Hao ambapo hawana au hawafuati hayo Maandiko yako hawatafufuka?
Ufufuo ni wa watu wote siku ya Kiama, tangu Adamu hadi mtu wa mwisho kabisa kuzaliwa kabla ya kuja kwa Kristu mara ya pili.
Ama mtu alisoma Biblia au hakusoma, alimwamini Mungu au hakumwamini, wote watafufuliwa -- ili kila mtu apate ijara ya matendo yake.
Kama unaamini kuna hayo maisha baada ya kifo na mazuri kwanini usitangulie kwa hiari na kwanini mtu akijaribu kujitoa roho ashitakiwe wakati anaenda kwenye maisha mengine?
Tofauti na wapagani, Wakristu tunaamini kwamba hapa duniani tuko kwa makusudi maalumu tunayopaswa kutimiza.
Mojawapo kuu ni kuufahamisha ulimwengu kuhusu upendo mkuu wa Mungu na msamaha Wake kwa wadhambi.
Sasa mjumbe wa Mungu hawezi kutamani kuyaondoka maisha haya eti akimbilie umauti. It doesn't make sense. Does it?
Even if you were to die today, you would still have to wait in your grave until resurrection day.
Also, committing suicide is sin.
Mungu yupo kwa sababu mimi nimekuwa nikimuomba kupitia Babu na Bibi zangu ktk matatizo na mahitaji yangu na ninafanikiwa pasipo mdhuru mtu yeyote.
Pia wapo wanaonikosea au kunionea tu pasipo kosa lolote pia nimekuwa nikiwashitakia wanajibu kwa kuwaadhibu.
Hii ni dhana finyu, duni na potofu kuhusu Mungu.
Wapendwa wako waliokufa hawajui lolote huko kaburini.
Kama unafanikiwa kuzungumza nao, kama usemavyo, basi utakuwa unawasiliana na mizimu au mashetani.
Nao pia wana uwezo wa kukupa baadhi ya vitu upendavyo, kwa muda kitambo.
This is how they lie to you only to cast you into a dense pit of delusions.
Hii ni kweli na cha kujiuliza ni vipi Mungu ampendelee mtu na aache viumbe wengine wasifufuke wakati vyote viko na thamani sawa mbele yake i.e:ngome,mbwa,miti,samaki n.k. na vinategemeana na watu?
Ni akili ndogo kumkataa Mungu kisa tu hataokoa miti, bakteria, virusi, ndege, na wanyama wengine pamoja na mwanadamu siku ya mwisho.
Wewe ni aina ya wale watu wanaosema akijua iwapo wapendwa wake fulani na fulani hawapo mbinguni, yeye pia haoni sababu ya kuwa huko.
Unatakiwa kuelewa kwamba kifo ni matokeo ya dhambi. Dhambi ni uchaguzi wa hiari wa mwanadamu.
Mungu hakukusudia katika mpango Wake afe kiumbe hata mmoja. Aliumba ili viishi milele.
Someni hii kitu iko na mwamsho fulani ati!!!!
It's just a worded conglomeration whose content is full of garbage.
Watu wamekufa miaka million iliyopita hawajazaliwa tena af tuje kuzaliwa sie kwa uspesho gan tulonao?
Umejuaje hilo? Hebu fafanua hiyo miaka milioni. Ni milioni moja au milioni ngapi?
Tangu Adamu na Hawa, tuna miaka 6,000 tu ya binadamu duniani.
Geology may be very amusing, but also gravely deceptive at times. Any reasonable individual would be unfazed by it's novelties.
Si ni yule Mungu asiyeweza. Hajui kusoma na kuandika,alisubili waja wake wamuandikie na wamtangazie.
Mungu hawezi kukufanyia kamwe kitu ambacho amekupa uwezo wa kutenda wewe mwenyewe.
Sisi wanadamu ndio mikono tendaji ya Mungu duniani. Anamtumia mwanadamu ili kutimiza makusudi Yake matukufu.
Aliwavuvia wanadamu wakaiandika Biblia. Aliwapa ujumbe kupitia maono, nao wakaandika kwa kutumia lugha yao inayoeleweka kwa wanadamu.
Biblia wangeiandika malaika, bila shaka ingekuwa imejaa lugha waielewayo malaika.
Ila yenyewe ni kwa ajili ya mwanadamu, hivyo ina lugha na maneno yaelewekayo kwa mwanadamu.
Think! Stop being brain dead and prejudiced against matters so reasonably clear.
shida ni kwamba dunia imekuwepo kwa bilion of years,sasa huo ufufuo umekuja kuongelewa baada ya Yesu kuzaliwa
Kwanza tambua ufufuo ulihitajika kwa sababu ya kifo. Kifo kilisababishwa na dhambi.
It means dhambi ilipoingia tu, mwanadamu alifundishwa kuhusu msamaha wa Mungu kupitia Kristu, na ukombozi ambapo Mungu humpatia yeyote amwaminiye.
Jiulize hili swali kwanza
Kabla hujaja hapa duniani ulikuwa wapi?
Nafikiri utarudi ulikokuwa
Ulikuwa katika mawazo ya Mungu. Alikujua hata kabla ya wakati. Anamjua kila mtu tangu mwanzo.
