Mkuu, hata nisipoamini kuwa kuna Mungu ni sawa tu na kuamini kuna Mungu, hakuna tofauti yoyote ya kifizikia.
Mi nimemua kuwa mfuasi wa dini ya kikristu, kwa sababu kadhaa, lakini kubwa ni maamuzi tu binafsi!!
Lakini kwa maoni yangu, kuwa mfuasi wa dini au dhehebu flani angalau kunaleta ahueni na faraja kwamba shida tupitiazo yupo ambaye atatutatulia kwa imani.
Pia, kujumuika na watu kwa lengo flani, kunawafanya muwe na mahusiano ambayo yanaweza yakaleta matokeo chanya baina yenu, kama vile upendo, faraja, ushirikiano, n.k
Sababu hizo haziifanyi imani niliyonayo iwe ndio sahihi kuliko imani za wengine.
Na wala kiwa katika imani hii, hakuniwezeshi kuwaaminisha watu wasio wa imani yangu waamini, kumuona na kujua kuwa kweli Mungu yupo. Uwepo wa Mungu mimi siujui ukweli wake aisee!!
Bwana
Tz mbongo, Je, imani yako ndio sahihi kuliko za wengine!?