kwa mwezi kuwa mfumo wa kulipana kwa lisaa la kazi.

Hao unaosema wamefanikiwa wametoka huku kwa mwezi wanalipana kwa lisaa. Hii inasaidia sana kupunguza gharama za uendeshaji wa taasisi na kupunguza uzembe kazini.

Hapa tz kuna watu wanalipwa mishahara kwa kazi ambazo hawafanyi na wamekalia kukaa kwenye position ambazo hawana uwezo nao, wamezing'ang'ania kweli kweli kama mashipa pumbavu.

Siku tutakapoamua kama taifa kupitia mijadala ya wazi na bungeni kuwa watu walipwe kwa makadirio ya lisaa la kazi mtaona sasa ufanisi utakavyopanda na kazi zitakavyokuwa rahisi kufanyika.

Saa hii mtu analazimika kukaa kwenye eno la kazi kwa kuripoti saa moja asubuhi na kutoka saa kumi na moja au kumi na mbili jioni. Hii inakupa picha kuwa huyu mtu kwanza kiufanisi hawezi kuwa vizuri kwa masaa yote hayo kila siku.

Halafu mshahara anaopata hautaweza mtosha maana anatumia masaa yote sehemu moja kisha akirudi nyumbani familia inamngoja alipe bili ambazo zinakula mshahara wote aliosubiria mwezi mzima.

Huu ni upotezaji wa muda, upotezaji wa nguvu kazi, upotezaji wa rasilimali na kubwa zaidi ni upotezaji wa target ya kuyafikia maendeleo kwa kasi.
 
Samcezar

Hii itasaidia nini kama mlipaji na yeye hawezi ku-break even ? Ndio maana nikauliza kama una mfanyakazi wa ndani unamlipaje ? Je anao uwezo wa kujikimu na unachomlipa ?

Pili Kama kuna watu kumi wanataka hio kazi ya kulipwa kwa masaa huyu anaweza akachukua robo unayochukua wewe unadhani kutoka kwenye salary mpaka wages kutasaidia nini ?

Tatu hata sasa watu wanalipana kwa masaa (ndio maana kuna siku na muda wa kazi) Pia kukazia hapa kwenye wages bado itakuwa yaleyale unless unaweza kusema hakuna overtime ni flat late (ila hio itamsaidia vipi anayelipwa)?

Utaona hapa issue ni competition na ili uweze ku-compete kwa bei unahitaji kupunguza overheads (na mishahara ni mojawapo ya hizo overheads)

Na hapo bado sijaanza kuongelea automation....
 
Back
Top Bottom