Kila kitu kinachofanyika na kutokea duniani, tayari Mungu alishakiona hata kabla.
yaani niache kula bata za duniani nisubiri za mbinguni ntakua kichaa
Sasa wewe kumbe tatizo lako ni kula mabata, ndipo akili yako imeishia?
Wengine wanawaza mambo makuu zaidi ya ulaji tu wa mabata.
As if usipoyala hayo mabata, ukafa, utakuwa umemisi chochote? Akili ama kweli ni mali.
labda unambie alieandika hayo ni malaika na sio binadamu kama mimi ndo nitaanza kusoma hvo vitabu, haiwezekani nijaze akilini mwangu fikra za mtu mwingine.
Kumbe vitabu vya saikolojia, historia, sayansi na hesabu ulivyojaza ubongoni vimeandikwa na malaika?
Will you try to be consistent even for five minutes?
Yawezekana Mungu alikuwepo baadae akatoweka baada ya kuumba watu ktk matabaka mbalimbali then akapotea au kufariki ili kuweka muendelezo kama walivyo WACHAWI na nguvu zao za kujificha asilaumiwe
Hivi kweli uwezo wa fikra zako kuhusu mungu wako ndipo hapo umegota?
neno Mungu si kitu kilicho hai, ni njama tu ya utapeli wa hali ya juu iliyotengenezwa,
Na nani? Lini? Wapi? Nangoja ufafanuzi.
Siyo kwamba wewe ndiye tapeli?
Kama kweli yupo,muombe kitu uone kama atakupa. Ugua,uombe uone kama utapona.
Hapo sasa utakuwa unahitaji msaada au unamjaribu?
Ukimwomba Mungu kwa imani, anatenda. Wala hakuna shaka juu ya hilo.
kwa wasiomuamini,tuache tule upepo maana tunajua tukienda huko ni kuchezewa akili kwa hiyo hatutaki hizo sanaa na kuaminishwa mambo yasiyo na kichwa wala miguu.
Ebu tupe hata vigezo 3 vya uwepo wake
Unataka vigezo 3 vya uwepo wa Mungu, wakati huohuo unataka uachwe ule upepo? Halafu, hivi nani kakushika kwani eti?
Wewe si Mtanzania? Kitabu cha Efeso au Wafilipi kinakuhusu nini wewe?
Kwa hiyo wewe hapo vitabu vyote ulivyo navyo au usomavyo, wameandika Wabongo tu?
Mimi nikiomba MUNGU kupitia BABU na BIBI zangu nafanikiwa
Huu unaitwa umizimu ama ushetani. Usiseme tena hujaambiwa.
Naamini huwezi ukamuomba MUNGU direct pasipo kupitia kwa waliokuleta duniani na ukafanikiwa ,NEVER!!
Asee! It's very saddening that your picture of God is very rudimentary.
How in the world would a holy and loving God put off a sincere prayer from His dear children?
DINI zote ndiyo za michongo kwani zinawahubiri WAAFRIKA kwa kuwatoza HELA na MALI.
Nitajie chama hata kimoja ambacho hupaswi kutoa michango yako ili kukisaidia.
Sadaka katika suala la imani ina makusudi makubwa sana, kwa mhusika na kwa kazi ya injili.
By the way, usisahau unakuja mikono mitupu duniani, ukifa unatoweka mikono mitupu.
Mali na utajiri vinapaswa vitumike kwa kusudi maalumu, plus kuwasaidia wahitaji.
Even successful individuals such as Bill Gates and Cristiano Ronaldo know very well that philanthropic lifestyle is the only pathway to true fulfillment and happiness.
Wazungu na Waarabu walitumia dini/tamaduni zao kupitia Biblia na msahafu ili kufanikisha unyonyaji
Kauli yako ni sawa na kusema hutaki reli kwa sababu aliijenga mkoloni, tena kwa kumtesa babu yako.
Ulishawahi kuelewa maana ya msemo: Usimtupe jongoo na mti wake?
Mungu aliumba viumbe hai na visivyo hai ambavyo tunavishuhudia tangu mwanzo wa ulimwengu huu vikiwepo.
Ni wapi MUNGU aliumba vitabu vyake na kama ni hivyo vya Biblia cha Wazungu na msahafu cha Waarabu
Biblia haina Uzungu wala Uarabu wala Uchina. Naamini na Msahafu uko hivyo pia.
Mungu anakuona wewe kama mwanadamu, na wala siyo kupitia rangi ya ngozi yako.
Halafu, nisaidie kujua Mzungu ni nani? Mwenye ngozi nyeupe au anayeishi Ulaya?
Na Mwafrika ni nani? Mwenye ngozi nyeusi au anayeishi Afrika?
Kuhusu vitabu vya Mungu, tambua kwamba kila kitu unachoona duniani ni kitabu cha Mungu cha mafunzo ili kumwelewa zaidi.
-uumbaji wa asili, akiwemo mwanadamu, kitabu cha Mungu
-hali za wanadamu, matatizo, mateso, mauti, hivi vyote ni vitabu vya Mungu
-Biblia ni kitabu maalumu cha Mungu.
Kama kungekuwa na mwanzo wa dunia kwa wote kwa siku moja basi ningeamini kuna mwisho wa dunia kwa wote kwa siku moja.
Lakini kama kila mtu alizaliwa hapa duniani kwa siku yake basi hata mwisho wake niwa peke yake hivyo hakuna ujinga huo wa mwisho wa dunia.
Again, this is a preposterous logic.